Zijue sababu za jeshi letu JWTZ kutokutoa kichapo kingine kwa M23, kama tulivyotoa mwaka 2013 hadi 2014

Zijue sababu za jeshi letu JWTZ kutokutoa kichapo kingine kwa M23, kama tulivyotoa mwaka 2013 hadi 2014

Hakuna cha aibu mkuu. Hii ni diplamasia yenye faida kwetu. Wanajeshi kuwa kule wanalipwa. Lakini pia tulieenda kumchapa hatumchapi kwa kuhofia kwamba tukimchapa kisawa sawa ataacha kutumia bandari yetu kupitisha mizigo yake.
Ardhi ya Congo sisi haituhusu, sasa hatuwezi kukubali kumpoteza mtu anaeiingizia nchi yetu mamilioni ya shilingi kupitisha mizigo yake katika ardhi yetu kwa sababu ya kuisaidia Congo.

Vita hii tunaweza kuichukulia serious kama adui atasogea kuiteka Kigoma au Kagera. Ila kama ni vita vinavyopiganwa Congo basi acha jeshi letu likatengeneze mamilioni bila kuharibu uhusiano na yule tunaetakiwa kumtwanga.
Hata kongo wanapitisha mizigo yao bongo na wanatupa faida kubwa kuliko rwanda
 
soko la Kongo ni kubwa kuliko la Rwanda ni swala tu la kukaa mguu sawa.
kibaya zaidi ubinafsi wa viongozi wetu unatuletea tabu kubwa kwetu.
ifike sehemu nafikiri Mama kwa heshima kabisa apumzike.
ukipoteza askari wawili kati ya mia ni kwamba umepoteza 2% ya askari ulionao lakini familia imepoteza 100% ya mzazi au mtu waliyemtegemea katika maisha yao hivyo kama anaona haina tija na inaguza maslahi binafsi na yuko tayari kula haramu kwakuwa ni DAMU ZA WATU wasio na hatia basi ajiunge moja kwa moja m23tuwapige wakongo vinginevyo wanaokufa pia ni waafrika wenzetu kwa mali zao.
Mkuu mbona haueleweki.. Mara useme soko la Congo kubwa kuliko la Rwanda, mara umlaumu raisi kwa vifo vya askari wawili ambao wametumwa kulinda hilo soko kubwa la Congo lisichukuliwe lote.

Sasa hapo point yako ni nini?
Kuwarudisha nyumban askari unaosema wanakufa ili hilo soko kubwa la Congo unalosema hapa tulikose lote?

Au unamaanisha nini?
 
Hata kongo wanapitisha mizigo yao bongo na wanatupa faida kubwa kuliko rwanda
Kwahiyo ndio tuamue kuchagua upande mmoja, ili tuuchangie upande mungine ambao haujawahi kutuchokoza, wala kutuvamia katika ardhi yetu?
 
Hakuna cha aibu mkuu. Hii ni diplamasia yenye faida kwetu. Wanajeshi kuwa kule wanalipwa. Lakini pia tulieenda kumchapa hatumchapi kwa kuhofia kwamba tukimchapa kisawa sawa ataacha kutumia bandari yetu kupitisha mizigo yake.
Ardhi ya Congo sisi haituhusu, sasa hatuwezi kukubali kumpoteza mtu anaeiingizia nchi yetu mamilioni ya shilingi kupitisha mizigo yake katika ardhi yetu kwa sababu ya kuisaidia Congo.

Vita hii tunaweza kuichukulia serious kama adui atasogea kuiteka Kigoma au Kagera. Ila kama ni vita vinavyopiganwa Congo basi acha jeshi letu likatengeneze mamilioni bila kuharibu uhusiano na yule tunaetakiwa kumtwanga.
Upuuuuziiiii!!Hizo hizo silaha zinazopita bandarini kupitia mfadhili uliyesema,Ndizo hizo hizo kunasiku zitakuja kututwanga tukiwa tumeshiba makande yanayotokana na hizo pesa anazolipa kupitisha Silaha.
 
Njia nyepesi ya kuwafurusha waasi ni kuwahamisha wakazi kwa muda eneo salama atakekaidi atahesabika ni muasi ahera Ina muhusu.
Ifanyike operation kama IDF ilivyofanya Gaza kuwashughulikia Hamasi kwa kuwahamisha wakazi wa Gaza kabla ya kushusha moto ambao magaidi wa Hamasi wakaomba poo.
Kwann tucheke na wahuni wachache Wanasababisha nchi za maziwa kukosa amani.
 
Nilimaanisha kujenga reli kuelekea Rwanda
Oh hapo nimekuelewa mkuu. Lakini kumbuka katika huo ujenzi Rwanda pia imekubali kuchangia, wakati Zambia haijatoa mchango wowote ili reli iweze kufika kwao.

Mpaka leo TAZARA imekwama kwa sababu ya kukosa maelewano mazuri kuhusu namna ya kuijenga upya reli ya TAZARA.

Lakini Rwanda linapokuja swala la kuleta maendeleo katika ardhi yake na raia wake, nchi hiyo ipo tayari kutumia gharama yoyote ili ifanikishe jambo hilo. Nafikiri hilo hata wewe unalijua.

So serikali haiwezi ku deal na nchi ambayo haiko tayari kushirikiana nayo kifedha kupelekea maendeleo katika nchi yao.

Waswahili wanasema "mkono mtupu haulambwi".
 
Njia nyepesi ya kuwafurusha waasi ni kuwahamisha wakazi kwa muda eneo salama atakekaidi atahesabika ni muasi ahera Ina muhusu.
Ifanyike operation kama IDF ilivyofanya Gaza kuwashughulikia Hamasi kwa kuwahamisha wakazi wa Gaza kabla ya kushusha moto ambao magaidi wa Hamasi wakaomba poo.
Kwann tucheke na wahuni wachache Wanasababisha nchi za maziwa kukosa amani.
Wazo lako zuri mkuu.
 
Upuuuuziiiii!!Hizo hizo silaha zinazopita bandarini kupitia mfadhili uliyesema,Ndizo hizo hizo kunasiku zitakuja kututwanga tukiwa tumeshiba makande yanayotokana na hizo pesa anazolipa kupitisha Silaha.
Hawana ujanja wa kututwanga.
, maana silaha zao zote wanazopitisha bandarini tunazijua vizuri. Hivyo hawana ujanja wa kututisha kupitia silaha hizo.

Ndomaana Kikwete kipindi kile cha kutaka kuingia nao vitani, alipoenda pale Kagera katika sherehe za kuwakumbuka mashujaa wetu waliofariki katika vita vya Uganda.

Alisema watanzania laleni usingizi vizuri tena kwa kutulia. Kwa sababu jeshi letu na serikali yetu ipo kazini kuhakikisha hakuna mende yoyote atakaevuka mpaka kuja kufanya shambulizi katika ardhi ya Tanzania.

Alisema hivyo kwa sababu silaha zao zote alikuwa anazijua, nchi yao yote alikuwa anaijua na udhaifu wao wote alikuwa anaujua.

Wewe umeshiba mihogo na kulala chini ya mti kuhesabu ndege wanaopita angani huko kijijini kwenu. Hivyo mambo ya jeshi na uwezo wake hauwezi kuyajua. Naapa mbele ya Mungu kwamba huna unalojua kuhusu jeshi letu.
 
Hawana ujanja wa kututwanga.
, maana silaha zao zote wanazopitisha bandarini tunazijua vizuri. Hivyo hawana ujanja wa kututisha kupitia silaha hizo.

Ndomaana Kikwete kipindi kile cha kutaka kuingia nao vitani, alipoenda pale Kagera katika sherehe za kuwakumbuka mashujaa wetu waliofariki katika vita vya Uganda.

Alisema watanzania laleni usingizi vizuri tena kwa kutulia. Kwa sababu jeshi letu na serikali yetu ipo kazini kuhakikisha hakuna mende yoyote atakaevuka mpaka kuja kufanya shambulizi katika ardhi ya Tanzania.

Alisema hivyo kwa sababu silaha zao zote alikuwa anazijua, nchi yao yote alikuwa anaijua na udhaifu wao wote alikuwa anaujua.

Wewe umeshiba mihogo na kulala chini ya mti kuhesabu ndege wanaopita angani huko kijijini kwenu. Hivyo mambo ya jeshi na uwezo wake hauwezi kuyajua. Naapa mbele ya Mungu kwamba huna unalojua kuhusu jeshi letu.
Kulikuwa na ulazima gani kuandika hayo maneno hapo chini?Wewe unajua Jeshi mana ni chakula chao wakiwa vitani,Shwaain
 
Niaje waungwana

Kwanza kabla ya kuelezea sababu za jeshi letu kutokutoa kichapo kwa M23, naomba kwanza nianze kuwapa historia tukufu ya jeshi letu la JWTZ au TPDF kwa nchi mbali mbali za Africa na Dunia kwa ujumla.

JTWZ chini ya baba wa taifa letu hayati mwl. Julius K. Nyerere ndio iliyoongoza mapambano yasioshindwa ambayo kwa asilimia kubwa yalisaidia nchi za Zimbabwe, Msumbiji, Afrika Kusini, Namibia na Angola kuwa katika mikono salama, na amani ya kudumu mpaka leo.

Idi Amin alitaka kujichanganya eti aichukue Bukoba, matokeo yake imechukuliwa nchi yake mwenyewe, halaf yeye akatoka nduki.

JWTZ hiyo hiyo chini ya utawala wa hayati mzee Ally Hassan Mwinyi ndio iliyotoa kichapo kitakatifu kwa jeshi la Burundi ambalo lilitaka kuteka sehemu ya mkoa wa Kigoma, kwa kisingizio cha kuja kuwapiga waasi wa CNDD-FDD ambao walikuwa wakipambana na serikali ya Burundi chini ya uongozi wa raisi meja Pierre Buyoya (rip).

Ni kwamba Buyoya na serikali yake walikuwa wanadai kwamba serikali ya Tz imekuwa ikitoa msaada wa kuwahifadhi waasi hao katika maeneo ya mpakani mwa Mkoa wa Kigoma na Burundi. Hivyo dawa ya kukomesha jambo hilo ilikuwa ni kuivamia Tz (Buyoya sijui nani alimhadaa ashike moto kwa mkono), kuichapa na kuteka maeneo yote aliyodai yanatumiwa na waasi nchini kwetu kufanyia training na kupanga mipango ya kuingia Burundi kufanya maangamizi mara kwa mara.

Basi bwana Buyoya akaamuru jeshi lake lifanye ambush kupitia mipaka ya ardhini na majini. Aisee kilichotokea kwa upande wa Burundi mpaka leo ni hasara kwa nchi yao.

Kuna jamaa fulan Mrundi anasema kuwa sehemu hiyo iliyoangukiwa na kombora kutoka Tz mpaka sasa hapajawahi kuota chochote, na wala kujengwa chochote. Ni kama vile ardhi imeunguzwa hata kwa kutumia kutengenezea tofali za kuchoma haifai kudadeki. Baada ya lile tukio Buyoya na warundi wenzie wakawa wapole na askari waliokuwa wanalinda mipaka ya majini na ardhini kwa upande wa Burundi akawasogeza mbali mno kutoka mpakani.

Chini ya utawala wa raisi Kikwete kuna raisi alikuwa ashapinduliwa hapo Comoro, ikabidi aje kuomba msaada wa kumrudisha madarakani. Ni kitendo cha masaa tu raisi akarudishwa na wahuni waliopanga mapinduzi wakatiwa nguvuni.

Pia chini ya Kikwete raisi wa Burundi hayati Pierre Ngurunziza alikuwa ameshapinduliwa na kuambiwa abaki huku huku Tz alipokuwa amekuja kwa mkutano wa amani. Baada ya ujinga huo, Kikwete akatuma kikosi kidogo tu cha wanajeshi wa kumrudisha nchini kwake salama na kuwatia nguvuni wapuuzi wachache waliompindua raisi wao. Bila kuchelewa jeshi letu likamrudisha Ngurunziza, ila wapinduaji wakafanikiwa kutoroka na kukimbilia nchi jirani.

Chini ya utawala huo huo wa Kikwete jeshi letu lilitoa kipondo ambacho kilisababisha waasi wa M23 kutimkia Uganda na Rwanda. Na hii ni baada ya raisi wa Rwanda mhe. Paul Kagame kumletea dharau Kikwete na jeshi letu hali iliyosababisha Kikwete adili na kila kinachompaka Kagame jeuri. Alianza na wanyarwanda waliokuwa wanaishi nchini kinyume cha sheria, baadae akarukia Congo kuwafyeka M23 ambao waliaminika kuwa ni jeshi dogo la Rwanda. Kisha akasogeza jeshi mkoa wa Kagera kuwa tayari kuingia Kigali, sema hekima Za mzee Mwinyi na Mkapa zilichangia kumfanya Kikwete asivaamie Rwanda kumtoa adui yake.

Tukiachana na hayo. Tushapandikiziwa vikundi vya waasi kwa mgongo wa dini huko Tanga, Kibiti nk. Lakini jeshi letu halijawahi kucheka na kima wote tumewaangamizi kwa muda mfupi sana.

Hizo operations zote nilizoeleza hapo juu zilitekelezwa na TPDF bila kushindwa wala kurudi nyuma. Hivyo uwezo wa kumpiga adui toka miaka hiyo tulikuwa, tunao na tutaendelea kuwa nao. Huu ndio ukweli halisi.

Sasa tukija kwa hii vita ya sasa ya M23. Kuna watu wanajiuliza iweje M23 hii tulioichapa wakati wa Kikwete imetushinda wakati wa Samia!!

Ukweli ni kwamba jeshi letu lipo imara, vizuri na tayari kwa mapambano wakati wowote bila kujali ni nani aliepo madarakani. Kikubwa ambacho hufanyika ni kuliongezea jeshi silaha za kisasa, mbinu mpya za kijeshi, nguvu na morali zaidi za kulitumikia jeshi la wananchi. Pia jeshi letu hupambana kupitia amri ya amiri jeshi mkuu na wasaidizi wake. So kama amiri jeshi mkuu haoni tija yoyote ya jeshi letu kupambana huko Congo na kwengine basi jeshi letu halitopambana.

Sasa kinachoendelea Congo kwa sasa ni tofauti na kile kilichokuwa kinaendelea kipindi kile cha 2013 hadi 2014. Kipindi kile tuliingia vitani kivita kweli kweli, huku amiri jeshi mkuu wa Tz akiwa na lengo la kumshikisha adabu amiri jeshi mkuu mwenzake wa nchi jirani. Hivyo ilikuwa ni vita ya serious ndiomaana tuliwachapa M23 bila huruma hadi wakakimbia wenyewe na kuacha silaha zao.

Lakini hii vita ya sasa hivi Congo sisi hatukwenda ki serious kwa sababu raisi amegundua kwamba hii vita haina faida yoyote kwetu. Sana sana tunaweza kupata hasara zaidi kuliko faida.

Hii ni kwa sababu mfadhili mkubwa anaewafadhili hawa M23 ndio mtu wa kwanza au wa pili kupitisha mizigo yake katika bandari yetu na ardhi yetu. Analipa mabilioni ya ushuru kila siku au kila week.

Hivyo tukiingia kwenye vita na mtu huyu ni sawa sawa na kuukata mkono wako mwenyewe unaokulisha. Kumbuka kwamba mfadhili huyo ana ukaribu na amiri jeshi mkuu wetu haswa kuhusu maswala ya kibiashara , upitishaji wa mizigo na ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi yetu na nchi ya mfadhili. Sasa tukiwa serious kumtwanga itabidi atukimbie na kwenda kushirikiana na nchi nyingine kama vile Kenya nk.

Hizo ndio sababu kuu za sisi kutoiadhibu M23 kama kipindi kile. Serikali inaangalia hasara na faida inayopata kupitia vita hivi. Tukiwachapa basi hasara itakuwa kubwa kuliko faida. Lakini kwa vile sisi ni sehemu ya SADC na tumechaguliwa kwenda Congo. Basi acha jeshi letu litulie kule kujilia watoto wa kinyamulenge hadi muda ukapofika kurudishwa nyumban waruri kuendelea na maisha. But ukweli utabaki pale pale kwamba hapa East Africa hakuna jeshi wala kikundi cha wahuni kama hicho cha M23 ambacho kitaweza kupambana na JWTZ.
Bro kikwete hakufukuza wanyarwanda wanaoishi TZ, kule kagera, kwa taarifa yako, Rwanda kuna Watusi na wahutu, TZ kuna wanyambo, wanyankore, hawa wote ni jamii moja, kama ilivyo kwa Maasai wa TZ na Kenya, au mjaluo wa TZ na Mluo wa, Kenya!
 
Oh hapo nimekuelewa mkuu. Lakini kumbuka katika huo ujenzi Rwanda pia imekubali kuchangia, wakati Zambia haijatoa mchango wowote ili reli iweze kufika kwao.

Mpaka leo TAZARA imekwama kwa sababu ya kukosa maelewano mazuri kuhusu namna ya kuijenga upya reli ya TAZARA.

Lakini Rwanda linapokuja swala la kuleta maendeleo katika ardhi yake na raia wake, nchi hiyo ipo tayari kutumia gharama yoyote ili ifanikishe jambo hilo. Nafikiri hilo hata wewe unalijua.

So serikali haiwezi ku deal na nchi ambayo haiko tayari kushirikiana nayo kifedha kupelekea maendeleo katika nchi yao.

Waswahili wanasema "mkono mtupu haulambwi".
Mimi nashangaa kuna reli ya tazara lakini malori mamia kwa mamia kila siku yanatoka dar to mbeya - to Zambia na kurudi kila siku. Njia ya dar to mbeya ingewekwa vizuri tungefaidika pakubwa. Tatizo viongozi wetu sio wafanyabiashara
 
Bro kikwete hakufukuza wanyarwanda wanaoishi TZ, kule kagera, kwa taarifa yako, Rwanda kuna Watusi na wahutu, TZ kuna wanyambo, wanyankore, hawa wote ni jamii moja, kama ilivyo kwa Maasai wa TZ na Kenya, au mjaluo wa TZ na Mluo wa, Kenya!
Mkuu acha kwanza mihemko ili uwe na muda wa kusoma vizuri kilichoandikwa, uwe na muda mzuri pia wa kutafakari unachoandika. Na zaidi uwe na muda mzuri wa ku comment bila kupindisha pindisha mada husika.

Mimi nimezungumzia wanyarwanda ambao walikuwa hawana vibali na sio wale wenye vibali. Halaf kingine sikuzungumzia watusi bali wanyarwanda wasiokuwa na vibali kwa umoja wao. Haijalishi ni muhutu, mtusi au mtwa.

Kingine ambacho nataka nikufahamishe ni kwamba sio kila mtusi ni Mnyarwanda. Kuna watusi ambao ni warundi pyu na hao ndio waliowasaidia watusi wa Rwanda kuingia kigali kutokea Burundi.

Wakati wa vita ya Rwanda, Burundi ilikuwa inaongozwa na watusi wa kirundi. Hivyo chini ya utawala wa wahutu huko Rwanda kuna watusi wengi walikimbilia Burundi kuomba hifadhi kwa watusi wenzao waliokuwa kwenye uongozi (Power),

Sasa sio kila mtusi anaeishi hayo maeneo uliyosema eti ni wanyarwanda. Wengine ni warundi pyu na wengine ndo kama hao uliosema. Lakini point yangu ni kwamba mimi sijazungumzia watusi, bali nimezungumzia wanyarwanda waliokuwa wanaishi Tz bila vibali huku wengi wao wakijifanya ni watanzania.
 
Mimi nashangaa kuna reli ya tazara lakini malori mamia kwa mamia kila siku yanatoka dar to mbeya - to Zambia na kurudi kila siku. Njia ya dar to mbeya ingewekwa vizuri tungefaidika pakubwa. Tatizo viongozi wetu sio wafanyabiashara
Mkuu wewe nafikiri sio mfuatiliaji wa mambo ya kimataifa. Ni kwamba njia ya kuelekea Rwanda, Congo na Burundi ina watu wengi wenye tija kuliko njia ya kuelekea Zambia na Malawi. Ni kwa sababu wewe haujawahi kufuatilia nchi ambazo zimekuwa zikitumia zaidi bandari yetu.

Halaf kingine Zambia ni kama Kenya. Ukiritimba ni mwingi sana. Haiwezi kupitia miezi 6 au mwaka bila kusikia malori yetu yamezuiwa kuingia Zambia nk.

Lakini huu upande mungine wa Rwanda, Burundi na Congo longo longo kama hizo huwa hazipo.

Hata hivyo naamini siku serikali ikiona njia ya huko Zambia inatija basi itajenga barabara nyingi zaidi ya zilizopo sasa. Tatizo wanaangalia tija ya nchi husika.

Unaweza kuwa na watoto wanne lkn ukaona kabisa mmoja ndio ana upendo, heshima na faida zaidi na wewe. Huku wengine wakiishia kuwa mateja wasiokujali wala kukuthamini. Kama mzazi ni lazima utawekeza akili na matumaini zaidi kwa yule anaekujali.
 
Mkuu mbona haueleweki.. Mara useme soko la Congo kubwa kuliko la Rwanda, mara umlaumu raisi kwa vifo vya askari wawili ambao wametumwa kulinda hilo soko kubwa la Congo lisichukuliwe lote.

Sasa hapo point yako ni nini?
Kuwarudisha nyumban askari unaosema wanakufa ili hilo soko kubwa la Congo unalosema hapa tulikose lote?

Au unamaanisha nini?
hapa kuna mawili huwenda mimi sikukuelewa au wewe hukunielewa pia lakini katika yote kila mmoja wetu arudi kusoma ujumbe wa mwenzake kisha tunaweza kuja na jibu zuri.
 
hapa kuna mawili huwenda mimi sikukuelewa au wewe hukunielewa pia lakini katika yote kila mmoja wetu arudi kusoma ujumbe wa mwenzake kisha tunaweza kuja na jibu zuri.
Ni kweli mkuu.
 
Njia nyepesi ya kuwafurusha waasi ni kuwahamisha wakazi kwa muda eneo salama atakekaidi atahesabika ni muasi ahera Ina muhusu.
Ifanyike operation kama IDF ilivyofanya Gaza kuwashughulikia Hamasi kwa kuwahamisha wakazi wa Gaza kabla ya kushusha moto ambao magaidi wa Hamasi wakaomba poo.
Kwann tucheke na wahuni wachache Wanasababisha nchi za maziwa kukosa amani.
Angalia usije ukahamishwa wewd tu
 
Back
Top Bottom