Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Mkuu ili kufungiwa umeme kuna vifaa vinahitajika hivyo kukiwa na upungufu wa hata material ya aina moja huwezi kufungiwa mpaka yakamilike hivyo Tanesco nao wanapenda kupata wateja wapya ili shirika lipate mapato na sio kwamba wanachelewesha makusudi
Chalii, wanayoongea au kuyaandika hapa usidhani wanayatunga. Hizi adha na usumbufu upo tena ni mkubwa sana. Mimi mwenyewe kwangu inahitajika nguzo moja tu lakini ni mwezi wa tatu sasa hamna kitu. Hapo hapo ukiwaambia Tanesco wanakujibu kuwa hawana nguzo na walizokuwa nazo wanawafungia wateja wa mwezi 10/2016. Ina maana hao wa mwezi wa kumi hadi sasa wana miezi zaidi ya saba. Material gani yanakosekana kwa miezi saba kama kweli mnafanya kazi yenu na mnawajibika? Kwahiyo mteja wa mwezi huu atapata umeme mwezi wa kwanza mwakani (2018). Sasa kuna haja gani ya kudanganya watu?
 
Bei inategemea na umbali hivyo ndank ya mita 30 ni 321000 mijini na 177000 vijijini.ikizidi hapo inategemea na umbali uliopo
Acheni UPUUZI nyinyi, watu wanakaa hadi miezi sita kisa nguzo. Kwanini mlichukua pesa zao kama hamkuwa na vifaa? Wezi wakubwa nyie.
 
TANESCO TAZARA wanakera sana. Niliomba kubadilishiwa tariff kutoka tariff 1kwenda tariff 4 wakaniambia watakuja kunitembelea wajue vitu nilivyonavyo. Baada ya kuja kwangu wakanitaka nifike ofisini. Na baada ya kufika ofisini jibu nililopewa na mhasibu ni kuwa tatumia umeme mwingi kwa mwezi hadi kufikia unit 139. Lakini nilipomwambia hata hamsini hazifiki kwa mwezi, akanijibu inanibidi niendelee kutumia hadi mwezi wa sita. Cha kushangaza ambacho sijakipenda wamenibambika nanunua tariff 1 kwa sh 350! Inaumiza sana. Mpaka sasa kwa miezi 3 nimetumia jumla ya units 139.99 mpaka muda huu naandika. Sasa sababu ya kunipandishia bei kutoka bei ya sh 292 hadi 350 wakati mita haidaiwi na wamenikatalia kubadilishiwa tariff ni nini?
 
Ukanda wa Temeke maeneo ya TUANGOMA(TOANGOMA) kuna UMEME na baadhi ya nyumba ambazo kimpaka ziko MKURANGA (mkokozi village) zimepewa umeme kupitia Temeke lakini eneo kubwa la kitongoji cha MKOKOZI ambacho kimepakana na Temeke hakuna Umeme
Swali kwann eneo hili la MKOKOZI lisipewe Huduma toka TEMEKE
 
Mm nimelipia nguzo 3 mwezi was September leo mwezi wa June miezi 10 karibia milioni 2 nilizolipa kwa miezi 10 ningezifanyia Biashara zingenisaidia
 
Shukran
 
Kama nyumba ipo mbali na nguzo za Umeme, mtu anaambiwa alipie gharama kubwa ili kuongeza nguzo ipi aweze kupata Umeme, ila nguzo bado zinabaki Mali yenu, na mtu mwingine akija kuunganisha katika nguzo niliyolipia Mimi wala sirudishiwi hata nusu ya gharama, je hii ni Sawa,
 
Kwanza niwapongeze kwa kuja humu, nadhani ninsehemu sahihi sana ya kujipima na kujifanyia self evaluation.
Kimsingi Tanesco Mnasumbua sana mwezi sasa nipo gizani hamjafika kufanya savei. Najiandaaa kununua solar tu niachane na nyie.
 


Hii si sawa aisee
 

Hivi karibuni kutakuwa na Maombi ya kufuata ILI KUONDOLEWA LINE YA UMEME YA TANESCO!

[HASHTAG]#WatchThisSpace[/HASHTAG]
 
Sasa mimi UMEME nataka sasa wayaringi imefanywa Na MTU ambaye asiye sajiliwa itakuwaje? Naomba msaada wenu.
 
Nina malalamiko yangu kuhusu shirika langu ili la tanesco, iweje nipewe gharama za kuhunganishiwa umeme then naenda kuripa after kulipa naambiwa nisubiri kupigiwa simu ya kuunganishiwa umeme then nakaa baada ya masiku kenda natumiwa sms kuwa niendelee kuwa mvumilivu naendelea kuwa mvumilivu baada ya siku kwnda tena natumiwa sms kuwa niendelee kuwa mvumilivu maana kuna uwaba wa vifaa, hapo ndo nimestaajabu uwaba wa vifaa wakati mimk nimeshalipa pesa yenu mkanunulie ivyo vifaa, daaah naendelea kuishi giza tu mnakera sana kwakweli,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna tatizo la nyaya za umeme,eneo la Mbagala Nzasa kwa Mwarabu.
Karibu na bar iitwayo KAHOMBA au karibu na Nursery School iitwayo MONTESSORI nyaya hizi ziko chinichini saana kiasi cha kuhatarisha usalama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…