Zile pesa za mechi ya Simba na Yanga iliyoahirishwa ndiyo zimeliwa?

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,282
Reaction score
117,244
Wadau Ile mechi ambayo iliepekwa saa moja usiku halafu Yanga wakagoma wakaondoka.

Taarifa yake ya fedha ikoje!?Zile hela zilienda wapi?Au ndo zimeliwa?

Kuna anaekumbuka labda maelezo yeyote?

Nazungumzia mechi ya Simba na Yanga ilioshindikana kuchezwa huku watu walishaingia uwanjani
 
Zimeliwa zile za LUKU kipindi kile tumeshindwa kununua umeme baada ya bwana yule kuchomoa betri itakua hizo za uwanjani, watanzania wamezoea kupigwa sio kitu kigeni hiki
 
Hazijaliwa Simba alikuwa mwenyeji sema Sasa hivi wameanzisha Tania ya kutotangaza mapato ili waive vizuri
 
Kama ulikata tiketi na udhibitisho unao, basi una haki ya kuzipeleka mamlaka mahakamani.
Hata suala luku pia unaweza kulipeleka mahakamani.
 

Ile mechi ilichezwa siku za mbele na yanga ikashinda 1 -0 . Watu waliingia walitumia tiket zile zile za hela ile ile kuingilia uwanjani..
 
Bongo nyoso, watu washafunga hesabu mgao umeisha.
 
Watu washasoma na hitma shughuli imeisha kitambo sana.
 
Tuulizie na hizi za juzi yanga vs simba ngapi zimepatikana hazijatangazwa kama kawa
 
Tulirudishiwa hela zetu kwenye kadi tukaingia tena
 
Wenye message ya muamala walitumia kuingia mechi iliyofuata pia waliotumia card walirudishiwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…