Zilianza Pointi 8,Zikaja Pointi 5 Naona kwa mbali zikibaki pointi 2

bryan2

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
3,323
Reaction score
4,679
Leo imechezwa michezo kadhaa ya Ligi kuu ya Vodacom Tanzania ila macho na masikio ya wengi yalikua kule Mbeya kwenye uwanja wa Sokoine mtanange Kati ya Wenyeji Tanzania Prison na Wageni wao Timu ya Simba

Mpaka mwamuzi wa kandanda lile anapuliza kipenga cha mwisho matokeo ni Tanzania Prison 2 na Simba 1 na hivyo Simba kuacha pointi zote 3 pale Mbeya

Pambano hilo limenogesha utamu wa ligi kuu hasa kwa timu mbili Hasimu/Watani wa jadi timu ya Yanga na Simba

Kwani Mpaka sasa Simba anaongoza ligi akiwa na pointi 35 akiwa amecheza michezo 15 na mtani wake Yanga akiwa wa pili na pointi zake 30 ila akiwa kacheza jumla ya michezo 14 hivyo akiwa na faida ya mchezo mmoja mkononi

Endapo timu ya Yanga itashinda mchezo wake wa kiporo itakua na jumla ya pointi 33 na kuwa na pengo la pointi 2.

Je Yanga atafanikiwa kushinda mchezo wake wa mwisho kabla ya mapumziko ya ligi kuanza na kupunguza pengo la pointi dhidi ya mpinzani wake?

Tusubiri.
 
Simba na Yanga siyo timu za kuamini sana mara nyingi zinachezea kwenye mwanasport na champion
 
Mikoani kugumu sana kwa hawa jamaa wa simba na bado ndo kwanza kumekucha
 
Litimu la hovyo hovyo,halafu linajipangia eti ooooh "tutamaliza round ya kwanza bila kufungwa" Na bado ligi ipo nusu.
 
walipangiwa mechi 6 mfululizo nyumbani sasa hizo 6 watacheza ugenini raundi ya pili Simba kazi wanayo maana TFF. sijui wanatumia kanuni gani ya ovyo kupanga hivyo..
 
walipangiwa mechi 6 mfululizo nyumbani sasa hizo 6 watacheza ugenini raundi ya pili Simba kazi wanayo maana TFF. sijui wanatumia kanuni gani ya ovyo kupanga hivyo..
Sisi kipindi hicho tunachapa kuku kwa mrija tuu pale uhuru
 
Litimu la hovyo hovyo,halafu linajipangia eti ooooh "tutamaliza round ya kwanza bila kufungwa" Na bado ligi ipo nusu.
Sijui tuwaombe Tff angalau waongeze game moja moja kwa kila timu kabla ya kufungwa kwa round ya kwanza??

Ikitokea jamaa wanaweza kukata rufaa UN
 
Kwa hiyo yanga imepanda kiwango eeeeh!!
Aisee unauliza tena kama mechi ya Arsenal na Man utd itakua live Supersport!!

Kiwango cha Yanga kipo juu siku zote manake ndo bingwa mtetezi
 
Mabingwa wa round ya kwanza[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…