Zilipendwa ananiomba ushauri, nimsaidieje?

:twitch:Mwambie wewe upo tayari kuhamia kwake na kuwa mume ***** kwake! Hivyo aachane na huyo anayetaka ahamie Mbagala na akukaribishe wewe Mwenge ili mwendeshe maisha yenu pamoja! Ila ukubali kuwa house-boy wake tu!!!!!!!!!!!!!!!!!:sick:


Utajuaje kama ndicho kilinikimbiza toka kwake??
mazee kumbuka huyo ni mke wa mtu, hata kama wancomflict na kwa sasa wametengana lakini ndoa yao haijasambaratika.
Hakuna namna yeyote mimi na yeye tunaweza kuendesha maisha pamoja.
I have my own life and i'm enjoying:coffee:
 
mme wa huyu dada ana matatizo
kwani akikaa kwenye hiyo nyumba na akaendelea kulipa kodi ya nyumba yeye ni tatizo???
Na gari kwa nini iuzwe ???
Mambo mengine bwana ni hekima kidogo inahitajika

jamani,,huwezi jua huyo jamaa yanampata yapi kwa huyo mama kwani story yenyewe ni ya upande mmoja.

 
we mwambie huyo zilipendwa wako aachana na huyo jamaa na wewe jibebe huyo demu inaonekana bado anakutaka.kula mzigo
 
Wadau naomba mnisaidie kuchanga mawazo.

Zilipendwa wangu tuliyeachana miaka mitano iliyopita amenipigia simu anaomba ushauri.

Pole sana mtani, huyu wa-longi wako mshauri aende kwa mchungaji kanisani kwao vinginevyo atakutia majaribuni bure!
 
Wakati mwingine sio lazima uwe na jibu la kumpa ndugu yangu, maana kuna ka mtego hapo! I hope you are a man enough to know what am saying!

hapa kama kweli vile.
Nahisi mwanamke anaficha sababu.
 
Kwanza nampa pole huyo dada kwa hayo yote,
Pili inaonekana we ni mtu mhimu sana kwake ndo maana hakumuuliza jirani, shost wala mshauri nasaha wa mambo ya ndoa "japo sina uhakika km hakufanya hvyo"
Kaanae chini, mwambie maisha hayaishii hapo, kwamba there z a life hata bila ya huyo jamaa! Si mtu wa type yake, he has no support 2 her as father of family, zaidi ninachokiona mimi huyo jamaa hajiamini, closed thinkng, possessing past eras mentality ya kwamba mwanaume ndo anafanya kila kitu...otherwz utupe sbb aither kagundua kuna mtu alisuport "weak reason"
Dada ana kazi, kanunua gari, kaaford kodi ya nyumba mwenge, so anaweza kuendesha maisha yake na mtoto wake mwambie asongeshe maisha yake wala asiende mbagali.
 

Ukishaachana na mwanamke yoyote dunia hii ya leo mkalie mbali tena move on with your life. Otherwise utakuja kugeuzwa emotional punching bag na utashindwa ku-move on. I've been there. Hiyo mambo ya eti sijui naomba ushauri sijui nilikuwa nakusalimia tu yoote hiyo ni gear ya kukuingia. Move on with your life and you'll always be at peace!!.:coffee:
 
Ushauri ni mwingi wa kutosha umepewa; Mimi naona hapo wamekutana fahari wawili na hawawezi kaa zizi moja, ili uhusiano udumu lazima mmoja ajaribu kujishusha na hapo upande wa pili kama una hekima utaongeza upendo zaidi, lakini kutunishiana misuri ni hatari.

Inaonekana huyo mwnaume alipohamia kwa mwanamke mambo yalikuwa shwali lakini baadaye mwanamke alikunjua makucha na kumbeza mwanaume.

Mwaka mzima umepita sipati picha nani hasa alipuuza hadi muda huo bila kutatua tatizo ndio wanashituka saa hizi, au wameshasuluhisha sehemu mbalimbali bado imeshindikana.

Lakini jamani Mbagala si bado ni DSM kwa nini asihamie tu! Kuna watu ndoa zao ni mikoa tofauti itakuwa hii ya mbagala.

Nilishawahi shiriki mgogoro fulani mwanamke alikuwa na kiwanja cha urithi Mbezi Beach lakini mwanaume alikataa kushiriki kwa namana yoyote kutoa hela yake kuendeleza kiwanja husika, ikabidi mwanamke akubali wakiuze na sasa wana nyumba nzuri Kigamboni maisha ya ndoa ya amani yanaendelea.
 

umenena vyema kaka, hekima hii ni kubwa sana. ubarikiwe na Bwana
 
Mbona kila mtu karukia huyo bwana?????, Mwita atuambia hii stori ya upande wa Ex. Wake, ambae ni Mke, Bado hatujapata Stori ya upande wa huyo Bwana. Mbona kizazi cha leo mnarukia mambo haraka haraka, hizi pupa zenu ndio mwakosa mazuri.

Mimi nionavyo kwa mtazamo wangu, huyu bwana hana raha na vitu vya mkewe, mke ana mnyanyapaa mume kwa sababu vitu ni vyake.. Haya mambo yako jamani, kwanza dada zetu twajua upungufu wenu, pengine akuta umechua gari lake umebeba rafiki zako hata wa kiume, akusimamisha....maneno mbele ya marafiki. Haya mara umerudi kuchelewa, ulikuwa na gari, umeonekana maeneo mengine, maneno.

Huyu Bwana mi naona ameshiba na hizo kero za mkewe, ataka wawe na gari LAO, nyumba YAO!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…