Zilipendwa ananiomba ushauri, nimsaidieje?

Zilipendwa ananiomba ushauri, nimsaidieje?

Mtalaka hatongozwi mzee. Huyo ndo vile kakukumbuka. Ushauri kitu gani bwana.....mi sio tatizo hapo.

Acha fitna mazee,
hatukuwahi kuoana kwahiyo hatukuwahi kupeana talaka,
sasa anakuwaje tena mtalaka?
 
Shemeji,

Habari yako kwanza maana unapotea sana wewe!!

Huyo Mdada unahakika na kile anachokwambia?? Kwanini nasema hivyo inawezekana wamekosana na Mumewe kwa sababu nyingine na kapigwa chini sasa anakutafuta mrudiane kijanja na wasiwasi huo kabisa mimi.

Pili iweje huyo mwanaume ahame leo wakati wamekaa wote kwa muda hakujua kama hapo ni nyumba aliyolipia mkewe?? Ukipata hayo majibu ya maswali utaelewa.

Kuna mtego na hizo sababu za jamaa kuondoka si za kweli. Na kama ni kweli huyo mwanaume anamapungufu sana.

Nitarudi baadae
 
ni vizur aheshimu maamuzi ya mme wake iwapo hayawezi kuathiri maendeleo yao
 
Shemeji,

Habari yako kwanza maana unapotea sana wewe!!

Huyo Mdada unahakika na kile anachokwambia?? Kwanini nasema hivyo inawezekana wamekosana na Mumewe kwa sababu nyingine na kapigwa chini sasa anakutafuta mrudiane kijanja na wasiwasi huo kabisa mimi.

Pili iweje huyo mwanaume ahame leo wakati wamekaa wote kwa muda hakujua kama hapo ni nyumba aliyolipia mkewe?? Ukipata hayo majibu ya maswali utaelewa.

Kuna mtego na hizo sababu za jamaa kuondoka si za kweli. Na kama ni kweli huyo mwanaume anamapungufu sana.

Nitarudi baadae

shemeji mie sijambo, sijapotea sana isipokuwa mara nyingi ninakuwa "hard newz room"

hata mimi aliponipigia simu kwanza nilishangaa kwakuwa ilikuwa ni almost miaka miwili tangu tulipopotezana kimawasiliano.

lakini pia nilijaribu kumdadisi sana ili kujua ukweli halisi wa ugomvi wao. Ninaweza kukuhakikishia kwamba kuna ukweli kiasi fulani ingawa imeniwia vigumu kuthibitisha madai yake kwani hata mumewe simjui.

Alichonisisitizia ni kuwa yule bwana kabla hawajaoana alikuwa na chumba kimara lakini kadri mapenzi yalivyonoga akaamua kuhamia kwake hadi wakafunga ndoa, sasa sijui jamaa amekutwa na maswaibu gani hadi kutaka bibie auze gari na kupanga nyumba atakayolipia yeye.

Nakusubiri shem, najua hapo kwako busara na kapiriensi zimejitosheleza.
 
Maty,
Haya maneno ya signature yako yanaweza kuwa na ujumbe mzito kwa huyu shostito, au we unasemaje?

"If you love something, set it free. If it comes back, it was, and always will be yours. If it never returns, it was never yours to begin with"

umeona eeee mprintie hii maneno my dia hii mistari michache inamtosha sana
 
Inawezekana kuna zaidi ya unachoambiwa.

Umetuletea upande mmoja wa story na kwa haraka tunaweza kumlaum huyo mume.
What if amekuwa akimsimanga especially during heated moments kwa maneno kama "mwanaume gani wewe...."; "huoni wanaume wenzio..."; "wewe nawe ni mwanaume.....? n.k

Kwa kawaida binadamu hatupendi kulinganishwa na "washindani wetu" maana huamsha kujihami. Ni dhambi kwa mfano kumlinganisha mwenzi wako na walioko nje. Kama kuna jambo unataka ajirekebishe mwambie nini wewe unapenda akifanye.

Miaka fulani ya nyuma nilipoteza kazi, nikawa sina kipato for three good years yet my woman preserved me kwa kila kitu.
At this point hatukuwa tumeoana BUT she went ahead marrying an unemployed person. After 1yr ya ndoa I got employed, now can supply mahitaji yake na familia na change inabaki. Hakunipanda kichwani hata siku moja!

Sioni kama wewe utakuwa mshauri wake mzuri hasa ukichukulia wewe ni Ex- wake.
Simply mwambie aongee na wasimamizi wa ndoa yao
 
Nakupa ushauri,uufanyie kazi alafu ulete Feed Back hapapa siyo unapotea.

Katika ndoa kuna majuku ya mwanaume na majukua ya mwanamke.it took soo many years of cultural try and errors to have these roles for a man and woman.
Majukumu ya Mume ktk ndoa.
Usalama wa Familia- e.g Ukisikia wezi nje utamtuma Mkeo aende kuangalia kuna nini?sometime unajua kuwa hapa lazima upokee kichapo lakini haina jinsi inabidi ukikubali kwa kuwa in jukumu lako kama Baba.eg.2 Gari limeharibika fundi kaja unamtuma mkeo au unaenda mwenyewe.Taa mbovu,bomba limepasuka etc mifano iko mingi tu hata ulaya its the same way.
Kufikiri kwa niaba ya familia ,msaidizi wa fikra ni mke,ila final Decision ni ya Mume.
Hapa haina ujanja ukifanya maamuzi mabovu kama baba basi familia ukoo wote utakulaumu,hata siku moja uwezi kusema eti lillikuwa wazo la mama.ktk bible kuna mstari kuwa Mwanaume ni kichwa cha familia ....

Kuprovide Lishe ya Familia,mke anaweza kuchangia ila siyo Awe the Main bread Winner na baba upo tuu utekelizi majukumu hayo.
Kuprovide chakula ni jambo la msingi sana,hata kama hauna employment just go out,beba zege,fagia barabara,just do anything usikae ndani usubiri Wife alete.hapo ndio respect inakuja,muulize mwanamke yeyote ambaye amepitia kuwa main breadwinner.

Mshauri rafiki yako Arudi kwa Mumewe Mbagala ,Gari auze wanunue anayotaka ,kama huyo rafiki yako anajali Family atamfuata mumewe ila kama hapendi family mwambie AMuache awe Single mother then mzee utakua na extra Spare tyre.


Majukumu ya Mke ni mengi sana kuliko hayo,na ni ya muhimu sana ili iwe familia kwani bila mke nyumba haiwi nyumba.Mume ana majukumu machache ya msingi .Punde MUME akiyatelekeza majukumu yake ,hapo ndipo kuwa mume kunaisha na inferiority complex zinapoanza.
Wadau naomba mnisaidie kuchanga mawazo.

Zilipendwa wangu tuliyeachana miaka mitano iliyopita amenipigia simu anaomba ushauri.

Anasema mume wake amemtelekeza yeye na mtoto wake tangu alipokuwa na ujauzito wa miezi minne.Huyu shostito anafanya kazi kampuni moja ya simu na mumewe anafanya kazi serikalini.

Kisa cha mume kumkimbia ni kuwa mwanamke amekaidi kutekeleza matakwa yake. Mume anataka mkewe auze gari aliyonunua kabla hawajaoana na wahame toka kwenye nyumba wanayoishi mwenge iliyolipiwa na mke.Mume alihamia nyumbani kwa mkewe kabla hawajaoana, na mwanamke alinunua gari kabla hawajaoana, na jamaa hakuchangia hata senti moja.

Mwanamke kakataa kuuza gari ila amekubali kuhama nyumba kwa masharti kwamba iwe ni maeneo ya mwenge, sinza, kinondoni, ubungo ama mabibo. Mumewe anataka wahamie mbagala, kwamba ndipo anaweza kumudu kulipa kodi ya nyumba, hataki mkewe aongeze hata senti.Mume kuona mwanamke hatekelezi matakwa yake akaona isiwe tabu, kafunga virago amehamia mbagala.

Wadau mnisaidie, nimshaurije huyu shostito?
 
umeona eeee mprintie hii maneno my dia hii mistari michache inamtosha sana

Nashukuru bibie,
Naendelea kuratibu ushauri wenu, najua nitatoka na mawazo mazuri sana hapa, yanaweza kumfaa, ingawa bado sijafahamu kutoka upande wa ili.
 
hatuwezi kujua kila kitu kinachoendelea hapo. hayao aliyokueleza huyo zilipendwa wako ni ya upande mmoja. inawezekana naye anamfanya ajisikie inferiority kwa kuwa yeye kipato chake ni kidogo na kamkuta mke ana hatua kubwa ya kimaisha. kuna mawili hapo, aither ni inferioritu complex ambayo ni purely psychological issue au ni mke ana ubinafsi na mali zake alizochuma akiwa peke yake hadi mume anakosa amani.

kama lolote kati ya hayo limeishaleta tabu, ni vizuri mwanaume akapewa counseling badala ya kumpuuza ili naye sauti yake na nafasi yake kama mwanaume uhuishwe ndani ya ndoa yake. ushauri nasaha ukiwa unaendelea mwanamke ajitahidi kufuata anachopenda mwanaume huku akimshirikisha kila hatua na ikibidi ampe suti kubwa zaidi kwani mwenziye tayari kishaathirika kisaikolojia, kisha waanze maisha upya kwa pamoja, nyumba, magari ni vitu vya kupita tu na huyo mwanaume anayemdharau huwezijua Mungu kamuhifadhia nini stooni mwake, aweza kuwa siku moja juu kumzidi yeye na ndipo atakapoona haya hata kumdondoshea chozi la huba.

all in all, Mungu ametuita katika amani. ndoa isiyo na amani isyo ndoa na Mungu hapendezewi nayo. kuishi mbagala kwa amani ni bora mara milioni kuliko kuisho oysterbay au masaki bila amani? sembuse mwenge?
 
Inawezekana kuna zaidi ya unachoambiwa.

Umetuletea upande mmoja wa story na kwa haraka tunaweza kumlaum huyo mume.
What if amekuwa akimsimanga especially during heated moments kwa maneno kama "mwanaume gani wewe...."; "huoni wanaume wenzio..."; "wewe nawe ni mwanaume.....? n.k

Kwa kawaida binadamu hatupendi kulinganishwa na "washindani wetu" maana huamsha kujihami. Ni dhambi kwa mfano kumlinganisha mwenzi wako na walioko nje. Kama kuna jambo unataka ajirekebishe mwambie nini wewe unapenda akifanye.

Miaka fulani ya nyuma nilipoteza kazi, nikawa sina kipato for three good years yet my woman preserved me kwa kila kitu.
At this point hatukuwa tumeoana BUT she went ahead marrying an unemployed person. After 1yr ya ndoa I got employed, now can supply mahitaji yake na familia na change inabaki. Hakunipanda kichwani hata siku moja!

Sioni kama wewe utakuwa mshauri wake mzuri hasa ukichukulia wewe ni Ex- wake.
Simply mwambie aongee na wasimamizi wa ndoa yao


Kwa kuzingatia hilo ndo maana nikaja kutafuta ushauri wenu hapa.
Manake nilijaribu kujiuliza kulikoni aniombe ushauri mimi huku akijua kwamba alitoka kwangu ndo akaenda kuolewa na huyo bwana?
Anyway, ngoja niendelee kuratibu maoni ya wadau ili mwisho wa siku niwe na uamuzi sahihi.
 
hatuwezi kujua kila kitu kinachoendelea hapo. hayao aliyokueleza huyo zilipendwa wako ni ya upande mmoja. inawezekana naye anamfanya ajisikie inferiority kwa kuwa yeye kipato chake ni kidogo na kamkuta mke ana hatua kubwa ya kimaisha. kuna mawili hapo, aither ni inferioritu complex ambayo ni purely psychological issue au ni mke ana ubinafsi na mali zake alizochuma akiwa peke yake hadi mume anakosa amani.

kama lolote kati ya hayo limeishaleta tabu, ni vizuri mwanaume akapewa counseling badala ya kumpuuza ili naye sauti yake na nafasi yake kama mwanaume uhuishwe ndani ya ndoa yake. ushauri nasaha ukiwa unaendelea mwanamke ajitahidi kufuata anachopenda mwanaume huku akimshirikisha kila hatua na ikibidi ampe suti kubwa zaidi kwani mwenziye tayari kishaathirika kisaikolojia, kisha waanze maisha upya kwa pamoja, nyumba, magari ni vitu vya kupita tu na huyo mwanaume anayemdharau huwezijua Mungu kamuhifadhia nini stooni mwake, aweza kuwa siku moja juu kumzidi yeye na ndipo atakapoona haya hata kumdondoshea chozi la huba.

all in all, Mungu ametuita katika amani. ndoa isiyo na amani isyo ndoa na Mungu hapendezewi nayo. kuishi mbagala kwa amani ni bora mara milioni kuliko kuisho oysterbay au masaki bila amani? sembuse mwenge?

Ahsante MJ,
mawazo yako ni mazuri sana, kweli habari niliyonayo ni ya upande mmoja.
Sasa kumpata ama kuongea na mumewe ndo pagumu.Kwanza kabisa sifahamiani nae, na hata kama nikisema nitafute kufahamiana nae si rahisi kiasi hicho kuanza kumzungumzia mambo ya ndoa yake.
Lakini pia si vibaya kuanzia hapo kwa habari ya upande mmoja, kutokana na mawazo yenu, kama yeye ndo mwenye matatizo na kama atajitambua basi huenda ataona ni wapi pa kujirekebisha ili kuinusuru ndoa yake.
 
Nakupa ushauri,uufanyie kazi alafu ulete Feed Back hapapa siyo unapotea.

Katika ndoa kuna majuku ya mwanaume na majukua ya mwanamke.it took soo many years of cultural try and errors to have these roles for a man and woman.
Majukumu ya Mume ktk ndoa.
Usalama wa Familia- e.g Ukisikia wezi nje utamtuma Mkeo aende kuangalia kuna nini?sometime unajua kuwa hapa lazima upokee kichapo lakini haina jinsi inabidi ukikubali kwa kuwa in jukumu lako kama Baba.eg.2 Gari limeharibika fundi kaja unamtuma mkeo au unaenda mwenyewe.Taa mbovu,bomba limepasuka etc mifano iko mingi tu hata ulaya its the same way.
Kufikiri kwa niaba ya familia ,msaidizi wa fikra ni mke,ila final Decision ni ya Mume.
Hapa haina ujanja ukifanya maamuzi mabovu kama baba basi familia ukoo wote utakulaumu,hata siku moja uwezi kusema eti lillikuwa wazo la mama.ktk bible kuna mstari kuwa Mwanaume ni kichwa cha familia ....

Kuprovide Lishe ya Familia,mke anaweza kuchangia ila siyo Awe the Main bread Winner na baba upo tuu utekelizi majukumu hayo.
Kuprovide chakula ni jambo la msingi sana,hata kama hauna employment just go out,beba zege,fagia barabara,just do anything usikae ndani usubiri Wife alete.hapo ndio respect inakuja,muulize mwanamke yeyote ambaye amepitia kuwa main breadwinner.

Mshauri rafiki yako Arudi kwa Mumewe Mbagala ,Gari auze wanunue anayotaka ,kama huyo rafiki yako anajali Family atamfuata mumewe ila kama hapendi family mwambie AMuache awe Single mother then mzee utakua na extra Spare tyre.


Majukumu ya Mke ni mengi sana kuliko hayo,na ni ya muhimu sana ili iwe familia kwani bila mke nyumba haiwi nyumba.Mume ana majukumu machache ya msingi .Punde MUME akiyatelekeza majukumu yake ,hapo ndipo kuwa mume kunaisha na inferiority complex zinapoanza.

Daaa majukumu ya MWANAUME na MWANAMKE ni kweli..
Lakini najaribu kufikiria hivi, si kila mwanaume anaweza kutimiza kila
jukumu, wakati mwingine Mungu anaweza akampa hata mwanamke akili
ya kufanya jambo ambalo lingedhaniwa limefanywa na mwanaume.

Halafu huyu jamaa sijui namchukulia je, kama vile ana wivu pia,
Yani kwa sababu gari hajalinunua yeye auze, kwa sababu nyumba hajapanga yy
wahame. Halafu wahamie Mbagala kutoka Mwenge,
Daaaaaaaaaaaa, mi kwa huyo wala nisingemsikiliza mara mbili.

Wanaume mi nawapenda na ninawaheshimu, lakini mwanaume mjinga,
na ambaye hajijui kama ni mjinga, asiyetumia akili, apite tu pembeni
hata kama nilikusoea tukawa na watoto wanne, bado hubadiliki.
Nenda tu baba.
 
Matatizo ya ndoa huwa yanatatuliwa na wanandoa wenyewe,
mara nyingi huwa sipendi kutoa ushauri hasa kwenye maswala ya ndoa,
maana ni rahisi sana pale watu wanapokuja kuweka mambo yao sawa ukaonekana kama vile ulikua unataka kuvuruga, kwa hiyo ndugu yangu kama unaweza usijihusishe sana na hayo mambo ya hiyo familia,
nadhani kuna watu wengi tu wa karibu na familia hiyo wanaweza kusuluhisha hilo lililojitokeza, hivi ina maana gari tu na nyumba vinaweza kumwondoa mume nyumbani na kwenda kupanga sehemu nyingine? inawezekana tatizo ni kubwa na pia inawezekana hujaelezwa ukweli kuhusu hilo tatizo.
 
hatuwezi kujua kila kitu kinachoendelea hapo. hayao aliyokueleza huyo zilipendwa wako ni ya upande mmoja. inawezekana naye anamfanya ajisikie inferiority kwa kuwa yeye kipato chake ni kidogo na kamkuta mke ana hatua kubwa ya kimaisha. kuna mawili hapo, aither ni inferioritu complex ambayo ni purely psychological issue au ni mke ana ubinafsi na mali zake alizochuma akiwa peke yake hadi mume anakosa amani.

kama lolote kati ya hayo limeishaleta tabu, ni vizuri mwanaume akapewa counseling badala ya kumpuuza ili naye sauti yake na nafasi yake kama mwanaume uhuishwe ndani ya ndoa yake. ushauri nasaha ukiwa unaendelea mwanamke ajitahidi kufuata anachopenda mwanaume huku akimshirikisha kila hatua na ikibidi ampe suti kubwa zaidi kwani mwenziye tayari kishaathirika kisaikolojia, kisha waanze maisha upya kwa pamoja, nyumba, magari ni vitu vya kupita tu na huyo mwanaume anayemdharau huwezijua Mungu kamuhifadhia nini stooni mwake, aweza kuwa siku moja juu kumzidi yeye na ndipo atakapoona haya hata kumdondoshea chozi la huba.

all in all, Mungu ametuita katika amani. ndoa isiyo na amani isyo ndoa na Mungu hapendezewi nayo. kuishi mbagala kwa amani ni bora mara milioni kuliko kuisho oysterbay au masaki bila amani? sembuse mwenge?

Miss Judy nakubaliana na wewe asilimia mia moja,
Lakini kuna kitu najiuliza, hebu tufikirie mwanaume mwenye akili, na utashi,
Mwanaume mwenye kuyajua maisha, na mwenye uwezo wa kuamua kama mwanaume,
Mwanaume ambaye ni msaada kwa mwanamke, kuna mambo huyajui yeye anakufundisha,
na kukuongoza.

Aliweza je kukubali kwa moyo wake wote kuhamia nyumbani kwa huyo mdada,
Ok, labda kuna vitu, vya tofauti ameviona, ilibidi atumie akili ya kiume hapo, sio ya kusema uza,
gari hamia Mbagala, tuangalie na maisha yalivyo, unahama Mwenge unafanya kazi Airtel,
unahamia Mbagala tena kwenye nyumba ya kupanga ni akili hiyo.

Basi angekomaa, akajenga au hata kama ni kupanga kwa ustaarabu na akili,
Na habari ya kuuza vitu ambavyo mmeshapewa na Mungu bila sababu sio akili.
Akili ya mwanaume naiamini ndo maana anaweza hata akukudanganya mpaka uje,
ugundue unadanganywa ushachoka, labda kwa sababu ya neema ya Mungu tunawagundua.

Sasa atumie akili hizo hizo kuhakikisha anakwenda sawa na huyu dada.
Na maendeleo yanakuwepo.
Mambo yakuanza sifuri hakuna.
Akomae na maisha amzidi basi, kama tatizo ni hilo.
 
Zilipendwa wangu tuliyeachana miaka mitano iliyopita amenipigia simu anaomba ushauri.

HAPO KUWA MKWELI - JAMANI MMEACHANA FIVE YEARS - BADO UNA MAWASILIANO NAYE??? ANAJUA ULIPO - ANAJUA UNAKOFANYA KAZI/BIASHARA ETC. HADI SIMU .................MMMMMMM ..... mwambie akishaolewa asahau ZILIPENDWA... au anataka "baby come back" - yaani kama hamkuweza kuishi pamoja - mbona bado anakuona wa MAANA HADI ANATAKA USHAURI KWAKO????

HATA HIVYO MWAMBIE - MAPENZI SIO MATERIAL THINGS - AKAE NA MUMEWE "WASHAURIANE" - WAMWOMBE MUNGU - JIBU LITAJITOKEZA.................... KWANI MUNGU ANAFANYA NJIA PASIPO KUWA NA NJIA
h
 
Zilipendwa wangu tuliyeachana miaka mitano iliyopita amenipigia simu anaomba ushauri.
HATA HIVYO MWAMBIE - MAPENZI SIO MATERIAL THINGS - AKAE NA MUMEWE "WASHAURIANE" - WAMWOMBE MUNGU - JIBU LITAJITOKEZA.................... KWANI MUNGU ANAFANYA NJIA PASIPO KUWA NA NJIA
h

Preacher, big up.
 
MWambie ukipenda embe penda na mzizi wake.

MWambie ajipe moyo abaki kwenye nyumba yake huyo jamaa ni mzushi na mbabaishaji.

Nia na madhumuni ya huyu mwehu ni kumtawala mke wake mengine ni visingizio visivyo na maana.
 
Zilipendwa wangu tuliyeachana miaka mitano iliyopita amenipigia simu anaomba ushauri.

HAPO KUWA MKWELI - JAMANI MMEACHANA FIVE YEARS - BADO UNA MAWASILIANO NAYE??? ANAJUA ULIPO - ANAJUA UNAKOFANYA KAZI/BIASHARA ETC. HADI SIMU .................MMMMMMM ..... mwambie akishaolewa asahau ZILIPENDWA... au anataka "baby come back" - yaani kama hamkuweza kuishi pamoja - mbona bado anakuona wa MAANA HADI ANATAKA USHAURI KWAKO????

HATA HIVYO MWAMBIE - MAPENZI SIO MATERIAL THINGS - AKAE NA MUMEWE "WASHAURIANE" - WAMWOMBE MUNGU - JIBU LITAJITOKEZA.................... KWANI MUNGU ANAFANYA NJIA PASIPO KUWA NA NJIA
h

Nimekusoma kiongozi,
Katika dunia hii, ama ndani ya nchi hii ya kambarage kama mtu anakutafuta hawezi kushindwa kukupata.
Hivi unadhani mtu mliyekutana naye katika mazingira ya chuo atapata shida kukupata?
We unajua chuoni unakutana na maelfu ya watu, sasa ukitoka dsm hata ukienda kujichimbia serengeti utapatikana tu kiongozi.
btw, nimekusoma vizuri sana.
 
Mwambie Never depend on anyone for your life.., mwambie aendelee kujijenga yeye na kulea watoto wake.., Huyo mwenza wake alikuwa mzigo na hafai. Akumbuke kwamba yeye sasa ndio baba na mama..., She needs to be Strong.. Mpe hii Verse ya Mariah Carey Hero

And then a hero comes along With the strength to carry on
And you cast your fears aside And you know you can survive
So when you feel like hope is gone Look inside you and be strong
And you'll finally see the truth That a hero lies in you
 
:twitch:Mwambie wewe upo tayari kuhamia kwake na kuwa mume ***** kwake! Hivyo aachane na huyo anayetaka ahamie Mbagala na akukaribishe wewe Mwenge ili mwendeshe maisha yenu pamoja! Ila ukubali kuwa house-boy wake tu!!!!!!!!!!!!!!!!!:sick:
 
Back
Top Bottom