ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

wakuu naomba mnisaidie nyimbo za
1. binadamu hawana shukrani -ndanda kosovo na fm academia. unakibwagizo sasa wanaanza kulia eeeh nuhu..eeeh nuhu tufungulie safina. naomba mniwekee hapa wadau
2. nadhan ni mao santiago kama sikosei anasema "marafiki wote wamenikimbia sasa upendo tulipatana umefika wapi.... kibwagizo cha kula kwake vichochoroni,kulala kwake vichochoroni.

naombeni mnisaidie huu wimbo wadau.
 
Ni bendi ya Legho stars na Tshimanga Kalala Asosa. Kausuki.
 
ni pm namba yako nikutumie kwa whatsaap kuweka siwezi hapa hii UPDATE ya sasa JF inayeyusha
 
Mkuu bado hujapata hii ngoma
 
makumbele hadi kesho haichuji bro
 
SUPER RAINBAL, hakika kazi zao zilisimama ju ya mstari. Huu wimbo aliurudia Binti Ajulikanae kama Rubby mwana dada machachari kweli kweli.
 
weeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee Wacha Nkuguse na Kitu cha MONICA alichinipigia Mawestro King Kiii...

Mama nipe nauli nkamfuate Monica, amekimbia zambia na Treni ya Mizigo,
Kisa cha kukimbia madeni yamemzidi, doti Kumi za Khanga alizokopa hajalipa,
Anatafutwa na Polisi popote apatikane, na mimi rafiki yake niko njee kwa dhamana,
Nililala Rumande siku mbili kituon, usumbufu nlio upata kwa kwel sina raha.

Naona bora niende zambia, nikamtafute monica..............................
........................
...........................
 
NYIMBO ZOTE ZA WAZEEE WAQ KAZI, TABORA JAZZY. ACHA KABISA
SEGERE MATATA SEGUA SEGUA, IKO VILE.
1.0 CHAKULA KWA JIRANI,
2. 0 MOLA TUJALIE, 3.0 KILIMO,
NYIMBO ZA MOROGORO JAZZY: NILIPOTEZA UFUNGUO WA SANDUKU LANGU PALE CHUO CHA USHIRIKA MOSHI ( ENZI HIZO) WAKATI NALISAKA RHUMBA LAKE , NA YEYE ALIKUWA NDIYO ANAELEKEA kENYA FOR RECORDING RIP MM
 
Jamani hii zamani kila mtu ana zamani yake. Wengine ss zamani yetu nia ya"tatizo kwetu mbagala ukaniona mapenzi siwezi" lazima muweke wazi zamani kuanzia mwaka gani?
 
Samahani wadau,kuna hii taarab moja hivi ambayo kiitikio chake wanasema;
"Yaillah shoga si shoga (kumbe ni hasidi eeh)
Nalia shoga si shoga (kumbe ni hasidi eeh)"

Kwa anayeifahamu jina au mwenye nayo anisaidie,maana ni moja kati ya taarab nilizokuwa nazikubali sana.
 
 
WANASEMA URUDIE KASONGO YA MAQUIS DU ZAIRE cover song by Kawele Mutimuana

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…