Elections 2010 Zilizokamatwa Tunduma zimetua "Ngerengere"

Elections 2010 Zilizokamatwa Tunduma zimetua "Ngerengere"

Kieleweke

Member
Joined
Jun 23, 2009
Posts
79
Reaction score
8
taarifa zinaenea kwamba zile karatasi za kura zilizokuwa zimekamatwa kule Tunduma kwenye lori inasemekana zimerudishwa Zambia na badala yake zimeingizwa nchini kwa ndege bila kutua kwenye kiwanja chochote cha ndege za abiria, bali sasa zimetua kwenye kiwanja cha ndege za kijeshi kwenye kambi ya Ngerengere, mkoani Morogoro.

Imetumika mbinu ileile kama ya Meremeta kwani ukiongelea Meremeta basi inaelezwa kwamba ni suala la kijeshi na hivyo ni suala la ulinzi na usalama wa Taifa na halipaswi kuongelewa. Na kwa sababu Ngerengere hapakanyagiki kiurahisi basi hata ndege ikitua pale hakuna anayeweza kuweka wasiwasi.

Ndiyo sababu si rahisi kumsikia hadharani mtu akitaja kwamba zile kura tayari zimo nchini lakini sasa ziko Ngerengere zikisubiri kusambazwa kulikopangwa.

Baada ya kufanikisha kuziingiza sasa imebaki kuzisambaza ktuoka hapo Ngerengere jeshini. Hivyo inabidi kukaa mkao wa kujua kuwa hilo lipo.

Tuendelee kusambaratisha mbinu hata kwa kutaarifiana hivi.
 
Asante kwa taarifa mkuu. Mungu yu upande wetu tutashinda. Hii vita ni ya kiroho na kimwili na sasa tutamwomba Mungu awaumbue mchana kweupe.
 
Hivi hawa jamaa wanadhani watatawala milele? Me nagopa kufungiwa ninge2kana dunia nzima hapa!
 
Mwaka huu Tanzania inakombolewa. Hata kama wanafanya siri wataumbuka mchana kweupe
 
Sasa kama jambo hili lina ukweli nchi inaelekea pabaya, ndo maana nchi hii haisongi mbele, viongozi wakipatikana bila ridhaa ya wananchi hata mungu hawezi kutoa baraka zake. Tumuombe sana mora kwa nguvu zake hizo kura ziangamizwe na pia sisi tuwe tayari ku-take risk ili kulinda haki yetu.

WAO WANA PESA NA SHETANI SISI TUNA MUNGU, UPANDE UPI UTASHINDA?
 
taarifa zinaenea kwamba zile karatasi za kura zilizokuwa zimekamatwa kule Tunduma kwenye lori inasemekana zimerudishwa Zambia na badala yake zimeingizwa nchini kwa ndege bila kutua kwenye kiwanja chochote cha ndege za abiria, bali sasa zimetua kwenye kiwanja cha ndege za kijeshi kwenye kambi ya Ngerengere, mkoani Morogoro.

Imetumika mbinu ileile kama ya Meremeta kwani ukiongelea Meremeta basi inaelezwa kwamba ni suala la kijeshi na hivyo ni suala la ulinzi na usalama wa Taifa na halipaswi kuongelewa. Na kwa sababu Ngerengere hapakanyagiki kiurahisi basi hata ndege ikitua pale hakuna anayeweza kuweka wasiwasi.

Ndiyo sababu si rahisi kumsikia hadharani mtu akitaja kwamba zile kura tayari zimo nchini lakini sasa ziko Ngerengere zikisubiri kusambazwa kulikopangwa.

Baada ya kufanikisha kuziingiza sasa imebaki kuzisambaza ktuoka hapo Ngerengere jeshini. Hivyo inabidi kukaa mkao wa kujua kuwa hilo lipo.

Tuendelee kusambaratisha mbinu hata kwa kutaarifiana hivi.

Asante kwa uzalendo wako wa kutupa taarifa hizi. Bila hivyo tungejuaje?

Ama kweli, fisadi akishikwa pabaya, hujishikia hata kwenye ubua, bila kujua kwamba hapo ndipo anguko lake.
 
Hizi ndio taarifa zinazoumiza kichwa kwa sasa. Bora watu washinde na kushindwa kwa haki kuliko hila. Hili li nchi hata ukimpa shetani ataliktaaa!!!
 
taarifa zinaenea kwamba zile karatasi za kura zilizokuwa zimekamatwa kule Tunduma kwenye lori inasemekana zimerudishwa Zambia na badala yake zimeingizwa nchini kwa ndege bila kutua kwenye kiwanja chochote cha ndege za abiria, bali sasa zimetua kwenye kiwanja cha ndege za kijeshi kwenye kambi ya Ngerengere, mkoani Morogoro.

Imetumika mbinu ileile kama ya Meremeta kwani ukiongelea Meremeta basi inaelezwa kwamba ni suala la kijeshi na hivyo ni suala la ulinzi na usalama wa Taifa na halipaswi kuongelewa. Na kwa sababu Ngerengere hapakanyagiki kiurahisi basi hata ndege ikitua pale hakuna anayeweza kuweka wasiwasi.

Ndiyo sababu si rahisi kumsikia hadharani mtu akitaja kwamba zile kura tayari zimo nchini lakini sasa ziko Ngerengere zikisubiri kusambazwa kulikopangwa.

Baada ya kufanikisha kuziingiza sasa imebaki kuzisambaza ktuoka hapo Ngerengere jeshini. Hivyo inabidi kukaa mkao wa kujua kuwa hilo lipo.

Tuendelee kusambaratisha mbinu hata kwa kutaarifiana hivi.

Licha ya hawa jamaa kupenda kutumia mbinu chafu. Kila kitu kina mwisho wake. Hivyo mwisho wake uko njiani.
 
mhhhhhhhhhh tatizo si wote wanaompenda mkwere aendelee wao wao wanajeshi wanatoa siri na hao usalama
 
mmmmh!!! inatisha' lakini watanzania tusikatishwe tamaa na hao wahuni, sie tujitokeze kupiga kura.
 
Mkuu Kieleweke, kwanza asante kwa taarifa hizo.

Ila kama una data za uhakika naomba taarifa hizo uziweke vichwa vya habari kwenye magazeti ya Tanzania daima, Mwananchi na Nipashe kati ya kesho na Jumamosi. Ili wananchi wote wasaidie ulinzi ili kuwaumbua hao mafisadi.
 
mhhhhhhhhhh tatizo si wote wanaompenda mkwere aendelee wao wao wanajeshi wanatoa siri na hao usalama

Siyo kutompenda bali kumchoka. Kama hujamchoka mkwere baada ya miaka yake mitano basi utakuwa na mdudu kichwani.
 
KAMA MUNATAKA SAURCE YA WIZI WA CCM muulizeni Lyatonga Mrema uchaguzi uliopita pale kura yake aliojipigia na kuambiwa kwenye kituo chake hakupata hata kura moja huu ndio usanii wa Chukua Chako Mapema.
 
KAMA MUNATAKA SAURCE YA WIZI WA CCM muulizeni Lyatonga Mrema uchaguzi uliopita pale kura yake aliojipigia na kuambiwa kwenye kituo chake hakupata hata kura moja huu ndio usanii wa Chukua Chako Mapema.

@font-face { font-family: "Times New Roman"; }@font-face { font-family: "ArialMT"; }p.MsoNormal, li.MsoNormal, div.MsoNormal { margin: 0in 0in 0.0001pt; font-size: 12pt; font-family: "Times New Roman"; }table.MsoNormalTable { font-size: 10pt; font-family: "Times New Roman"; }div.Section1 { page: Section1; }
Makame ni mnufaika wa mabadiliko ya Katiba

Hadi Februari 2005 sifa za Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilitajwa na Ibara ya 74 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa zifuatazo:

Tume ya Uchaguzi
74.-(1) Kutakuwa na Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano ambayo itakuwa na wajumbe wafuatao watakaoteuliwa na Rais:-
(a) Jaji wa Mahakama Kuu au Jaji wa Mahakama ya Rufani, ambaye atakuwa mwenyekiti;
(b) Makamu Mwenyekiti ambaye atakuwa mtu anayeshika, aliyewahi kushika au anayestahili kuteuliwa kushika madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu au Jaji wa Mahakama ya Rufani;

(c)wajumbe wengine watakaotajwa na sheria iliyotungwa na Bunge.

Lakini ili kumlinda Jaji Makame aendelee kushika nafasi hiyo sifa hizo zilibadilishwa katika Mabadiliko ya Kumi na Nne ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaliyofanywa tarehe 7 Februari 2005 na kukubaliwa na Raisi Mkapa mnamo tarehe 6 Aprili 2005.

Ibara ya 74 (1)(a) na (b) hivi sasa inasomeka:

74 (1) (a) Mwenyekiti ambaye atakuwa ni Jaji wa Mahakama au Mahakama ya Rufani au ni mtu mwenye sifa ya kuwa wakili na amekuwa na sifa hizo kwa muda usiopungua miaka kumi na mitano (Nimeongeza msisitizo)

(b) Makamu Mwenyekiti ambaye atakuwa ni Jaji wa Mahakama au Mahakama ya Rufani au ni mtu mwenye sifa ya kuwa wakili na amekuwa na sifa hizo kwa muda usiopungau miaka kumi na mitano (Nimeongeza msisitizo)

Kwa minajili hiyo ni wazi kuwa Jaji Lewis Makame amenufaika na mabadiliko hayo na kwa hiyo ndiyo maana anaendelea kuibeba CCM katika utendaji wake. Ni lazima kuyasema hayo na kumtaka yeye na Tume kuthibitisha uadilifu na kuaminika kwao.
 
Hiyo njama ya kuiba kura ipo na inafanywa na watu wa NEC, Ikulu jana nilisema kuwa kuna ofisi ya kuiba kura ipo karibu na ofisi ya Tume ya Taifa ya Haki za Binadamu na Ofisi ya Makamu wa Raisi hapo ndipo mikakati yote ya kuiba kura inafanywa. Nilitaja kuwa mmoja wa watu hao alikuwa Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi aliyerudi CCM na ni mpambe mkubwa wa Kikwete. Nimeonyesha vilevile jinsi Katiba ilivyobadilishwa kumfanya Makame aendelee kuongoza NEC na kwa hiyo kazi yake ni kuhakikisha kuwa CCM inashinda.
 
Back
Top Bottom