Sheghwede
JF-Expert Member
- Mar 30, 2013
- 277
- 123
Miaka kadhaa iliyopita, Zimbabwe waliingia kwenye machafuka ya wenyewe kwa wenyewe mara baada ya uchaguzi mkuu uliomrudisha Robert Mugabe Madarakani. Suluhisho likawa ni kutengeneza serikali ya mseto, Tsvangilai akawa Waziri Mkuu.
Kenya nao waliingia katika dimbi hilohilo 2007/08, wakapigana na kuuana. Mwisho wa siku suluhisho ikawa ni serikali ya mseto, Raila Odinga akawa Waziri Mkuu.
Katika vurugu hizo Zimbabwe ilipita pagumu, yafuatayo yakatokea.
1. Watu wengi walijeruhiwa ama kufa, na wengine kuihama nchi
2. Uchumi ulidorora, wali maharage ukauzwa ZWD 70,000,000,000/= na soda ikauzwa ZWD 60,000,000,000. Baada ya serikali mseto ikabidi kufuta sarafu, mpaka leo wanatumia USD
3. Wameishia kuwa na vikwazo vya kimataifa
kwa upande wa Kenya,
1. Watu wengi walijeruhiwa, kufa na kuikimbia nchi kwa muda mfupi
2. Uchumi uliguswa kwa mbali sana, na hiyo haikugusa kabisa mfumo wao wa fedha.
3. Hawakukutana na vikwazo vya kimataifa
Tafakari ni hii, kama wote Zimbwabwe na Kenya walipitia njia inayofanana ingawa katika mazingira tofauti ya kikatiba, kwa nini Zimbabwe mambo yawaendee kombo kiasi hicho wakati Kenya ni kama waliinama tu halafu wakainuka?
Hili ni jambo la kujifunza sana kutoka kwa wakenya, kwani nchi nyingi za kiafrika zilipoingia katika vita ya wenyewe ndio imekuwa kaburi lao. Kenya ndio imepinga hilo, imeingia katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, na bado wameinuka na wanasonga mbele. Mimi nasema tuwaige, wamepita pagumu na wamevuka, huo ni ukomavu mkubwa.
Kila nchi ya Afrika ni prospective victimu, mhanga mtarajiwa, wa yale yaliyotokea Kenya na Zimbabwe. Ivory Coast wamepita njia hiyo, na nchi nyingi za Afrika ya Magharibi, na zinasuasua baada ya bonde hilo.
Narudia tena, tujifunze kwa Kenya, they proved that they can go against the rally
Kenya nao waliingia katika dimbi hilohilo 2007/08, wakapigana na kuuana. Mwisho wa siku suluhisho ikawa ni serikali ya mseto, Raila Odinga akawa Waziri Mkuu.
Katika vurugu hizo Zimbabwe ilipita pagumu, yafuatayo yakatokea.
1. Watu wengi walijeruhiwa ama kufa, na wengine kuihama nchi
2. Uchumi ulidorora, wali maharage ukauzwa ZWD 70,000,000,000/= na soda ikauzwa ZWD 60,000,000,000. Baada ya serikali mseto ikabidi kufuta sarafu, mpaka leo wanatumia USD
3. Wameishia kuwa na vikwazo vya kimataifa
kwa upande wa Kenya,
1. Watu wengi walijeruhiwa, kufa na kuikimbia nchi kwa muda mfupi
2. Uchumi uliguswa kwa mbali sana, na hiyo haikugusa kabisa mfumo wao wa fedha.
3. Hawakukutana na vikwazo vya kimataifa
Tafakari ni hii, kama wote Zimbwabwe na Kenya walipitia njia inayofanana ingawa katika mazingira tofauti ya kikatiba, kwa nini Zimbabwe mambo yawaendee kombo kiasi hicho wakati Kenya ni kama waliinama tu halafu wakainuka?
Hili ni jambo la kujifunza sana kutoka kwa wakenya, kwani nchi nyingi za kiafrika zilipoingia katika vita ya wenyewe ndio imekuwa kaburi lao. Kenya ndio imepinga hilo, imeingia katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, na bado wameinuka na wanasonga mbele. Mimi nasema tuwaige, wamepita pagumu na wamevuka, huo ni ukomavu mkubwa.
Kila nchi ya Afrika ni prospective victimu, mhanga mtarajiwa, wa yale yaliyotokea Kenya na Zimbabwe. Ivory Coast wamepita njia hiyo, na nchi nyingi za Afrika ya Magharibi, na zinasuasua baada ya bonde hilo.
Narudia tena, tujifunze kwa Kenya, they proved that they can go against the rally