Elections 2010 Zitto aanza ziara mikoa ya Pwani na Kusini

Luteni

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
2,274
Reaction score
302
Waliokuwa wanasema Chadema haikujipanga kwa kampeni walikosea, baada ya Zitto kusawazisha mambo nyumbani ameanza kampeni zake katika mikoa ya Pwani na Kusini kwa lengo maalum.
NAIBU katibu mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe ametinga wilayani Kibaha kuwaomba wananchi kumuongezea nguvu bungeni kwa kuwachagua wabunge wengi kadri iwezekanavyo wa kambi ya upinzani ili kwa pamoja waweze kwenda kuibana serikali ili iweke mazingira mazuri ya maisha wa Watanzania.

Mgombea huyo wa ubunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini aliueleza umati mkubwa wa wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni wa chama hicho kuwa katika kipindi hiki anahitaji wasaidizi wengi bungeni ili kila mmoja kwa nafasi yake akatetee maisha ya wananchi ambao wengi wao ni masikini na kwamba akiachwa yeye peke yake, atachelewa kukamilisha dhamira yake ya kuhakikisha kila mtu anakuwa na maisha bora.

Zitto alitoa ombi hilo juzi kwenye viwanja vya Mwendapole wakati wa mkutano wa kampeni wa Chadema. Zitto, mmoja wa wabunge waliojipatia umaarufu kutokana na uwezo wa kujenga hoja na kuibana serikali, alisema amelazimika kusafiri kutoka Kigoma kwa ajili ya kuwaomba wananchi wamuongezee nguvu bungeni.

"Ndugu zangu wa mkoa wa Pwani, hakuna asiyefahamu (kashfa ya zabuni ya ufuaji umeme wa dharura iliyokwenda kwa kampuni ya) Richmond na (wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje) EPA," alisema Zitto.

"Haya mmeyajua baada ya kazi nzuri iliyofanywa na wawakilishi wenu ambao ni wabunge kutoka kambi ya upinzani, bila hao msingesikia na wala msingejua na mngeendelea kutafuniwa fedha zenu za kodi ambazo kwa sasa zingesaidia kuinua maisha yenu.

"Hivyo, ili tuweze kuibua mengine, maana ninaamini yapo mengi tu, mniongezee nguvu kwa kunipa wabunge wengi kadri iwezekanavyo hapo Oktoba ili kwa pamoja tukafanye kazi ambayo muda si mrefu mtaona manufaa yake."

Kiongozi huyo alisema miaka 50 ambayo serikali iliyopo madarakani imekaa imetosha kabisa kuthibitisha kuwa imeshindwa kutimiza matakwa ya watu wake na hivyo sasa ni kipindi cha mapinduzi na kuwataka wananchi wakiweke chama kingine chenye dhamira ya kuinua maisha ya watu wake, ambacho alikitaja kuwa ni Chadema.

Monday, September 20, 2010

Mgombea ubunge jimbo la kibaha mjini.




Mgombea Ubunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini,kwa chama cha CHADEMA,Mh Zitto Kabwe jana alianza rasmi mzunguko wa nchi nzima kuwasaidia wagombea Ubunge na Udiwani wa CHADEMA katika majimbo na Kata zao.Jana alikuwa mjini Kibaha akimnadi mgombea Ubunge kwa jimbo hilo la Kibaha Mjini ,Bw.Habibu Mchange.​



Nikimnadi mgombea wetu wa ubunge Kibaha Mjini-HABIBU MCHANGE





Wananchi walijitokeza















Nikimnadi mgombea udiwani Kata ya Kibaha-Patrick Kinunda​


 
Dogo anafanya vitu vyenye akili sana
huwezi kutarajia anakuja na ubunifu huu mzuri
Zitto we backing you up just tuwakilishe vyema.
 
Habari njema sana hizi... Zitto peke yake anatosha kufuta nyayo za mama Salma, Riizi wani na Dk Bilal... Njoo hadi Mbeya kwa Sugu braza Zitto.
 
Habari njema sana hizi... Zitto peke yake anatosha kufuta nyayo za mama Salma, Riizi wani na Dk Bilal... Njoo hadi Mbeya kwa Sugu braza Zitto.
Nafikiri Zitto amepelekwa sehemu zenye vibandiko vingi kama sikosei Mbeya atatinga kamanda mwenyewe.
 
Good plan Chadema..Zitto make the most of it..mwaga sumu, washa moto mkali october 31st kielewekeeee...
 
Huyu nitishio kwa wazee na vijana!
You have my full support broda!
 
Jk naona kwa sasa ana hofu ya CCM kushindwa uchaguzi mbaya zaidi kushindwa uku yeye akiwa Mwenyekiti.
Uchunguzi wa Synovate na vijana wa kazi usalama wa Taifa unatosha kumnyima usingizi.
Mwendo sasa ni kuchakachua matokeo by any means
 
safi sana Zito.
Kaitangaze CHADEMA kusini kwani familia ya JK imeipaka matope mno huko.
 
Kazi nzuri sana hii, ni kweli tunahitaji upinzani kukomaa Bungeni. Pia tunahitaji kiongozi mwenye calibre ya Dr. Slaa!!

Go Zitto Go...!! Hamasisha wananchi wamchague Dr. Slaa na wabunge wa upinzani!!
 
Tunakukubali zitto, endelea na kasi hizo. Tunasubiri october 31.
Kwa sababu hawaoneshi kwenye Luninga, twende kimya kimya tutafika tu.
Big up mzee
 

Zito wa ukwe -e!!

God Bless you Papii
 
chanja mbuga zitto
mikakati yenu ni mizuri sana
tumechoka hawa watu
ukweli unahitaji makamanda wengi wa kukusaidia
 
NImeipenda startegy yako na chama Mkuu Zitto.
Mnapita kule walikojihahakikishia ushindi na kuvuruga; hadi keleweke!!

Go Zitto, Go Slaa....
 
CHADEMA all the way......sisi hatutumii familia, tunatumia Vichwa ndani ya chama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…