Zitto Alazwa Muhimbili

Status
Not open for further replies.
Tuchange mchango wa kumpeleka India au South Africa akapimwe vizuri, hivi Zitto ana mke
 
Du wangwe ndani ya nyumba na wala hata hana huruma!
Wangwe...Acha kijana apate nafuu kwanza bana.
 
Tanzania imekuwa nchi ya kutisha sana. Inapotokea mtu anagusa maslahi ya mafisadi halafu akaugua ghafla ni lazima watu tushtuke kutokana na mafunzo tuliyopata katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Amina aligusa mahala padogo tu, matokeo yake akaugua kimchezomchezo mwishowe yakawa makubwa hadi leo bado tunaomboleza. Balali alijua kitu fulani kuhusu wizi wa BOT tu, akaugua ghafla hadi leo hatujui alikuwa akijua nini.

Historia za namna hiyo zimenifanya niwe nachukulia kwa uzito sana swala lolote la mtu kuugua ghafla huku ikijulikana kuwa mtu huyo alikuwa anapingana na mafisadi. Inawezekana kabisa kuwa Mh. Zitto ana tatizo la kawaida kabisa lakini position yake katika mduara wa kisasa hapa kwetu inanifanya niwe concerned sana. Nitafurahi sana kupata updates kuhusu hali ya mheshimiwa huyu; kama kuna anayejua kuwa anaendeleaje tafadhali sana atuarifu.
 


Baada ya kuweka post hii nilipata taarifa kwa pembeni ikionyesha kuwa Mheshimiwa Zitto anaendelea vizuri. Mungu ashukuriwe
 
Baada ya kuweka post hii nilipata taarifa kwa pembeni ikionyesha kuwa Mheshimiwa Zitto anaendelea vizuri. Mungu ashukuriwe

..atapona na kujaaliwa afya njema.

..nadhani ni maradhi ya kawaida na yanaweza pia yakawa yamechangiwa na kazi nyingi.

..ndio ubinadamu huo.
 
Ni kweli..Kazi ya Bungeni leo pia ilkuwa NGUMU SANA!
Tunasubiri kuona Mchango wake na pia mapendekezo yake hopefull yatafanyiwa kazi so that we can move forward.
 
Ni kweli..Kazi ya Bungeni leo pia ilkuwa NGUMU SANA!
Tunasubiri kuona Mchango wake na pia mapendekezo yake hopefull yatafanyiwa kazi so that we can move forward.

..kumbe at times unakuwa na imani pia.
 

Mama mzazi wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, Shida Salum na bibi wa mbunge huyo, wakimfariji mbunge huyo aliyelazwa katika hospitali ya Muhimbili Jumatano Dar es Salaam.
 
Zitto Kabwe hatakiwi kuwepo kabisa katika mjadala wa wizara ya madini na nishati kwani wezi wanajua kabisa kwamba moto utawaka hapo bungeni.
 
Nakutakia afya njema Mh. Zitto na tunakuombea upone ili urudi kwenye majukumu both kwa familia yako na Taifa lako kwani sote twakuhitaji
 
Kamanda Zitto;

Twakuombea Heri Na Upone; Wewe Ni Rare Species Katika Taifa Letu Na Uwepo Wako Utasaidia Sana Vijana Kujenga Ujasiri Na Kujua Upande Wa Pili Wa Shilingi Kwa Mambo Mengi

[ila Naogopa, Hawa Wabunge Machachari Mbona Kama Afya Zao Nitaka Kunitisha?]

May God Protect You And All Those Who Stand For Right Things
 
POLE SANA ZITTO KABWE. MUNGU ATAKUPONYA NI KAWAIDA BINADAMU KUUGUA.

Nyani Ngabu, unanisikitisha sana kwa post zako vipi Ndg nani kakuudhi kiasi hicho, nimekuwa nikisoma threads zako lakini sasa unanitolea imani, tafadhali cool down.
 
pole Sana Zitto Kabwe. Mungu Atakuponya Ni Kawaida Binadamu Kuugua.

nyani Ngabu, Unanisikitisha Sana Kwa Post Zako Vipi Ndg Nani Kakuudhi Kiasi Hicho, Nimekuwa Nikisoma Threads Zako Lakini Sasa Unanitolea Imani, Tafadhali Cool Down.

Manyani Ndivyo Yalivyo.....!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…