Zitto baada ya kauli yako, usishangae Msajili akaishukia ACT - Wazalendo

Zitto baada ya kauli yako, usishangae Msajili akaishukia ACT - Wazalendo

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Nimesikiliza clip yako twitter kuhusu ni nini mtafanya mwaka huu iwapo mtashinda Uchaguzi halafu msikabidhiwe Serikali.

Kwanza nikupongeze kwa kutokurudi nyuma hasa ukizingatia barua ile ya Msajili kwa chama chenu. Hata hivyo,pamoja na pongezi hizi, nawashauri mjiandae kwa lolote maana ni kama umeweka acid kwenye kidonda kibichi.

Hakika umeamua kuwa "ngangari" na kwa namna hiyo,naamini unawapa moyo na ujasiri walio nyuma yako kama kiongozi ingawa kusema huwa ni jambo moja, na kuteleza huwa ni jambo lingine, but all in all, unaonyesha msimamo thabiti.

Hongera kwa kutomungunya maneno.
 
Kwanza nikupongeze kwa kutokurudi nyuma hasa ukizingatia barua ile ya Msajili kwa chama chenu.Hata hivyo,pamoja na pongezi hizi, nawashauri mjiandae kwa lolote maana ni kama umeweka acid kwenye kidonda kibichi.
Aah! "Kidonda ni Kidonda'tu mkuu Salary, mbele ya 'acid', haijalishi ni 'kidonda kibichi' au 'kidonda sugu'.

Naona maneno aliyotumia Zitto ni mazito kwamba umeshindwa kuyabeba na kuyaleta hapa.
 
Nami ninetafakari ile kauli nikasema nchi ya mizengwe hii watamuandama. "tutachukua ushindi" wanaweza kutafsiri wanavyojua wao. Lakini naangalia mazingira ya tanzania kuchukua ushindi ulioporwa naona pagumu kwa woga wa watanzania! Watamuandamana na lile li Msajili bomu, itakuwa kazi!
 
Nami ninetafakari ile kauli nikasema nchi ya mizengwe hii watamuandama. "tutachukua ushindi" wanaweza kutafsiri wanavyojua wao. Lakini naangalia mazingira ya tanzania kuchukua ushindi ulioporwa naona pagumu kwa woga wa watanzania! Watamuandamana na lile li Msajili bomu, itakuwa kazi!
Jamaa kaamua kujilipua.
 
Mbona ni maneno ya kawaida tu.

Ni maneno ya kutaka haki bin haki kwenye uchaguzi wa mwaka huu

Kwamba atakayeshinda kihalali atapongezwa, ila ushindi ukiwa ni wa kupora hakuna kujikunyata!. Maneno mazuri sana hayo, na ndivyo inavyopaswa iwe!

Halafu jifunze kuweka maneno kifuani, siyo kila kauli unakimbilia kuianzishia mada JF.

Wapinzani sijui mnapigania nini, mnakuja kusnitch mitandaoni badala ya kutoa sapoti CCM ing'oke

Mambo mengine mnayakuza bila sababu, halafu mnawapa watawala sababu za kufanya uhuni wao!

Au na huu ni mpango mkakati wa vyama vingine vya upinzani kuionea wivu ACT kwa kulamba bingo huko Zanzibar?

Zitto ajue kuwa kuna watu wana wivu nae, watamshambulia mitandaoni, watamsnitch, watafanya kila wanaloweza ACT isifanikiwe, kwa hiyo awe makini sana
 
Mbona ni maneno ya kawaida tu

Halafu jifunze kuweka maneno kifuani, siyo kila kauli unakimbilia kuianzishia mada JF.

Wapinzani sijui mnapigania nini, mnakuja kusnitch mitandaoni badala ya kutoa sapoti CCM ing'oke

Mambo mengine mnayakuza bila sababu, halafu mnawapa watawala sababu za kufanya uhuni wao!

Au na huu ni mpango mkakati wa vyama vingine vya upinzani kuionea wivu ACT kwa kulamba bingo huko Zanzibar?
Kwa akili yako, Msajili anategemea JF kujua Zitto kaongea mini?

Alafu kwani hata zile kauli za mwanzo hazikuwa ni za kawaida tu?

Hapa Zitto anajua anajua anachokifanya kwani anaelewa hivi sasa anafuatiliwa kila anachosema.
 
Kwa akili yako, Msajili anategemea JF kujua Zitto kaongea mini?

Alafu kwani hata zile kauli za mwanzo hazikuwa ni za kawaida tu?

Hapa Zitto anajua anajua anachokifanya kwani anaelewa hivi sasa anafuatiliwa kila anachosema.

Msajili naye anaangalia reaction za watu mitandaoni. Akiona jambo limezua mjadala interest inaongezeka zaidi, ilimradi atimize nia yake ovu

Nakushauri vitu ambavyo wewe unadhani vinaweza kutumika kuumiza upinzani usivianzishie mada.

Watawala wanatafuta excuse na legitimacy ya kuhalalisha uharamu!
 
Mbona ni maneno ya kawaida tu.

Ni maneno ya kutaka haki bin haki kwenye uchaguzi wa mwaka huu

Kwamba atakayeshinda kihalali atapongezwa, ila ushindi ukiwa ni wa kupora hakuna kujikunyata!. Maneno mazuri sana hayo, na ndivyo inavyopaswa iwe!

Halafu jifunze kuweka maneno kifuani, siyo kila kauli unakimbilia kuianzishia mada JF.

Wapinzani sijui mnapigania nini, mnakuja kusnitch mitandaoni badala ya kutoa sapoti CCM ing'oke

Mambo mengine mnayakuza bila sababu, halafu mnawapa watawala sababu za kufanya uhuni wao!

Au na huu ni mpango mkakati wa vyama vingine vya upinzani kuionea wivu ACT kwa kulamba bingo huko Zanzibar?

Zitto ajue kuwa kuna watu wana wivu nae, watamshambulia mitandaoni, watamsnitch, watafanya kila wanaloweza ACT isifanikiwe, kwa hiyo awe makini sana

We jamaa muoga sana... kwamba kauli ya mwanasiasa kama Zitto unaweza ificha twitter isionekane?
Usnitch wa huyu bwana upo wap hapo.... just his concern...
Kwamba kutaka kutoa CCM madarakani ndio kila mtu aimbe iyele iyele
 
Siku tu nikihakikishiwa na nikijiaminisha pasi na shaka tena kwa 100% kuwa Zitto Kabwe ni ' Mpinzani ' wa Kweli nchini basi nitaanza Kumuelewa.
 
NEC ikishamtangaza mshindi wa Urais hata kama amepora hadharani, mchezo unaishia hapo na vyombo vya dola vinaingia kazini huku Mahakama ikiwa imefungwa miguu, mikono na mdomo. Maalim Seif, Zitto na huyu huyu Membe wanalifahamu hili vizuri sana

Hizi drama za Zitto alipaswa kuzianzisha kitambo sana na sio jioni hii. Sijui kwanini wanasiasa humute for 5 years na kuanza kulilia Tume Huru miezi michache kabla ya uchaguzi
 
Msajili naye anaangalia reaction za watu mitandaoni. Akiona jambo limezua mjadala interest inaongezeka zaidi, ilimradi atimize nia yake ovu

Nakushauri vitu ambavyo wewe unadhani vinaweza kutumika kuumiza upinzani usivianzishie mada.

Watawala wanatafuta excuse na legitimacy ya kuhalalisha uharamu!

Mkuu nadhani umemuelewa vibaya mleta mada, kwenye post yako ya juu na hii. Kwani Zito ameanzisha hiyo mada humu mitandaoni ili isiwe na reaction? Ama reaction itakuwa kwenye mada hii, ila ile ya Zito ambayo ndio original itakosa reaction? Labda useme kuwa Zito kaileta hiyo post huko twitter, lakini hataki iwe na reaction kuepusha msajili kuichukulia ACT hatua. Unakwama wapi mkuu?
 
Back
Top Bottom