battawi
JF-Expert Member
- Mar 29, 2014
- 2,712
- 2,577
Halmashauri haiwezi kuleta taswira ya chamaSio kweli masmuzi ya halmashauri hufanywa na baraza la madiwani na meya wao .Ujiji iko chini ya ACT wazalendo walitakiwa waeleze walichoweka kwenye Ilani iliyopita walikitekelezaje kwenye halmashauri Yao ambako wao ndio waamuzi
Ikiwa Mfumo wa nchi ni CCM na Mabavu kila uchao unatarajia nini?
Ngoja tukamate dola uone Mabadiliko ya sera , na Tuweke sera ya Kitaifa itakayoshirikisha wadau wote w nchi vikiwemo vyama vya siasa Tanzania kwa pamoja ili tuweke kitu uniform kwa kila atakayekuja afuate bila kupindisha.
Ngoja Tubadili katiba ili iwe na milango ya uhuru na haki kwa kila mtanzania , kwa katiba hiyo vyombo vya Dola vitapangiwa majukumu yao bila kutumiwa na wanasiasa.
Jeshi latalinda mipaka.
Polisi watawalinda Raia.
Serikali italindwa na Uadilifu na utekelezaji ulio sawa na Bunge ndilo litakalo iwajibisha serikali ipasavyo bila ya kuhofu kutumbuliwa.
Mahakama itasimamisha Haki kwa kila raia. Sisa haitaingia mahakamani ng'o.
Waandishi wa Habari watakuwa huru kuchunguza na kutoa habari kwa Umma,wakizua kitu cha uongo ,mahakama zipo huru kwa kila aliguswa na kulalalmika.