Zitto Kabwe adai barua yake kwa Benki ya Dunia inapotoshwa. Asema hajazuia mkopo kwa Tanzania bali amewatetea watoto wanaopata ujauzito wakiwa shuleni

Zitto Kabwe adai barua yake kwa Benki ya Dunia inapotoshwa. Asema hajazuia mkopo kwa Tanzania bali amewatetea watoto wanaopata ujauzito wakiwa shuleni

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo), amedai kuna upotoshaji kuhusu barua aliyoiandikia uongozi wa Benki ya Dunia (WB) kuhusu mkopo wa Dola za Marekani milioni 500 ambao Tanzania imeomba kwa benki hiyo.

Akiwa mjini Toronto, Canada juzi, Zitto alidai si lengo lake kuzuia misaada nchini ila anafanya hivyo ili kuwalinda watoto wa kike wanaopata ujauzito wakiwa katika masomo kwa kile alichodai kuwapo ubaguzi katika mfumo rasmi wa elimu nchini.

“Kwanza kuna upotoshaji wa suala hili zima kwa sababu nimeandika barua siyo kuzuia misaada ila kuitaka Benki ya Dunia kabla ya kutoa mkopo kwa Serikali ya Tanzania, izingatie kuwa mkopo ule unakwenda kuwabagua watoto wa kike ambao wamepata ujauzito na kuzuiwa kurudi shuleni," alidai.

Wiki iliyopita baada ya kuibuliwa kwa suala hilo bungeni jijini Dodoma, Spika wa Bunge, Job Ndugai, alimtaka Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Profesa Adelardus Kilangi, kuchunguza kitendo hicho cha Zitto ili kuona kama kuna jinai au la.

Alisema uchunguzi huo unapaswa kufanyika ili kama kutaonekana kuwapo kwa jinai, mbunge huyo achukuliwe hatua kufuatia hoja binafsi iliyowasilishwa bungeni na Mbunge wa Siha, Dk. Godwin Mollel (CCM), aliyetaka kuchunguzwa kwa jambo hilo.

“Mbunge mwenzetu atakaporudi, labda anaweza akatufafanulia wenzake, Mheshimiwa Zitto Kabwe kuandika barua Word Bank (Benki ya Dunia) kwamba nchi yetu ikose fedha za mkopo ambazo lengo lake ni elimu kwa sababu ya tofauti za sera," Spika Ndugai alisema.

Akijenga hoja yake siku hiyo ili aungwe mkono na wabunge, Dk. Mollel alisema: “Nasimama kwa Kanuni ya 47(1) ili kuomba kuahirisha shughuli za Bunge ili kujadili jambo la dharura. Hapa juzi mwenzetu Zitto ameandika barua kwenye Benki ya Dunia, na alipoandika barua kwenye Benki ya Dunia, alitaka fedha zizuiliwe ambazo zingekuja kusaidia elimu Tanzania.

“Lakini, pesa hizo zingekuja tungejenga shule tano kubwa kwa kila wilaya, tungeweza kuwaweka bwenini watoto zaidi ya 2,000 wa kike ambao mwisho wa siku hata kiwango cha mimba kwa taifa letu kingeshuka sana."

Alisema wabunge waliapa bungeni kwa kutumia Katiba ya Tanzania na katiba hiyo imetaja dhahiri maadui wa taifa ukiwamo umaskini, ujinga na maradhi.

Alisema unapogusa kwenye eneo hilo la elimu ina maana umefuta ujinga, umaskini na maradhi, hivyo akadai Zitto anapaswa kuchukuliwa hatua kwa kuwa amevunja katiba.


Muungwana blog
 
wakiwa katika masomo kwa kile alichodai kuwapo ubaguzi katika mfumo rasmi wa elimu nchini.

“Kwanza kuna upotoshaji wa suala hili zima kwa sababu nimeandika barua siyo kuzuia misaada ila kuitaka Benki ya Dunia kabla ya kutoa mkopo kwa Serikali ya Tanzania, izingatie kuwa mkopo ule unakwenda kuwabagua watoto wa kike ambao wamepata ujauzito na kuzuiwa kurudi shuleni," alidai.
Kazi ya mbunge si kuwasiliana na benki ya dunia kwa kutumia ofisi ya bunge na karatasi zenye nembo ya bunge

kaanza kulia lia shughuli iko pale pale no return
 
Sikubaliani na hoja ya Zitto hata kidogo, tatizo la mimba kwa wanafunzi ni tatizo dogo sana na chanzo chake ni tamaa za hao wanafunzi na ukosefu wa maadili kunakoambatana na kiburi Cha kutosikiliza kwa makini maonyo ya wazazi, walimu na walezi.

Kama, Kuna ambao ni wahanga wa vitendo vya unyanyasaji wa kingono au ubakaji na wamepata mimba hao ni kweli wanahitaji kurudi shule lakini wanatakiwa kujengewa shule zao ili wawe wanapata msaada wa kisaikolojia zaidi na pengine Zitto kama angekuwa na akili timamu angetoa mapendekezo ya kuwasaidia wahanga zaidi kuliko hao wanaoneng'eneka.

Suala la mwanafunzi aliyepata mimba kurudi shule sikubaliani nalo kabisa kwa sababu Kuna siku darasa litakosa wanafunzi kabisa kisa wanafunzi Wana mimba wanahitaji kujifungua au wanaomba likizo ya uzazi. Hapo Nani wa kulaumiwa?
 
miss zomboko,

Mhe. Zitto relax unapokuja kwa matao yao chini bado anayeumia ni mtanzania maskini kukosa haki yake ya kielimu, tunakuunga mkono 100%
 
Sidhan kama wanamaanisha kuwa mwanafunzi arudi kuendelea na masomo huku akiwa mjamzito!!!unapotosha kimasihara!!!
Hoja ni kuwa Mara baada ya kujifungua arudi kupata elimu ambayo ni haki ya kila mtanzania kikatiba!

Sent using Jamii Forums mobile app
Utaratibu huko nyuma ulikuwaje kwa wanaopata ujauzito? Ukielewa ndio utajua upotoshaji wa Zitto.

Pengine Zitto ana maslahi mapana ya wanafunzi wazazi bila kuangalia athari za wanafunzi hao kwa wenzao. Hii màda inatukumbusha juu ya zitto Kusubiri kushindwa kwa Rais Magufuli au serikali ni Kamari mbaya sana. Serikali ya awamu ya tano ni itashinda kwa sababu…
 
miss zomboko,
Zitto Kabwe tuna taarifa zake Nzito huko Kigoma. Kumbe upo kwenye hali mbaya hivyo nyumbahaikaliki. Na bado mpaka wake zako watakukana, Marafiki zako watakukimbia. Vijana wamekuchoka na wanakuogopa haswa baada ya kujiridhisha kuwa una kikosi chako maeneo mbalimbali wengi wakiwa Kagunga. Vijana wameabarishana kuwa uliwakimbia Vijijini katika Jimbo la Kigoma Kaskazini kutokana na kukutwa uki wnga huko Kagunga. Kijana mdogo una Wang unaongozwa na wanaojiita Wazee kumbe ni sehemu ya kikosi cha kchaw.
Waganga wako wamepanga kuachana nawewe eti umeingiliwa na gund, ila Wanasubiria uwatoe za ulinzi uchaguzi Mkuu 2020😎😎😎😎😆😆😆😆. Wameona haueleweki mambo yako.
 
KARLO MWILAPWA,
eti tamaa zao, jinga kabisi hili, badala ya kusema wanarubuniwa na wenye akili!!? umekaa wee unaandika upumbavu huu!!? yaani akili yako ndio imeishia hapo, pole sana zwazwa!
 
KARLO MWILAPWA,
eti tamaa zao, jinga kabisi hili, badala ya kusema wanarubuniwa na wenye akili!!? umekaa wee unaandika upumbavu huu!!? yaani akili yako ndio imeishia hapo, pole sana zwazwa!
 
Kazi ya mbunge si kuwasiliana na benki ya dunia kwa kutumia ofisi ya bunge na karatasi zenye nembo ya bunge

kaanza kulia lia shughuli iko pale pale no return
Hongera Zitto kwa kuujuza ulimwengu ufisadi unaofanywa na serikali ya CCM!
 
hakuna pesa za kununua shule za ccm, kwa bei ya kununua ndege, halafu mje kutupiga virungu mkipata fedha za world bank ,sisi wananchi tutakaolipa deni,
zitto shika hapo hapo, watupe baada ya uchaguzi
 
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo), amedai kuna upotoshaji kuhusu barua aliyoiandikia uongozi wa Benki ya Dunia (WB) kuhusu mkopo wa Dola za Marekani milioni 500 ambao Tanzania imeomba kwa benki hiyo.

Akiwa mjini Toronto, Canada juzi, Zitto alidai si lengo lake kuzuia misaada nchini ila anafanya hivyo ili kuwalinda watoto wa kike wanaopata ujauzito wakiwa katika masomo kwa kile alichodai kuwapo ubaguzi katika mfumo rasmi wa elimu nchini.

“Kwanza kuna upotoshaji wa suala hili zima kwa sababu nimeandika barua siyo kuzuia misaada ila kuitaka Benki ya Dunia kabla ya kutoa mkopo kwa Serikali ya Tanzania, izingatie kuwa mkopo ule unakwenda kuwabagua watoto wa kike ambao wamepata ujauzito na kuzuiwa kurudi shuleni," alidai.

Wiki iliyopita baada ya kuibuliwa kwa suala hilo bungeni jijini Dodoma, Spika wa Bunge, Job Ndugai, alimtaka Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Profesa Adelardus Kilangi, kuchunguza kitendo hicho cha Zitto ili kuona kama kuna jinai au la.

Alisema uchunguzi huo unapaswa kufanyika ili kama kutaonekana kuwapo kwa jinai, mbunge huyo achukuliwe hatua kufuatia hoja binafsi iliyowasilishwa bungeni na Mbunge wa Siha, Dk. Godwin Mollel (CCM), aliyetaka kuchunguzwa kwa jambo hilo.

“Mbunge mwenzetu atakaporudi, labda anaweza akatufafanulia wenzake, Mheshimiwa Zitto Kabwe kuandika barua Word Bank (Benki ya Dunia) kwamba nchi yetu ikose fedha za mkopo ambazo lengo lake ni elimu kwa sababu ya tofauti za sera," Spika Ndugai alisema.

Akijenga hoja yake siku hiyo ili aungwe mkono na wabunge, Dk. Mollel alisema: “Nasimama kwa Kanuni ya 47(1) ili kuomba kuahirisha shughuli za Bunge ili kujadili jambo la dharura. Hapa juzi mwenzetu Zitto ameandika barua kwenye Benki ya Dunia, na alipoandika barua kwenye Benki ya Dunia, alitaka fedha zizuiliwe ambazo zingekuja kusaidia elimu Tanzania.

“Lakini, pesa hizo zingekuja tungejenga shule tano kubwa kwa kila wilaya, tungeweza kuwaweka bwenini watoto zaidi ya 2,000 wa kike ambao mwisho wa siku hata kiwango cha mimba kwa taifa letu kingeshuka sana."

Alisema wabunge waliapa bungeni kwa kutumia Katiba ya Tanzania na katiba hiyo imetaja dhahiri maadui wa taifa ukiwamo umaskini, ujinga na maradhi.

Alisema unapogusa kwenye eneo hilo la elimu ina maana umefuta ujinga, umaskini na maradhi, hivyo akadai Zitto anapaswa kuchukuliwa hatua kwa kuwa amevunja katiba.


Muungwana blog
Mhuni huyu Zitto. Hii ni sawa na Mtu aliyejinyea mbele ya watu na kudai alikuwa anajaribu kujamba. Mahojiano yote BBC na kwenye barua yanaonyesha nia ya dhati ya Zitto kuitaka Benki ya Dunia KUZUIA FEDHA HIZO ZISIINGIE NCHINI. sasa anaona kila mtu anamlaumu anasingizia upuuzi!
 
Back
Top Bottom