Zitto Kabwe ataka Simba waweke mchakato wazi

Mimi kwa uelewa wangu, may be hiyo 1,000,000,000 ni kama kampuni iwe na mtaji angalau kiasi hicho
 
Mkuu unaelewa ata utaratibu wa kutangaza tenda lakini? Kwenye tenda yoyote Ile lazima kuwe na amount ambayo inatajwa kama kiingilio au mtaji, so Simba wangeweza ata kuandika 10ml ila mshinda zabuni ukaskia katoa 1bil, so sio kweli kwamba Simba walijilimit ispokuwa Huo ndio utaratibu wa kutangaza tenda, labda uhoji vitu vingine

Na kuhusu mwaka 2020/2021 Huo ni msimu wa ligi au mwaka wa kimpira na sio mwaka wa kuisha mkataba, kwahiyo Kwa lugha nyepesi ni kwamba huyo mshinda zabuni ataanza kutumikia nafasi yake msimu wa 2020/2021 na sio 2019/2020, mbona Mambo Mengine madogo sana na hayaitaji degree kuelewa, au kwakuwa zito kauliza nawewe umeona uulize Tu
 
Mbona MO hakwenda ofisi za FCC kulalamikia ucheleweshwaji wa taratibu za mabadiliko ya Club ya Simba? ni mwendo wa kutweet tu pengine tusingeyajua haya yote...
 
Ujuaji tu huyu Kenge.Siasa imemshinda.
 
Uwazi wa nini kwani ninyi mna timu hiyo timu ni ya Mo na ndio maana hata mchakato wa kumpata Ceo hamkushirishwa ninyi pokeeni mkija kuzinduka nyumba imeanguka
 
Hivi ungetoa hoja yako bila kejeli usingeeleweka. Mimi kudeal na mambo ya tenda ndio shuguri zangu, hiyo tenda ina mapungufu mengi lakini sio kila mtu anayehoji anakuwa nq mawazo hasi mengine ni kuwekana sawa ili wakati mwingine waboreshe.
Kutangaza tenda ya mwaka mmoja halafu ukatoa mkataba wa miaka miwili hiyo kitu haijakaa sawa hapo mzabuni mwingine anaweza kupinga tukapoteza muda kwenye malumbano badala ya kuelekeza nguvu kwenye mashindano yanayotukabili.
Kutangaza tenda kwa jina tofauti na jina linalotoa mkataba pia ni kosa na makosa kama hayo ndiyo yanafanya mchakato kukwama fcc
 
Sidhani kama mambo ya tenda ndio mambo yako Samahani lakini kama nilikosea au nitakosea, ingekuwa ni mambo yako sidhani kama ungehoji Kwa nini bid ya Simba ilikuwa 1bil

na kama mambo ya tenda yangekuwa yako usingehoji Kwa nini kwenye tenda unaongelewa mwaka 2021 maana ni season

kama mambo ya tenda yangekuwa ni yako ungeelewa kuwa hadi mshinda zabuni anatangazwa ujue competitors hawanaja appeal

Na mwisho kabisa sidhani kama mambo ya tenda ni mambo yako maana ungeelewa kuwa Simba ipo kwenye mchakato wa kuchange kuwa kampuni ndomana kwa sasa walitumia jina la Simba kama taasisi Ila pesa inaingia kweny account ya kampuni maana yake mchakato upo ukingoni kumalizika

Labda nikuulize hivi unajua wanachama na mashabiki hasa wanataka nini kutoka kwenye hivi vilabu bya Simba na Yanga? Na Kama hutojali Naomba unieleweshe kitu kimoja huyo mwanachama au shabiki atapata hasara gani endapo Huo mchakato utakuwa sio wazi na haujafata utaratibu?
 
Mkuu Nadhani Club ni kampuni. Huwezi kusajili BRELA “Simba sports club” ukaishia hapo bila kuspecify. Kuna brand name na kuna company name. Timu ni moja tu ya bidhaa za kampuni.
Mfano, team kama Man Utd imesajiliwa kama PLC (public limited company), inayoendesha bidhaa ya Man Utd club.... I stand to be corrected [emoji120][emoji120]
 
Inawezekana.mambo ya tenda siyo yangu, kwa kichwa changu cha ngumbaru unaweza kutangaza tenda ya mwaka mmoja ukatoa mkataba wa miaka miwili, unaweza kutangaza tenda kwa jina la Simba sport club ukatoa mkataba wa Simba sport club limited.
Badala ya kudandia hoja juu soma tenda ilivyotangazwa halafu uje na hoja bahati nzuri kuna mdau ameleta tangazo la tenda pitia soma kwanza.
 
Tatizo sio kuwa simba sport club au simba sport club limited tatizo ninkuchanganya vitu viwili kwenye swala moja
 
Nafikiri nia yake ni kila mwanasimba hata wakule nyumbani mpitimbi aelewe mchakato mzima.....
 
Muda ni mwl mzuri sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…