SAGAI GALGANO
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 47,706
- 69,281
Huyu maza alikuwa mkewe wa dhalim kwa kinuktaNi jambo jema
Huyo Mhagama kaacha madudu kibao Utumishi
Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huyu maza alikuwa mkewe wa dhalim kwa kinuktaNi jambo jema
Huyo Mhagama kaacha madudu kibao Utumishi
Eti Babu Tale naye ni mbunge,vichekesho haviishi TanzaniaMle bungeni wamejaa wajinga
Yaani huyo naona kazi yake siku zote bungeni, huwa ni kuja na miongozo' tu bungeni kuzuia mijadala yenye tija Kwa wananchi....kaazi kwelikweli.Ni jambo jema
Huyo Mhagama kaacha madudu kibao Utumishi
Ndio sababu kama yule shetani kama ataiona pepo basi ujuwe motoni ni myths tu, hakuna kitu kama hicho.Ule uchaguzi wa 2020 ilikuwa hujuma tupu
Au anatumika !!?? You never know !!Kama mwanasiasa Zitto yupo well informed na uwa na arguments za msingi.
Shida yake ni mtu anaeishi na kinyongo saa zingine inabidi atunge uongo or mislead people to justify his viewpoint ya mtu asiempenda, hana misimamo rasmi ni ngumu kuelewa agenda yake ya muda mrefu anataka atimize malengo gani ya siasa binafsi na chama chake, ana nunulika kirahisi na kuweza kutumika kama chawa; madhara yake as a brand anaonekana ni mtu inconsistent na sio wa kuaminika ata anapoongea hoja za msingi.
Bora hata ya Lissu either unamkubali au la; lakini unajua anasimamia nini. Hoja yoyote anayoizungumzia ata kama hujui maneno atakayo tumia, lakini una idea ya mtazamo atakao utoa kabla ya hata kumsikiliza. Mfano kwa Lissu CCM sio watu wazuri in general, ila wamezidiana viwango vya ukatili tu na kwenye kuiba.
Wengine wenye consistent kwa siasa za Tanzania ni Chalamila (kwenye kuwapa watu ukweli wasiopenda kusikia), Makamba (with over ambitions plans za maendeleo without proper strategies to attain those goals) na Bashe (kama Makamba with grandiose ideas but limited knowledge).
Wanasiasa wengine wapo wapo tu wanaenda na upepo kama huyu Zitto ata anapoongea vitu vya msingi jamii inaanza kumu ignore kwa sababu yeye mwenyewe anaharibu brand yake kwa kutokuwa consistent kwenye misimamo ya siasa na kupenda majungu; ni mtu hovyo kweli.
Kitu kizuri ni kwamba Rais Smaia Suluhu anaendelea kulishughulia hili suala la viongozi wabadhilifu kwahiyo hawa wabunge hawastui nchi iko mikono salama Watanzania tuna amani sana chini ya uongozi wa Rais Samia SuluhuAmeandika Zitto Kabwe, kiongozi wa ACT Wazalendo:
CAG akishatoa ripoti yake AMEMALIZA. Ripoti yake ni ya mwisho. Ni FINAL. Kazi inayofuata ni ya Bunge.
Umma ujue kwamba, kabla CAG hajatoa ripoti yake Serikali hupewa nafasi ya kujibu hoja za Ukaguzi. Baada ya Ripoti kutoka majibu sio kwa Serikali tena, ni kwa Bunge.
Wakati wa mchakato wa Ukaguzi Maafisa Masuuli hudharau na kuzembea kujibu hoja kwenye ‘Exit meeting’. Baada ya CAG kutoa ripoti Rasmi na kuonyesha madudu, maafisa masuuli wanalia lia.
Nimeona Waziri Jenista Mhagama na Naibu Spika Zungu wakijaribu kuzuia Wabunge kuongelea ripoti ya CAG eti kanuni haziruhusu. SIO KWELI.
Wana mislead Bunge. Siku 21 Naibu Spika anazosema Serikali inapewa NI SIKU 21 KABLA YA CAG KUANDAA RIPOTI YA MWISHO sio baada ya ripoti kutoka. Ripoti ikishatoka ni mali ya umma, inajadiliwa na kila mtu. Wabunge wana Haki hiyo pia.
Kwa Mujibu wa Sheria ya Ukaguzi Serikali ilipaswa kuwasilisha Bungeni mpango wa majibu ya hoja za CAG Pamoja (concurrently) na ripoti ya CAG. Serikali haijafanya hilo Kwa hiyo hawana Haki kuwazuia Wabunge kuzungumzia ripoti ya CAG.
Ni aibu kubwa kwamba wakati Umma unamsifia Rais kwa uwazi mkubwa kuhusu ripoti ya CAG, Bungeni, Wawakilishi wa Wananchi wanazuiwa kujadili eti mpaka Novemba!
Wananchi watahisi kuwa Serikali inataka kuficha kitu.
Namna Rais Samia amelishughulikia Suala la CAG report Ndio njia sahihi: Uwazi>Uhuru wa mjadala>Hasira >Hatua>Maelekezo>hatua zaidi zatakiwa!
Bunge lisizuie mjadala. Acha Watu waongelee hoja za CAG. Huo Ndio mchakato wenyewe.