Zitto Kabwe: Kwaheri John Magufuli, Buriani Tingatinga

Zitto Kabwe: Kwaheri John Magufuli, Buriani Tingatinga

Umefanya jambo jema Zitto, hujawa mnafiki wala kumkandia marehemu, umempa sifa zake nzuri na kumkosoa pale alipozingua. Maturity ya hali ya juu

Tundu Lissu ndio my favorite politician lakini ana mapungufu ya kuwa too radical...I hope atabadilika
Nakubaliana na wewe
Tundu Lissu anatakiwa awe na amani na nafsi yake, ili machungu aliyopitia mikononi mwa 'Tingatinga' yasiwe kikwazo katika maisha yake hapa duniani.

Tundu Lissu needs to be at peace with himself now that John Pombe Magufuli is no more. And add the fact that President Madame Samia Suluhu Hassan visited him during his difficult period in a Nairobi Hospital, Tundu Lissu should pray for peace in his heart.
 
Yapo mkuu, kwa Jeikei alikuwa ananufaika huku alifungiwa milango, hawa wanasiasa ni opportunistic sana na sikweli kwamba wanapambania maslahi ya wananchi bali familia zao tu
 
Chuma hakununua ilikuwa ukijipendekeza kwake ili aamini unayoyasema alikuwa anaweka sharti la kuhamia CCM. Hakutaka hadithi na kupigapiga maneno
Kwa hiyo ukijipendekeza kwake anakupokea, anaitia nchi hasara kwa chaguzi za marudio, kisha anakushindisha kinguvu ili kukurudisha kwenye nafasi yako ileile?

Michezo ya kuchezea kodi za wananchi, hana lolote
 
Kwa Heri John Magufuli, Buriani Tingatinga

Zitto Kabwe

Imenichukua karibu wiki nzima kuandika, japo kidogo, kukuaga Rais Magufuli. Unajua kwanini ninapata ugumu kuandika japo napenda sana kuandika tanzia kiasi huwa nawaza nani ataandika tanzia yangu na ataandika nini.

Lakini pia imenichukua uzito kuandika kwa sababu ya kuchoka. Kuchoka sababu ya vifo vingi sana.

Tangu mwaka umeanza vifo vimekuwa vingi sana. Wazee wetu wengi wametangulia mbele ya haki. Mwenyekiti wangu wa Chama Maalim Seif Sharif alitangulia mbele ya haki mwezi mmoja tu kabla yako kutokana na maradhi ya Korona. Tofauti na viongozi wengine, Maalim aliweka wazi maradhi yake na sisi kama chama tulitangaza hadharani hilo ili Watanzania wachukue tahadhari.

Watu ambao nilikuwa nawaona kama Wazee wangu, Walimu wangu na washauri wangu kama Prof. Benno Ndulu walitangulia mbele ya haki wiki chache kabla yako. Nawe pia ulipoteza mtu wako wa karibu katika kazi Balozi John Kijazi mwezi mmoja kabla ya umauti kukufika. Hakika robo ya kwanza ya mwaka 2021 imekuwa mtihani mkubwa kwa nchi yetu. Tumepoteza watu wengi sana, na wengi kutokana na ugonjwa wa COVID-19 yaani Korona.

Nimepata nguvu leo kukuaga Rais kwa sababu licha ya machungu mengi moyoni mwangu nina kumbukumbu nzuri nawe. Nilipopata ajali wakati wa kampeni ulikuwa tayari kutoa kila msaada ili niweze kupona. Ulinipa faraja nikiwa hospitalini Maweni Kigoma na pia Aghakan Dar es Salaam kwa kunipigia simu mara kwa mara kunijulia hali. Ninaamini ulikuwa unaniombea kupona ili kuendelea na kazi zangu ambazo kubwa hasa ni kukukosoa kisera. Hukupenda kukosolewa, lakini pia naamini ulikuwa umeshazoea kupopolewa nasi. Wakati mwengine uliamini nakuchukukia binafsi. Wasaidizi wako walikuwa wanasema. Hapana. Sikukuchukia. Sikukubaliana tu na namna yako ya kuendesha Nchi yetu.

Rais, mara kadhaa niliamua kukushauri ama hadharani au faragha kuhusu masuala mbalimbali ya nchi yetu. Mara nyingi hukuchukua ushauri huo. Haikuwa lazima uchukue ushauri wangu kwani wewe ulikuwa na taarifa nyingi Zaidi kuliko Mtanzania mwengine yeyote. Mara chache ulipochukua ushauri nilifarijika. Kwa mfano ulipokwenda Benki Kuu na kuamua kurejesha akaunti ya madeni Benki Kuu nilikupigia simu kukueleza sio sawa. Utarudisha EPA. Ulinisikiliza kwa makini na siku ya pili ukamwita Gavana Ndulu kubadilisha maamuzi yako. Nilifarijika sana kwani uamuzi wako ulikuwa unairudisha nchi yetu nyuma katika masuala ya usimamizi wa Fedha za Umma.

Rais, umetufunza mengi katika muda ambao umeongoza nchi yetu. Umetufunza uthubutu wa kufanya maamuzi. Umetufunza ujasiri wa kusimamia unachoamini. Hata hivyo umetufunza umuhimu wa Taasisi katika Jamhuri yetu. Miaka Sita ya Uongozi wako imetuonyesha kuwa Mtu mmoja anaweza kufanya lolote atakalo bila kujali lolote. Hili funzo ni lazima tulifanyie kazi ili akitokea Kiongozi mwengine kama wewe asiweze kufanya atakalo. Mara kadhaa ulichukua maamuzi ya kuvunja Katiba yetu. Nilipoamua kwenda mahakamani kukupinga kumwondoa kazini Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na kukushinda katika hatua za awali kwa Mahakama kutoa Uamuzi kuwa Rais anaweza kushtakiwa ukapeleka sheria Bungeni kuwanyima haki Watanzania kukushtaki.
Hii haipaswi kutokea tena Tanzania. Umetufunza.

Rais, ulichukua uongozi wa Nchi yetu demokrasia ikiwa imeshamiri. Demokrasia ndani ya vyama vya Siasa na miongoni mwa vyama vya siasa. Hata ndani ya chama chako kulikuwa na demokrasia kubwa. Miaka Sita ya Uongozi wako hakuna aliyekuwa anaweza kusimama kukupinga ndani ya chama chako. Uliteua unayemtaka hata kama hana historia ya Chama chako. Kwa sisi wa upinzani ulihakikisha tunasagwa. Ulitumia Polisi na Mahakama na baadaye Tume ya Uchaguzi kurudisha nchi kwenye mfumo wa Chama kimoja. Uliona demokrasia ni kero kwako. Hili pia ni funzo kubwa. Kwamba tunapaswa kujenga vyama vyetu kuwa imara kuzuia mambo kama haya kutokea tena. Uhuru haupatikani kwenye kisahani cha fedha, Mwalimu Nyerere alipata kusema. Umetupa funzo kubwa.

Rais, dhamira yako kwa Tanzania siwezi kuishuku. Sikuwahi kuwa na mashaka na mapenzi yako kwa Nchi yetu. Ulitaka Tanzania ipige hatua kubwa za maendeleo japo tulitofautiana kuhusu dhana ya maendeleo ni nini haswa. Kwako wewe miradi mikubwa mikubwa ya Umeme, Madaraja, Reli, Madege, majengo ya vituo vya afya na kadhalika ndio ilikuwa tafsiri ya Maendeleo. Hakika ulijitahidi kujenga Nchi. Kila mtu anakupongeza kwa hilo.

Lakini Rais, hukujitahidi kujenga Taifa. Watakaofuata baada yako hawana budi kujielekeza kujenga Taifa hata kama ni muhimu kumalizia miradi yako ya kujenga Nchi. Bila Taifa lenye watu waliostaarabika, wenye upeo na ujuzi, Nchi haiwezi kudumu. Msingi wa Nchi ni Taifa. Miaka Sita ya wewe kujenga Nchi lazima ifuatwe na miaka Zaidi ya Kumi na Sita ya kujenga Taifa. Taifa ni Watu na Tunu zake.

Tingatinga, John Pombe Magufuli, hatukukubaliana kwenye mambo mengi. Ni kawaida ya wanadamu kutokubaliana. Ni kawaida katika demokrasia kupingana kwa mawazo. Miaka Sita ya Uongozi wako kuna mambo yalitokea Tanzania nisingependa kuyaona yakitokea tena. Watu kupotea hovyo, Wabunge kupigwa risasi hadharani na kutofanyika uchunguzi wowote, kuvunja vunja misingi ya utumishi wa Umma kwa kuteua Wanasiasa katika madaraka ya Utumishi wa Umma, kuvuruga Uchaguzi na kuwanyima haki wananchi kuchagua viongozi wanaowataka, raia kunyanganywa pasipoti zao za kusafiria, watu wasio na hatia kubambikiwa kesi na kukaa gerezani miezi mingi kama sio miaka na hali ya watu kuishi kwa hofu. Kwa kuwa naamini haya yote hayatatokea tena Tanzania baada yako, nimekusamehe duniani na akhera, Fi Dunia, Wal’Akhera!

Rais John Pombe Magufuli, wakati tunakuhifadhi leo katika nyumba yako ya milele kijijini kwako Chato Mkoani Geita, ninakuombea kwa Mungu ailaze roho yako mahala pema. Mungu akupunguzie adhabu ya kaburi. Mungu akusamehe dhambi zako zote. Pumzika kwa Amani.
 
Kaburini hakuna Adhabu.
Kaburi ni kama trash bin/ Dampo la mwili usio na uhai.


Wewe unadhani kaburi linalozungumzwa hapa ni lile shimo inamofukiwa maiti???----- sasa kama kaburi ni hilo shimo vipi kwa wale watu wanaokufa na maiti zao zinasambaratika kabisa mfano kifo cha moto nk, je wao hawatakuwa na adhabu za kaburini??.

Kaburi linalotajwa hapo ni kaburi la roho (Barzakh) ambamo roho ya mtu huifadhiwa kusubiri siku ya kiyama kwa ajili ya hukumu, ndani ya barzakh roho ya mtu huanza kupata rasharasha ya pepo au moto kulingana na matendo uliyofanya ukiwa hapa duniani, hivyo kaburi analoliongelea mh, Zitto ni kaburi la roho.
 
Zitto bana! Kwa Mkwere ulikaa kimya, kwa Magu asee mzee wa kutupa mawe. Ngoja tuone kwa mwenzio Samia....stay tuned!
Tatizo lipo kwako siyo Kwa ZITTO, Hivi Zitto kilichompa umaarufu ni nini..? siyo kuibua hoja mbalimbali zilizowavutia watanzania kuzifuatilia na kumfuatialia Zitto mwenyewe....? Udini, ukanda n.k ni vikinzani vinavyowafanya wengi mshindwe kufikiri kwa ufasaha. Zitto alipata umaarufu mkubwa kipindi cha huyo Mkwere unayemsema maana Zitto Hakuwa mwanasiasa active kipindi cha "Anko" Ben.

Zitto aliingia Bungeni awam sawa na JK, Lakini alikuwa mwiba kwenye serikali ya JK kuliko ya JPM sijui wewe unatumia takwimu za wapi.


Imani zenu zakidini zinawafanya mnashindwa kufikiri vizuri
 
zzk moja kati ya vijana bright na zawadi ya kipekee katika taifa hili.ahsante kwa kutambua mchango chanya wa JPM Rais wa wanyonge
 
Kwa Heri John Magufuli, Buriani Tingatinga

Zitto Kabwe

Imenichukua karibu wiki nzima kuandika, japo kidogo, kukuaga Rais Magufuli. Unajua kwanini ninapata ugumu kuandika japo napenda sana kuandika tanzia kiasi huwa nawaza nani ataandika tanzia yangu na ataandika nini...
Nimekuona mtu mwenye busara sana siyo sawa na Tundu Lissu anayeropoka tu .
 
Kwa Heri John Magufuli, Buriani Tingatinga

Zitto Kabwe

Imenichukua karibu wiki nzima kuandika, japo kidogo, kukuaga Rais Magufuli. Unajua kwanini ninapata ugumu kuandika japo napenda sana kuandika tanzia kiasi huwa nawaza nani ataandika tanzia yangu na ataandika nini....
Binafsi nimekuelewa Mh. Zitto, hata wabaya wana mazuri machache.
 
Mh. Zito hukupunguza wala kuongeza. Kwa kweli utawala wa hayati Magufuli, umetupa funzo kubwa. Umetuonesha katiba yetu ilivyo mbaya. Hayati Magufuli ametuonesha ni namna gani katiba yetu ilivyo hovyo, inavyompa uwezo Rais kujifanyia chochote, kiwe kibaya au kizuri bila kubughudhiwa.

Kama Taifa tukatae mambo yale yaliyotuumiza sana wakati wa utawala wa marehemu, kutokea tena. Katiba yetu irekebishwe haraka. Tusipofanya hivyo, kuna siku atatokea Rais mwingine atakayeitumia vibaya katiba kuzidi hata akivyofanya Magufuli.
 
Kwa Heri John Magufuli, Buriani Tingatinga

Zitto Kabwe

Imenichukua karibu wiki nzima kuandika, japo kidogo, kukuaga Rais Magufuli. Unajua kwanini ninapata ugumu kuandika japo napenda sana kuandika tanzia kiasi huwa nawaza nani ataandika tanzia yangu na ataandika nini...
Amen.
 
Back
Top Bottom