Zitto Kabwe Na Ajenda Yake Moja

Zitto Kabwe Na Ajenda Yake Moja

Tatizo kubwa Zitto akitoka ndani ya siasa ambazo zipo Active ajue atakuwa hana mvuto tena kwa watu hataweza kuona umakini wake na pia uhodari wake, Na kaka yangu Zitto kwa kuwa wewe ni mmoja wa Wana JF sikiliza tukwambie, Ukiacha kugombea ubunge mwaka 2010 sijui itakuaje kwa sasa, Unataka kazi yako umwachie nani?? Huyu jamaa alisema yale ambayo watu wengi sana wamekwambia na hata Kaka Zako na Ndugu zako. Mimi kwa Mtazamo wangu ni kwamba Simama Imara siku zote na Daima simamia hoja yako ukiacha kuwa ndani ya Bunge sijui sauti yako itatoka wapi?? Niliyasema haya sana. Asante sana
 
Zitto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya UMMA. Muulizeni kapokea bahasha ngapi na za kiasi gani toka TANESCO, DAWASA, ATC, PPF,.....

Mkulu, posho kwa wajumbe wa kamati ni haki yao.Na hiyo Zitto aliiweka wazi kabisa alipokuwa akijitambulisha kwenye mkutano na wakuu wa mashirika yote ya umma.

Na hii lilikuwa echoed na wajumbe wote wa kamati ile na hata mzee mkono alikuwepo kwamba wabunge wanastahili kulipwa posho katika vikao vyao vya kamati na mashirika ya umma na posho hiyo itolewe kwa uwazi (transparently).

Sasa kuchukua posho ya mashirika ya umma si hoja,lete hoja nyingine.

Katika umri wake Zitto ni mmoja kati ya viongozi wazuri sana ambao nchi hii imewahi kujaliwa kuwa nao. Mpangilio wa hoja zake,upana wa uelewa wake wa mambo,bidii ya kujifunza na kuvifahamu vitu ni second to none.

Jamani Zitto yuko kwenye level nyingine,tunapaswa kujifunza kutoka kwa watu wa calibre ile na si kuwabeza kwa kupokea posho ambayo kimsingi imehalalishwa si rushwa ile.
 
Haa huo ni ubinafsi kwani lazima mtu ajenge shule au hospitali jimboni kwake?je hamjui Zito kwa uchangiaji wake ameokoa pesa ngapi ambazo amenufaisha taifa zima ili hali huyo Mkono na Lukuvi wananufaisha majimbo yao tu,Watanzania lini tutaacha ubinafsi,nani yuko juu anayetetea masilahi ya taifa na yule anayeangalia jimbo lake tu,kwanza hizo hela za Mkono zina mkono wa ufisadi,kumbuka kesi za benki kuu chini ya rafiki yake Balali kwa siku alikuwa analipwa dola ngapi kutetea uozo.Na je huyo Lukuvi si ni mtu wa mtandao,mbona tunajisahau,ama kweli WATANZANIA NDIO TULIVYO
 
Mimi nataka kaka yangu endelea kugombea mpaka mwisho wake na pia itakuwa raha kwa Taifa lote Tanzania na kuwa ujumla kama Taifa
 
Nakumbuka alitaka kuisaidia TANESCO kununua mitambo chakavu ya DOWANS/RICHMOND? Akaona ni heri DAWASCO ifutwe ili ibaki DAWASA ambayo ni mfuko wa nyuma wa suruali za wanasiasa!

Zitto kama mwenyekiti wa kamati ya fedha ya mashirika ya umma amekuwa akiangalia namna ya kuyasaidia mashirika ya umma ili yaweze kujiendesha kwa ufanisi.Kwahiyo amekuwa akichukua maoni mbali mbali kutoka kwa mashirika na kusaidia kuyafikisha kwa serikali ili iweze kuyatekeleze na hivyo kuyaimarisha mashirika haya.

Suala la Mitambo chakavu inaweza kuwa alikuwamisled na Menejimenti ya TANESCO lakini sijasoma mahali popote kwamba kamati ilipendekeza kufutwa kwa DAWASCO au DAWASA.Kama alitaka kufanya hivyo ni soo lakini labda aliona kuna umuhimu wa kufanya hivyo.

Mambo mengine ni policy issues ambazo Zitto anaweza tu kuyasemea bungeni,na kama angeyasema hayo bungeni nafikiri yangekuwako katika hansard na isingekuwa siri yako tu wewe Wildcard!
 
Mimi hizi porojo za Zitto hazina maana kwangu, siku zote mazuri hujitenga, na watu kuyashuhudia sio kumwaga misifa mingi kama robot.Ningekuona wa maana kama ungetoa thatmini ya mafanikio jimboni mwake k.v. mashule, hosipitali, maji, barabara.Wanaotakiwa kuhusishwa na mafanikio directly ni watu wa jimbo lake.huwezi kuanza kutetea watu milion 30 + huku kwako bado kuna matatizo...naomba kuwasilisha hoja
 
JIMBONI KWAKE KAJENGA SHULE NGAPI?MAJI,VITUO VYA AFYA N.K naomba Mwandishi wa Zitto aende jimbo la MKONO au kwa LUKUVI ISMANI-IRINGA.

kwani zito ndio anatakiwa kujenga shule na hela zake za mfukoni????

mkono!!!! hizo hela za bot za kesi za uongo ndio zinakufanya uongeeeee
 
Haa huo ni ubinafsi kwani lazima mtu ajenge shule au hospitali jimboni kwake?je hamjui Zito kwa uchangiaji wake ameokoa pesa ngapi ambazo amenufaisha taifa zima ili hali huyo Mkono na Lukuvi wananufaisha majimbo yao tu,Watanzania lini tutaacha ubinafsi,nani yuko juu anayetetea masilahi ya taifa na yule anayeangalia jimbo lake tu,kwanza hizo hela za Mkono zina mkono wa ufisadi,kumbuka kesi za benki kuu chini ya rafiki yake Balali kwa siku alikuwa analipwa dola ngapi kutetea uozo.Na je huyo Lukuvi si ni mtu wa mtandao,mbona tunajisahau,ama kweli WATANZANIA NDIO TULIVYO

Sera ya majimbo ni ya Chadema sasa kama naibu katibu mkuu anashindwa kusimamia sera yake ni kichekesho.
lakini Kumbuka kuwa wananchi wa MWANDINGA ndio waliomchagua kwa mkataba wa kuwatumikia,hiyo ndiyo kazi yake ya kwanza.Mahitaji ya jimboni yanatakiwa kutatuliwa na mbunge wao kama shule,maji na afya.kama Lukuvi sio mtandao alikuwa kwa Sumaye.

Zitto ana source nyingi za kupata pesa yeye ni mshauri wa Rais wa Ujerumani anashindwa kumuomba rais wa Ujerumani amjengee shule?

Zitto sio mbunge wa Taifa ni wa Mwandiga na pia hoja kama Buzwagi imechukua muda gani kiasi ashindwe kuwatumikia watu wake?Slaa anatoa hoja za kitaifa lakini jimboni kwake kaimarisha vitu vingi acha kumpotosha Zitto na kumfanya msaliti kwa watu wake, mimi na wewe tusingemjua bila watu wa Mwandiga,tuwatendee haki watu wake tuache ubinafsi.

Mwenyekiti wa Chadema ameimarisha jimbo lake la Hai,Katibu Mkuu ameimarisha KARATU, vipi umdanganye Naibu Katibu mkuu kuwa yeye ni mtu wa Taifa na si jimbo lake la uchaguzi? issue ya BUZWAGI aliisema siku moja tu bungeni,siku zilizobaki awatumikie watu wake ambao sisi sote tuna deni nao kwa kutuletea mwanasiasa mahiri kama Zitto.
 
kwani zito ndio anatakiwa kujenga shule na hela zake za mfukoni????

mkono!!!! hizo hela za bot za kesi za uongo ndio zinakufanya uongeeeee

Kwanini tusimuulize Slaa kajenga shule nyingi jimboni kwake kwa pesa zipi?acheni kumpotosha Zitto akapoteza mwelekeo. Zitto ana connection nyingi hashindwi kujenga shule wala zahanati.

Mkono ni mfano mmoja wa watu wanaopenda maendeleo,kwani LIYUMBA kawafanyia nini watu wake kwa pesa za BOT? SLAA anajua ana deni na watu wake hivyo anafanya kila linalowezekana kuwapelekea maendeleo,hajibweteki na vilemba vya ukoka kama hivi mnavyomvisha ZITTO ILI AJISAHAU JIMBONI kwake.
 
JIMBONI KWAKE KAJENGA SHULE NGAPI?MAJI,VITUO VYA AFYA N.K naomba Mwandishi wa Zitto aende jimbo la MKONO au kwa LUKUVI ISMANI-IRINGA.

Kazi ya mbunge sio kujenga shule, vituo vya afya etc.
 
Mimi hizi porojo za Zitto hazina maana kwangu, siku zote mazuri hujitenga, na watu kuyashuhudia sio kumwaga misifa mingi kama robot.Ningekuona wa maana kama ungetoa thatmini ya mafanikio jimboni mwake k.v. mashule, hosipitali, maji, barabara.Wanaotakiwa kuhusishwa na mafanikio directly ni watu wa jimbo lake.huwezi kuanza kutetea watu milion 30 + huku kwako bado kuna matatizo...naomba kuwasilisha hoja

Karibu kwa Mchango wako wa kwanza wenye ujumbe mzito kuliko michango elfu moja ya baadhi ya wana JF humu.

Zitto aliingia mkataba wa kuwatumikia watu wake na hajafanya hilo,anasema hivi sasa anamiliki magari matano ndani ya miaka mitatu ya bungeni, chanzo chake ni watu wa Mwandiga waliompa ile fursa ya yeye kuwa Mbunge na kupata marupurupu hayo. sio sisi JF tuliompa nafasi hiyo.bahati mbaya wachangiaji wengine hapa wana roho mbaya na kuwachukia watu wa Mwandiga wasipelekewe maendeleo na mbunge wao.

Basil Mramba amejenga shule 32 jimboni mwake na mbili za ghorofa kwa msaada wa Waarabu, Yona pamoja na nafasi zote hajafanya kitu kwao.Anna Kilango anapiga vita ufisadi lakini hasahau watu wake wa SAME MASHARIKI kuwapelekea maendeleo.

DR.Salim Ahmed Salim analaumiwa na watu wake kwa kutokupeleka maendeleo kwao.wema huanzia nyumbani,Lwakatare kwa nafasi ya ubunge wa bukoba mjini miaka mitano iliyopita amewafanyia mambo mengi watu wake.kwanini Zitto tumdanganye kuwa ni kamanda wa nchi?
 
Kazi ya mbunge sio kujenga shule, vituo vya afya etc.

Mbona Slaa anajenga shule na zahanati?watu wa Mwandiga hakuna aliye na exposure kama ya Zitto,asipofanya Zitto nani atafanya? Karatu kuna wasomi wengi lakini Slaa bado yuko mstari wa mbele kutimiza wajibu wake wa kujenga mashule n.k

acha wivu kwani watu wa Mwandiga wamewakosea nini?ukimsomesha mtoto akapata kazi na akajimudu kimaisha,halafu akawa anaenda kuwasaidia watu wa mbali na kumwacha mzazi wake itakuwa sawa? Seif Shariff Hamad anathamimiwa na watu wake wa PEMBA kwa kuwapelekea maendeleo alipokuwa muwakilishi wao hiyo ndiyo siri yake.

kama Zitto atajisahau kwa kuwasikiliza nyinyi basi huko mbele atakuja kuijutia nafsi yake kama anavyokosa raha DR.SALIM mbele ya wapemba wenzake.
 
kanda2,

..mimi na wewe tumebishana sana ktk mijadala mingine lakini ktk hili la kuwashinikiza wabunge kufanya kazi ya kupeleka maendeleo majimboni kwao niko na wewe 100%.

..binafsi mbunge akiendeleza jimbo lake anatusaidia Watanzania wote.

..Zitto akiweza kuhamasisha ujenzi wa shule zenye viwango jimboni kwake ina maana mimi jokaKuu nikitupwa transfer kwenda Kigoma sitakuwa na wasiwasi wanangu watasoma wapi.

..Benki wa wananchi wa Mwanga, iliyoanzishwa kwa juhudi za CD Msuya na wananchi wenzake, ikistawi na kujitanua, Watanzania wote tutaweza kupata mikopo huko.

..kama Zitto atakuwa amejikita ktk masuala ya kitaifa tu, na kusahau kuhamasisha maendeleo jimboni kwake, basi atakuwa amewaangusha wananchi waliomchagua.
 
kanda2,

..mimi na wewe tumebishana sana ktk mijadala mingine lakini ktk hili la kuwashinikiza wabunge kufanya kazi ya kupeleka maendeleo majimboni kwao niko na wewe 100%.

..binafsi mbunge akiendeleza jimbo lake anatusaidia Watanzania wote.

..Zitto akiweza kuhamasisha ujenzi wa shule zenye viwango jimboni kwake ina maana mimi jokaKuu nikitupwa transfer kwenda Kigoma sitakuwa na wasiwasi wanangu watasoma wapi.

..Benki wa wananchi wa Mwanga, iliyoanzishwa kwa juhudi za CD Msuya na wananchi wenzake, ikistawi na kujitanua, Watanzania wote tutaweza kupata mikopo huko.

..kama Zitto atakuwa amejikita ktk masuala ya kitaifa tu, na kusahau kuhamasisha maendeleo jimboni kwake, basi atakuwa amewaangusha wananchi waliomchagua.

Rombo kila kata ina shule za sekondari nne,Mwanga asipofanya Msuya atakuja Maghembe,Daniel Yona.Asha Rose Migiro,Mgonja,Mtoto wa Msuya Mathayo David,Prof Maghembe na wengi sana.

lakini alikotoka Zitto akitoka yeye anaweza kuja mbunge mwingine KANDA2 elimu yake darasa la saba na hana exposure,connection n,k anaweza kuwa na nia nzuri ya kuwaendeleza watu wake lakini hana resource,hana connection nani anamjua wa kumsaidia?

Zitto Kabwe ni kama kasomeshwa na kijiji ili aende kuwakomboa kwa kuwaletea maendeleo watu wake,afanye utaratibu wa kujua NDESAMBURO kafanya nini jimboni kwake Moshi mjini?amepeleka vitu vingi sana,Augustine Mrema ndiye alikuwa msemaji wa issue za kitaifa au kulipua mabomu kama Zitto,lakini pamoja na hayo amefanya mambo mengi ya msingi kwa watu wa jimbo lake kiasi ya kwamba akiomba ubunge anapewa aliwainua kwenye zao la kahawa na kujenga mabarabara.

Ukienda jimbo la Mufindi utaona kazi nzuri ya mbunge wao Mungai,inatakiwa watu wa jimbo la Zitto wawe wa kwanza kunufaida na jasho la mtoto wao,kwani mabomu bungeni wako wengi wa kulipua akimpa Slaa atalilipua,Selelii atalilipua,Anna Kilango analilipua,akilileta hapa JF tutalilipua,lakini asipokwenda kusaidia watu wake jimboni hakuna Mwanajf au Seleli anaweza kwenda kumwakilisha jimboni kwake.

Zinduka Zitto achana na hawa wapambe nuksi wasiokutakia mema wala jimbo lako. Wapemba waliofanikiwa kielimu ni nguvu za Seif Shariff huko nyuma, SEIF aliwahi kuwatengenezea connection ya skolaships kwa watu wake kwenda nje ya nchi kusoma.

waziri mkuu Pinda pamoja na kuwa waziri mkuu wa TAIFA kila kukicha yuko Sumbawanga.
 
Mkulu, posho kwa wajumbe wa kamati ni haki yao.Na hiyo Zitto aliiweka wazi kabisa alipokuwa akijitambulisha kwenye mkutano na wakuu wa mashirika yote ya umma.

Na hii lilikuwa echoed na wajumbe wote wa kamati ile na hata mzee mkono alikuwepo kwamba wabunge wanastahili kulipwa posho katika vikao vyao vya kamati na mashirika ya umma na posho hiyo itolewe kwa uwazi (transparently).

Sasa kuchukua posho ya mashirika ya umma si hoja,lete hoja nyingine.

Katika umri wake Zitto ni mmoja kati ya viongozi wazuri sana ambao nchi hii imewahi kujaliwa kuwa nao. Mpangilio wa hoja zake,upana wa uelewa wake wa mambo,bidii ya kujifunza na kuvifahamu vitu ni second to none.

Jamani Zitto yuko kwenye level nyingine,tunapaswa kujifunza kutoka kwa watu wa calibre ile na si kuwabeza kwa kupokea posho ambayo kimsingi imehalalishwa si rushwa ile.
Mkuu,
Tunatofautiana kwenye uelewa wa mambo haya. Kamati hii posho yake inalipwa na Ofisi ya Bunge tu na sio Mashirika ya UMMA inayoyasimamia na kuangalia utendaji wake. Kama, kwa mfano, bahasha ya Zitto toka TANESCO ina milioni 5, unategemea ataikosoa nini menejimenti ya Dr Rashid? Bahasha hizi ni rushwa ya wazi. Na ndio maana mashirika haya yanaendelea kufa. Hayana usimamizi kuanzia kwa CAG, Kamati ya Bunge hadi Bodi za Wakurugenzi. Zito yuko level gani? Taarifa kama za Buzwagi zimebadilisha nini kwenye mkataba ule? Taarifa anazokomaa nazo anapelekewa na Watanzania kama mimi na wewe. Au ndio kama yale niliyoyasikia Bungeni juzi, mbwa anamjua anayempa chakula hamjui aliyekitafuta!
 
Masanilo.

HUU NDIO USHAURI WANGU KWA ZITTO. PIA TIZAMA NA ULE MJADALA WA ZITTO HATAGOMBEA 2010 NILIVYOMSHAURI KWA NIA SAFI KWA WATU WAKE WA MWANDIGA.
 
Zitto Ni Kichwa labda ameona bunge ni usanii m2pu ndo maana hataki kugombea tena. Namshauri agombee U-rais
 
zitto ni mfano wa kuigwa kwa yale muhimu aliyoyafanya mpaka sasa kama alivyoelezewaa na mwandishi..

demokrasia yetu inahiyaji kukua na chachu ya uongozi wa aina ya zitto ni wa kuigwa hasa na vijana wanaotamani mabadiliko katika taifa lao..obama ametukumbusha akiwa Ghana..ulimwengu ni ule tunaoutaka...

changamoto anazokumbana nazo ni za kawaida tuu na ili tusonge mbele tunahitaji utajiri wa mawazo wenye kukosoana ili kusonga mbele..

zitto kuuunga mkono dowans haikuwa kosa kwani alikuwa na hoja za msingi na sio kupewa chochote na wamiliki wake..

Big up zitto and never give up...tupo nyuma yakoooo
 
JIMBONI KWAKE KAJENGA SHULE NGAPI?MAJI,VITUO VYA AFYA N.K naomba Mwandishi wa Zitto aende jimbo la MKONO au kwa LUKUVI ISMANI-IRINGA.

Mkuu umetoka nje ya hoja. Kuna baadhi ya wabunge ni kweli wametoa hela zao za mfukoni kujenga shule au zahanati. Lakini ni wangapi? Huyu Lukuvi kajenga shule kwa hela zake? Maana tuache ushabiki. HELA ZITUMIKE ZA SERIAKLI TUKUSIFU WEWE MBUNGE KUWA UMEJENGA? NO WAY LABDA KUWA UMEPIGA KELELE. Lakini pia hii inadibi tuwaachie wananchi wa Kigoma kaskazini kwani wao ndiyo wanajua vipaumbele vyao vilikuwa nini. Na yeye aliahidi nini.

Tumesikia WAZIRI MKUU AKISEMA ZITTO ANAJISIFU KUWA AMELETA MAENDELEO, AKASEMA BARABARA ZIMEJENGWA NA CCM WHICH IS NOT TRUE KWANI CCM HAWAJATOA HATA CENT YAO MOJA
 
Back
Top Bottom