Pre GE2025 Zitto Kabwe: NEC na Uhalali wa Kisheria Dhidi ya Uhalali wa Kisiasa

Pre GE2025 Zitto Kabwe: NEC na Uhalali wa Kisheria Dhidi ya Uhalali wa Kisiasa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2014
Posts
631
Reaction score
1,577
UHALALI KISHERIA v UHALALI KISIASA

#NECijiuzulu #INECiingie

Kuanzia keshokutwa tarehe 12 April 2024 Sheria Mpya ya Tume Huru ya Uchaguzi inaanza kutumika kwa mujibu wa GN no. 225 ya 29 Machi, 2024.

Endapo masharti ya Kifungu cha 5 cha Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ya Mwaka 2024 hakitafuatwa basi, hatutakuwa na tume iliyo ofisini, kwa sababu Tume ni Makamishina na Mwenyekiti wao.

Kujibanza kwenye kifungu cha 27 cha Sheria mpya hakuna mantiki yeyote. Najua wengi, kwa bahati mbaya hata wana mageuzi wa muda mrefu, wamelalia kwenye hoja hii dhaifu kuhalalisha Tume ya sasa kuendelea. Watu wanaowaza hivi wangekuwa Afrika Kusini wangemwacha Mandela afie jela kwa sababu apartheid ilikuwa halali kisheria, lakini apartheid HAIKUWA HAKI wala halali kisiasa.

@TumeYaUchaguzi ya sasa ikibakia ofisini baada ya tarehe 12/4/2024 itakuwapo kisheria lakini HAITAKUWA NA UHALALI WA KISIASA. Mchakato wa uchaguzi ni mchakato wa kisiasa tena wenye misingi ya TRUST.

Tunataka #NECijiuzulu ili #INECiingie

Zitto Kabwe
Mzee mstaafu wa Mwandiga
 
UHALALI KISHERIA v UHALALI KISIASA

#NECijiuzulu #INECiingie

Kuanzia keshokutwa tarehe 12 April 2024 Sheria Mpya ya Tume Huru ya Uchaguzi inaanza kutumika kwa mujibu wa GN no. 225 ya 29 Machi, 2024.

Endapo masharti ya Kifungu cha 5 cha Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ya Mwaka 2024 hakitafuatwa basi, hatutakuwa na tume iliyo ofisini, kwa sababu Tume ni Makamishina na Mwenyekiti wao.

Kujibanza kwenye kifungu cha 27 cha Sheria mpya hakuna mantiki yeyote. Najua wengi, kwa bahati mbaya hata wana mageuzi wa muda mrefu, wamelalia kwenye hoja hii dhaifu kuhalalisha Tume ya sasa kuendelea. Watu wanaowaza hivi wangekuwa Afrika Kusini wangemwacha Mandela afie jela kwa sababu apartheid ilikuwa halali kisheria, lakini apartheid HAIKUWA HAKI wala halali kisiasa.

@TumeYaUchaguzi ya sasa ikibakia ofisini baada ya tarehe 12/4/2024 itakuwapo kisheria lakini HAITAKUWA NA UHALALI WA KISIASA. Mchakato wa uchaguzi ni mchakato wa kisiasa tena wenye misingi ya TRUST.

Tunataka #NECijiuzulu ili #INECiingie

Zitto Kabwe
Mzee mstaafu wa Mwandiga
Je kwenye tume hiyo watumishi wote watakuwa wana ccm tu au watachukuliwa kutoka vyama mbali mbali vya siasa na makundi mbali mbali ya watu?
 
Mandela lazima kageuka kaburini mwake.

Apunguziwe adhabu hiyo kaburini. Amen

...ngoja tuone hawa wapingaji wa Tume hii, Je, Watapambana 2025? Je, Watakataa matokeo hata pale watakapochaguliwa eti kwa sababu kuna watu "wamejibanza"?

Kweli Siasa sio Sheria! whatever that means
 
Back
Top Bottom