Zitto Kabwe ni mpinzani halisi mwenye contents. Tatizo wapinzani wanapingana

Zitto Kabwe ni mpinzani halisi mwenye contents. Tatizo wapinzani wanapingana

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
NIlipata wasaa wa kumsikiliza Zitto kwenye mkutano wa hadhara kwanza wa ACT Wazalendo 2023 pale uwanja wa Zakhem Mbagala.

Niseme kwa kukiri kwamba, kiongozi huyu ambaye ameanzia na kukulia Upinzani ana viwango vyote sahihi vya kuitwa mwanasiasa mwenye hoja. Katika kuunda hoja na kuzijengea misingi yake anatumia msingi wa facts ambazo kwa vyovyote anazitafiti kwanza.

Inawezekana kibinadamu ana mapungufu yake lakini kimantiki na kisiasa yupo mbali sana na wanasiasa wakongwe kama Freeman Mbowe na wengineo. Huyu kijana anaweza kuvaa viatu vya Dkt. Slaa kwenye mizania ya siasa nchini.

Nilikuwa namuona John Mnyika ambaye sasa amepanda na kuwa katibu Mkuu CHADEMA kuweza kuwa na nyota kali ya kisiasa lakini mi ukweli usiopingika namna Zitto Zuberi Kabwe ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja na kuweza kushawishi wasikilizaji kwa mbali sana.

Ni wito wangu wazee waliomzunguka chini ya Mzee Duni Hajji kuendelea kumjenga Zitto ili aweze kujenga jukwaa la wanasiasa mahiri wenye fikra chanya mbadala za kujenga nchi yetu.
 
kabwela zito ni fala tu. Na katika wanasiasa wenye mwisho mbaya mbaya mbaya yupo top 5. Tungoje
 
Kweli wewe ni msanii maana zitto ni msanii pia ,wasanii mmefahamiana

USSR
 
Ni kweli anajua kujenga hoja na ni mastermind mzuri Sana wa kuficha ukweli ndani ya hoja , Kwa vile tuna kundi kubwa la wajinga ni rahsi watu hao kumwamini
 
Na mm ndiyo nashangaa. Walifanya lini huo mkutano? Mbona wamefanya kimya kimya wananchi hatujaambiwa?
Wabongo mnajua sana kusagia kunguni.

Wanancho walijaa sana kwenye mkutano ule.

Nilipita eneo lile nikakuta watu wengi pale nilipofika home nikawasha itv kuufuatilia
 
Ni kweli anajua kujenga hoja na ni mastermind mzuri Sana wa kuficha ukweli ndani ya hoja , Kwa vile tuna kundi kubwa la wajinga ni rahsi watu hao kumwamini
Wapinzani wanapingana
 
Dr Mollel anastahili PhD ya heshima kwa kweli.
 
Wanasiasa wa Kigoma ni mtihani!
Ref; marehemu Kabulu.....
Ni biskuti ya chuma kwa maneno na appearance inapendeza lakiní haitafuniki!
 
Back
Top Bottom