Zitto Kabwe, Pemba sio Kigoma

Zitto Kabwe, Pemba sio Kigoma

Moja kati ya nyuzi za kijima sana kuwahi kuzisoma humu; hivi hayati Maalimu Seif anaweza kua na ushawishi Kigoma au hata Tabora?

Ieleweke kila mtu ana ngome yake, Maalimu alikua anakubalika Pemba na baadhi ya wana Unguja, hilo wala halina mjadara but the same Maalimu Seif hakua na ushawishi wowote bara; miaka yake yote akiwa katibu mkuu CUF, lini CUF imewahi kupata wabunge wa kuchaguliwa walau 5?

Hao wa term ya mwisho ya Kikwete walipatikana kwasababu ya ushawishi wa Chadema/UKAWA. Sioni ni kwanini umeamua kutengeneza uzi wa kumwambia Zitto kuhusu Zanzibar/Pemba ilihali kijana wa watu ni MUHA wa Kigoma.
 
Najaribu kuwaza kitu gani kimekufanya uandike hii post katikati ya majonzi mengi. Umeshindwa kabisa kuficha chuki yako dhidi ya Zito? kweli mtihani huu.
Chuki tu za KIJINGA tu; badala ya kufikiria mbadala wa maalimu Seif mtu anaanzisha tu chuki zake kwa mtu ambaye wala sio Mpemba
 
Najaribu kuwaza kitu gani kimekufanya uandike hii post katikati ya majonzi mengi. Umeshindwa kabisa kuficha chuki yako dhidi ya Zito? kweli mtihani huu.
Hata mimi sijamuelewa anataka kumwambia nini Zito?
 
Inaonekana kabisa hamjui siasa na Wala hamfuatilii zbar Kuna mtu anaitwa Jusa Salim,na mwingine Juma khaji duni mnawajua hao? Vichwa Sana kuhusu zito Bado Yuko relini hacha wivu wa kumchimbia shimo wakati kila mtu hatobaki Kama alivyo usimnyooshee zito vidole jinyooshee wewe Kwanza you will not stay forever as you are.
 
Ni mda Sasa vichwa bora kuwai tokea TOKA mfumo wa vyama vingi tz, nazungumzia kutoka chama bora tz CHADEMA, kufanya Jambo makini ili roho za watanzania wenzetu wazanzibar, ziweze kutulia, tafuta vichwa makini TOKA pemba na Zanzibar KWA ujumla mfanye Jambo ili kumuenzi vizuri mh seif (RIP)
 
Upo sahihi kabisa na sasa naiona ACT ile tulio izoea inajirudia kwenye ngozi yake halisi.
Maalim seif akiringia rasilimali watu na hicho ndio kikuu katika mustakbali wa kisiasa kule zanzibar na bara, kama zilitumika dakika 6 wananchi kumfuata ACT kwanini zisitumike ata dakika 10 wananchi kuunga mkono viongozi waliobaki??

Wazanzibar wanahitaji mabadiliko kwa vyovyote iwavyo leo na kesho, usiandikie mate ni suala la muda tu, utajaiyona kasi ya ajabu.
 
Jana tumeshuhudia maziko ya Mwanasiasa mkongwe yaliyofanyika huko Pemba Zanzibar kijijini Nyali Mtambwe na kuona jinsi wananchi wa huko walivyokuwa na simanzi nzito mithili ya kuwa wameondokewa na mfalme wao. Na wengi walionekana kama kuwa sasa ndio basi tena hakuna wa kuja kuwapigania. Maana nilisikia baadhi ya watu wakizuiwa kulia ili wasije kukufuru.

Ni wazi kuwa kwa wapemba Maalim Seif wao walimchukulia kama mkombozi, hata kama angerudi CCM basi Pemba ingerudi kuwa ngome ya CCM.

Sasa ameondoka, hivi kwa akili ya kawaida Zitto anaweza kuwa na ushawishi huko Pemba kiasi cha kutuliza mizuka ya Wapemba?

Pemba tunaiijua tangu mwaka 1995 ulipofanyika uchaguzi mkuu wa vyama vingi ni Maalim Seif alikuwa akituliza hasira za Wapemba ambao kwao wanaona kama wanakandamizwa kwa kila namna.

Tusisahau kuwa hata hata baada ya uchaguzi wa 2000 na machafuko makubwa kutokea ni ushawishi wa Maalim uliosababisha kupatikana kwa muafaka wa kisiasa. Hata maridhiano ya kisiasa yaliyopelekea kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa huko Zanzibar ni sababu Maalim Seif alitumia ushawishi wake kupoza joto Pemba.

Zitto baada ya kuona mambo magumu huku bara ulikuwa unatembelea mgongo wa Maalim Seif huko Pemba. Na unatakiwa kujua Wapemba sio kondoo kama jamaa zako. Huu ndio mwisho wa janja zako.
Pumzika kwa amani baba yetu,babu yetu mola akupokee katika mwanga wa milele amina
 
Back
Top Bottom