Zitto Kabwe: Tangu lini Rais anaheshimu Bunge? Kosa la Lugola ni kufanya dili kwa kumzunguka Rais, hoja ya Bunge ni kisingizio tu

Zitto Kabwe: Tangu lini Rais anaheshimu Bunge? Kosa la Lugola ni kufanya dili kwa kumzunguka Rais, hoja ya Bunge ni kisingizio tu

Sub imefanyika pale katoka Ukimwi anaingia Ebola......"come pain",GE by October ni'mnyuko!!!!
Rais Magufuli anasema Kangi Lugola na wenzake wamesaini Mkataba bila ruhusa ya Bunge. Hii ndio standard? Mkataba Gani? Mbona kama hiyo ndio standard wengi hawapaswi kuwepo ofisini hata yeye mwenyewe.

Ujenzi wa Chato Airport Shs 69 bilioni haukupitishwa na BUNGE

Ununuzi wa Helkopta 13 USD 200m za kumlinda yeye Rais haukupitishwa na Bunge

Mkataba wa SGR haukupitishwa na Bunge, Shs 5 Trilioni

Mkataba wa passport mpya haukupitishwa na BUNGE, shs 230 bilioni

Ununuzi wa ndege haukupitishwa na BUNGE, 1.5 Trilioni. Juzi Serikali imesaini Mkataba na Boeing kununua ndege ya pili ya Dreamliner kwa Mkopo ( lease purchase) BILA RUHUSA YA BUNGE wala huo mkopo haumo kwenye mikopo iliyoruhusiwa na BUNGE

Mkataba wa Barrick haukupitishwa na BUNGE

Rais aliidhinisha Fedha Shs 600 bilioni kutoka Benki Kuu ili kununua Korosho zilizoleta hasara ya USD 500m ( Shs 1.2 Trilioni) bila idhini ya Bunge.

Tangu lini Rais anaheshimu Bunge?

Kuna jambo. SIO HILI AMESEMA Rais. Najua kosa la Kangi kafanya Dili kwa kumzunguka Rais. Rais amekasirika. Rafiki yangu Kangi hakujua kuwa hakuna DILI nchini bila mkono wa Rais. Hoja ya BUNGE ni kisingizio tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabla ya kuliangazia hili, tufahamu wigo Wa majukumu ya waziri Wa mambo ya ndani na mamlaka ya raisi na uraisi kama kiongozi Mkuu Wa nchi.
Hata uugeuzegeuze vipi huo urais...; palipo na taratibu na sheria ni shurti taratibu na sheria zifuatwe na yeyote, hata yeye na taasisi yake.

Kama taratibu na sheria hazifai, kuna pia 'taratibu' na kanuni zinazotakiwa kufuatwa kuzibadili ili ziendane na hayo wanayoyataka wao.

Haiwezekani nchi ikaendeshwa kwa mihemko ya kucha na kuchwa na mtu au hiyo mnayoiita taasisi.
 
na wewe rudi shule tena darasa la 3 B.

Maamuzi ya ki inchi hayatekelezwi na bunge..kazi za bunge ni kutunga sheria na kuishauri serikali..Rais ana Mandet ya kuchukua maamuzi bila kuishirikisha muhimili wowote na hata mbwiga yoyote kama wewe na bwana wako zzk
 
Rais ni taasisi na Waziri ni mtu. Zitto anakurupuka!
Wewe ndio unakurupuka unadhania walioweka utaratibu wa kuendesha nchi kwa bajeti inayopitishwa na bunge hawakuwa na akili??kwenye awamu hii ni mambo mangapi yameibuka tu bila kupitia bungeni?hiyo taasisi ya uraisi ambayo inapanga bajeti tu itakuwa ya kwanza duniani!!!!
 
Achani ujinga wa kupewa matango pori na huyo zito wenu.Maamuzi ya ki inchi hayatekelezwi na bunge..kazi za bunge ni kutunga sheria na kuishauri serikali..Rais ana Mandet ya kuchukua maamuzi bila kuishirikisha muhimili wowote na hata mbwiga yoyote kama wewe na bwana wako zzk
wacha kuandika ugoro, weka kifungu hapa kinachosema rais ana uwezo wa kufanya kinyume na bajeti iliyopitishwa na bunge.
 
Achani ujinga wa kupewa matango pori na huyo zito wenu.Maamuzi ya ki inchi hayatekelezwi na bunge..kazi za bunge ni kutunga sheria na kuishauri serikali..Rais ana Mandet ya kuchukua maamuzi bila kuishirikisha muhimili wowote na hata mbwiga yoyote kama wewe na bwana wako zzk
Rudi darasani!!kwenye mambo ya fedha rais anaweza akatumia kiasi fulani cha bajeti endapo tu kuna mambo fulani ya dharura na kuna utaritibu umewekwa wa kuufuata!!ili kuitumia hiyo pesa lakini kwa kuwa nchi ina MBWIGA kama wewe kwa asilimia 99.9 mambo yanaonekana ya kawaida tu angalia wenye akili zao huko USA hata wenzake na trump chama kimoja wamemkalia kooni!!bunge linakzai kuu mbili tu hiyo ya kuishauri serikali ni minor!!!
 
Zitto unachosahau, Baba kwenye familia huwa hakosei, na akikosea anazonjia zAke za kumwambia...

Hicho anachokisemA akasome vzr katiba ya nchi,juu ya majukum ya rais kwa manufaa ya Uma..

Sio swala kukiuka kanuni,ila kutekelezA kwa manufaa ya uma...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rudi darasani!!kwenye mambo ya fedha rais anaweza akatumia kiasi fulani cha bajeti endapo tu kuna mambo fulani ya dharura na kuna utaritibu umewekwa wa kuufuata!!ili kuitumia hiyo pesa lakini kwa kuwa nchi ina MBWIGA kama wewe kwa asilimia 99.9 mambo yanaonekana ya kawaida tu angalia wenye akili zao huko USA hata wenzake na trump chama kimoja wamemkalia kooni!!bunge linakzai kuu mbili tu hiyo ya kuishauri serikali ni minor!!!
Si nimekwambia akili yako inafanana na ujinga wako.dharura ni nini.
Jambo lingine ambalo watu kama we we unafanya ulinganisho wa USA Na Tz MNA akili nyinyi?Na usomi wako wa kuunga unga unakaa kusubiri matokeo ya Uzito wa sungura Na tembo..kweli wewe ni Timamu
 
S
Si nimekwambia akili yako inafanana na ujinga wako.dharura ni nini.
Jambo lingine ambalo watu kama we we unafanya ulinganisho wa USA Na Tz MNA akili nyinyi?Na usomi wako wa kuunga unga unakaa kusubiri matokeo ya Uzito wa sungura Na tembo..kweli wewe ni Timamu
siwezi bishana na mtu ambaye upo malinyi lakini akili yako inashikiliwa lumumba(praise team)
 
Kikatiba Tanzania rais yuko juu ya sheria yani yeye hana hatia kwa lolote atakalofanya
Kwahiyo hata msipanic Kangi kazingua acha ashughulikiwe kwa sababu hana mamlaka aliyonayo raisi ya kuamua anachotaka na akakifanya bila kuulizwa
Upinzinzani wangejielewa wangepambana kwa namna zote kuhakikisha katiba inapatikana
Na kutoa elimu ya uraia kwa raia hata kwa vipeperushi


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom