Raphael Alloyce
Senior Member
- Nov 15, 2020
- 128
- 372
Ila Zitto! 😁😁😁Wakuu,
Baada ya purukushani na kuwepo kwa vitendo vya wizi na udanganyifu kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kiongozi mstaafu wa ACT Wazalendo amewahimiza wananchi kususia na kugomea viongozi wa Serikali za Mitaa waliochaguliwa
Zitto amesema kuwa hakuna haja ya wananchi kuzipa imani serikali na viongozi walioingia kwenye madaraka kwa njia ya udanganyifu.
============================================
Na hii ndo approach nzuri. Hamna kususia uchaguzi lakini unasusia viongozi waliochaguliwa. CHADEMA mjifunze hapa
View attachment 3165324
Napata wasiwasi kama Kiongozi Mstaafu wa #ACT-Wazalendo, Kaka Zitto Kabwe, kweli anajua majukumu ya viongozi hao kwenye jamii na changamoto zinazowakumba jamii kila siku zinazohitajika kutatuliwa na viongozi hao kila siku. Kuhamasisha wananchi kususia huduma za kijamii ni kama kumshauri mtu aache kula wakati wote akijua njaa haina huruma wala subira. Je, unafahamu kwamba huduma hizi za msingi mara nyingi ndizo tegemeo kuu la wananchi wa kipato cha chini, uchumi wa kati na wenye vipato vikubwa?
Kaka Zitto, ni vyema ukajikita katika kushauri wanachama na viongozi wa chama chako kutangaza sera na mipango madhubuti ya kuleta maendeleo badala ya kuwaingiza wananchi kwenye migogoro isiyo na tija. Siasa si porojo, ni mkakati na utekelezaji wa mipango inayowagusa watu moja kwa moja.
Kama mtazidi kuendelea na mikakati ya "kuzurura" bila dira ya wazi, 2025 haitakuwa mbali, na matokeo yake ni "mgaragazo" wa kishindo kama drum ya Halleluya! 😀😀😀
Kwa ushauri wa bure, jenga ajenda zinazojibu changamoto za wananchi. Masuala ya elimu, afya, ajira, na uchumi yanahitaji mwelekeo thabiti. Badala ya kutegemea porojo za kisiasa, elekezeni nguvu zenu kujenga sera zinazotegemewa na watu wa kawaida.
Mfikishieni Zitto ujumbe huo😁😁😁
Kila la heri, Kaka Zitto. 👊