Uchaguzi 2020 Zitto Kabwe: Viongozi wa Upinzani tulikaa pamoja tukakubaliana kwa Upande wa Urais asimame Tundu Lissu

Uchaguzi 2020 Zitto Kabwe: Viongozi wa Upinzani tulikaa pamoja tukakubaliana kwa Upande wa Urais asimame Tundu Lissu

Kuna chama cha ukanda...

Viva Magu 2020 to 2030
Kitu Magufuli anasahau au anafanya kusudi ni kwamba;Watanzania hawataki kubaguana kwa kutumia
Kabila
Dini
Ukanda
Uvyama
Sasa ninachokiona kwa kiongozi huyu anajitahidi kutugawa kwa kutumia vyama. Naona upinzani unatumia nafasi hiyo kutuunganisha,
Ninavyo ona mimi kwa Tanzania kutugombanisha kwakutumia vyama imegonga mwamba, labda polisi wabariki hili lakini najiuliza na nimekosa majibu nikuulize mgombea wa Polepole iwapo utabahatika kuwapata washindi wote watokane na chama chako lengolako nini?hapo baadae!
 
Screenshot_20200930_095942_com.android.chrome.jpg
 
Hivyo hakuna kuungana mkono ni uongo, aachwe membe afanye kampeni zake huko mtama.
Kura za CCM ndio zitagawika maana BM kuna wahafidhina waliohama nae!!
Ila kimiujizamiujiza wako wanaowaza ati atagawa kura za upinzani!!!
 
Hivi kuna mahali nchi hii act ina ,, ufuasi mkubwa“ ? Na ni wapi huko? Na je ni kigezo gani kinatumika kwa maana nijuavyo mimi act ina Mbunge mmoja tu, sasa huo ufuasi mkubwa mnaouongelea ni upi?
ACT ni mbadala wa CUF. Mikoa ya kusini ina ufuasi mkubwa.
 
Hivi kuna mahali nchi hii act ina ,, ufuasi mkubwa“ ? Na ni wapi huko? Na je ni kigezo gani kinatumika kwa maana nijuavyo mimi act ina Mbunge mmoja tu, sasa huo ufuasi mkubwa mnaouongelea ni upi?
1. Usisahau kwamba ACT ya sasa ni pamoja na pande kubwa la CUF! Baadhi ya mikoa, hususani Lindi, Mtwara na Zanzibar bado kuna wafuasi wengi tu waliokuwa CUF na sasa wanaiunga mkono ACT, bila kusahau baadhi ya maeneo ya Dar es salaam!

2. Na pia ndo maana nikasema ufuasi mkubwa wa ACT/Membe!! Hapo ina maana, unaweza kuta baadhi ya maeneo ACT kama ACT ana ufuasi mdogo lakini Membe kama Membe ana ufuasi mkubwa! Sasa ukifanya a + A unapata kitu cha kueleweka!

3. Almost kila chama kina mahali pake ambako kina ufuasi mkubwa, hata kama ufuasi huo ni wa watu 100 kwa mkoa mzima! Provided kwenye mikoa mingine yote ufuasi wao haufiki hata watu 20, basi kule kwenye unshaken number of 50-100 followers basi ndiko kwenye ufuasi wake mkubwa huko!!
 
Kwani Mgombea haruhusiwi kujitoa ?! Akasema anaona hana ushawishi hivyo kuamua kujitoa?!.

Yote uliyoeleza sawa lakini katafute overall general election results za 2015 utaona, kina Dovutwa na Ahmad Rashid wa ADC hata hawa ACT na Mugwila wao, walipewa kura kwa mtindo wa vote distribution na kumbakizia Magufuli na ccm percentage kubwa hili kuhalalisha ushindi wao.

Kujitoa na kutokuwepo kwenye ballot paper ndio njia sahihi ya kumuunga mkono LISU.
Suala la kujitoa nilishalifikiria lakini kwa sasa naona halitasaidia sana kwa sababu ile ile kwamba, kuna uwezekano mkubwa NEC wameshapa makaratasi, na hata kama zoezi halijakamilika, watasema tu wameshachapa ili mradi tu Membe asiondolewe kwenye karatasi za kupigia kura!

Lakini kwa upande mwingine, ma-CCM hayaaminiki haya kwahiyo inaweza kuwa risk kujitoa moja kwa moja!!! Nasema hayaaminiki kwa sababu Lissu akiyabana kisawasawa kiasi cha kukosa pumzi, wala hayaoni aibu haya kutumia kila hila kama ile ya kumsimamisha kufanya kampeni na hata kusema amekiuka hili na lile na hivyo anaondolewa!!

So, huku Membe kajitoa, TL anapigwa zengwe la kufa mtu... what next?! Kama ma-CCM yaliweza kufuta uchaguzi kule ZNZ baada ya kuona yamebanwa hata kupumua hayawezi unadhani yanaweza kushindwa kumpiga ban mgombea?!
 
Kitu Magufuli anasahau au anafanya kusudi ni kwamba;Watanzania hawataki kubaguana kwa kutumia
Kabila
Dini
Ukanda
Uvyama
Sasa ninachokiona kwa kiongozi huyu anajitahidi kutugawa kwa kutumia vyama. Naona upinzani unatumia nafasi hiyo kutuunganisha,
Ninavyo ona mimi kwa Tanzania kutugombanisha kwakutumia vyama imegonga mwamba, labda polisi wabariki hili lakini najiuliza na nimekosa majibu nikuulize mgombea wa Polepole iwapo utabahatika kuwapata washindi wote watokane na chama chako lengolako nini?hapo baadae!

Politics meaning: The activities assiciated with the governance of the country, and electoral politics is conducted to get a group which distributes resources and status.
 
Pamoja na kuungana lakini bado hakuna impact yeyote.
Ninachoona ni wapinzani wameongeza kiwango cha malalamiko kuliko mapambano ya sera nzuri na zenye mvuto.
Mpaka utakapoacha utegemezi ndipo utaelewa kuwa ulikuwa unakomenti ujinga!
 
Hatari kaka kama watanzania tutakubali hili
Uchaguzi huu ndio kete ya kuyakataa hayo.. Walikuwa na uwakika na hili na walishaliandalia mazingira kuhakikisha linakuja kufanikiwa. Hakuna aliyetegemea kama Lissu angerudi, angepitishwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama walichotaka kukiua kuzima upinzani, pia hawakutegemea support aliyopata toka kwa wananchi na somo la uraia analolitoa kila akiwa anahutubia.
 
Kiongozi wa cha chama cha ACT-Wazalendo taifa Zitto Kabwe amesema endapo wananchi wa mkoa wa Katavi watawachagua viongozi wa upinzani watahakikisha wanaletea mabadiliko katiko sekta ya afya, maji na elimu.

Ameyasema hayo alipokua akizungumza na wananchi wa manispaa ya Mpanda katika uwanja wa Sikonge na kusema kuwa a endapo watapata ridhaa upinzani watahakikisha wanatatua kero za wakulima sambamba na kuboresha maisha ya watanzania.

Aidha amewaomba wananchi wa jimbo la Mpanda mjini kumchagua mgombea ubunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Rhoda Kunchela na kusema kuwa wao kama vyama upinzani wameona ni vyema kusimamisha wagombea wanaoweza kumshinda mgombea wa CCM.

Akizungumzia nafasi ya urais kiongozi huyo amesema viongozi wa upinzani wamekaa kwa pamoja na kuona ni vyema kumsimamisha mgombea urais kupitia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Tundu Lissu.

Chanzo: Mpanda Radio
Good
 
Back
Top Bottom