Zitto: Mradi wa Kabanga Nickel ni Mradi wa Barrick uliofichwa kupitia kampuni ya LZ Nickel ya Uingereza

Zitto: Mradi wa Kabanga Nickel ni Mradi wa Barrick uliofichwa kupitia kampuni ya LZ Nickel ya Uingereza

Sasa Zana za Kilimo unadai hiyo kampuni haina ujuzi wowote kuhusu madini, huku tena unasema LZ ni Barrick. Sasa Barrick hana ujuzi wa Madini
August unaleta siasa.
A company is an individual entity, Nikimiliki kampuni mbili X, na Y kila moja inajitegemea japo zote zangu
Ni mchezo uleule tu wa Barrick kuwa na share kwenye ACACIA lakini this time it seems wanaiown hiyo kampuni 100%
 
Hii nchi dawa ni kiumane tu maana wasimamizi hawako upande wa raia wako upande wa mabeberu kupitia bakshishi wanazopewa kwenye mavikao ya kujadiliana mikataba huko!
 
Una ambiwa ile inchi wao wana akili ya kuiba kura TU..[emoji1787]

Yani hapo huwaambii kitu asee[emoji23]
 
Jamaa aache siasa za hovyo, huku mtaani kuna lundo la vijana hawana ajira serikali inafanya juhudi kuokoa kundi kubwa la wasio na ajira waweze kunufaika na nchi yao anatokea mtu mmoja na politics zisizo na tija hii nchi wapo watu wengi tu wenye mapenzi mema na nchi yao huyo jamaa asione watanzania wote ni wezi, tunaomba serikali liganga na mchuchuma nayo iharakishwe tunataka uchumi wa nchi ukue na kipatao cha mtu mmoja mmoja kiongozeke, hongera kwa serikali ya awamu ya sita kwa kuweza kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji kuja kuwekeza kwetu huyo jamaa anaejifanya anajua kila kitu sababu anatamba na hela za Act anaona kila mmoja ni kama yeye.
 
Barrick wasingemuachia mtu huu mgodi. Kwanza wao ndo walifanya Utafiti miaka nenda rudi wakibeba mawe kupeleka Afrika kusini wakidai wanapelekea sample za Utafiti.

Barrick kushirikiana na Geita Gold Mining Limited na ndugu zao Stanley Mining Services wanajua nini kipo pale Rulenge wanapoita Kabanga.

Ukiona Barrick, GGML Stanley sehemu wanapigana Vikumbo, ujue sio bure.

Nahisi Wakina Kabudi walimdanganya Magufuli, asingekubali kufanya nao biashara hivi hivi wakati bado tunawadai kishika Uchumba

Serikali ilipokea Dola Billioni 40(TSH 100 Mil) kutoka kampuni ya Barrick ikiwa ni sehemu ya kishika uchumba cha Dolla Millioni 300 ambayo Barrick iliahidi kuipa serikali ili kumaliza mgogoro wa madini.

Hadi anapewa Mgodi wa Kabanga Nickel alikuwa hajamaliza hata kulipa kishika Uchumba na Magufuli akafa. Kabudi kakaa kimya kama hajashiriki chochote kwenye makubaliano ya kishika uchumba.

Wangetoa hii hela, rais Samia asingekopa til 1. Hii nchi Mkoloni wetu ni Barrick na anakumbatiwa na Watawala.
Hongera kwa kujazia nyama hii mada. Nashauri pia wengine waidadavue mada ya Zito badala ya kuanza siasa tena
 
Usiri wa mikataba ya Madini bado ni tatizo kubwa ambalo linaondoa imani ya wananchi kuwa miradi hii ina maana yoyote kwao.[emoji106][emoji3578]
 
Andiko ni zuri, ila hatujui ukweli uko wapi kiuhalisia, kwa sababu ni taarifa ya upande mmoja.

Kungekuwa na taratibu za kupata majibu kutoka upande wa pili, upande wa akina Kabudi ingekuwa ni jambo jema sana, lakini sote tunajuwa hilo hapa kwetu haliwezekani.


Hata hivyo, kuna mambo muhimu kayagusia ndugu Zitto, kwa mfano hiyo asili mia 16 ambayo hutufunika macho wengi wetu.

Lakini inaumiza zaidi, inapofikia mahala mambo kama hili hapa chini kutopewa nafasi na watu ambao ni zao la moja kwa moja la juhudi za waasisi wa nchi hii. Hawa akina Kabudi, ndio walikuwa wakisemwa kwamba ni vijana wanaotumwa kwenda kuhemea ili kuiondoa nchi yao kwenye jamga la njaa.
Hawa ndio waliopewa vibaba vya mwisho ghalani ili waje wakalijenge taifa lao!
Ona sasa jambo kama hili hapa chini ambalo ni vigumu kutoamini yaliyoandikwa hapa.

Mimi nadhani inalazimu tujaribu utaratibu walionao nchi kama China. Watu wanaokosa uzalendo kama hawa wasipewe nafasi ya kuchezea maisha ya waTanzania.
Hakika, nafikiri serikali pia ije pupambanua hili ili ijiondoe kwenye lawama. Na kuonyesha kinachoatakiwa na kinachoendelea
 
Barrick wasingemuachia mtu huu mgodi. Kwanza wao ndo walifanya Utafiti miaka nenda rudi wakibeba mawe kupeleka Afrika kusini wakidai wanapelekea sample za Utafiti.

Barrick kushirikiana na Geita Gold Mining Limited na ndugu zao Stanley Mining Services wanajua nini kipo pale Rulenge wanapoita Kabanga.

Ukiona Barrick, GGML Stanley sehemu wanapigana Vikumbo, ujue sio bure.

Nahisi Wakina Kabudi walimdanganya Magufuli, asingekubali kufanya nao biashara hivi hivi wakati bado tunawadai kishika Uchumba

Serikali ilipokea Dola Billioni 40(TSH 100 Mil) kutoka kampuni ya Barrick ikiwa ni sehemu ya kishika uchumba cha Dolla Millioni 300 ambayo Barrick iliahidi kuipa serikali ili kumaliza mgogoro wa madini.

Hadi anapewa Mgodi wa Kabanga Nickel alikuwa hajamaliza hata kulipa kishika Uchumba na Magufuli akafa. Kabudi kakaa kimya kama hajashiriki chochote kwenye makubaliano ya kishika uchumba.

Wangetoa hii hela, rais Samia asingekopa til 1. Hii nchi Mkoloni wetu ni Barrick na anakumbatiwa na Watawala.
Bila shaka Ni typing error [emoji116]

"Serikali ilipokea Dola Billioni 40(TSH 100 Mil) kutoka kampuni ya Barrick"
 
kama wazungu wametuzidi maarifa Kwenye mkataba kwa mara nyingine tuanze upya mechi
Au labda taratibu, sheria, Kanuni na miongozo inakata kuanza upya? Yaani daily kwenye kila issue utasikia tumepigwa. Hata ahadi ya kishika uchumba huenda ilikuwa bosheni tu
 
Wanasiasa bana! Yaani wao ulaji wao ni katika kutafutiza kasoro, makosa, ufisadi, popote pale kwa namba yoyote ile. Ali mradi wamejaliwa talanta ya kuongea tu!

No! Tushawachoka nyie career politicians. Nyie akina Zitto njooni kitaa na nyie muanze kuzitafuta hela kwa jasho na damu, na nyie wekezeni kwenye miradi mtengeneze ajira kama wanaume wanavyofanya, fanya hivyo kwa miaka mitano tu nje ya ya siasa zenu za kuviziana halafu baada ya hapo rudi kwenye siasa tena.

Yaani mijitu miaka nenda rudi ni kutafutizana ufisadi kwenye madini, kwenye ununuzi wa ndege, kwenye kila kitu yaani. Watu wanafanya vitu nyie ni kutafutiza makosa tu. Mnaboa yaani tu.

Nirudie tena iwekwe sheria kwamba mwanasiasa yeyote awe na kazi nyingine halali nje ya siasa.
 
Kabudi sio mtu
Ukimkuta anaongea mishipa imemtoka
 
Laana ya kuwa na madini katika Africa haiwezi liacha Tanzania salama kwani Tanzania iko Africa.
Ukiona wazungu wanatusifia sana ujue kuna wanachotaka kwetu. Mimi siyo mtabiri lakini soon Tanzania inaweza kuja kuwa kama Zaire ya Mobutu
 
Zitto ni kibaraka wa mabeberu tu,hana jipya.kigeugeu.

Juzi juzi kaisifia tanesco,leo anaiponda tena.yani hana rangi kabisa.
 
August unaleta siasa.
A company is an individual entity, Nikimiliki kampuni mbili X, na Y kila moja inajitegemea japo zote zangu
Ni mchezo uleule tu wa Barrick kuwa na share kwenye ACACIA lakini this time it seems wanaiown hiyo kampuni 100%
Kuna shida gani kama Barrick anamiliki iyo Kampuni?

Zitto ni mfutini na mtu aliyejaa chuki tu anayetumika kwa maslahi binafsi!

Nilikuwa natofautiana na Magufuli kwenye maeneo mengi hasa Nepotism na Ukiukwaji wa haki za Binadamu ila kwenye suala la Madini namuunga mkono Magufuli!


Zitto ni muhuni anayetumika na watu wahuni kwa maslahi yao!

Anasema mikataba isifanywe na GNT wakati GNT ni timu yenye wataalam wa mambo yote kuhusu mikataba ikiwemo Sheria, uchumi, kodi n.k

Anasema tume wa Madini ndo wasimamie mikataba hao tume ya madini wana uwelewa juu ya masuala ya Sheria? Mikataba? Kodi na Uchumi?


Kwa kifupi kwenye hili simuungi mkono zitto! Ndo aliyemshauri Magufuli kufukuza kampuni za kununua korosho LINDI na Mtwara alafu baadae akaja kumlalamikia kuwa serikali imeingilia kati soko la korosho Lindi na Mtwara!

Zitto ni muhuni tu!
 
Wanasiasa bana! Yaani wao ulaji wao ni katika kutafutiza kasoro, makosa, ufisadi, popote pale kwa namba yoyote ile. Ali mradi wamejaliwa talanta ya kuongea tu!

No! Tushawachoka nyie career politicians. Nyie akina Zitto njooni kitaa na nyie muanze kuzitafuta hela kwa jasho na damu, na nyie wekezeni kwenye miradi mtengeneze ajira kama wanaume wanavyofanya, fanya hivyo kwa miaka mitano tu nje ya ya siasa zenu za kuviziana halafu baada ya hapo rudi kwenye siasa tena.

Yaani mijitu miaka nenda rudi ni kutafutizana ufisadi kwenye madini, kwenye ununuzi wa ndege, kwenye kila kitu yaani. Watu wanafanya vitu nyie ni kutafutiza makosa tu. Mnaboa yaani tu.

Nirudie tena iwekwe sheria kwamba mwanasiasa yeyote awe na kazi nyingine halali nje ya siasa.
Niliwai sema ufisadi Tanzania ni nadharia zinazotengenezwa na wanasiasa kwa maslahi ya kisiasa! Hakuna jipya
 
Back
Top Bottom