Zitto: Mradi wa Kabanga Nickel ni Mradi wa Barrick uliofichwa kupitia kampuni ya LZ Nickel ya Uingereza

Msitegemee kwamba nitaikosoa serikali ya Samia - Zitto Kabwe
Hapa ndio mnafeli?hizo zake ni za kweli au sio kweli?na sidhani kama alisema hatakosoa,kukosoa atakosoa,ila sio Kwa style ile ya Magufuli,
 
Kama sio kweli,je,serikali haioni umuhimu wakutoa ufafanuzi?hoja mzito kama hizo unasema huwezi kununua,ndio kawaida yenu kupinga Pinga kila hoja zinazotolewa na wapinzani,Buzwagi 2007,Zitto alipingwa hivi hivi,EPA,Dr. Slaa alipingwa pia,scandal kibao huwa mnapinga
 
Huyu ni bingwa wa siasa za kugawa watu na kupenya. anajua huyu ni wa 5 na wa 6 ana nafasi sasa ya kuweka wake.
Huu ni upuuzi wakushindwa kujadili hoja za mtu,na kuleta propaganda zisizo na tija
 
Nilifikiri watu wenye akili wameisha JF nimefurahi kujua kuwa bado mpo
 
Zitto hivi Barrick wakikuandikia demand note ukathibitishe madai yako mahamani utaweza?

Mambo ambayo huna uhakika nayo ni vizuri ukanyamaza.
 
Na miradi ya NSSF mwenyekiti wa PAC alikuwa pinga pinga, na kamati ya Bomani mjumbe mojawapo alikuwa Pinga Pinga
 
Zito Kabwe la yuko kimya kwenye maswala muhimu ya kitaifa kwa sababu yupo pale kimaslahi. Huyu ndiye mvujisha siri zote za Serikali wakati wa JPM kupitia Rais SSH. Joka la kibisa. Ipo siku inawangojea tupo wazima tunawaangalia.
JPM ni hayati keshazikwa, nadhani unatafuta hasira ambazo zitaishia kukuumiza tu nafsini mwako.
 
Mtazamo wangu haya maelezo ni ya kutumwa na ushindani wa kibiashara wa makampuni makubwa.Nia pia ni kushawishi serikali kubadilisha kamati ya akina Kabudi.Haya mambo ya kutumwa yalituathiri sana huko nyuma ikafikia hadi mashaka ya viongozi au kamati ya bunge kula rushwa.
 
Aisee huu upigaji kwenye madini yetu utaisha lini?
Tulifikiri Magufuli kafanya jambo la maana kwenye madini kumbe naye kaingia mkataba usiokuwa na kichwa wala miguu

Changamoto ya waTanzania au Waafrika ni kwamba tunawekeza matumaini yetu kwa individuals baada ya kupambania mifumo bora na ya kudumu kwa ajili yetu na vizazi vijavyo. Wanasiasa wanatudanganya na sisi tunakubali kirahisi kwamba watatuondolea matatizo yetu lukuki yanayotukabili huku tukisahau kwamba wanasiasa hao hao ndo chanzo kikubwa cha haya matatizo yetu.

Ukweli ni kwamba kuna mamilion ya watanzania waliwekeza imani na uwezo wao wa kufikiri kwa Magufuli wakiamini kwamba ndo mtu sahihi. Wengine walithubutu hata ku-support uamuzi wa JPM kuvunja katiba, kusigina haki za watu na mengine mabaya, wakiamini kwamba ilikuwa gharama stahiki kuyapata "maendeleo". Lakini ukweli ni kwamba JPM alionekana anafanya kazi kwa sababu kwanza ali-control uhuru wa wananchi kupata habari na kujieleza (JPM alikuwa ni adui wa ukweli). Wananchi wengi walikuwa wanaambiwa yale aliyotaka wayajue au wayasikie. Kiongozi asiyependa ukweli, anayependa giza badala ya nuru si kiongozi mwema. Imagaine mpaka maprofesa wanapewa kazi si kwa ujuzi bali kwa hisani ya kuwatoa jalalani!

Mimi mpaka leo siamini kwamba JPM alikuwa ni kiongozi bora-alikuwa bora kiongozi (alikuwa kiongozi wa kawaida tena wengine walimzidi). Lakini kama mfaidika wa utawala wake, naweza kusema alikuwa kiongozi mzuri kuliko wote waliowahi kutokea-ingawa ukweli wote tunaujua! Maendeleo siyo madaraja au barabara (ni sehemu tuu). Mpaka leo TZ inaheshimika kwa sababu ya misingi ya mwalimu aliyoijenga. Kiufupi Taifa letu mpaka leo tunakula pension ya kazi aliyofanya mwalimu.

Unless tuwekeze kwenye mifumo ya uongozi, hata huyu Mama ataondoka atatuacha mikono mitupu, tutaanza kuimba vigelegele kwa mrithi wake.... Ndo maana ukiongelea swala la katiba utapingwa na kupewa majibu marahisi (Kenya wana katiba mpya mbona wana changamoto za utawala nk). Ukweli ni kwamba watawala wanajua wanachokifanya. Ukitaka kuwatawala watu, wapumbaze, waite wanyonge au wadunishe. Ndo maana mpaka leo "wanyonge" wanamkumbuka JPM. Lakini ukweli ni kwamba, ukishaitwa mnyonge wamekumaliza. Utu wako umedumazwa. Unategemea hisani ya wengine kuiona kesho. Na katika hilo JPM alifanikiwa sana!

Kwa Tanzania sioni tukitoka hapa tulipo kirahisi, kwa sababu juhudi zote za maendeleo zinafanyika kama hisani ya watawala. Na uwajibikaji ni utashi wa mtu mmoja mmoja. CCM imewafanya watu- vijana kwa wazee wawe waoga, wasiojiamini, wanaoamini kwamba uwezo wao wa kuiona kesho au kutengeneza maisha yao wenyewe yapo mikononi mwa watawala.

Aliyoyaandika Zitto si mageni na ni mengi sana ambayo hatuyajui. Na kipindi cha JPM haya yasingejulikana kwa sababu mazingira yaliyokuwepo yalikuwa hayaruhusu haya tuyajue.

Kwangu mimi JPM alikuwa mzalendo na mthubutu, aliyeipenda nchi yake. LAKINI siiombei nchi yangu ije ipate tena kiongozi wa aina yake.
 
Absolutely brilliant
 
Zito Kabwe yuko kimya kwenye maswala muhimu ya kitaifa kwa sababu yupo pale kimaslahi. Huyu ndiye mvujisha siri zote za Serikali wakati wa JPM kupitia Rais SSH. Joka la kibisa. Ipo siku inawangojea tupo wazima tunawaangalia.
Anazungumzia issue ya madini lakini sio gas. πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚
 
Zito Kabwe yuko kimya kwenye maswala muhimu ya kitaifa kwa sababu yupo pale kimaslahi. Huyu ndiye mvujisha siri zote za Serikali wakati wa JPM kupitia Rais SSH. Joka la kibisa. Ipo siku inawangojea tupo wazima tunawaangalia.
Sioni mbaya kama Zitto alikuwa analikisha Siri za Serikali ya JPM. Ile ilikuwa ni Serikali ya DHULUMA sana, kwa hiyo yeyote aliyechangia kuidhoofisha ni SHUJAA.
 
Kila kona ni kupigwa tuu, gas sio yetu tena na hata dhahabu hakuna tulichopata zaidi ya mashimo, sasa hii nickel watabeba bure inayoonekana, Mkapa alikuwa anaonekana very smart lakini huwezi kuamini jinsi mikataba ya ovyo kabisa ilivyo sainiwa wakati wa utawala wake na JK ndio kabisa kauza sijui kagawa gas yote ambayo ingeweza kutupa umeme nchi nzima kwa mika 100 ijayo, huwezi kuamini vitu vinavyofanywa na hawa viongozi wetu sometimes unafikiri uko ndotoni
 
Zitto na makamba hawafai kuwa marais ila uwaziri ni wazur ,ni bora arudi magu kuliko zitto
 
Ninachojua nikua zito anajua fika kua kizazi hiki ni Cha mazoba, hata akiongea upupu, lazima majority watamwamini.
Sisi wachache tunaoelewa tunashindwa kumdhibiti.
Na Hawa wawekezaji watamwita na kumziba mdomo kwa milioni kadhaa.

Hiyo ndo style yake ya maisha, maisha ya kitapeli. Kiboko yake alikua JPM. Alipauka hatari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…