Zitto: Ni Kutumiwa na GMO, Tamaa za Umaarufu au ni Kutosoma Ripoti Mbalimbali

Zitto: Ni Kutumiwa na GMO, Tamaa za Umaarufu au ni Kutosoma Ripoti Mbalimbali

kibokomchapaji

Senior Member
Joined
Aug 18, 2017
Posts
165
Reaction score
307
Zitto kabwe amefilisika sana. Maneno yake kuhusu upungufu wa chakula nchini hayana mashiko.

Bodi ya Takwimu (NBS) ndio wa kwanza kusema kuna mfumuko wa bei.

Benki ya Dunia (WB) ikasema umasikini umepungua nchini hivyo watu wanamudu gharama za kununua vyakula.

Aidha, ripoti ya Utafiti wa kina wa WB inasema hakuna umasikini wa chakula kwani taifa lina chakula cha kutosha.

Katika uchumi wa sasa, serikali haifanyi ukiritimba hivyo serikali huwa na ghala lake, wafanyabiashara na wakulima huwa na maghala yao. WB ilitembelea kote humu na kukuta tani 341,136.41.

Zitto amechukua ripoti ya ghala moja na kujidanganya mwenyewe na wafuasi wake.

Mbaya zaidi, wakati WB inasema kilimo kimekua nchini na kutushauri tuimarishe kilimo, Zitto anasema tununue chakula.

Hatutaki serikali inunue chakula, Huu ndio utegemezi alioupinga baba wa taifa.

Mimi nadhani anatumiwa na mataifa yanayolima chakula kwa wingi kwa kutumia mbegu za GMO zenye madhara kwa afya.

Rashid Kilogi
Kigoma, Ujiji.
 
_”Kuna siku alikosoa ujenzi wa barabara, umeme, vituo vya afya na kadhalika huku akisema serikali ingeimarisha kilimo tu”_ amesikika mkulima wa Mahindi Kibaigwa akihoji.

Wakulima wenzake wanahoji pamoja naye; Bidhaa zao zitakwendaje sokoni bila barabara? Watalima vipi kama hawana afya njema endapo hakuna vituo vya afya? na kadhalika.

Wakati bado wanatafakari kauli ya Zitto, leo Desemba 17, amewachefua zaidi wakulima kwa kuitaka serikali iendelee na utaratibu wa zamani wa kununua chakula kutoka nchi za nje badala ya kuiomba serikali iimarishe kilimo cha Watanzania.

Hayo aliyoyaandika kwenye ukurasa wake wa Twitter anafanya hivyo kumfurahisha nani? Wakulima wa hapa Tanzania wamemkosea nini Zitto Kabwe?

Hivi amesahau kwamba asilimia 70 ya Watanzania wanategemea shughuli za kilimo? Hivi hana huruma na Watanzania eti wategemee kuagiza chakula kutoka nje!! Anataka tukanunue DRC au Burundi ambako ndiko anafanyia biashara zake za mahindi na maharage!! Hata kama alitoka Burundi au DRC sisi hapa ni kwetu. Lazima tulime na tuuze. Huko nje anakotaka tukanunue ni kwa nani?

Zitto anapoteza umaarufu wake wenye tija na anajikita katika siasa za Ulaghai. Hii haitamsaidia ila inamdidimiza. Ipo siku atanikumbuka kwa maneno haya.

*Dr. Zainab Rashid*
17/12/2019
 
Zitto analeta siasa hadi kwenye masuala ya msingi. . .hizi kiki anazozitafuta hazitomsaidia lolote.Awasikilize wakulima. . ."wao nido wa wataalam".
 
kigoma ujiji ya nyoko
Zitto kabwe amefilisika sana. Maneno yake kuhusu upungufu wa chakula nchini hayana mashiko.

Bodi ya Takwimu (NBS) ndio wa kwanza kusema kuna mfumuko wa bei.

Benki ya Dunia (WB) ikasema umasikini umepungua nchini hivyo watu wanamudu gharama za kununua vyakula.

Aidha, ripoti ya Utafiti wa kina wa WB inasema hakuna umasikini wa chakula kwani taifa lina chakula cha kutosha.

Katika uchumi wa sasa, serikali haifanyi ukiritimba hivyo serikali huwa na ghala lake, wafanyabiashara na wakulima huwa na maghala yao. WB ilitembelea kote humu na kukuta tani 341,136.41.

Zitto amechukua ripoti ya ghala moja na kujidanganya mwenyewe na wafuasi wake.

Mbaya zaidi, wakati WB inasema kilimo kimekua nchini na kutushauri tuimarishe kilimo, Zitto anasema tununue chakula.

Hatutaki serikali inunue chakula, Huu ndio utegemezi alioupinga baba wa taifa.

Mimi nadhani anatumiwa na mataifa yanayolima chakula kwa wingi kwa kutumia mbegu za GMO zenye madhara kwa afya.

Rashid Kilogi
Kigoma, Ujiji.
 
Zitto ni mnafiki na Beberu hafai kuigwa ni ndumilakuwili


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Zito mtaalam wa kucheza na akili za watu akitupia jambo husubiri kuungwa au kukosolewa ili apate kuchuja ayatakayo..
Hana kheri wala shari ni mtu wa malengo yake huko mbele ya safari yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kati ya Zitto na wewe nani ni maalufu?
 
Tatizo huwa muda wote anatafuta namna ya kuiambia dunia kuwa serikali haifanyi kazi ndo maana huwa anakurupukia takwimu na kujifanya mchambuzi kumbe anataka wadhamini wake wamuone mpambanaji.
 
Back
Top Bottom