Majighu2015
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 2,937
- 3,959
Manchester, Uingereza.
Mchezaji wa kimataifa wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic amejiunga rasmi na klabu ya Manchester United ya Uingereza huku akitamba kuandika kumbukumbu mpya katika historia ya ligi ya England.
Mchezaji huyo aliyekuwa akicheza na klabu ya PSG ya Ufaransa amesaini mkataba wa mwaka mmoja na tayari kocha wake Jose Mourinho amesema kuwa haihitaji kutoa sababu nyingi kuelezea kwa nini ameamua kumsajili mshambuliaji huyo kwa vile ‘ takwimu zinajieleza’.
Wawili hao walikutana kwa mara ya kwanza wakati walipokuwa katika klabu ya Inter Milan ya Italia na kwamba sasa wanakutana tena wakiwa nchini Uingereza.
Ibrahimovic ambaye amekuwa akisifika kwa kupachika mabao ya kushtukiza ameandika kwenye mtandao wake wa Twitter akisema kuwa ‘”ninayo furaha kubwa kujiunga na klabu hii lakini jambo kubwa kwangu ni kufanya kazi tena kocha Jose”
Hongereni man utd. Kifaa hicho ingawa ni kibabu.
Mchezaji wa kimataifa wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic amejiunga rasmi na klabu ya Manchester United ya Uingereza huku akitamba kuandika kumbukumbu mpya katika historia ya ligi ya England.
Mchezaji huyo aliyekuwa akicheza na klabu ya PSG ya Ufaransa amesaini mkataba wa mwaka mmoja na tayari kocha wake Jose Mourinho amesema kuwa haihitaji kutoa sababu nyingi kuelezea kwa nini ameamua kumsajili mshambuliaji huyo kwa vile ‘ takwimu zinajieleza’.
Wawili hao walikutana kwa mara ya kwanza wakati walipokuwa katika klabu ya Inter Milan ya Italia na kwamba sasa wanakutana tena wakiwa nchini Uingereza.
Ibrahimovic ambaye amekuwa akisifika kwa kupachika mabao ya kushtukiza ameandika kwenye mtandao wake wa Twitter akisema kuwa ‘”ninayo furaha kubwa kujiunga na klabu hii lakini jambo kubwa kwangu ni kufanya kazi tena kocha Jose”
Hongereni man utd. Kifaa hicho ingawa ni kibabu.