Zoezi la TANESCO la kubadili Mita limejaa Usumbufu, Utapeli na Ubabaifu

Zoezi la TANESCO la kubadili Mita limejaa Usumbufu, Utapeli na Ubabaifu

Shark

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2010
Posts
29,775
Reaction score
29,746
Kwema Wakuu,

Mimi ni mkaazi wa Kitongoji Kimoja wilaya ya Kinondoni hapa Dar es Salaam. Jumatatu nilipigiwa simu na watu wa TANESCO kunifahamisha kua Kwa kua number ya mita yangu inaanzia na 24... basi nitabadilishiwa mita hiyo kesho yake yaani juzi.

Juzi Jumanne kweli walikuja asubuhi kubadili wakanipa mita mpya. Mita waliyoitoa awali ilikua na units 56 lakini wao walinipa ya kwao yenye units 10 tu. Walisema hizo units 10 ni offer ya mita mpya lakin za awali hazipo tena. Huu ni utapeli wa wazi wazi. Ni uporaji na unyang'anyi waliojihalalishia, na hakuna uhalali wowote wa hili.

Baada ya kuweka mita mpya hiyo asubuhi wakaniambia watatuma number (token) za kufungulia hiyo mita. Nimesubiri mpaka usiku sijapata hiyo token, imekuja kutumwa jana mchana (zaidi ya masaa 24) Sina umeme, usumbufu ulioje. Waniibie units na umeme wasinipe.

Nimepokea token haifanyi kazi, kama vile ilikua wrong token. Customer Care ya TANESCO mmoja akasema kua inakua ngumu kutatua tatizo langu Kwa wakati sababu huu mradi hauko chini ya TANESCO moja Kwa moja, ni mradi wa mtu au kampuni binafsi. Yaani Ubabaifu uliopitiliza, watu wanajua mpaka number ya mita yangu lakin sio wa TANESCO .

Mpaka muda huu sina umeme kwangu toka juzi asubuhi (zaidi ya 40 hrs). Kama walikua hawajajipanga ni bora wangesitisha kwanza hili zoezi. Units mnazopora sio halali yenu kabisa, muangalie namna ya kutulipa.
 
Huu nao ufisadi TANESCO mjitafakari mimi pia mita yangu iliharibika siku wanafunga mpya nikawauliza units haziwezi hamishiwa kwenye mita mpya wakajiuma uma pale wakaondoka nikaachana nao tu
 
Kwema Wakuu,

Mimi ni mkaazi wa Kitongoji Kimoja wilaya ya Kinondoni hapa Dar es Salaam. Jumatatu nilipigiwa simu na watu wa TANESCO kunifahamisha kua Kwa kua number ya mita yangu inaanzia na 24... basi nitabadilishiwa mita hiyo kesho yake yaani juzi.

Juzi Jumanne kweli walikuja asubuhi kubadili wakanipa mita mpya. Mita waliyoitoa awali ilikua na units 56 lakini wao walinipa ya kwao yenye units 10 tu. Walisema hizo units 10 ni offer ya mita mpya lakin za awali hazipo tena. Huu ni utapeli wa wazi wazi. Ni uporaji na unyang'anyi waliojihalalishia, na hakuna uhalali wowote wa hili.

Baada ya kuweka mita mpya hiyo asubuhi wakaniambia watatuma number (token) za kufungulia hiyo mita. Nimesubiri mpaka usiku sijapata hiyo token, imekuja kutumwa jana mchana (zaidi ya masaa 24) Sina umeme, usumbufu ulioje. Waniibie units na umeme wasinipe.

Nimepokea token haifanyi kazi, kama vile ilikua wrong token. Customer Care ya TANESCO mmoja akasema kua inakua ngumu kutatua tatizo langu Kwa wakati sababu huu mradi hauko chini ya TANESCO moja Kwa moja, ni mradi wa mtu au kampuni binafsi. Yaani Ubabaifu uliopitiliza, watu wanajua mpaka number ya mita yangu lakin sio wa TANESCO .

Mpaka muda huu sina umeme kwangu toka juzi asubuhi (zaidi ya 40 hrs). Kama walikua hawajajipanga ni bora wangesitisha kwanza hili zoezi. Units mnazopora sio halali yenu kabisa, muangalie namna ya kutulipa.
Mkuu nenda mwenyewe kwa Wakala mkuu ukanunue Umeme utapata namba na token za kufungulia na iyo unit 10 walizokupa sio offer utakatwa , mm nilienda pale Fire kituoni chaa Oryx
 
Mkuu nenda mwenyewe kwa Wakala mkuu ukanunue Umeme utapata namba na token za kufungulia na iyo unit 10 walizokupa sio offer utakatwa , mm nilienda pale Fire kituoni chaa Oryx
Nimekuja kutatua usiku huu. Nimeambiwa kua mita mpya niliyowekewa ilikua number zake haziko updated kwenye mfumo wa Tanesco. Yaani wamefunga dude tu lakini halitambuliki TANESCO .

Kuhusu units sijajua mkuu kama ni mkopo. Lakini vyovyote iwavyo zile units za mita ya Mwanzo walizochukua ni wizi wa mchana kweupe.
 
Back
Top Bottom