Zoezi la ukusanyaji taka ambalo wanachaji Tshs 3,000 hadi 5,000 kila kaya bila kutoa risiti za kielektroniki lina baraka za mamlaka?

Nyinyi ndio mnaendeleza watu kuibia serikali
 
Hao ni wezi kama wezi wengine tupaaze sauti yetu ifike kwa mh rais. Serikali ilipiga marufuku risiti za gerezani. Unaipotezea serikali mapato na nani alikuwambia diwani na mwenyekiti walipwe kwa kodi za taka?
 
Uwazi kwenye malipo ni muhimu, unaweza kufikiria unawalipa vizuri kumbe pesa inaishia kwa diwani na watendaji wachache.
Kuna ubaya gani kama mtaa unakuwa msafi na taka wanazoa? Wakubwa wanapiga fedha hutaki na hawa wadogo nao wapate?
 
Utoapo malipo dai risiti kinyume na hapo unawasaidia majizi kukuibia.tena ziwe za kielectronic.
 
Huo utaratibu una baraka zote kutoka kwenye baraza la kata na mitaa yake..tatizo vikao vya wananchi vikiitishwa hamtokei kujadili haya..mwisho wasiku mnaishia kulaumu na kuhoji..chamsingi kesho j3 nenda katani au ofisi ya mtendajibwa mtaa akakupatie ufafanuzi.

Naamini utajibiwa vyema kuhusiana na suala zima la utoaji wa risiti.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…