Zuhura Yunus kudai uteuzi wake ulikuwa wa kushtukiza, hakuwa na taarifa ni kweli? Kwanini hakujuzwa?

Zuhura Yunus kudai uteuzi wake ulikuwa wa kushtukiza, hakuwa na taarifa ni kweli? Kwanini hakujuzwa?

Leak

JF-Expert Member
Joined
Feb 22, 2012
Posts
52,916
Reaction score
43,505


’Changamoto zitakuwepo lakini nitamudu kazi’’

Mkurugenzi wa mawasiliano ikulu nchini Tanzania, Zuhura Yunus amezungumza na BBC na kueleza ni jinsi gani amepokea taarifa ya uteuzi wake.

Kabla ya uteuzi huo bi Zuhura Yunus alikuwa mtayarishaji wa vipindi na mtangazaji wa idhaa ya Kiswahili ya Shirika la utangazaji la Uingereza BBC.

Bi Zuhura anachukua nafasi ya bwana Jaffar Haniu ambaye amepangiwa kuchukua majukumu mengine kulingana na Taarifa iliyotiwa Saini na kaimu mkurugenzi wa mawasiliano ya rais.
-
Uteuzi wake unakuja miezi kadhaa baada ya kuandika kitabu chake cha wasifu wa Biubwa Amour Zahor mwanaharakati mwanamke wa kisiasa wakati wa mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964.
Mkurugenzi mpya wa mawasiliano ikulu -Tanzania ameiambia BBC kuwa uteuzi wake ulikuwa wa kushitukiza na wala hakuwa na taarifa kama ameteuliwa kwenye nafasi ya kuwa msemaji wa ikulu!

Anasema alikuwa amelala akashangaa simu za watu mbali mbali zinaita nakulia!

Anasema ni kitu ambacho hakutegemea kabisa!

Source: BBC Swahili
 
Wenzetu huko Duniani utaskia Rais anategemewa kumteua Fulani kuwa fulani…hii inasaidia Mhusika kujiandaa kisaikolojia na wakati mwingine watu kutoa taarifa zake muhimu kabla ya Uteuzi

Nimewahi kumsikia Fedrick Sumaye kuwa aliitwa saa 9 kamili jioni kwenye Makazi ya Rais wakati huo Mpambe wa Rais alikuwa kishaelekea Bungen kwa Mzee Msekwa kupeleka jina

The same to Mzee Pinda anasema akiwa na Rafiki yake Mh. Paul Kimiti wanajadili nani atamrithi Lowassa akashangaa Gari za 'Kaunda suti' zinakuja kumbeba

Tabia hii iliwahi kumgharimu jamaa aliekataa uteuzi wakati wa Mwamba bwana Maendeleo akajikuta kapoteza kazi Tigo

Hayati Mzee wetu yeye alikuja na kali kuliko…anatumbua Jumapili usiku hadi nguo za kazini ushaandaa
 
Swali muhimu, ameajiriwa kama Expert au tuna uraia pacha tayari.

Uraia wake kwa sasa ni wa Uingereza. Nafasi nyeti kama hiyo kupewa mwingereza sio kitu kidogo.

Tunaomba ufafanuzi kutoka kwako Zuhura au serikalini.
 
Tetesi za yeye kupewa hiyo nafasi zilishakuwepo mwanzo, na sijui ni kwa vipi baada ya zile tetesi akaamua kuondoka BBC then after ndio akateuliwa na Rais, sasa kwa hiyo picha sioni kwa vipi alikuwa hajui kama palikuwepo na huo mpango.
 
Nyerere miaka yake yote ya Utawala Personal Secretary wake alikuwa Mdada mrembo wa Kiingereza hadi alipostaafu bado aliendelea nae…

cha kushangaza zaid yule Bibi aliandika kitabu cha Maisha yake na mengi kuhusu uhusiano wake wa 'kikazi' na Kambarage na akaomba kizunduliwe 30 years baada ya kufa kwake…wachambuzi wana bashiri kina mengi sana
Swali muhimu, ameajiriwa kama Expert au tuna uraia pacha tayari.

Uraia wake kwa sasa ni wa Uingereza. Nafasi nyeti kama hiyo kupewa mwingereza sio kitu kidogo.

Tunaomba ufafanuzi kutoka kwako Zuhura au serikalini.
 
Nyerere miaka yake yote ya Utawala Personal Secretary wake alikuwa Mdada mrembo wa Kiingereza hadi alipostaafu bado aliendelea nae…

cha kushangaza zaid yule Bibi aliandika kitabu cha Maisha yake na mengi kuhusu uhusiano wake wa 'kikazi' na Kambarage na akaomba kizunduliwe 30 years baada ya kufa kwake…wachambuzi wana bashiri kina mengi sana
Yule PA alikuwa mzungu au mhindi?
 
Nyerere miaka yake yote ya Utawala Personal Secretary wake alikuwa Mdada mrembo wa Kiingereza hadi alipostaafu bado aliendelea nae…

cha kushangaza zaid yule Bibi aliandika kitabu cha Maisha yake na mengi kuhusu uhusiano wake wa 'kikazi' na Kambarage na akaomba kizunduliwe 30 years baada ya kufa kwake…wachambuzi wana bashiri kina mengi sana

Nimesoma mahala, hata Mandela mtu wa karibu kabisa alihakikisha anaoshwa, anakula na kuvaa vizuri alikuwa mzungu.

Sipingi Diaspora kushiriki kujenga Taifa, infact ninaunga mkono wapewe nafasi.

Muhimu hili swali lijibiwe, liwekwe wazi, kwamba diaspora wanaweza kugombea au kuteuliwa kwenye nafasi yoyote serikalini kama Ukurugenzi, Uwaziri kugombea ubunge au Urais, nafasi yoyote.
 
Si kweli. Uteuzi kama unakunyemelea kuna aina mbili wapo wateuliwa wanaloby au kuanza kuulizia ulizia nafasi fulani napenda nifanyekazi na wengine wanateuliwa kwa uwezo wao.

Tetesi huwa zinaanza mapema japokuwa inaweza isifahamike ni nafasi gani haswa unateuliwa lazima alipokea emails na simu pia kumuuliza kuhusu kurudi nyumbani kufanya kazi. Lazima wakuandae kisaikolojia. Na ni haki ya mteuliwa kujua job description na benefit package.

Navyohisi hii nafasi alitaka apewe kikeke lakini akachomoa ndio wakaona wampe Zuhura.

Naona wabongo wamekomaa na uraia wake ila wamesahau kwamba Hata Salva alikuwa na residency ama sio uraia wa UK maana mkewe na wanae wote makazi yao yalikuwa kwa malkia.a

Sent from my Infinix X605 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom