Zuhura Yunus kudai uteuzi wake ulikuwa wa kushtukiza, hakuwa na taarifa ni kweli? Kwanini hakujuzwa?

Zuhura Yunus kudai uteuzi wake ulikuwa wa kushtukiza, hakuwa na taarifa ni kweli? Kwanini hakujuzwa?

Wenzetu huko Duniani utaskia Rais anategemewa kumteua Fulani kuwa fulani…hii inasaidia Mhusika kujiandaa kisaikolojia na wakati mwingine watu kutoa taarifa zake muhimu kabla ya Uteuzi

Nimewahi kumsikia Fedrick Sumaye kuwa aliitwa saa 9 kamili jion kwny Makazi ya Rais wakati huo Mpambe wa Rais alikuwa kishaelekea Bungen kwa Mzee Msekwa kupeleka jina

The same to Mzee Pinda anasema akiwa na Rafiki yake Mh.Paul Kimiti wanajadili nani atamrithi Lowassa akashangaa Gari za 'Kaunda suti' zinakuja kumbeba

Tabia hii iliwahi kumgharimu jamaa aliekataa uteuzi wakati wa Mwamba bwana Maendeleo akajikuta kapoteza kazi Tigo


Hayati Mzee wetu yeye alikuja na kali kuliko…anatumbua Jumapili usiku hadi nguo za kazini ushaandaa
Yule Jamaa wa Tigo aliyekataa teuzi alipoteza kazi?ilikuwaje?
 
Nimesoma mahala, hata Mandela mtu wa karibu kabisa alihakikisha anaoshwa, anakula na kuvaa vizuri alikuwa mzungu.

Sipingi Diaspora kushiriki kujenga Taifa, infact ninaunga mkono wapewe nafasi.

Muhimu hili swali lijibiwe, liwekwe wazi, kwamba diaspora wanaweza kugombea au kuteuliwa kwenye nafasi yoyote serikalini kama Ukurugenzi, Uwaziri kugombea ubunge au Urais, nafasi yoyote.
Nchi nyingi duniani masikini na tajiri, kubwa na ndogo zinatoa uraia pacha ! Tanzania tunakwama wapi ?? Ni roho mbaya au nini ?
 
Naona msemaji anaanza kujifunza "kufukia mashiko". Sidhani kama malaika wa haki akiwa mbele yake atasema hivyohivyo😆
 
Nchi nyingi duniani masikini na tajiri, kubwa na ndogo zinatoa uraia pacha ! Tanzania tunakwama wapi ?? Ni roho mbaya au nini ?
Nchi nyingi duniani masikini na tajiri, kubwa na ndogo zimeongozwa na vyama tofauti. Tanzania tunakwama wapi?? Ni roho mbaya au nn ?
 
Sidhani kama nikweli cos tayari alishaaga BBC.......alijua anakoenda bila shaka
Aseme alikuwa anaenda wapi? Je ni kuanzisha consultancy firm ya Comms? au nini? Ndo watu wanavyo badili gia angani wanapoelekea jumba jeupe. Overall, ni swala la kutafuta maisha tu.
 
Nyerere miaka yake yote ya Utawala Personal Secretary wake alikuwa Mdada mrembo wa Kiingereza hadi alipostaafu bado aliendelea nae…

cha kushangaza zaid yule Bibi aliandika kitabu cha Maisha yake na mengi kuhusu uhusiano wake wa 'kikazi' na Kambarage na akaomba kizunduliwe 30 years baada ya kufa kwake…wachambuzi wana bashiri kina mengi sana
Miaka ya giza hiyo mkuu, Tz kulikua hakuna wasomi.
Ni sawa na kusema mbona zamani kutoka dar hadi mwanza ilikua vumbi tupu.
 
View attachment 2105553
Mkurugenzi mpya wa mawasiliano ikulu -Tanzania ameiambia BBC kuwa uteuzi wake ulikuwa wa kushitukiza na wala hakuwa na taarifa kama ameteuliwa kwenye nafasi ya kuwa msemaji wa ikulu!

Anasema alikuwa amelala akashangaa simu za watu mbali mbali zinaita nakulia!

Anasema ni kitu ambacho hakutegemea kabisa!
Huyu mama hasemi ukweli mbona mimi nilisoma mahali tangu December, 2020 wakati ametoa notice ya kuacha kazi BBC walisema amepewa kazi na SSH sasa leo anasema alistukizwa sio kweli
 
Hivi lakini kabla si nilisikia anakwenda kuwa Mkurugenzi pale Azam Media akichukua nafasi ya Mzee Chaz Hilary?
 
Muongo tu, sio kweli eti kashtukizwa, atapigwa chini sasa hivi, aache kufanya watu hawajui kitu, nafasi kama hiyo lazima ana pre information zote.
 
N
Huyu mama hasemi ukweli mbona mimi nilisoma mahali tangu December, 2020 wakati ametoa notice ya kuacha kazi BBC walisema amepewa kazi na SSH sasa leo anasema alistukizwa sio kweli
Ni mwanahabari, ameanza vizuri kazi yake kubwa ni ku-spin, propaganda, kufanya visivyoaminika viaminike.

Labda ataiweza.
 
Back
Top Bottom