Hapa Waziri kayakoroga!
Tuliopitia JKT ,tena kwa mwaka mzima, tunajua kuwa huwezi kuchanganya mavazi ya kijeshi na ya kiraia.
Hapo pichani gazeti ka Guardian leo page 2, waziri kavaa Olive Military uniform , halafu na kapelo ya mtaani.
Kwa hizi military uniforms inabidi JWTZ itoe mwongozo jinsi...
Nimekusikia ukisema kuwa hutafunga mipaka kuzuia chakula kuuzwa nje. Nakupongeza sana kwa hili. Kwa miaka mingi hilo suala limekuwa likimnyonya sana mkulima. Limedhoofisha na kilimo chetu.
Uamuzi wako unaweza pandisha bei ya chakula. Unaweza leta lawama, lakini ni uamuzi sahihi. Kilichobaki...
Leo Waziri wa Kilimo ametamka hadharani kuurejesha Mfumo wa Ununuzi wa Mbolea BPS ambao ulifutwa Juni 2021 na kusababisha mfumko mkubwa wa bei za Mbolea nchini kwani wafanyabiashara waliuza mbolea kwa bei wanayoitaka wao bila kuwepo usimamizi wa Serikali.
Jambo hili lililalamikiwa sana na...
"Jambo muhimu la kiongozi ni kusikiliza watu wake, viongozi hamna monopoly right ya wisdom, viongozi hawana monopoly right ya truth, viongozi hawana monopoly right ya wao wako sahihi kila siku na mheshimiwa mwenyekiti hakuna jambo muhimu katika kupanga mipango yoyote duniani kama takwimu"...
Kumekuwepo na sintofahamu kubwa kuhusiana na Kauli ya Waziri wa Kilimo kuilazimisha Central Bank kutoa upendeleo kwa Benki mpya ya Bashe inayoitwa Benki ya Ushirika ili kuweka masharti nafuu ya utoaji wa mikopo.
Pia, nimeona Bashe ameingia kwenye mzozo kuhusiana na ruzuku ya Mbolea na kuleta...
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema hawataiomba Benki Kuu ya Tanzania bali watailazimisha kutengeneza mfumo utakaowezesha Benki ya Ushirika kupata upendeleo wa kurahisisha utoaji wa mikopo kwa wakulima
Pia soma Waziri Bashe aipaka matope Tanzania Kimataifa
Kauli ya Waziri Kilimo Hussein Bashe kuilazimisha na kuishinikiza Benki Kuu ya Tanzania kuacha kusimamia sheria zilizopo na kufanya upendeleo kwa Benki ya Ushirika katika mfumo wa utoaji wa mikopo.
1. Benki Kuu ya Tanzania imeanzishwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na...
Wana JF Wakulima tunataka kuona bei ya mbolea inashuka nchini, pia tunataka kuona mikakati ya Serikali ya kushusha bei ya mbolea lakini maelezo aliyoyatoa Waziri Bashe hayaleti unafuu wowote kwa wakulima.
Tatizo la Bei ya mbolea kupanda haliwezi kumalizwa na ruzuku kwani ruzuku inayotolewa...
Bashe ametoa Siri aliyoificha kwa muda, kuwa Magufuli alitaka amtumbue na amuuweke ndani. CHEKI VIDEO
Waziri Bashe amesema, alipoteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Kilimo alikumbana na sakata la korosho ambapo ghala la Serikali lilijaa korosho, na korosho mpya zilikuwa zinaingia.
Ili kukabiliana...
Nimetembelea ukurasa wa World Bank ambako Bashe alichota bei na kuzilinganisha na mwaka huu, 2022.
Kwa maoni yangu, Waziri huyu hafai au an ufahamu mdogo. Lakini pia naona bunge likishangilia kila mtu anayetumia kelele kujidai kutetea wananchi. Hapa Bashe alitumia kelele kutetea wakulima...
Nchi hii imekuwa na shida sana tunasifia watu kwa jinsi wanavyofanya ziara au kuongea majukwaani, hizi siyo njia sahihi. Tunatakiwa kuwapima kwa matunda.
sasa nasikia kila kona watu wanamsifia Bashe ni bora tuweke vigezo sahihi vya kumtazama na hivyo vigezo ni kupima ameleta mabadiriko gani...
Dodoma. Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amemcharukia Waziri wa zamani wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ambapo amesema ni hatari kwa mbunge wa muda mrefu kuupotosha umma.
Mpina wakati akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka 2022/2023 bungeni leo...
Mimi ni mmojawapo wa wakulima tulioingia mkataba na wizara ya Kilimo kuzalisha mbegu bora za kilimo kupitia wakala wa uzalishaji wa mbegu bora za Kilimo; ASA.
Ni takribani miezi 9 sasa tangu Agosti na September mwaka 2021tulizalisha na kuuza mbegu kwa mujibu wa mkataba wa uzalishaji hadi sasa...
Huo ndio ukweli mchungu kwani huwezi kuwa mzalendo na mwenye uchungu na nchi hii halafu ukawa mwana-CCM isipokuwa Nyerere, mtu kama Sokoine na wengine wachache sana.
Wengi huko ni wasaka fursa, fursa ambazo huwezi kuzipata ukiwa upinzani na wengine wako katika hicho chama ili wabaki salama...
Rais Samia Suluhu Hassan anazindua Ugawaji wa Vitendea kazi kwa Maafisa Ugani nchini ikiwemo Pikipiki 2,000, Vifaa vya Kupima afya ya Udongo (Soil agro scanner) 143, simu janja 384 na visanduku vya ufundi vya Maafisa Ugani 3,400.
#TunaImaninaSamia
#Hakunakinachosimama
#KaziInaendelea.
------...
Nadhani wote tunashuhudia namna wabunge wanavyolinda na kupiga kelele zinapotajwa posho na maslahi Yao. Ni mashuhuda kwamba Mzee Pinda linapokuja suala la ufugaji wa nyuki yupo radhi afunge safari kwenda Kwa Mhe. Mkubwa wa nchini kulitolea ufafanuzi, tunafahamu nguvu watakayotumia akina Zitto...
Ameandika Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe katika ukurasa wake wa Twitter. Nina Faham maumivu ya bei ya mbolea sio kwa kuambiwa bali kwa kuyaishi basi na mimi binafsi ninajua kama mkulima. Tuna maelekezo ya Mh Rais kuhusu hali ya mbolea nawaomba Ndg zangu tuwe na subira, msimu ujao wa kilimo...
Amani iwe nanyi,
Habari kuu kwa sasa duniani ni kupanda kwa bidhaa adimu kutokana na vita vinavyoendelea vya Russia v Ukraine.
Bidhaa adimu kama mafuta na Gesi zinazidi kupanda kwa kiwango cha kutisha na Mataifa yenye mafuta na Gesi Afrika yameanza kukamatia fursa kuongeza mapato yake kwa...
Mimi sio mpenzi sana wa siasa za watu ila napenda kukiri kuwa so far, kati ya watu ninaowaona wana akili na wanaweza kushika vizuri kijiti kutoka kwa Mama Samia coming 2030 ni Ndug. Hussein Bashe. Ana vision zisizotofautiana sana na Mama Samia hasa kwenye uwezeshaji, uwekezaji na biashara ivo si...
Ni lazima tupongeze pale ambapo mtu anafanya vizuri. Hussein Bashe ameleta muonekano mpya wa kilimo, ubunifu na uwekezaji.
Bashe akipewa muda kilimo cha Tanzania kitaenda mbali sana. Tatizo ni kwamba sehemu nyingine hakuna ubunifu wa kutosha. Huyu anajitahidi sana hasa ukizingatia ni kijana...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.