Mkazi wa Kalaki katika kaunti ya Ogwolo nchini Uganda amemnyonga mtoto wake wa miezi 9 baada ya kutopokea hela za serikali wanazopewa watu wasiojiweza kipindi hiki cha COVID19.
Mkuu wa Wilaya ya Kalaki, Paul Kalikwani amesema mtuhumiwa mwenye umri wa miaka 35 aliwaambia wanakijiji wenzake kuwa...
Inafahamika kuwa tume ya wataalamu iliyoteuliwa kushauri kuhusiana na ugonjwa huu ilitoa mapendekezo yake.
Inafahamika kuwa % kubwa ya mapendekezo ya tume hiyo yamepokelewa na yako katika hatua mbalimbali za utekelezaji.
Hata hivyo katika yote, mawili haya yangalipo yakielea angani yakiendelea...
Mkapa anapoelekea kutimiza mwaka 1 tangu kututoka yafuatayo ni baadhi ya mawaidha kutokea Mkapa foundation:
1. Wanathamini msukumo wa Mama Samia kupambana na janga hili la Corona kisayansi
2. Wanathamini msukumo mpya wa serikali kuelekea chanjo
3. Wanaelezea umuhimu wa chanjo
4. Wanaelezea...
SERIKALI imefanya maboresho ya miundombinu kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kwa ajili ya upimaji wa virusi vya corona kwa wasafiri wanaoingia nchini.
Hayo yamesemwa jana na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi wakati alipotembelea uwanja huo akiwa na...
SOCIAL DISTANCING
Hakuna asiyejua hii ndo key element ya kupunguza maambukizi ya magonjwa yanayofanana na Corona. Nimeanza na hilo Tangazo hapo juu ili hili suala lieleweke kwa sababu tukiacha matangazo ya uwepowa Corona nchini ambayo yanahusishwa na "Kujenga Mazingira ya kupata misaaa" kutoka...
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Dorothy Gwajima amesema hadi kufikia Julai 8, 2021 jumla watu 408 walibainika kuwa na ugonjwa wa corona huku 284 wakitumia mitungi ya oksijeni.
Dk Gwajima ametoa taarifa hiyo leo Jumamosi Julai 10, 2021 wakati akitoa elimu ya...
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye athibitisha mkoa wake kuwa na wagonjwa 12 wa CoVID-19, RC Andengenye amesema kuwa miongoni mwao 6 wanatibiwa hospitalini na wengine wamejitenga nyumbani.
====
Mkoa wa Kigoma umeripotiwa kuwa na wagonjwa 12 wa Corona ambapo wengine wamejitenga...
Waziri wa afya Dkt. Gwajima amesema wagonjwa wa Corona wanaongezeka hivyo wananchi wachukue tahadhari.
Kwa sasa elimu ya kupambana na Corona inatolewa na Wakuu wa Mikoa na Wilaya kwa sababu kirusi kinabadilika badilika na sisi tunabadili style ya kukikabili kwani Wizara ina mambo mengi sana ya...
Serikali imesema hali ya COVID19 ni janga na Mfumo wa Huduma za Afya umekufa. Hospitali za muda mfupi zimeanzishwa kote Nchini humo lakini Wizara ya Afya inasema hazitoshi, na wana changamoto ya utoaji Oksijeni
Taifa hilo limekuwa likirekodi idadi kubwa ya maambukizi ambapo visa 9,823 na vifo...
Mh Freeman Mbowe amesambaza video mitandaoni ikimuonyesha akiweka wazi kabisa ugonjwa uliomuua kaka yake Charles Mbowe, kuwa ni COVID 19, huu ndio uongozi wa kupigiwa mfano, Mh Mbowe ameamua kuweka wazi jambo hili ili kuweka ushuhuda wa uwepo wa Corona nchini Tanzania.
Mbowe sasa rasmi ni...
Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Aifello Sichalwe amewaagiza Watumishi wote wa Afya katika Mamlaka za viwanja vya ndege kujilinda wenyewe kwa kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Corona kwa kuvaa barakoa, kunawa mikono mara kwa mara kwa sabuni na maji safi tiririka.
Dkt. Sichalwe...
Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Jonson amesema kuwa yeye ataendelea kuvaa barakoa katika maeneo ya watu wengiImage caption: Waziri Mkuu Boris Jonson amesema kuwa yeye ataendelea kuvaa barakoa katika maeneo ya watu wengi.
Waziri mkuu, Boris Johnson, alisema alitarajia kupunguza sheria za Covid...
Hatimaye serikali ya awamu ya sita ilitangaza rasmi uwepo wa ugonjwa hatari wa Corona hapa nchini. Hii ikienda sambamba na kutolewa kwa maelekezo thabiti ya hatua gani za kuchukuliwa tunaposubiria kuwasili kwa chanjo.
Hatua hii ni njema kabisa ya kupongezwa na kila mzalendo na hasa kila...
Habari hii hapa chini kuhusu ongezeko la maambukizi mpya ya corona huko Israeli, nchi iliyochanja raia wake wengi kiasilimia kuliko nchi nyingine yeyote duniani, inaonesha jinsi ambavyo Magufuli was all right kuhusu corona, namna ulivyo ugonjwa ambao itabidi tujifunze kuishi nao kama...
Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya kuhusu Serikali ulimwenguni kote kulegeza masharti ya Ugonjwa wa COVID19 mapema ikisema wanaofanya hivyo wapo hatarini kulipa gharama kubwa kwa kutaka maisha kurejea kama awali.
Onyo hilo limekuja kufuatia hofu juu ya Kirusi aina ya Delta ambacho...
Baada ya kuenea kwa maambukizi ya virusi vya corona duniani mwanzoni mwa mwaka jana, dunia ilianza kutafuta chanjo, na hadi kufikia mwishoni mwa mwaka, kampuni kubwa tano za Pfizer-BioNTech, Moderna, AstraZeneca na Johnson & Johnson zilikuwa zimetengeneza chanjo za kukabiliana na ugonjwa huo...
Kuanzia Jumatatu bila kuvaa barakoa stendi ya Magufuli hakuingiliki tena.
Hata hivyo inashangaza kwanini kuwataka wenye mabasi kuwa na sanitizers kwa ajili ya abiria.
Kama ilivyo kwa barakoa, afya ya mtu ni wajibu wake mwenyewe. Hizi za kutwishana majukumu ya wengine ndiyo chanzo cha kupalilia...
Corona ni ugonjwa hatari wa kuambukiza kwa njia ya hewa, Rais alitakiwa kufahamishwa kuwa sasa anaingia wodi ya wagonjwa wenye corona ili ajiandae kimwili na kiakili, pia ahiari mwenyewe kuingia au kutoingia wodi ile.
Rais ameonekana hadharani kushitushwa kwa kujikuta katikati ya wagonjwa wa...
Madaktari Bingwa wa magonjwa ya mfumo wa upumuaji wamesema kirusi cha wimbi la tatu la ugonjwa wa Covid-19, kimekuja na mbinu tofauti na za kificho kutokana na dalili zake kuu nne.
Dalili hizo zimetajwa kuwa ni:
Mate kukauka mdomoni,
Kupata vipele mikononi na miguuni,
Kuharisha na
Damu kuganda...
Je, ni kweli kwamba baada ya kufanya majaribio kwa watu waligundua kwamba mtu anatakiwa achanjwe mara 2 ndio awe na kinga tosha, ila baada ya utafiti sasa wamebadilika tena, wanasema unatakiwa uchanjwe mara 3 ndio uwe na kinga?
Kwahiyo ile kauli ya hayati kwamba tusubiri kwanza ilikuwa na mashiko?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.