Ndimi mimi Kitumbika, mtunzi wa mashairi,
moyoni nafadhaika, kuitunza hii siri,
leo ndiyo natamka, nitasema sighairi,
dunia yaenda kombo, zichukuliwe hatua.
kuna vita kila kona, watoto wawa yatima,
kwa wakubwa na vijana, majumbani wamehama,
duniani wauwana, wanayumbishwa na vyama,
dunia yaenda...