Unakuta mtu uko city centre kulingana na ubora wa nyumba yako anatokea mpangaji anakwambia sijui mbona kwa OMARY anapangisha chumba 50000 na vina umeme na maji wewe tu ndo unapangisha 60000.
kwa OMARY kwenyewe ndo hapo👆
alafu uje kwa ABDALAH 👇utake kupanga kwa bei hiyohiyo,,,,,.
kwa mfumuko...
Kwa sasa karibia kila kitu kimepanda bei hadi soda na hakuna matarajio ya bei kushuka.
Chanzo cha hali hii ni nini?
Wanasiasa mbona wako kimya siyo CCM wala Chadema hakuna anayehoji, kulikoni?
Maendeleo hayana vyama.
Ndugu zangu watz wenzangu nadhan mtakuwa nami juu ya kinachoendelea kwa sasa katika nchi yetu
Wafanyabiashara saiz wanajiamulia bei gan watupige na kila siku wanapandisha bei hasa wakijisikia kitu ambacho ni hatar sn kwa usalama wa nchi
Kibaya zaid pamoja na bei za vitu kupanda kila siku yan...
Bei ya nyama kwenye mji wa Mtwara manispaa ya Mtwara/Mikindani imepanda ghafla kutoka shilingi 8,000 kwa kilo ya nyama mchanganyiko hadi shilingi 9,000, nyama ya steki toka shilingi 10,000 hadi 12,000 kwa kilo moja.
Malalamiko ya mfumoko wa bei yamekuwa makubwa.
Kuanzia bei ya chakula, vipuri, mafuta, vifaa vya ujenzi nk.
Hii ni hali halisi sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania. Takwimu zinazotolewa na TBS zinaonesha kuwapo na ongezeko la bei za vitu mbalimbali. Hali hii ipo pia nchi nyingine kama...
Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara ameitaka tume ya ushindani FCC kutoa ripoti kwa Serikali ikieleza kwanini Vinywaji baridi na Vifaa vya ujenzi vimepanda bei.
Waziri ametoa siku 3 kwa ripoti ya Soda na siku 7 kwa vifaa vya ujenzi ziwe zimemfikia kwani inashangaza kusikia Soda zimeadimika...
Ndivyo hali ilivyo Zanzibar, watu walianza kuvimilia vumilia sasa kila mzanzibar analia na vitu vya chakula kupanda bei tena kwa speedi ya kutisha sana.
1. Mkate wa Boflo ambao ndio mkate kila mzanzibar anakula sasa ni Tshs 250/- badala ya 200/=
2. Mchele ambao ndio chakula kikuu kwa maisha ya...
Kama alivyoshindwa waziri Makamba kumsaidia rais kwenye suala la umeme na Nchemba umeshindwa vibaya sana kila kukicha vitu vinapanda bei kwa kasi ya ajabu bila wafanyabiashara kukemewa na mtu yoyote.
Kama una mshahara wa chini ya millioni 1 kujenga utakusikia kwenye bomba tu.
Hali mtaani inatisha sana, karibu kila kitu kimepanda bei, kuanzia maduka ya ujenzi hadi maduka ya vyakula, hadi pipi zimepanda bei.
Kipato cha Mtanzania kiko palepale na asilimia kubwa ya vijana hawana ajira wala kipato chochote.
Sahivi ukininunua mafuta ya elfu moja ya kupikia hayatoshi...
Haya maisha kadri mtu mmoja anavyozidi kukopa huko nje na kuleta pesa hizo humu ndani kumekuwa na mfumuko wa bei katika bidhaa nyingi sana. Yaani kila bidhaa masokoni madukani na popote bei imezidi kupanda kila wakati hadi kusababisha wananchi kuwa na maisha magumu kila kukicha. Hadi najiuliza...
Kwa siku za karibuni kila kitu kimepanda ukianzia vyakula, vifaa vya ujenzi, mafuta n.k. Nawauliza Ofisi ya Takwimu kwa sasa mfumuko wa bei bado ni single digit au double digit?
Habari mbaya sana Mtaani kila Kona Rais anasemwa vibaya na mambo yanaenda Kombo, Bei ya Vyakula kama Mahindi na Mchele vimepanda maradufu Ndani ya Awamu ya Samia.
Mafuta ya Kula Bei imeongezeka karibia nusu, Diesel imepanda na kusababisha Nauli kuongezeka Vijijini, Nguo na vitu vya kawaida...
Hapa Tanzania bwana siku hizi, kiila kitu utasikia lawama zinaenda kwa mama wa watu Rais Samia. Yani hata mahali hahusiki kabisa utasikia analaumiwa Mama wa watu kiasi kwamba tunajiuliza mnabebesha mizigo asiyostahili kiwa sababu yeye ni mwanamke na ninyi mmezoea viongozi wanaume au ndio hizo...
Tumeshuhudia kila kitu kupanda bei, ndio kila kitu kasoro vinywaji tu. Tulizoea kelele na ukosoaji mkubwa enzi za JPM na muhanga mkubwa kabisa akiwa ni JK.
Sioni hayo yakiwa kama zamani hii ina maana gani?
Kila kitu holela, bidhaa aina zote bei juu na ni ndani ya muda mchache sana, serikali imeshindwa kazi, ijiuzulu.
Mwaka jana pamoja na kovidi kutisha kwa kiwango cha hali ya juu hatukuwa na mfumuko wa bei kiwango cha sasa.
Inaonekana Serikali tayari mikononi mwa walanguzi
Habarini ndugu,
Hivi sasa bei za bidhaa kuanzia bidhaa za majumbani kama sabuni, mafuta na vinginevyo mpaka mbolea ,vifaa vya ujenzi n.k vimepanda bei.
Bei zimekua kubwa sana kiasi mtu wa kawaida kuzimudu inakua shida.
Vifaa vya ujenzi ambavyo vingi tunatengeneza hapa hapa nchini navyo...
Siku zote nimekuwa naamini kuwa mfumuko wa bei ni kitu kibaya hadi juzi kati nilipoona kinyume chake kwenye kitabu kimoja. Kabrasha hilo linasema kuwa mfumuko wa bei hadi wa 20 percent unasaidia kukuza uchumi.
Huu unasaidia kutengeneza ajira na kuchangamsha shughuli za kiuchumi. Linaendelea...
Forum kama hii ilitakiwa sahivi kuwe na mjadala mkali wa kuelezea kwanini kuna mfumuko wa bei na kutoa mapendekezo ya nini cha kufanya ili kutatua,badala yake naona kimya tu na mijadala myengine tu ndo imeshika hatamu.
Tusisahau historia ya Forum hii imekuwa ni chachu ya kuleta mabadiliko...
Kwa sasa kila kitu kimepanda sana. Hali ya maisha inazidi kuwa mbaya. Baada ya mwaka mmoja, kama hali itaendelea kuwa hivi, uchumi wetu utaanguka.
Hali mbaya ya kiusalama inayochochewa na uchumi ulioanguka kutokana na mfumuko wa bei itakuwa dhahiri.
Serikali na Taasisi zake, kwa bahati mbaya...
Bidhaa za nyama, gesi ya kupikia, mkaa na viazi mviringo zimetajwa kuongeza mfumuko wa bei kutoka asilimia 3.8 Agosti hadi asilimia 4.0 kwa Septemba mwaka huu.
Taarifa ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Oktoba 8 jijini Dodoma, imetaja bidhaa nyingine zilizoongeza mfumuko wa bei ni ngano na...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.