15% ya Bodi ya Mikopo; Sheria inasemaje?

Wakati naanza chuo nilijaza fomu ya mkataba wa kukatwa asilimia 8 ya mshahara.
Kama nimekatwa asilimia 15 mwezi huu je hizo asilimia zilizoongezeka nilizisaini wapi? Kama zile fomu za bodi ni mkataba je ongezeko la asilimia 15 nimekubaliana na bodi lini? Kinachotumika hapa ni ubabe.
 
Wewe unadhani ila mnatakiwa kulioa na watu wengine wasome sio kudhani dhani wakati mnakopeshwa mliona burudani vyuoni mliishi kwa burudani na kula bata kwenye kulipa mnalalamika.
Lipeni Maskini na wanyonge wengine watumie
 
"LHRC tunajiandaa kuandaa kesi kupinga malipo ya bodi ya mikopo ya 15% kwa waliopata elimu ya juu tutakuwa na kikao na mawakili jumanne next week saa 10 ofisi za LHRC karibuni mawakili pia mje kwa wingi."

Advocate Patience Mlowe
Fanyeni haraka
 
Hivi elimu bure hadi chuo kikuu haiwezekani?
 
Tume huru naitamani lakin itawezekana kwel maana Imaan imepotea kabisa kwa ..........
 
 
Chukulia mfano wa sheria ya road reserve ambayo ni mita 30. Mtu yyte atakaye jenga ndani ya mita 30 kutoka barabara kuu nyumba yake hubomolewa bila fidia. Je ikitokea sheria imebadilishwa na kuwa mita 60, waliojenga ndani hizo mita watalipwa fidia?
 
Wanasheria hasa TLS fuatilieni ukandamizaji huu.
 
Wewe unadhani ila mnatakiwa kulioa na watu wengine wasome sio kudhani dhani wakati mnakopeshwa mliona burudani vyuoni mliishi kwa burudani na kula bata kwenye kulipa mnalalamika.
Lipeni Maskini na wanyonge wengine watumie

Kwani tukilipa 8% hayo sio malipo?

Tunachokisema hapa sio kupinga kulipa,ni kuvunja mkataba.Sisi tumesaini 8% now wanataka tulipe 15% kinyume na makubaliano yetu
 
Kwani tukilipa 8% hayo sio malipo?

Tunachokisema hapa sio kupinga kulipa,ni kuvunja mkataba.Sisi tumesaini 8% now wanataka tulipe 15% kinyume na makubaliano yetu
Makubaliano vipi wewe acha siasa lipa pesa na wenzako watumie acha ubinafsi.
Nchi yetu ni ya mwanyonge na masikini hvyo tutumie wote
 
Makubaliano vipi wewe acha siasa lipa pesa na wenzako watumie acha ubinafsi.
Nchi yetu ni ya mwanyonge na masikini hvyo tutumie wote
dah!, ndugu wewe inaonekana elimu yako ni ndogo sana mkuu!, napata mashaka kua pengine hata kuandika unaandikiwa, watu wanaongea sheria humu sio siasa unazoleta, jua kua mkataba ni sheria kwaiyo kinacholalamikiwa humu ni cha kisheria na sio cha kisiasa kama unavyozani wewe na upeo wako, you are not a great thinker sijui kakuleta nani humus JF
 
kwenye swala la mkopo mkopeshaji ndo anahaki shida zenu ndo ziliwafanya mkope hvo mkopeshaji ndo anadictate.
Sasa kama mnaona mnaonewa hajafuata mkataba msilipe basi
 
Mahakama si zipo simuwasongeshe bodi mahakamani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…