Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 10,448
- 8,705
Unathibitisha tena kuwa wewe ni authority wa historia ya wakina Sykes. Na kuhusu wakina Sykes, nilijua kuhusu mchango wao kabla ya wewe kuandika. Tofauti na wewe unavyotaka kutuaminisha mapambano ya uhuru hayakuwa ya watu wa Gerezani peke yao. Hao wakina Sykes na wengine uliowataja wasingekubalika kwa wanyakyusa bila wakina Mwakangale, Kanda ya ziwa bila wakina Bomani, Kilimanjaro bila wakina Mbowe, mission quarter bila wakina Phombeah na sehemu nyingine ni watu kama wakina Kasanga Tumbi, Rupia wazee wako wasingeona ndani. Bila wakina Robert Makange na gazeti lake kazi ingekuwa ngumu. Mimi sikatai mchango wa wakina Sykes, Mwapachu na wengine. Ninachopinga ni wewe kuwavisha joho la udini wakati wengi wao walikuwa Nationalists kuliko wadini ndio maana waliwakubali watu kama Dr. Kyaruzi, Julius Nyerere, Oscar Kambona na wagalatia wengine tu katika mpambano wa kudai uhuru. Hao wakina Sykes walikuwa wapiga muziki, watu wa Klabu, leo unataka kuwageuza wapigania ukombozi wa waislamu na sio watanzania wote?Fundi...
Nimependa sana hii kuwa mimi siyo ''authority,'' historia ya uhuru wa Tanganyika bali ni ''authority,'' wa akina Sykes.
Umenikosha sana hapa.
Ulikuwa unajua mchango wa akina Sykes katika kupigania uhuru wa Tanganyika kabla mimi sijawaandika?
Historia ya TANU ya Kivukoni ilikuwepo toka 1981 na iliwafuta akina Sykes na wapigania uhuru wengi mbona hukusema kitu ulikuwa kimya?
Unajua kuwa umuhimu wa akina Sykes katika historia ya uhuru wa Tanganyika ni kuwa ni wao katika wale waasisi wa African Association ndiyo walioandika historia ya AA na kuacha nyaraka ambazo ndizo hizi nimezitumia kuandika historia yao na historia ya kuamka kwa Waafrika kudai haki zao katika nchi yao.
Huyu ni baba yao Kleist Sykes mwaka wa 1929.
Sasa njoo kwa watoto Abdul na Ally hawa wanaanza harakati 1942 wakiwa Burma.
Nimetumia nyaraka za Sykes kuandika historia ya TANU na historia ya Julius Nyerere.
Kuna yeyote mwenye ushahidi wa picha na nyaraka wa historia ya Nyerere katika TAA kuanzia alipokutana na Abdul Sykes 1952 na kutiwa katika uongozi wa juu 1953?
Umepata kuona au kusoma popote pale historia ya Nyerere kama nilivyoieleza katika kitabu cha Abdul Sykes?
Sikujua kama kurudisha historia ya zaidi ya miaka 50 iliyofutwa ni udini.
Vipi wale walioifuta historia hii na kuweka ya kwao nini kiliwasukuma kufanya hivyo?
Haikuwa uoga wa kuona kuwa Waislam watakuwa kila mahali katika historia ya TANU na kudai uhuru wa Tanganyika?
Kaa kitako jitulize na fikiri iweje Nyerere afikie mahali asahau hata kama alimkuta Abdul Sykes Secretary na Act. President wa TAA pale alipompokea Dar es Salaam 1952?
Asahau pia aligombea na yeye nafasi ya urais wa TAA.
Inawezekana vipi Nyerere atoe medali 3, 979 wakati anaacha uongozi na Abdul na Dossa hawamo katika orodha ile?
Unajua nini alisema alipoulizwa na watu wake wa karibu kuhusu hili?
Mimi nimewarejesha katika historia Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Sulemaiman Takadir, Sheikh Abdallah Rashid Sembe, Sheikh Mohamed Yusuf Badi, Halima Selengia, Tatu bint Mzee. Mama bint Maalim, Amina Kinabo, Nyange bint Chande, Zarula bint Abdulrahman kwa kukutajia wachache katika wanawake waliopigania uhuru wa Tanganyika.
Si akina Sykes peke yao.
Naijua historia kubwa ya Tanganyika kutoka kila pembe.
Sikuwapiga Mama Mkello na Mohamed Mkwawa picha sebuleni kwangu.
Picha hizo nimezipiga majumbani kwao Tanga nikiwa na Ann Lee.
Mimi haya mambo kaka nayajua na si kwa kuwa mimi nina akili kuwapita watu wengine.
Hii historia imekuwapo nyumbani kwetu mimi mdogo wala sikuwa najua nashuhudia jambo kubwa katika historia ya Tanganyika na Zanzibar.
Hivi hujajiuliza kwa nini akina Sykes walinifungulia mimi ile hazina ya nyaraka zao na si mtu yeyote yule.
Hivi unajua baada ya historia ya kweli kuwa hadhir kila mtafiti akienda kuwahoji akina Sykes na kutaka kuona nyaraka zao jibu lao ni, ''Mohamed Said keshaandika someni kitabu chake.''
Unajua kwa nini wanasema maneno haya?
Leo tunaisoma upya historia ya Nyerere na historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.
Hivi hujajiuliza kwa nini Dr. Ghassany alinichukua mimi kama msaidizi wake katika utafiti wa kitabu chake na si mtu mwingine yeyote yule?
Jiuilize maswali haya yote na jaribu kupata majibu.
Hivi unajua kuwa ni Abdul Sykes na Dossa Aziz ndiyo waliompeleka Nyerere Zanzibar kumjulisha kwa Karume?
Baba yangu alikuwa rafiki mkubwa wa Abdulaziz Twala na Jaha Ubwa wote hawa ASP na wanamapinduzi na waliuliwa baada ya mapinduzi.
Inawezekana kweli mimi si ''authority,'' lakini wengi wakitaka kujua mambo wanakuja kwangu hata jopo la Prof. Shivji walioandika Biography of Julius Nyerere walikuja kunihoji na nikawapa picha na baadhi ya Nyaraka za Sykes.
Hii ndiyo nafasi yangu katika historia ya Tanganyika na Zanzibar.
View attachment 2058609
Kulia Prof. Issa Shivji, Prof. Saida Yahya Othman na Dr. Ng'wazi Kamatha wakinihoji nyumbani kwangu kuhusu Julius Nyerere wakati wanatafiti maisha yake kwa ajili ya kitabu chake.
Kupiga picha na kuhojiwa na watu kama Issa Shivji hakukufanyi authority wa historia ya Tanganyika, bali authority wa sehemu ya historia ya Tanganyika. Badala ya kutuwekea mapicha ukinywa chai nao weka mahali walipo ku cite kama source ya maandiko yao! Wewe unatoa anecdotal evidence ambazo unajipa authority ambayo sio yako. Kitabu kuwa Library of Congress sio ushahidi kuwa wewe ni authority maana ile ni maktaba na inakusanya maandiko karibu yote yanayofanyika Marekani.
Unasema uliwaona wakina Sykes katika party zao wakati Ally Sykes alikuwa active katika muziki katika miaka ya mwisho ya 1940s ( ulikuwa haujazaliwa). Ally Sykes na Peter Bernard walitoa nyimbo zao 1947, Ally Sykes na bendi yake the Merry Blackbirds nao walitamba katika miziki ya dansi ya early 1950s wakati ulikuwa haujazaliwa maana ulienda middle school 1960s. Wewe tambia nyimbo za wakina Salum Abdallah Yazide, sio za Ally Sykes.
Unasema Dennis Phombeah alikuja baadae lakini unakiri kuwa kadi ya 5 ya chama cha TANU alipewa yeye. Ni yale yale ya kutaka kuwazima wagalatia.
Wewe unaona tu kuwa Nyerere aliwanyima medali ndugu zako waislamu, niambie kama aliwapa medali wakina Kyaruzi, Phombeah, Kirilo n.k. na wagalatia wengi tu waliopigania uhuru wa nchi ya Tanganyika. Unajifanya hauoni yaliyompata Oscar Kambona na wakina Kassanga Tumbo.
Mimi shida yangu na wewe ni pale unapotaka kutuaminisha kuwa ni ndugu zako wa kiislamu peke yao ndio waliopigania uhuru. Unafanya kosa lile lile ambalo wapambe wa Nyerere walitaka kutuaminisha kuwa ni yeye peke yake ndie aliyepambana na mkoloni. Ninachojua mimi ni kuwa wakina Sykes walipigania uhuru wetu kwa kushirikiana kikamilifu na wengine bila kujali dini, kabila au rangi zao. Watu kama nyinyi ndio mnataka ku distort mchango wao kwa kuingiza udini.
Amandla....