2025 pombe basi - ni kahawa majani ya chai na maziwa

Pombe zinatesa sana wakuu kama sisi wengine tukinywa ni kujuta tu namuomba sana MUNGU anipe njia ya kutoka katika hii hali
 
usijiendekeze kiongozi
jikane kidogo
fanya maamuzi magumu
omba sana kwa mola wako
Napambana sana namuimba sana Mungu huu mwaka niachane kabisa na vyombo kwanzia leo tarehe moja nisiguse kabisa
 
Pombe inatabia yakukupa majuto ikiwa inakupelekesha, hasa ukutane na zile kali za Manzese au Buguruni, huwa zinatesa sana na kuleta majuto mengi.

Ujinga mwingine, pombe zinakupa hamu yakufanyana, sasa muda zinapokupa hiyo hamu huwa hujali, kukamata dude unapiga pipe asubuhi unaamka na hang'over mbili, moja ya K na nyingine ya pombe, lazima utoe nadhiri ya kuacha pombe, ila ikikata sasa baada ya siku mbili tatu mzuka unarudi tena.

Commitment ya kuacha pombe inahitaji ujasiri sana, na wale msiokunywa hii kitu msijaribu kabisa maana addiction yake ni mbaya sana.

Mwenyezi Mungu akufanyie wepesi katika fikra zako hizi za kuacha pombe.
 
umesema vema kiongozi
Allah atujalie sote kutenda yakumpendeza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…