4% ya mapato kwenda Zanzibar kama Hoja ya Muungano

4% ya mapato kwenda Zanzibar kama Hoja ya Muungano

je ni kweli pesa iliyochangiwa na znz ndo iliyojengea jengo lao la bot znz?
Nimegundua humu jamvini huwa tunachangia amma kwa ushabiki au kwa kutokujua baadhi ya mambo. Afadhali umetoa mwanga. Chanzo cha mgao huu ni wakati EAC liyovunjika 1977 ilipokuwa inagawa mali zake kwa washirika. utakumbuka mgao wa Zanzibar uliingizwa Tanzania. Akatafutwa mshauri elekezi ambaye alishauri Zanzibar ipewe 4.5%. Bahati mbaya Serikali ikaamua 4% kwa kila jambo. Wakati tunadai hiyo 4% ni kubwa, pamoja na ufafunuzi huu, kuna jambo halisemwi na huwa hatutaki lisemwe; kwamba wakati wa kuanzisha BOT mwaka 1967 Zanzibar ilichangia 11.5% ya mtaji wa benki hiyo. Tokea wakati huo hakuna mgao wowote uliotolewa kwa Zanzibar kama mwanahisa mshirika mkubwa wa benki hiyo. Nadhani wakati tukijifaragua kwa dharau na kejeli tufike mahala tuukubali ukweli kwamba katika hili Zanzibar imedhulumiwa, inadhulumwa na itaendelea kudhulumiwa kwa jina kulinda muungano ikiwa hatutachukua hatua kurekebisha uendeshaji wa mambo yetu. Tuseme basi
 
Kuna mtu kasema kuwa TRA wanakusanya mpaka Zenji??? [emoji15]
TRA ipo Zanzibar, na inakusanya mapato. Ila baada ya migongano mingi ya kera miaka kadhaa nyuma ikaamuliwa kuwa mapato yanayokusanywa na TRA yabaki Zanzibar, ila bado hayo mapato yanayokusanywa Zanzibar hayafikii hata 20% ya hiyo 4%
 
Walioweka hesabu kwa vigezo hivi walikuwa realistic? Ugawiwe hata kama huchangii inawezekana wapi? Gharama za Majeshi ya Muungano tu pamoja ya kuwa ni siri kuu, sidhani kama ZNZ inaweza kuzihimili wenyewe. Na mimi nimetoa tu eneo moja kama mfano.
Kwa kumuongezea mwambie mishahara yote ya watumishi wa SMZ inaliowa na Tanganyika
 
TRA ipo Zanzibar, na inakusanya mapato. Ila baada ya migongano mingi ya kera miaka kadhaa nyuma ikaamuliwa kuwa mapato yanayokusanywa na TRA yabaki Zanzibar, ila bado hayo mapato yanayokusanywa Zanzibar hayafikii hata 20% ya hiyo 4%
Basi hao TRA wamelegea, kwamba TRA mapato ya Znz yanabaki znz ili yafanyeje? [emoji23]
 
yaani, kila mmoja akusanye mapato kwenye nafasi yake. kama ni watalii wanaenda zanzibar, wakatoe visa pale zanzibar kwasababu si nchi ile? kama ni kukusanya mapato basi kuwe na ZRA ya kwao, nchi mbili zikusanye mapato kila mmoja kwa nafasi yake halafu kila mmoja sasa achangie kwenye muungano.

litakalotokea hapo, zanzibar hawatakuwa na cha kukusanya zaidi ya visa za watalii kimuungano. mitandao ya simu watabaki na zantel yao tu ambao haitakuwa na faida kwasababu ya pupulation ya kisiwani, ni ndogo kufanya biashara hizo, the same applies kwa mabenki. tuishie kusema muungano unawafaidisha pande zote mbili na zanzibar inafaidika nao indirectly na wanakula kwa mgongo wetu sana.
Zanzibar wana bodivyao inayo kusanya mapato, inaitwa ZRB.sema sasa niwaoigaji kichizi, wanakusanya pesa wanatoa mifukoni mwao.
 
yaani, kila mmoja akusanye mapato kwenye nafasi yake. kama ni watalii wanaenda zanzibar, wakatoe visa pale zanzibar kwasababu si nchi ile? kama ni kukusanya mapato basi kuwe na ZRA ya kwao, nchi mbili zikusanye mapato kila mmoja kwa nafasi yake halafu kila mmoja sasa achangie kwenye muungano.

litakalotokea hapo, zanzibar hawatakuwa na cha kukusanya zaidi ya visa za watalii kimuungano. mitandao ya simu watabaki na zantel yao tu ambao haitakuwa na faida kwasababu ya pupulation ya kisiwani, ni ndogo kufanya biashara hizo, the same applies kwa mabenki. tuishie kusema muungano unawafaidisha pande zote mbili na zanzibar inafaidika nao indirectly na wanakula kwa mgongo wetu sana.
Zanzibar wana bidi yao inayokusanya mapato
 
TRA ipo Zanzibar, na inakusanya mapato. Ila baada ya migongano mingi ya kera miaka kadhaa nyuma ikaamuliwa kuwa mapato yanayokusanywa na TRA yabaki Zanzibar, ila bado hayo mapato yanayokusanywa Zanzibar hayafikii hata 20% ya hiyo 4%

Wafanye kuanzisha yao tu ZRA ishu imesolve tayari
 
Wanao ngangania huu muungano ni watanganyika siyo wa zanzibar na kila rais wa ccm asema yuko tayari kulinda mungano hata damu imwagike lkn mungano uwepo mashekhe wa uamsho wamo ndani kwa kutaka mamlaka kamili ya zanzibar
Watanganyika Hatuwezi kung'ang'ania muungano kwasababu hautunufaishi.
 
Usalama uliopo Mwanza unategemea ulinzi wetu ulio mikapani.
Umuhimu wa Mikoa ya Katavi,Songwe, Kigoma, Kagera, Mtwara, Mbeya, Kilimanjaro, Arusha, Mara, Rukwa, Tanga Pwani, Lindi na Ruvuma ni sawa sawa na Nchi ya Zanzibar ndani ya JMT.
Mpaka wetu wa Nchi katika Bahari Kuu unalindwa na vikosi vyetu vya Ulinzi na Usalama kwa pamoja na SMZ chini ya KMKM n. k hivyo ni wajibu wetu kuchangia.
Unajua kirefu cha KMKM?
 
Zanzibar ilikuwa nchi huru kabla ya Muungano, lakini ni mali halali ya Sultan wa Oman. Muungano ni ukuta tu uliojengwa kumzuia mwenye chake asidai haki yake aliyodhurumiwa na mapinduzi MATUKUFU. Zanzibar mkiona vema kujitenga mjue Sultani anaweza kuja kudai chake kama hajasamehe.
Zanzibar ni Mali ya watu weusi huyo sultan alikuja na kuiona Zanzibar ingalipo . Oman ndio Mali ya sultan. Sultan ni muarabu na wazanzibar asilia ni watu weusi . Katika awamu wa Samia Zanzibar itapaa kimaendeleo kwasababu ya 4% ya Jasho la watanganyika masikini wa Hukwo Rukwa. Muungano ni huu ilikuepo faida Kwa Zanzibar ili kuzuia sultan asirudi Zanzibar baada ya mapinduzi ya afro Shiraz's party. Ila kuhakika hauna faida yeyote Ile .
 
Kuna hoja nimekuta watu wanaongea, ni kuhusu kile ambacho mama amesema waziri wa fedha akakae na mwenzake wajadili na kusuluhisha katika kero za muungano. Ninaupenda sana Muungano,ninauunga mkono. lakini, nilijiuliza kitu kimoja, mimi kama mtu wa bara sitaki tupigwe pia kama wazenji wasivyopenda kupigwa.

1. hivi Zanzibar inachangia kitu gani kwenye kwa Tz bara kinachowastahilisha tuwagawie hiyo asilimia? Bara inafaidika nini toka Zanzibar?

2. Mgao unaoongelewa ni wa misaada toka nje, au ni mapato ya nchi (pato la madini bara, TRA, navitu vyote vya bara)?

3. kama ni mapato ya nchi, kwani TRA haipo Zanzibar ya kikwaokwao?

4. proportion ya wingi wa watu + ukubwa wa eneo vinazingatiwaje wakati wa kugawa pato ya muungano?

5. kwanini marais waliopita walikuwa hawashughulikii hilo jambo, kulikuwa na kitu gani walichokiona? including one of them who was Zanzibari.

6. kwa anayeelewa, naomba anieleweshe hili jambo kwasababu kama vile tu zanji wasivyopenda kupigwa, mimi kama mtu wa bara pia sipendi na sikubali.

Naongea hivi kwasababu watu wanavyoongea mtaani wanaongea kama vile kwasababu mama ni mzanzibar basi wanaona wazanzibar wanaweza kupitisha vitu vingi sana ambavo vilikuwa havipiti kwa awamu za nyuma ambazo nyingi hazikushikwa na rais wa zanzibar.

MWISHO: siongei kwa ubaya, wala kwa unafiki, ila ninaongea kinachoongelewa mitaani. Ninamwamini mama atafanya makubwa. Ila naamini tunatakiwa kuwa na busara ya hali ya juu kwasababu kuna mambo tunaweza kufanya tukifikiri tunajenga muungano kumbe ndio tunauweka kwenye mazingira ya kubomoka kabisa.
Tutalipa 4% kwa misingi gani?
Kwani Muungano tunaulipia mahari?
 
Kuna hoja nimekuta watu wanaongea, ni kuhusu kile ambacho mama amesema waziri wa fedha akakae na mwenzake wajadili na kusuluhisha katika kero za muungano. Ninaupenda sana Muungano,ninauunga mkono. lakini, nilijiuliza kitu kimoja, mimi kama mtu wa bara sitaki tupigwe pia kama wazenji wasivyopenda kupigwa.

1. hivi Zanzibar inachangia kitu gani kwenye kwa Tz bara kinachowastahilisha tuwagawie hiyo asilimia? Bara inafaidika nini toka Zanzibar?

2. Mgao unaoongelewa ni wa misaada toka nje, au ni mapato ya nchi (pato la madini bara, TRA, navitu vyote vya bara)?

3. kama ni mapato ya nchi, kwani TRA haipo Zanzibar ya kikwaokwao?

4. proportion ya wingi wa watu + ukubwa wa eneo vinazingatiwaje wakati wa kugawa pato ya muungano?

5. kwanini marais waliopita walikuwa hawashughulikii hilo jambo, kulikuwa na kitu gani walichokiona? including one of them who was Zanzibari.

6. kwa anayeelewa, naomba anieleweshe hili jambo kwasababu kama vile tu zanji wasivyopenda kupigwa, mimi kama mtu wa bara pia sipendi na sikubali.

Naongea hivi kwasababu watu wanavyoongea mtaani wanaongea kama vile kwasababu mama ni mzanzibar basi wanaona wazanzibar wanaweza kupitisha vitu vingi sana ambavo vilikuwa havipiti kwa awamu za nyuma ambazo nyingi hazikushikwa na rais wa zanzibar.

MWISHO: siongei kwa ubaya, wala kwa unafiki, ila ninaongea kinachoongelewa mitaani. Ninamwamini mama atafanya makubwa. Ila naamini tunatakiwa kuwa na busara ya hali ya juu kwasababu kuna mambo tunaweza kufanya tukifikiri tunajenga muungano kumbe ndio tunauweka kwenye mazingira ya kubomoka kabisa.
Point zako nimezipenda kinamna ila ungenikosha kama ungeliuliza kwa muangalio wako huo huo, jee deni la tanzania kwa nchi za nje linawahusu vipi zanzibar, ilhali matumizi yote ya mikopo hiyo hufanywa tanzania bara? Zanzibar hupata mikopo yao kutoka nje ya nchi kivyao sasa kwa nini wahusishwe na malipo ya madeni ya Tanzania?
 
Mkuu umefika Zanzibar? umeona wabara waliokuepo Zanzibar? 80% ya wafanykazi wa mahoteli ni wabara. sasa hiyo hoja ya kuwa wazanzibar bara wapo wengi haina mashiko, mana hata Zanzibar wabara wapo wengi
Wabara wanabaguliwa sana na wa zenji. Sababu ya wafanyakazi wengi kutoka bara ni kwa sababu wazenji ni wavivu hawataki kufanya kazi.
 
Zanzibar ipo ZRB inayokusanya mapato, lakini inakusanya mapato kwa mambo amabyo sio ya muungano tu.

Kwa maana TRA pia wako na idara hiyo ya mapato katika vitu visivyo vya muungano au???
Mambo haya nadhani ZRB Inasimamia:
Mapato ya Serikali za mitaa, usafiri na barabara Ingawa kuna TANROADS. Pia Kilimo, mifugo pamoja na Uvuvi. Lakini Ishu ya Magereza na biashara baina ya wazalishaji wa chini na kati.

Lakini swali la Msingi:
Je TRA Inatenganisha hivi vitu kwa upande wa Tanganyika au ndo sandakalawe Amina??? [emoji16][emoji16][emoji15]
 
Wabara wanabaguliwa sana na wa zenji. Sababu ya wafanyakazi wengi kutoka bara ni kwa sababu wazenji ni wavivu hawataki kufanya kazi.

Walinikata jina langu Kisa tu Mimi ni Msukuma na Nina shahada ya Awali ya Teknolojia wanewapitisha Astashahada ya Teknolojia wakina Kombo na Hamdani [emoji2959]
 
Wabara wanabaguliwa sana na wa zenji. Sababu ya wafanyakazi wengi kutoka bara ni kwa sababu wazenji ni wavivu hawataki kufanya kazi.

Kama wanabaguliwa sana kama unavyosema wangekwenda na wakaendelea kuishi?

Na tukisema wabara ni mambumbumbu hawawezi kufanya Biashara ndiomana wapemba wakawa wamejaa huko nami nitakua nimekosea?
 
Walinikata jina langu Kisa tu Mimi ni Msukuma na Nina shahada ya Awali ya Teknolojia wanewapitisha Astashahada ya Teknolojia wakina Kombo na Hamdani [emoji2959]

Mkuu ulikatwa wapi?

Favorism ni kitu ambayo ipo kila sehemu, hayo ni mambo ya kawaida tu kwenye Dunia.
 
Back
Top Bottom