5G vs Starlink

Starlink internet itapatikana mpaka Mpitimbi ndani ndani, hawa watoa huduma wetu wa sasa sehemu nyingi nje ya miji hakuna mtandao au mtandao uko chini
Yes starlink ipo vizuri huko vijijini, na hata vijijini siku hizi intranet fresh tu. ila mjini sidhani kama starlink atakuwa msaada
 
Kwa kujibu swali lako, 5g itanisaidia Kasi. Alafu mbona simu za 5G zipo hata za midrange zimejaa pale kariakoo. Hata starlink itahitaji simu ya smart ili kujiunga. Samsung a50s zipo za 5g kibao TU.
Starlink ni Dish, ni internet ambayo unatumia eneo moja tu, kama upo nyumbani utatumia tu hapo nyumbani huwezi tumia kwenye simu.
 
Boss Wakikuacha sana Starlink basi bei ni 100,000-150,000 kwa mwezi ila kikawaida anacharge around 200,000-300,000 kwa mwezi. Hizo za 30,000 ni kujipa tu Matumaini.
 
Kwa kujibu swali lako, 5g itanisaidia Kasi. Alafu mbona simu za 5G zipo hata za midrange zimejaa pale kariakoo. Hata starlink itahitaji simu ya smart ili kujiunga. Samsung a50s zipo za 5g kibao TU.
Hapo sasa unajipendelea. Na zingatia,bishara ni kuwafikia wengi si kulenga eneo furani
 
Starlink ina speed ya 5G sasa sijui unazungumzia kitu gani...

Starlink speed ni kuanzia 50 Mbps hadi 250 Mbps na 5G ni 50Mbps hadi 2 Gbps...

Starlink ina speed ya 5G na ikiingia Tanzania utaona inaitoa 5G kwa speed, hio 2Gbps sio kwa nchi kama Tanzania, labda Korea , Japan n.k.... usitegemee 5G ya bongo itafika hata 300 Mbps...

Latency starlink imeachwa kidogo ni kwa sababu starlink inafanya kazi mahala popote, hata uwe pori au kijiji cha aina gani hakuna network yenyewe inashika tena kwa speed kubwa... Latency sio issue zinaachana kwa milliseconds, i dont care kuhusu milliseconds..

Starlink ni nextlevel.. usifananishe na uchafu unaitwa 5G ya bongo...

Ukija kwenye price starlink ni kinara...

Huna akili...
 
Huduma Yoyote Ikiwa na Mshindani Inakuwa Bora Huduma za Mitandao yetu ni Hovyo kwa kuwa hwana mshindani wao..

Hiyo 3G nA 4G yenyewe Imewashinda kusambaa leo unataka wasambaze 5G labda Miaka 30 Ijayo
5G ipo Tanzania, useme tu coverage sio kubwa ipo katikati ya Miji. Huwezi pata speed ya 1GBps ama zaidi bila 5G.
 
Wacha Starlink akuje akili zikae sawa

Achana na 5G ..inachotakiwa ni Internet yenye kukidhi vigezo kwa Nchi nzima.

Haiwezekani uwe Ulanga /Mahenge uanze kuwaza kupitia pages zako za biashara na mails then na kifurushi uko nacho.
 
Latency ya starlink ni 100ms mpaka 150ms ukanda wetu, kusema imeachwa kidogo si kweli, 3G kibongo bongo ikiwa vizuri inafika hadi 30ms ina maana ina speed mara 3-5, 4G na 5G nyingi zina latency way better Than starlink.

Pia 5G speed kama una jiweza ipo hadi 1gbps Tigo na Voda pia walikua na option ya ku upgrade 1Gbps.
 
Starlink ni Dish, ni internet ambayo unatumia eneo moja tu, kama upo nyumbani utatumia tu hapo nyumbani huwezi tumia kwenye simu.
Unajidanganya sana, starlink wana mini starlink hivi sasa ina ukubwa wa tablet, na unazunguka nayo kwenye gari, au popote, hio 5G inafika hata nje ya mji?
 
Watoa huduma hawawezi kuwekeza zaidi ya hapa kwa sababu hawana ushindani, waje Starlink Satellite internet 🛰️ kuongeza ushindani wa biashara ya internet nchini. Nafikiri hii imekaa vizuri.
Watoa huduma sio tatizo tatizo ni TCRA na Serikali, kuna kipindi watoa huduma walikuwa wanatoa bundle bure before TCRA kuleta mambo ya be elekezi...

 
Kwa Nini tusiwape muda Hawa watoa huduma wetu kuwekeza 5G Yao iwepo kila mahali hapa nchini? Sababu Kwa Dunia ya Sasa hivi inahitaji internet yenye Kasi na 5G ipo vizuri kwenye Hilo?

Sent using my Iphone 16 pro max
Who cares hata wakija wengine elfu tisini ? Iwapo hatutoi gharama ya kodi zetu na ni mfanyabiashara mwenyewe ndio anafanya good luck to him / Ingawa mfanya biashara huyu ni mpuuzi na emotional hivyo sio vema kumtegemea pekee kuwa na back up...., Anaweza kuamka na kuamua kuzima....
 
Tatizo mna siasa nyingi yote ni kuiogopa starlink..
Starlink kwa huko US na EU n.k wana latency hadi 25ms ikizidi 60ms, hata kam Africa ni latency ya 100ms mbona ni nzuri tu!! Na uzuri wataboresha na sisi tutafika hizo 30ms...

Ndio maana nasema i dont care kuhusu latency zkiachama milliseconds, not a big deal, as long as speed ni nzuri inatosha sana...

Hizo 5G za 1Gbps mpaka ujiweze ulipie millions ndipo upewe hio speed tena baadhi ya maeneo ya mijini...
Upuuzi huu...

Starlink speed ni nzuri hata uwe kijiji hakina network.. utawatch youtube, stream netflix bila kukwama tena HD, wakati 3G inajifikiria...



Starlink ni bora zaidi...

Hio 5G wengi wenu speed mtapata ni 100 Mbps ambapo hata mwenye starlink atawazidi...


Halafu mnazungumza as if starlink ipo slow, starlink inaizidi hata hii 4G yetu ya hapa... Ina kasi sana..
 
Unajidanganya sana, starlink wana mini starlink hivi sasa ina ukubwa wa tablet, na unazunguka nayo kwenye gari, au popote, hio 5G inafika hata nje ya mji?
Kwamba unazunguka na dish, waya, power supply router etc kama hivi unakula mishe mishe zako
While you get poor latency, poor upload speed, and paying more than 1 million to get it?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…