8th Sullivan Summit Arusha Tanzania

8th Sullivan Summit Arusha Tanzania

Mkutano wa Sullivan: Rais Kikwete apongeza Vodacom Tanzania
Na Mwandishi Wetu, Arusha
�

RAIS Jakaya Kikwete ameipongeza Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania, kwa ushiriki wake mzuri katika mkutano wa Leon Sullivan unaomalizika leo jijini hapa.

�

''Ninawapongeza Vodacom Tanzania kwa ushiriki wao katika mkutano huu,'' alisema Rais Kikwete.

�

Alisema ushiriki wa sekta binafsi katika mkutano huo ni wenye manufaa na mchango mkubwa na kwamba, sekta hiyo ina nafasi kubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi.

�

Naye Hope Masters, Mtendaji Mkuu na Rais wa Taasisi ya Sullivan, aliipongeza Vodacom jinsi ilivyoshiriki na kwamba, ni mmoja wa wadau waliochangia mafanikio ya mkutano huo.

�

�Kwa namna ya pekee naipongeza Vodacom Tanzania kwa ushiriki wake wa karibu, ambao umeweza kufanikisha mkutano huu,� alisema Masters.

�

Vodacom Tanzania, ni mtandao rasmi wa mawasiliano katika mkutano huo ambao ulifunguliwa juzi usiku na Rais Kikwete. Pia, imetengeneza kituo maalum cha mawasiliano kinachotumiwa na Waandishi wa Habari kutoka sehemu mbalimbali za dunia wakiripoti matukio ya mkutano huo.

�

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Dietlof Mare alisema, Vodacom Tanzania inajisikia faraja kufanya biashara zake Tanzania, kutokana na sababu mbalimbali, zikiwemo amani, utulivu na ukuaji endelevu wa uchumi.

�

Mare alisema, mazingira hayo na sera nzuri za serikali, zimewezesha kampuni hiyo kuwekeza na hatimaye kukua mwaka hadi mwaka na kuwa mtandao unaoongoza.

� �

Alisema kwa kutambua Tanzania ni nchi inayoendelea na inayokabiliwa na changamoto katika ukuaji wa sekta mbalimbali, Vodacom Tanzania imekuwa ikiwekeza kuhakikisha maendeleo ya watu yanapatikana.

�

Alisema idadi ya wateja hai wa Vodacom Tanzania, wamekuwa wakiongezeka kila mwaka, hivi sasa Vodacom ina zaidi ya wateja �milioni nne, huku ikitoa ajira za moja kwa moja na zile ambazo sio za moja kwa moja kwa zaidi ya Watanzania 50,000.
 
Sokomoko,
Mimi ndiye critic mkubwa sana wa Andrew Young, Masters na mke wake na kuna thread moja nzuri tulipochangia mada hii, lakini naomba niseme ya kuwa siwezi kuwalaumu, at the end of the day kama wataamua kutake advantage of our weakness na kutunyonya, itabidi iwe hivyo. Let them be Americans first! Na sisi tuwe Tanzanians first! Tukisikia criticism ya Jk na CCm isiwe eti oo huyu ni mpinzani, ooo JF ni ya Chadema , bali iwe ni wake up call na kujirekebisha. Tulipoandika na kutoa tahadhari miezi 6 iliyopita na akina Jasusi kwamba Sullivan summit ni uzushi mtupu na wahusika ni matapeli tulipingwa humu ndani, sasa naona watu wanashangaa usanii wao! hate to say I told you so!!
 
Pamoja makampuni ya Simu kutokulipa kodi ipasavyo JK awamwagia sifa Vodacom
 
siamini kama tunatakiwa kutegemea chochote kutoka kwa hawa watu wa marekani. siamini, na sijaona hata mtu mmoja anaeweza kuwa investor hapa kwa wale waliokuja. nafikiri uwezo wao kifedha ni sawa tu na wakwetu. jana walichanga michango ya kuchangia shule ya msingi, huwezi amini, hata milion 60 hazikufika. wakati mafisadi ya kibongo yakianza kuchangisha wakati wa kampeni za ccm, huwa haipungui milion 300 kwa fundraising moja. sasa hawana cha ziada, pamoja na kwamba wanaweza wakasaidia kidogo kama wanaweza lakini, kututangazia utalii huko wanakoenda. hata hivyo siamini kama wanaweza, siamini kama wanaweza wakagaramikia kututangazia sisi utalii huko kwao, kwa hela gani waliyokuwa nayo? Chris turker mwenyewe walimtangaza kuwa ni tajiri, amechangia dola elfu tano. nimeshuhudia wengi wakichangia hadi dola mia tano, ambazo kama tukiamua wabongo kuanza kuchangisha(kama tulivyochanga wakati wa hawa wakina mama madaktari wanaotibu kansa ya matiti),yaani mewata, tunaweza tukafanya vyema kuliko wao.tusifikiri kuwa kuja kwa watuwa nje ndo mafanikio, pamoja na kwamba ni vizuri kama wanakuja.

hoja yangu moja ni hii, hata hawa watalii wakija sana, kama wakitangaza, siamini kama zile tourist companies za wahindi na wabongo wachache kule Arusha wanalipa kodi ya kutosha kwenye selikali ili tunufaike watz wote. kiufupi, mimi naona huu mkutano hauna manufaa sana. na hawa jamaa wamekuja kutalii zaidi. asante.

Naomba niongezee mkuu kwenye hoja yako yenye mshiko!
Hawa jamaa amekuja holiday hawakuja kama wawekezaji ila walikuja kwa ajili ya mapumziko mafupi.
 
Ndio maana wengi wa watanzania walioshiriki ni wachuuzi (vendors)............

Ina maana Muungwana kaingizwa mjini??? mbe!
 
Hivi mnaweza kuamini sasa hivi wakitambulisha nchi zilizoshiriki katika mkutano huu katika kikao cha marais Membe ametaja...United Republic of Tanzania na bila kusahau Zanzibar! I though ingekuwa Tanganyika na Zanzibar if that is the case.... Yaani yupo hapo anachemsha ile mbaya! Hawajui hata marais waliopo na alisahau kuwatambulisha!

....shekhe hukuona walikuwa wanatoss?? uliangalia glass ya membe aliweka nini ndani?? labda gongo ndo maana alilewa kiasi akasahau kuwa mdomo kazi yake nyingine ni kuongea....
 
Hao wanaopomgezwa inasemekana hawalipi kodi. Nani anatafuna hiyo pesa? Haya makampuni yaseme kama hayalipi yatozwe faini ili iwe fundisho.
 
....shekhe hukuona walikuwa wanatoss?? uliangalia glass ya membe aliweka nini ndani?? labda gongo ndo maana alilewa kiasi akasahau kuwa mdomo kazi yake nyingine ni kuongea....

Ingawa sina hakika kama Waziri Membe anakunywa gongo, lakini jana huyu waziri alipwaya sana. Alifanya utambulisho uliokiuka baadhi ya vipengele vya protokali. Akaanzia delegates, na Zanzibar kaitambulisha kama state. Halafu Rasi Kikwete akaingilia kati kumuomba Membe atambulishe Makamu wa Rais na mawaziri Wakuu waliokuwepo, Membe akaja kubwabwaja tena kutambulisha kama alivyoagizwa. Mara akamalizia kuwatambulisha Marais ambao nadhani angeanzia hao. Makubwa!!! Akiondolewa pale akawekwa Mh Mahiga aliyebobea sijuiatalalamika!!!???
 
Jamani wana JF nasikitika kusema mkutano mzima wa sullivan kwa upeo wangu kulikuwa ni utapeli na blabla nyingi,

Kwanza watanzania wa kawaida mpaka leo hii ukimuuliza maana ya mkutano huo na faida zake hajui.Jana waliulizwa na mtu kama are they practising what they preach yaaani waliishia kujiuma uma na hope akasema yeye anafeelings sana na Africa........mimi i dont get it.

Wabongo wengi hawajaelimishwa nini maana ya mkutano huu,Jana Olenaiko anahojiwa anasema eti anashangaa sana watu wamefanya kama ni maonyesho ya biashara wakati hiyo ni summit,jamani kweli ungekuwa mjini pale uone watu walivyohangaika kutengeneza mabanda kwa hela nyingi na bidhaa mpaka zina lebo za sullivan ........sidhani kama wangefanya hivyo bila kuambiwa.....kwa kifupi wamewamislead sana wafanyabiashara wadogo no wonder walitaka kumpiga mama Nagu kwa hasira.


Jamani mimi kwa upeo wangu hakuna kitu ......it was usaniiii...nimesikitika sana sana ........tutachezewa akili mpaka lini?????
 
siamini kama tunatakiwa kutegemea chochote kutoka kwa hawa watu wa marekani. siamini, na sijaona hata mtu mmoja anaeweza kuwa investor hapa kwa wale waliokuja. nafikiri uwezo wao kifedha ni sawa tu na wakwetu. jana walichanga michango ya kuchangia shule ya msingi, huwezi amini, hata milion 60 hazikufika. wakati mafisadi ya kibongo yakianza kuchangisha wakati wa kampeni za ccm, huwa haipungui milion 300 kwa fundraising moja. sasa hawana cha ziada, pamoja na kwamba wanaweza wakasaidia kidogo kama wanaweza lakini, kututangazia utalii huko wanakoenda. hata hivyo siamini kama wanaweza, siamini kama wanaweza wakagaramikia kututangazia sisi utalii huko kwao, kwa hela gani waliyokuwa nayo? Chris turker mwenyewe walimtangaza kuwa ni tajiri, amechangia dola elfu tano. nimeshuhudia wengi wakichangia hadi dola mia tano, ambazo kama tukiamua wabongo kuanza kuchangisha(kama tulivyochanga wakati wa hawa wakina mama madaktari wanaotibu kansa ya matiti),yaani mewata, tunaweza tukafanya vyema kuliko wao.tusifikiri kuwa kuja kwa watuwa nje ndo mafanikio, pamoja na kwamba ni vizuri kama wanakuja.

hoja yangu moja ni hii, hata hawa watalii wakija sana, kama wakitangaza, siamini kama zile tourist companies za wahindi na wabongo wachache kule Arusha wanalipa kodi ya kutosha kwenye selikali ili tunufaike watz wote. kiufupi, mimi naona huu mkutano hauna manufaa sana. na hawa jamaa wamekuja kutalii zaidi. asante.

You have made the point.Hapa tumeliwa kwenye mchezo wa karata tatu.Wangemsujudu Manji anagetoa zaidi ya hizo walizo sanya,Maana yeye analipa milion 100 watu waingia bure kuangalia mpira Kirumba Mwanza

This is boiling an empty pot expecting to get syrup
 
Ingawa sina hakika kama Waziri Membe anakunywa gongo, lakini jana huyu waziri alipwaya sana. Alifanya utambulisho uliokiuka baadhi ya vipengele vya protokali. Akaanzia delegates, na Zanzibar kaitambulisha kama state. Halafu Rasi Kikwete akaingilia kati kumuomba Membe atambulishe Makamu wa Rais na mawaziri Wakuu waliokuwepo, Membe akaja kubwabwaja tena kutambulisha kama alivyoagizwa. Mara akamalizia kuwatambulisha Marais ambao nadhani angeanzia hao. Makubwa!!! Akiondolewa pale akawekwa Mh Mahiga aliyebobea sijuiatalalamika!!!???

Membe naye alitia aibu sana kwanza hana confidence alikuwa kama mtoto,aliulizwa kwa nini ameisoma zanzbar kama nchi anasema eti si wameiandika kwenye list,imagine hata hakupitia list ile na yeye hawezi kureason kuwa lile ni kosa,,,alafu mimi simchukii ila amechemsha sana kuliko watu wote,,,jamani sio huyu mliyosema ana exposure na anaelewa mambo ya protokali...AMEBOA SANA SANA
 
angalao labda wauzaji wa rejareja, watoa huduma, hoteli wamefaidika na utalii. lakini hata mimi nimeona ni wachovu tu. hakuna mpango. wa kumfanya raisi ajishirikishe.
anyway, it was a big holiay to them.
I would like to see the budget.
 
..watu wa hoteli especially mr mrema ..kafaidika sana mkumbuke ana hold full or in trust main hotel zilizolaza wageni naongelea NGURDOTO,IMPALA, NA NAURA SPRINGS...Kama at least alilaza wageni 600..and kila mgeni akitumia at least 500$ per day ....bado zile dhifa alizoandaa ets...the guy must have made minimum 3million $ in minimal kwenye huu mkutano.....anyway its good kwa mtanzania mwenzetu..pesa ingeenda yote nje!.....

we need bigger convention meeting centre ..AICC should think of a hall of at least 10,000pax..baada ya sulllivan nchi nyingi zitapenda kufanyia mikutano arusha!!
 
..watu wa hoteli especially mr mrema ..kafaidika sana mkumbuke ana hold full or in trust main hotel zilizolaza wageni naongelea NGURDOTO,IMPALA, NA NAURA SPRINGS...Kama at least alilaza wageni 600..and kila mgeni akitumia at least 500$ per day ....bado zile dhifa alizoandaa ets...the guy must have made minimum 3million $ in minimal kwenye huu mkutano.....anyway its good kwa mtanzania mwenzetu..pesa ingeenda yote nje!.....

we need bigger convention meeting centre ..AICC should think of a hall of at least 10,000pax..baada ya sulllivan nchi nyingi zitapenda kufanyia mikutano arusha!!

Mzee Phillemon.. hii kauli yako ya mwisho msingi wake hasa ni nini?
 
..mwanakijiji..............huu mkutano uiliandaliwa na kamati maalum semi autonomy iliyokuwa FOREGN AFFAIRS..coodinator alikuwa mama mmoja mrembo ..she is good..ila jina nimesahau..[something like lailah]..wajumbe walikuwappo kina kassim mpenda et al

another poin for moderators...this thread has been here for the last one year itakuwa vema hizi sub thread zote za SULLIVAN ziletwe huku..kwa kuwa mkutano umeisha itasaidia kuwa na reference point moja!!!...ni maoni tu !
 
Mzee Phillemon.. hii kauli yako ya mwisho msingi wake hasa ni nini?

mwanakijiji motive ya hoja yangu ya ukubwa waukumbi imetokana na fact kuwa ..ukumbi wa simba pamoja na kupanuliwa umekuwa mdogo..wajumbe walikuwa wanazidi 3,000 hopefully ..wakati ule ukumbi uwezo wake hata wajumbe 2000 ni tatizo...that was bad!!

alafu pia mjue siku hizi kwa miji ya kitalii kama arusha catalogue ni CONFERENCE TOURISM ..wageni wanapenda party ,kutembelea vivutio sambamba na mikutano ..pia ni nzuri kwa communities za pale zitafaidika na kuonesha tamaduni zao ie ngoma....fikiria mkipata mikutano angalau sita kwa mwaka ya wajumbe 10,000....yaani wajumbe 60,000 kwa mwaka ...na at least kila mjumbe analipa dola 1,200 za ushiriki na malazi ...thats a big push to economy....LAZIMA WIZARA YA FOREGN WAAMUE HARAKA KUJENGA CONVENTION CENTRE PALE AICC...hata ikibidi ile ambayo wanataka kujenga dar wangeijenga ARUSHA ....kwa kuanzia ...wageni9 wengi huvutiwa na hali ya hewwa na pia hizo opportunity za kutembelea ngorongoro,na seringeti!!!...tukichelewa nairobi watatupiga bao...maana nao wana hali inayofanana na arusha ,..na wantangaza kuwa mgeni akifika kenyatta kufanya mkutano pia napata fursa ya kutembelea seringeti na ngorongoro..ambazo zipo karibu!@
 
mwanakijiji motive ya hoja yangu ya ukubwa waukumbi imetokana na fact kuwa ..ukumbi wa simba pamoja na kupanuliwa umekuwa mdogo..wajumbe walikuwa wanazidi 3,000 hopefully ..wakati ule ukumbi uwezo wake hata wajumbe 2000 ni tatizo...that was bad!!

alafu pia mjue siku hizi kwa miji ya kitalii kama arusha catalogue ni CONFERENCE TOURISM ..wageni wanapenda party ,kutembelea vivutio sambamba na mikutano ..pia ni nzuri kwa communities za pale zitafaidika na kuonesha tamaduni zao ie ngoma....fikiria mkipata mikutano angalau sita kwa mwaka ya wajumbe 10,000....yaani wajumbe 60,000 kwa mwaka ...na at least kila mjumbe analipa dola 1,200 za ushiriki na malazi ...thats a big push to economy....LAZIMA WIZARA YA FOREGN WAAMUE HARAKA KUJENGA CONVENTION CENTRE PALE AICC...hata ikibidi ile ambayo wanataka kujenga dar wangeijenga ARUSHA ....kwa kuanzia ...wageni9 wengi huvutiwa na hali ya hewwa na pia hizo opportunity za kutembelea ngorongoro,na seringeti!!!...tukichelewa nairobi watatupiga bao...maana nao wana hali inayofanana na arusha ,..na wantangaza kuwa mgeni akifika kenyatta kufanya mkutano pia napata fursa ya kutembelea seringeti na ngorongoro..ambazo zipo karibu!@

very keen observation...

a. Kwanini hizo kumbi ziwe mradi wa kufanywa na Serikali (MOFA) badala ya kuacha sekta binafsi? Unafikiri sekta binafsi inaweza kufaidika kwa kuwa na ukumbi wa kisasa wa namna unayoielezea?

b. Vipi kuhusu transportation within the city ni rahisi sana kutoka point A kwenda B bila misuko suko na kushikana mikono ili kuvuka barabara?

c. Kwanini mkutano haukuandaliwa na BET?
 
Hao wanaopomgezwa inasemekana hawalipi kodi. Nani anatafuna hiyo pesa? Haya makampuni yaseme kama hayalipi yatozwe faini ili iwe fundisho.

Dua,
Vodacom= Lowassa, Rostum. Go figure.
 
very keen observation...

a. Kwanini hizo kumbi ziwe mradi wa kufanywa na Serikali (MOFA) badala ya kuacha sekta binafsi? Unafikiri sekta binafsi inaweza kufaidika kwa kuwa na ukumbi wa kisasa wa namna unayoielezea?

b. Vipi kuhusu transportation within the city ni rahisi sana kutoka point A kwenda B bila misuko suko na kushikana mikono ili kuvuka barabara?

c. Kwanini mkutano haukuandaliwa na BET?


...upande wa usafiri kwenye jiji la arusha hali haikuwa mbaya ...msongamano ulidhibitiwa..na watu wa kule ni wasikivu pale wanapotangaziwa utaratibu...viwanja vya ndege viwili vilitosha sana kurahisisha safari za kutoka nje kupitia KIA na kwenda mbugani kupitia uwanja wa ndege wa KISONGO[KILIMO ANGA]...

BET ni specialized zaidi kuandaa maonyesho lakini kuna haja ya foregn na BET kushirikiana...

kingine tulichojifunza ni kuwa nchi za west africa wana combine TOURISM CONFERENCES, na CULTURAL FESTIVALS.. kupromote utalii wao..tena utaona kuwa wenzetu weuzi wanapenda sana cultural festivals...[mfano mzuri unaoshipukia ni zanzibar film festivals na DHOW COUNTRIES FESTIVALS]..tuboreshe na kutangaza hizi...na kuanzisha myingine kwenye miji ya kiutalii kama ARUSHA na BAGAMOYO.....Sioni kwa nini..kama bagamoyo wasiandae tamasha la utumwa na kuingia kwa ukiristo ukanda wa afrika mashariki...kanisa la kwanza lilkijengwa pale..na hawa watalii kutoka marekani wanapenda sana matamasha yanayoelezea haya.......au kwanini ARUSHA nao wasije na tamasha lao kuelezea tamaduni za makabila adimu kama maasai,baribaig,sonjo ,ambayo yana unique cultures ambazo hazijawa spoiled..
 
Mimi nashangaa badala yakutangaza au kukuza biashara ya TTCL wanatumia Vodacom!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom