90 Minutes in raid on Entebbe: Tukio la ukombozi wa mateka wa Israel Nchini Uganda - THUNDERBOLT

90 Minutes in raid on Entebbe: Tukio la ukombozi wa mateka wa Israel Nchini Uganda - THUNDERBOLT

OPERESHENI ENTEBE/OPERESHENI THUNDERBOLT

Tukio moja la dharura ambalo lilitokea mnamo juni 27 1976, wakati Yitzhak Hofi akiwa ndio kwanza amepokea kijiti cha ukurugenzi wa MOSSAD, ilikuwa ni dharura iliyohitaji suluhu kwa ustadi mkubwa, pamoja na bahati. Vijana mchanganyiko wenye asili ya kiarabu na wengine kijerumani waliteka ndege ya shirika la ndege la ufaransa, Air France Airbus 300. Ndege ilianzia Tel Aviv hadi Athens – Ugiriki, ambapo watekaji waliingia wakijifanya abiria wa kawaida kwa ajii ya safari ya kuelekea Paris, Ufaransa. Kwa kuwa safari ilianzia Tel Aviv, abiria wengi kati ya 248 waliokuwamo walikuwa waisrael.
Watekaji walijitambulisha kama mawakala wa ukombozi wa Palestina,(PLO) kisha wakatoa amri kwa rubani kurusha ndege hadi Entebe, Uganda ambapo dikteta jeuri na katili Idd Amin Dada alikuwa akitawala, naye alikubaliana na kitendo hicho na kuwapokea na kuwahifadhi watekaji. Masharti ya watekaji yalikuwa kuachiwa huru kwa wafungwa 40 wa kipalestina waliofungwa katika jela za Israel, pamoja na wafungwa 13 katika nchi zingine.
Abiria wa ki-israeli pamoja na wayahudi na wahudumu wa ndege waliokuwa waisrael, jumla wakiwa zaidi ya 100 walitenganishwa, kisha abiria waliobaki wapatao 148, raia wa nchi zingine waliachiwa huru pamoja na rubani, wakarudishwa Paris, Ufaransa.

Huko Paris, abiria wale wa nchi zingine walipofika walihojia na mawakala wa intelijensia wa Ufaransa na Israel. Wana-intelijensia walijifunza kadiri ilivyowezekana kuhusu watekaji na mahali walipohifadhiwa wayahudi na raia wengine wa Israel.
Wakati huo, Israel tayari ilikuwa na uhusiano wa siri na utawala wa Jomo Kenyatta wa Kenya. Uhusiano huo ulitengenezwa kwa makubaliano na jasusi David Kimche ambaye alitumia mwanya wa urafiki wa Jomo Kenyatta na mkulima wa kizungu mwenye asili ya Scotland, Bruce McKenzie. Mkulima huyo, Bruce Mckenzie alikuwa mzungu pekee kwenye baraza la Kenyatta, huku akitumiwa na shirika la intelijensia la Israel, MOSSAD. David Kimche aliyefanikisha urafiki huo anatajwa pia kutoa msaada kwa waasi waliopindua serikali ya kisultan ya Zanzibar, mnamo Januari 12 1964. Kazi yake ya kuzugia katika misheni zake za barani Afrika ilikuwa ‘kujifanya’ mwandishi wa habari wa kiingereza.
Basi kwa ya urafiki huo, Mossad kwa haraka walifika Kenya na kupatiwa msaada wa ndege ya mtu binfasi wa kenya ambayo waliittumia kupita juu ya anga la Entebe na kuchukua picha za maeneo ya mji huo ili kujua pa kuingilia na pa kutokea.

Wiki moja baadae, julai 4 1976, makomandoo wenye sare za kijeshi wa Israel, kikosi maalumu kilichoitwa sayeret Matkal (Scouting Generals) walitekeleza misheni ya kuwakomboa mateka kwa utulivu, ustadi mkubwa na kasi ya ajabu.
Ndege 2 kubwa za mizigo zilitua uwanjani kisha makomandoo 100 wa kiisrael walishuka wakiwa na magari yenye rangi za jeshi la Uganda kisha kuelekea eneo walipo watekaji. Wakati watekaji wakiduwaa na magari yale wakijua ni asjari wa Uganda, walistukia risasi zikimiminwa mfullulizo. Ndipo majibishano ya risasi yalipoanza huku michezo ya kutafutana na kujificha ikiendelea. Baada ya dakika 90, mateka waliokolewa. Watekaji wote 7 walikufa, askari 45 wa Idd Amin waliuawa na wengi kujeruhiwa. Mateka wanne walipoteza maisha, makomandoo wanne wa Sayeret Matkal walijeruhiwa na mmoja, aliyekuwa kiongozi wa kikosi hiko, Yonathan (Yoni) Netanyau, alifariki kwenye tukio hilo. Ilikuwa ni desturi katika vikundi vyote vya kijeshi na kiintelijensia vya Israel, kwamba kiongozi anakuwa mstari wa mbele katika misheni za hatari, kwanza kwa ajili ya kuwapa nguvu wengine na pia ni namna yao ya kuenzi utamaduni ulio katika simulizi zao za kale. Yonathan Netanyau alikuwa kaka wa Benjamin (Bibi) Netanyau, waziri mkuu wa sasa wa Israel. Waisrael hawakuwahi kuwa na furaha kubwa kuliko usiku ule wakati ndege za kijeshi zikitua kuwarudisha ndugu zao. Wanadamu wengi, marafiki na maadui walitamani kuwa waisrael usiku ule. Dunia iliitamani Israel kwa kukataa matakwa ya watekaji na kuwaokoa raia wake waliokuwa mateka katika ardhi ya mbali.

Sehemu ya Kitabu; Spies Against Armageddon, by Dan Raviv.
Imetafasiriwa na Christopher Cyrilo.
 
Tukio moja la dharura ambalo lilitokea mnamo juni 27 1976, wakati Yitzhak Hofi akiwa ndio kwanza amepokea kijiti cha ukurugenzi wa MOSSAD, ilikuwa ni dharura iliyohitaji suluhu kwa ustadi mkubwa, pamoja na bahati. Vijana mchanganyiko wenye asili ya kiarabu na wengine kijerumani waliteka ndege ya shirika la ndege la ufaransa, Air France Airbus 300. Ndege ilianzia Tel Aviv hadi Athens – Ugiriki, ambapo watekaji waliingia wakijifanya abiria wa kawaida kwa ajii ya safari ya kuelekea Paris, Ufaransa. Kwa kuwa safari ilianzia Tel Aviv, abiria wengi kati ya 248 waliokuwamo walikuwa waisrael.
Watekaji walijitambulisha kama mawakala wa ukombozi wa Palestina,(PLO) kisha wakatoa amri kwa rubani kurusha ndege hadi Entebe, Uganda ambapo dikteta jeuri na katili Idd Amin Dada alikuwa akitawala, naye alikubaliana na kitendo hicho na kuwapokea na kuwahifadhi watekaji. Masharti ya watekaji yalikuwa kuachiwa huru kwa wafungwa 40 wa kipalestina waliofungwa katika jela za Israel, pamoja na wafungwa 13 katika nchi zingine.
Abiria wa ki-israeli pamoja na wayahudi na wahudumu wa ndege waliokuwa waisrael, jumla wakiwa zaidi ya 100 walitenganishwa, kisha abiria waliobaki wapatao 148, raia wa nchi zingine waliachiwa huru pamoja na rubani, wakarudishwa Paris, Ufaransa.

Huko Paris, abiria wale wa nchi zingine walipofika walihojia na mawakala wa intelijensia wa Ufaransa na Israel. Wana-intelijensia walijifunza kadiri ilivyowezekana kuhusu watekaji na mahali walipohifadhiwa wayahudi na raia wengine wa Israel.
Wakati huo, Israel tayari ilikuwa na uhusiano wa siri na utawala wa Jomo Kenyatta wa Kenya. Uhusiano huo ulitengenezwa kwa makubaliano na jasusi David Kimche ambaye alitumia mwanya wa urafiki wa Jomo Kenyatta na mkulima wa kizungu mwenye asili ya Scotland, Bruce McKenzie. Mkulima huyo, Bruce Mckenzie alikuwa mzungu pekee kwenye baraza la Kenyatta, huku akitumiwa na shirika la intelijensia la Israel, MOSSAD. David Kimche aliyefanikisha urafiki huo anatajwa pia kutoa msaada kwa waasi waliopindua serikali ya kisultan ya Zanzibar, mnamo Januari 12 1964. Kazi yake ya kuzugia katika misheni zake za barani Afrika ilikuwa ‘kujifanya’ mwandishi wa habari wa kiingereza.
Basi kwa ya urafiki huo, Mossad kwa haraka walifika Kenya na kupatiwa msaada wa ndege ya mtu binfasi wa kenya ambayo waliittumia kupita juu ya anga la Entebe na kuchukua picha za maeneo ya mji huo ili kujua pa kuingilia na pa kutokea.

Wiki moja baadae, julai 4 1976, makomandoo wenye sare za kijeshi wa Israel, kikosi maalumu kilichoitwa sayeret Matkal (Scouting Generals) walitekeleza misheni ya kuwakomboa mateka kwa utulivu, ustadi mkubwa na kasi ya ajabu.
Ndege 2 kubwa za mizigo zilitua uwanjani kisha makomandoo 100 wa kiisrael walishuka wakiwa na magari yenye rangi za jeshi la Uganda kisha kuelekea eneo walipo watekaji. Wakati watekaji wakiduwaa na magari yale wakijua ni asjari wa Uganda, walistukia risasi zikimiminwa mfullulizo. Ndipo majibishano ya risasi yalipoanza huku michezo ya kutafutana na kujificha ikiendelea. Baada ya dakika 90, mateka waliokolewa. Watekaji wote 7 walikufa, askari 45 wa Idd Amin waliuawa na wengi kujeruhiwa. Mateka wanne walipoteza maisha, makomandoo wanne wa Sayeret Matkal walijeruhiwa na mmoja, aliyekuwa kiongozi wa kikosi hiko, Yonathan (Yoni) Netanyau, alifariki kwenye tukio hilo. Ilikuwa ni desturi katika vikundi vyote vya kijeshi na kiintelijensia vya Israel, kwamba kiongozi anakuwa mstari wa mbele katika misheni za hatari, kwanza kwa ajili ya kuwapa nguvu wengine na pia ni namna yao ya kuenzi utamaduni ulio katika simulizi zao za kale. Yonathan Netanyau alikuwa kaka wa Benjamin (Bibi) Netanyau, waziri mkuu wa sasa wa Israel. Waisrael hawakuwahi kuwa na furaha kubwa kuliko usiku ule wakati ndege za kijeshi zikitua kuwarudisha ndugu zao. Wanadamu wengi, marafiki na maadui walitamani kuwa waisrael usiku ule. Dunia iliitamani Israel kwa kukataa matakwa ya watekaji na kuwaokoa raia wake waliokuwa mateka katika ardhi ya mbali.

mr mkiki.
 
HAKIKA HII NDO MISHENI YA KIJESHI BORA ZAIDI KUWAHI KUFANYIKA AFRIKA MASHARIKI.

Siku ya tarehe 27 June mwaka 1976 ilianza kama siku nyingine yioyote ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa katika mji mkuu wa nchi ya Israel Tel Aviv, uwanja ujulikanao kama Ben Gurion International Airport. Moja kati ya ndege ambayo ilikuwa inafanya safari yake katika siku ya elo ilikuwa ni ndege ya kampuni ya Air Frace ambao walikuwa na ndege yao ya Air France Flight 139 ambayo ni ndege aina ya Airbus A300B4-203 yenye namba ya usajili mkiani F-BVGG (c/n 019).

Ndege hii ilikuwa inafanya safari yake katika siku ya leo kutoka Tel Aviv na ilikuwa inatarajiwa kutua katika uwanja wa ndege wa Charles DE Gaulle International Airport jijini Paris, Ufaransa. Baada ya taratibu na protokali zote za uwanja wa ndege kukamilika na abiria wote kukwea kwenye ndege, ndege iliruka kutoka kiwanjani ikiwa na abiria 190 ndani yake pamoja na ‘crew’ ya watu 12 (Marubani na wahudumu) ambamo asilimia kubwa ya abiria walikuwa ni raia wa Israel pamoja na watu wenye asili ya kiyahudi. Ndege iliruka kutoka Tel Aviv mpaka jijini Anthens, Ugiriki ambapo ilichukua abiria wengine wapatao 58. Baada ya hapo ndege iliruka pasipo kujua kwamba kati aya abiria hao 58 waliowachukua Ugiriki ndani yao kulikuwa na abiria wanne ambao walikuwa ni wanachama wawili wa kikundi cha Popular Front For The Liberation of Palestine – External Operations (PFLP-EO) kutoka Plaestina na wanachama wawili wa kikundi cha Revolutionary Cells kutoka nchini Ujerumani.

Baada ya abiria wote kukamilisha utaratibu na kupanda ndani ya ndege, ndege iliondoka uwanjani Athens mnamo amjira ya saa 6 na dakika 30 mchana kuelekea Paris, Ufaransa.
Dakika chache baada ya ndege kuruka rubani mkuu wa ndege ambaye ndiye alikuwa ameshikili ‘usukani’ Bw. Michel Bacos akasikia kelele nyuma ya ndege wanakokaa abiria (cabin). Ili kujiridhisha kwamba kila kitu kiko sawa, rubani Michel Bacos akamuagiza msaidizi wake mmoja wapo ambaye ndiye alikuwa injinia wa ndege aende kuangalia nini kilikuwa kinaendelea.
Mara tu baada ya msaidizi huyo kufungua mlango wa mbele wa chumba cha marubani, alikutana uso kwa uso na bastola usoni mwake iliyoshikiliwa na mtu ambaye mkononi alikuwa amebeba bomu la kurusha kwa mkono. Huku msaidizi huyo akiwa bado ameshikwa na bumbuwazi, mtu huyu mwenye bomu mkononi na bastola (jina lake anaitwa Wilfred Bose raia wa Ujerumani) alimsukuma yule injinia nakumrudisha tena ndani ya chumba cha marubani na kisha yeye mwenyewe pia kuingia.

Mara tu baada ya kufika ndani ya chumba cha marubani, akawaweka chini ya ulinzi marubani ambao bado walikuwa kwenye mshituko wa mshangao na kisha kumnyanyua rubani msaidizi kutoka kwenye siti yake na kukaa yeye. Baada ya kukaa kwenye siti ya rubani msaidizi kitu cha kwanza alichokifanya haramia huyu Wilfre Bose ni kuchukua microphone ambayo marubani huwa wanatumia kutoa matangazo kwa abria, na baada ya kuiweka microphone akatoa tangazo lake la kwanza, kwa sauti ya utulivu iliyojaa lafudhi nzito ya kijerumani, akawasema; *“..kuanzia sasa ndege hii inaitwa HAIFA 1, badala ya Flight 139..”*

Haifa ni eneo (mji) maarufu ulipo kaskazini mwa nchi ambayo abiria wengi waliopanda kwenye ndege hiyo walitambua kama Israel lakini watekaji hawa na watu wengine duniani wakitambua kama Palestina.

Mara tu baada ya tangazo hili kusikika kwenye vipaza sauti vya ndege, abiria wote licha ya kuwa kwenye mshituko mkubwa wa ghafla lakini moja kwa moja waling’amua ni nini kilikuwa kinaendelea. Flight 139 au Haifa 1 kama alivyoibatiza aliyetoa tangazo, ilikuwa imetekwa na maharamia.

Baada ya Tangazo hili, haramaia Wilfred Bose akamuamuru rubani Michel Bacos kuendesha ndege kuelekea mji wa Bengazhi, nchini Libya.
Baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Bengazhi nchini Libya, ndege ilitumia karbia masaa saba uwanjani hapo kwa ajili ya kujaza ndege mafuta. Katika masaa hayo saba kuna mwanamama Patricia Martel mwenye asili ya Uingereza lakini akiwa ameolewa nchin Israel miaka michache iliyopita alifanya ‘kituko’ ambacho kilikuja kuwa na manufaa sana baadae. Wakati ambao ndege inaendelea kujaza mafuta kwa masaa yote hayo, huyu mama ambaye ni nesi kwa taaluma, alianza kulalamika juu ya maumivu ya tumbo yaliyopitiliza. Aliwaeleza watekaji kwamba ana ujauzito. Maharamia haya yakaruhusu wahudumu wa ndege wamuhudumie mwananmke mwenzao kwa vile ambavyo wataweza kwa kuzingatia kwamba ana mimba. Baada ya kuhudumiwa kwa karibia saa nzima, Patricia akatumua ujuzi wake wa unesi akafanya alicho kifanya na ghafla akaanza kutoka damu kiduchu sehemu za siri. Baada ya damu hizi kidogo kuanza kumtoka na kulalamika kuwa maumivu yamemzidia ndipo hapa ambapo wahudumu wa ndege wakaripoti kwa maharamia kuwa mimba ilikuwa imetoka.

Kwa huruma na ili kuepusha taharuki ndani ya ndege maharamia hawa wakamuachia huru mwanamama Patricia Martel hapo uwanja wa ndege mjini Bengazhi ili aweze kupata uangalizi mzuri zaidi wa kidaktari.

Lakini ukweli ni kwamba Patricia hakuwa na mimba wala hakuwa na maumivu yoyote tumboni, alichokifanya ilikuwa ni uigizaji pamoja na kuchanganya utaalamu wake wa fani ya unesi na kuweza kuwahadaa maharamia hao.

Baada ya kuachiwa Patricia alikuwa ni mtu wa kwanza muhimu kutumiwa na Mossad kujua taarifa sahihi zaidi kuhusu nini hasa kilikuwa kinaendelea ndani ya ndege, kulikuwa na watekaji wangapi, jinsia zao, silaha zao na vingine vyote ambavyo alifanikiwa kuviona.
Baada ya hapa Bose akamuamuru tena rubani Michel Bacos kurusha tena ndege angani pasipo kumueleza kuwa wanaeelekea wapi.

Wakiwa angani ndipo alianza kumpa maagizo wapi hasa anataka waelekee. Upande wa abiria kwenye cabin ambao nao walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi na maharamia wengine waliosalia, wao hawaku wanafahamu hata ni wapi walikuwa wanaeleke. Ndege ilikuwa inaruka angani kwa karibia masaa 24. Abiria wengi walianza kuhisi labda ndege ilikuwa inaruka kuelekea China au labda Siberia, na vichwani mwao walikuwa wanajiuliza kwa nini walikuwa wanapelekwa huko.

Lakini laiti kama wangelijua mahali ambako walikuwa wanapelekwa basi wangetamani ndege hiyo ielekee kweli china.

Baada ya ya takribani masaa 24 ndege kuwa angani tangu iruke kutoka Bengazhi nchini Libya, hatimaye abiria walisikia ndege ikitua na kugusa Runway ya kiwanja cha ndege mahali fulani dunia walipowasili lakini wakiwa hawafahamu ni mwapi hasa walikuwa.

Baada ya matairi ya ndege tu kukanyaga lami za runaway na abiria kufungua ‘pazia’ (shutters) kwenye vioo vilivyopo pemnbeni mwa siti zao na kuangalia nje, mara moja wakaelewa wako wapi. Nje uwanjani kwenye lami, kulikuwa kumesimama lijitu la miraba minne lenye ngozi nyeusi tiiii likiwa na walinzi wa kijeshi na wengine waliovalia nguo za kiraia likiwa limezungukwa pande zote na walinzi hao. Mtu huyu mwenye umbo la kutisha kwa kipindi hiki alikuwa anajulikana ulimwenguni kote kutokana na matendo yake na ukatili wake. Kwa kutupa jicho mara moja tu haukuweza kukosea kujua kuwa pale kwenye lami uwanjani, alikuwa amesimama Generali Nduli Idd Amin Dadaa, ‘Field Marshal’. Swali lilokuwepo vichwani mwao lilikuwa limejibiwa tayari, wamepelekwa kwenye ardhi ya moja ya watawala ‘watemi’ na katili kuwahi kutokea juu ya uso wa dunia. Walikuwa nchini Uganda.

Baada ya ndege kusimama abria wote 248 ambao wengi wao walikuwa ni raia wa Israel na wayahudi, walishushwa kutoka kwenye ndege na moja kwa moja kupelekwa ‘terminal’ ambayo kwa wakati huo ilikuwa haitumiki. Mpaka muda huu wakang’amua kwamba hawakuwa ‘abiria’ tena kama ambavyo waliondoka Tel Aviv, bali sasa walikuwa ni mateka wa maharamia haya ya kijerumani, palestina na jeshi la Uganda.

Nchini Israel katika jamii ya masuala ya usalama walikuwa wako kwenye bumbuwazi kuu, matukio ya dizaini hii huwa ni ya kushtukiza na yanatokea kipindi ambacho ‘haujajiandaa’. Pia kwa kipindi hiki bado Idara ya Ujasusi ya Mossad hawakuwa na Intelejensia ya kutosha za nchi nyingi za kiafrika, akili yao na nguvu yao yote ilikuwa kwenyekudhibiti juhudi za nchi za kiarabu kufuta Israel kutoka kwenye eneo hilo walilopo. Kwa hiyo kitendo cha raia wao wengi kiasi hiki kutekwa na kupelekwa Africa kilikuwa si tu na changamoto ya namana gani wanawaokoa bali pia kulikuwa na changamoto ya uwepo wa Intelijensia ya kutosha kuhusu eneo la Entebbe, Uganda kuweza kufanya oparesheni yoyote ya kijeshi.

Ndipo hapa ambapo waziri mkuu wa kipindi hicho wa Israel Yitzhak Rabin akaitisha kikao cha maafisa wa ngazi za juu wa jeshi na Mossad na kuwauliza swali moja tu, “…tunafanayeje?”

Tayari zilikuwa zimepita siku tatu tangu ndege ya Air France Flight 139 kuondoka Tel Aviv na hatimaye kutekwa baada ya kuruka jijini Athens iliposimama kuchukua abiria. Lakini pia zilikuwa zimepita siku mbili tangu ndege hii kutua katika uwanja wa ndege wa Entebbe nchini Uganda. Katika siku zote mbili hizi tangu ndege hii itue uwanjani hapa, rais wa Uganda Idd Amin Nduli Dadaa alikuwa anafika uwanjani hapo kila siku “kuwajulia hali” mateka hao.

Kwa muda wa siku hizi zote mbili tangu ndege itue uwanjani hapo, magaidi hawa walioiteka ndege kwa kushirikiana na jeshi la Uganda kuchunguza majina ya kila abiria kama ambavyo yalikuwa yameandikwa kwenye pasport. Lengo lao la kufanya hivi ilikuwa ni kujaribu kufahamu uraia wa kila mateka waliye naye. Baada ya kufanya uchambuzi huu wa passport zote, hatimaye siku hii ya tatu, yaani tarehe 29 June 1976 kiongozi wa magaidi hawa Wilfred Bose akiwa na karatasi mkononi aliingi ndani ya terminal ambayo walikuwa wanaitumia kuwahifadhi mateka na kisha akaanza kusoma majina ya kila abiria. Alichokuwa anakifanya ni kusoma majina ya mateka ambao passport zao zilionyesha walikuwa ni raia wa Israel. Lakini pia alisoma majina ya mateka wengine ambao licha ya passport zao kuonyesha kuwa hawakuwa raia wa Israel lakini walikuwa na majina ya kiyahudi. Pamoja na hao pia mateka wote ambao walikuwa na uraia pacha na uraia huo mmojawapo ukiwa ni Israel basi nao waliunganishwa kwenye list hii.

Baada ya kuwatenganisha raia wote wa Israel na kuwaweka kwenye chumba kingine peke yao hapo hapo kwenye terminal, kuna mwanadada raia wa Ufaransa aliyeitwa Jocelyne Monier yeye jina lake halikuitwa kwenye ile list ya wanaotakiwa kutengwa kwenye chumba kingine (Waisrael na Wayahudi). Lakini ‘boyfriend’ wake alikuwa ni Muisrael na aliitwa jina na kutengwa na wengine katika kile chumba kingine. Mwanadada huyu ili kuonyesha kumtia moyo mpenzi wake na kupinga huu ubaguzi uliokuwa unafanywa na hawa magaidi, kwa hiari yake alijipeleka kwenye chumba cha mateka wa Kiisrael. Si mwanadada huyu pekee ambaye alifanya kitendo hiki cha ushujaa, lakini pia kulikuwa na mwanamama mwingine aliitwa Janet Almog (rai wa Marekani) na mateka mwingine aliyeitwa Jean-Jacques Mimouni (raia wa Ufaransa) nao kwenye kuonyesha hali ya kuwaunga mkono wenzao waliotengwa kwenye chumba kingine na kupinga ubaguzi uliokuwa unafanywa na maharamia hawa, nao walijipeleka kwa hiari yao kwenye chumba ambacho mateka hao walikibatiza jina “Chumba cha Waisrael”, ambacho mateka wote walijua fika kwamba kuna jambo baya maharamia hao walikuwa wamepanga kulifanya.

Licha ya maharamia kwa kushirikiana na jeshi la Uganda kufanya uchambuzi huu wa kina kuhusu uraia wa kila mateka waliye naye, lakini walifanya kosa kubwa sana ambalo lilkuja kuwagharimu sana hapo baadae. Kwenye uchambuzi wao wote huu walioufanya walishindwa kumng’amua mateka mmoja mwanajeshi wa Israel ambaye alikuwa ana uraia pacha na siku hiyo alikuwa anatumia passport ambayo sio ya Israel. Mateka huyu alikuja kuwa muhimu sana huko mbeleni kuwapatia Mossad Intelijensia mujarabu kabisa kuhusu watekaji, jengo wanaloshikilia mateka, na namana wanavyoshirikiana na jeshi la Uganda.

Siku iliyofuata yaani June 30, maharamia haya wakawaachia mkupuo wa kwanza wa mateka wasio raia wa Israel au wayahudi. Katika mkupuo huu wa kwanza waliachia mateka 48 ambao walikuwa ni wazee, watoto na akina mama wenye watoto wadogo.

Baada ya mkupuo huu wa kwanza wa kuwaachia mateka hawa wachache, maharamia wakaweka wazi matakwa yao ili waweze kuachia mateka wengine. Kwanza kabisa walitaka walipwe fedha kiasi cha dola za Kimarekani milioni 5. Na pili walitakakuachiwa kwa wafungwa 53 wenye asili ya kipalestina wanaotuhumiwa kwa ugaidi, ambao kati yao 40 walikuwa kwenye jela za Israel na 13 katika nchi nyingine za Ulaya. Watekaji hawa wakatoa ‘ultimutum’ kwamba kama matakwa yao hayatatekelezwa ndani ya masaa ishirini na nne yajayo (mpaka tarehe 1 July saa 8 mchana) basi wataanza kuua raia wa Israel mmoja baada ya mwingine.

Dunia nzima ni kama ilisimama kwa masaa kadhaa kutokana na sintofahamu iliyogubika kila mahali. Sintofahamu hii ililetwa na ukweli kwamba, ilikuwa inajulikana wazi kwa miaka yote kwamba Israel wana sera ya kutofanya mazungumzo au makubaliano na Magaidi. Kwahiyo kila mtu alikuwa nafahamu kuwa kuna uwezekano mkubwa ndani ya masaa 24 yajayo ulimwengu ukashuhidia watu zaidi ya 200 wakichinjwa kama kuku.

Nchini Israel kikao cha dharura cha baraza la mawaziri kilikuwa kimeitishwa na waziri Mkuu Yitzhak Rabin kujadili kuhusu hatua za kuchukua kuokoa raia wake ambao wameshikiliwa mateka huko uwanja wa ndege wa Entebbe, Uganda.

Hali ya kikao ilikuwa tete sana kutokana na kila dakika waliyokuwa wanaitumia kujadili ndivyo ambavyo walikuwa wanaikaribia saa 8 mchana ya tarehe 1 July. Walipowasilana na Ujerumani na Ufaransa ambao nao walikuwa na baadhi ya wafungwa wa Kipalestina ambao watekaji walitaka waachiwe… walipowaomba ushirikiano wao kuhusu kukabali kuachia hao wafungwa, Ujerumani na Ufaransa walikataa katakata kuachia hata mfungwa mmoja wa Kipalestina ambaye alikuwa kwenye magereza zao.

Sintofahamu ilizidi kuongezeka. Masaa yalizidi kuyoyoma. Saa 8 mchana ya tarehe 1 July ilizidi kukaribia. Harufu ya damu ilikuwa inabisha hodi mlangoni kwao. Licha ya weledi wao wote walionao lakini mbele yao waliona giza.

Inapaswa kukumbukwa kwamba Idd Amin aliwahi kupatiwa mafunzo ya weledi wa kijeshi nchini Isarel (Special Force Training). Kwa hiyo baraza la mawaziri likamuagiza Baruch Bar-Lev, kamanda mstaafu wa IDF ambaye alihusika kumpatia mafunzo ya kijeshi Amin kipindi yuko Israel na kufanikiwa kujenga naye ukaribu. Baraza la Mawaziri likamuagiza Baruck (marafiki zake humuita “Burka”) kufanya mawasiliano na Rais huyo wa Uganda ili kujaribu kumuomba awashawishi magaidi wanaoshikilia mateka kwenye uwanja wake wa ndege wa Entebbe wawaachie mateka hao bila masharti magumu.

Kupitia kwa Burka, Israel ilifikia mpaka hatua ya kumuahidi Idd Amin kuwa kama atafanikisha kuachiwa kwa mateka hao basi watatumia ushawishi walionao kuhakikisha kuwa Amin anatunukiwa tuzo ya amani ya Nobel.

Lakini Amin hakulegeza msimamo, akaendelea kuwasisitiza kuwa hakuna namna nyingine yeyote ambayo mateka hao wataachiwa bila masharti yaliyotolewa na watekaji kutimizwa.
Baada ya juhudi hii ya kumuhonga ‘tuzo’ kugonga mwamba, Waziri Mkuu wa Israel akawasiliana na serikali ya Marekani na kuwaomba wamshawishi Rais wa Misri Anwar Sadat ambaye alikuwa anaheshimiana sana na Amin ili amshawishi kuwaamuru magaidi yaliyoko uwanjani kwake Entebbe waachiemateka bila masharti magumu.

Amin bado akashikilia msimamo kwamba hakuna mateka atakayeachiwa pasipo masharti yaliyotolewa kutimizwa.
Juhudi hizi za kumshawishi Amin zilikula muda mwingi sana na hatimaye wakajikuta tayari kulikuwa kumekucha asubuhi. Mbele yao kulikuwa kumebakia masaa chini ya manane kabla ya damu ya zaidi ya watu 200 kumwagika.

Baraza la mawaziri la Israel likamuomba Amin aongee na watekaji wakubali kusogeza siku mbele ili kuipa serikali ya Israel muda wakutosha kushughulikia lojistiki na kushawishi Ujerumani na Ufaransa ili waweze kutimiza sharti la kuachiwa kwa wafungwa wa kipalestina 53 wanaotuhumiwa kwa ugaidi.

Rais Idd Amin baada ya kushawishiwa sana akakubali ombi hili na akaieleza serikali ya Israel kwamba ni siku tatu tu pekee zinaongezwa, yaani ikimaanisha kwamba siku zitaongezwa mpaka tarehe 4 July, saa 8 mchana. Serikali ya Israel ikakubliana na hili.

Mchana wa siku hiyo, serikali ilitoa taarifa rasmi kwa vyombo vya habari wakilaani vitendo vya kigaidi na hususani matukio ya utekeji wa raia wasio na hatia, na pia ikaendelea kusisitiza kuhusu sera yake ya kutojadili na magaidi. Lakini taarifa hii ikamalizia kwa kueleza kuwa kwa kujali zaidi uhai wa zaidi ya raia 200 ambao bado wanashikiliwa na magaidi hayo, na kujali maumivu ambayo familia zao na taifa zima linapitia, wamekubali kutimiza sharti la magaidi hao la kuwalipa fedha za kimarekani dola milioni tano pamoja na kuachiwa kwa wafungwa wa kipalestina 53 wenye tuhuma za ugaidi.

Ilikuwa ni moja ya matukio machache ambayo yaliishangaza dunia kwa Israel kukubali kushindwa hadharani. Kwa upande wa maadui wa Israel hii ilikuwa ni sherehe kubwa kwao. Na kwa upande wa Isarel na maswahiba zake hii iikuwa ni maombolezo makubwa.
Amin na wenzake kule Uganda walikuwa wanasherehekea baada ya taarifa hii kutolewa kwa vyombo vya habari. Walihsi kabisa harufu ya ushindi inanukia kwenye pua zao.

Kitu ambacho walikuwa hawafahamu ilikuwa ni kwamba, Israel walikuwa wanawafanyia ‘mchezo’ wa kisaikolojia ili Amin, jeshi lake na watekaji wajiamini kwa kuona kuwa ushindi umeegemea upande wao na hatimaye wajisahau kutokana na kujiamini huku.

NYUMA YA PAZIA

Huko Tel aviv, makamanda wa IDF na maafisa wa Mossad walikuwa wamekusanyika katika conference room ya mako makuu ya wizara ya ulinzi kuweka mkakati wa oparesheni ya uokozi (rescue mission) wa mateka wanaoshikiliwa katika uwanja wa ndege wa Entebbe, Uganda.
Kati ya watu muhimu ambao walikuwepo kwenye kikao hiki alikuwa ni Waziri Mkuu Rabin na Ehud Barak ambaye kipindi hicho alikuwa kamanda wa ngazi za juu kwenye jeshi anayeongoza kitengo cha Intelijensia ya jeshi (Military Intelligence).

Moja kati ya vitu muhimu ambavyo viliwasaidia ilikuwa ni taarifa ya intelijensia iliyoletwa na Mossad kwamba uwanja wa ndege wa Entebbe ulijengwa na kampuni ya Kiisrael inayoitwa Solel Boneh.

Kwahiyo muwakilishi kutoka katika kampuni hii ya ujenzi naye akaitwa kikaoni kwa ajili ya kuwasilisha michoro kuhusu jengo lote na uwanja wa ndege wa Entebbe ulivyo.
Lakini pia wakati huo huo kulikuwa na maafisa wa Mossad ambao walikuwa ufaransa kuwahoji wale mateka ambao walikuwa wameachiwa awali. Mtu muhimu zaidi ambaye alitoa taarifa nzuri kwa Mossad alikuwa ni yule afisa wa jeshi niliyemuelezea awali kwamba alikuwa na uraia wan chi mbili (Israel na Ufaransa) na siku hii alikuwa ametumia passport ya nchi ya ufaransa hivyo watekaji walimuachia pamoja na wenzake wa kundi la kwanza lile la watu 48.

Bwana huyu alitoa taarifa muhimu zaidi kuhusu kilichokuwa kinaendelea katika uwanja wa ndege wa Entebbe, kwa kuwa yeye tofauti na wenzake kutokana na uzoefu wake wa jeshi alikuwa aliweza kuwaeleza Mossad kuhusu ni salaha za namna gani watekaji walikuwa nazo, kulikuwa na ndege za aina gani za kijeshi pale uwanjani (Idd Amin aliamuru Air Force ya Uganda kulinda uwanja huo masaa 24), pia aliweza kuwaeleza kuhusu ‘rotation’ ya ulinzi ya jeshi la Uganda pamoja na taarifa nyingine muhimu ambazo abiria wengine wasingeweza kuzitilia maanani au kkuzieleza kwa ufasaha.

Baada ya kupata intelijensia ya kutosha, mkakati wa awali ambao ulipendekezwa na jeshi ulikuwa ni kutumia ndege ya kijeshi na kisha kudondosha makomando kwenye ziwa Viktoria na kutoka hapo watatumia boti za mpira kuvuka mpaka nchi kavu na hatimaye kuelekea uwanja wa ndege ambao haukuwa mbali sana na ziwa Viktoria.

Mkakati huu ulikuwa ni mzuri lakini ulihairishwa baada ya kupewa taarifa kuwa ziwa Viktoria lilikuwa na mamba wengi na ingeweza kuhatarisha uhai wa hawa makomando kabla hata ya kufika kwenye uwanja wa ndege. Kwahiyo ilikuwa dhahiri kwamba mkakati wowote ambao utawekwa ni lazima uwe wa kuvamia kutokea nchi kavu na ikiwezekana kutoka nchi jirani.

Changamoto kubwa zaidi ilikuwa ni usafiri. Yaani kwamba oparesheni hii ilikuwa si tu kwamba makomando wanaotumwa kutekeleza wanaenda kupambana na magaidi wanne tu walioteka ndege, bali ilikuwa ni kana kwamba wanaenda kupambana na jeshi zima la Uganda. Kwa hiyo kikosi cha makomando ambacho kitatumwa kwenda huko lazima kiwe na watu wengi wa kutosha na pia lazima wachukue silaha nzito za kutosha. Ili kufaniskisha safari yenye makomando wengi hivi na vifaa vizito ilikuwa ni lazima kutumia ndege kubwa za kijeshi zenye uwezo mkubwa pia na hakukuwa na chaguo zuri zaid ya kutumia ndege za kijeshi za LOCKHEED C-130 HERCULES. Sasa changamoto ilikuwa inakuja kwamba huwezi kurusha dege kubwa kama hii kwenda na kurudi kutoka Israel mpaka Uganda bila kujaza mafuta tena japo mara moja.

Katika kipindi hiki bado Israel walikuwa hawajawa na uwezo wa kufanya ‘Aerial Refuel’, yaani ndege kujazwa mafuta kwa kutumia ndege nyingine ikiwa angani. Lakini pia ilikuwa ni lazima madege hayo yakikaribia Uganda yaruke chini chini ili kukwepa kudunguliwa na kuikwepa rada ya kijeshi. Kwa hiyo ilikuwa ni lazima kupata nchi ndani ya afrika Mashariki ambao watakubali madege hayo ya kijeshi ya Israel kutua kwenye uwanja wake wa ndege na kujaza mafuta lakini pia kujiandaa na kuanzisha operation kutokea hapo na pia anga lao kutumika kuanzisha shambulizi la kijeshi kuelekea Uganda.

Sasa japokuwa nchi zote za Afrika Mashariki zilikuwa hazikubaliana na kitendo cha Rais wa Uganda kushirikiana na watekaji, lakini hakukuwa na hata nchi moja ambayo ilikuwa iko tayari kuingia kwenye mzozo na Idd Amin kwa kuruhusu viwanja vya vya ndege kutumika na ndege za jeshi la Israel au wanajeshi kujiandaa kuvamia Entebbe au pia kuruhusu anga lao kutumia na jeshi la Israel.

Ndipo hapa ambapo kwa haraka sana siku hiyo hiyo Waziri Mkuu Rabin akamtuma Ehud Barak na maafisa wachache wa Mossad kwenda Kenya kushawishi serikali ya Mzee Jomo Kenyatta iruhusu ndege za jeshi la Isarel kutumia kiwanja chao cha ndege. Ehud barak na wenzake hawakwenda tu moja kwa moja kwa Mzee Kenyatta, bali kwanza walienda kwa Waziri wa kilimo wa kipindi hicho Bw. Bruce McKenzie ambaye huyu aliwahi kuwa afisa wa Idara ya ujasusi ya Uingereza, MI6 na pia alikuwa swahiba mkubwa wa Ehud Barak.

Kwa hiyo Israel ikamtumia Bruce McKenzie kumshawishi Mzee Jomo Kenyatta kuruhusu anga la Kenya na viwanjavya ndege kutumiwa na makomando wa Israel na ndege zao.
Ehud Barak na maafisa wa Mossad hawakuishia hapa tu, bali pia walifanya vikao vya siri na wafanyabiashara wakubwa nchini Kenya wenye asili ya Israel na wale ambao walikuwa na ‘marafiki’ wa Israel kuwaomba watumie ushawishi wao wa kisiasa na kiuchumi wasaidie kumshawishi Kenyatta kukubali ombi la seriakli ya Israael viwanja vyao kutumika na ndege za kijeshi za Israel na makondo wake.
Baada ya mashinikizo haya kutoka kila upande, Mzee Kenyatta hakuwa na chaguo linguine zaidi ya kukubali ombi lao.

Bwana huyu McKenzie pia alikuwa na ndege yakebinafsi, na Ehud Barak akaona fursa. Walitumia ndege hii ya kiraia kuruka mpaka Uganda mijini Entebbe na kukatiza juu ya anga la uwanja wa ndege wa Entebbe na walipokuwa wanapita juu ya anga la uwanja wa ndege, Ehud Barak akatumia fursa hii kupiga picha kila eneo la uwanja. Kwa kuwa hii ilikuwa ni ndege ya kiraia, jeshi la Uganda hawakushughulika nayo.
Picha hizi zilizopigwa na Ehud Barak zilikuja kuwa na umuhimumkubwa katika maandalizi ya mwisho ya oparesheni ya makomando wa Isarel Kuvamia uwanja huu.

Mpaka kufikia hapa maandalizi yote muhimu yalikuwa yamekamilika.

WAKATI HUO HUO

Upande wa watekaji kule Uganda walikuwa wanasubria mifwedha yao dola milioni 5 za kimarekani.
Rais Idd Amin naye baada ya kufikia makubaliano na Israel kuwa masharti ya fedha na wafungwa wa kipalestina kuachiwa tarehe 4 July, naye ‘akarelax’ na akaona huo ndio muda wa kutekeleza majukumu Mengine akisubiria tarehe 4 July ifike.

Katika kipindi hiki Idd amin ndiye alikuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kwa kuzingatia utaratibu wa uenyekiti kuzunguka kwa kila nchi kwa mwaka mmoja mmoja na wiki hii alikuwa anatakiwa kwenye kikao cha Umoja wa Afrika kilichokuwa kinafanyika Mauritius. Kwa hiyo Amin akafunga safari kuelekea Mauritius kwenda kukabidhi kijiti cha Uenyekiti.

Ehud Barak aliposikia taarifa hii, kwa kutumia akili yake kubwa ya kuzaliwa aliyojaliwa na uzoefu wake wa ujasusi, aliona fursa adhimu kabisa hapa. Akawasiliana na walioko kikaoni huko Tel Aviv na kuwaeleza taarifa ambazo awali wote hawakuielewa.

Ehud Barak: “Idd Amin akiwa ndani ya Uganda huwa anatumia Mercedes Limousine katika msafara wake”

Waziri Mkuu Rabin: “Ok! Limefanyaje?’

Ehud Barak: “Nataka mtafute gari kama hiyo… Mercedes Limousine”

Waziri Mkuu Rabin: “la kazi gani?”

Ehud Barak: “siku ambayo kikosi cha makomando wakipanda kwenye ndege kutoka huko Israel kwenda Uganda, gari hilo nataka pia lipakiwe ndani ya ndge!”

Kwa dakika kadhaa wote ambao walikuwa wanamsikiliza pale kikaoni kupitia simu hakuna ambaye alielewa nini hasa Ehud Barak alikuwa anapendekeza.

Yalikuwa yamebaki masaa machache tu ambapo, weledi, ushujaa na uzalendo uliotukuka ulikuwa unaedna kudhihirika.

Siku ya July 3 mwaka huo 1976 saa 12 na nusu ya jioni takribani masaa kadhaa kabla ya kufikia deadline ya mwisho waliyopewa na watekaji (July 4), Waziri mkuu wa Israel Yitzhak Rabin alitia saini nyaraka ya kuidhinisha oparesheni ya kijeshi ya uokozi (rescue mission) ambayo iliwasilishwa mezani na Meja Jenerali Yekutiel Adam (maarufu kwa jina la “Kuti”) na Brigedia Generali Dan Shomron. Pia kwa mujibu wa nyaraka hiyo iliyosainiwa na Waziri mkuu, Shomron aliteuliwa kuwa Kamanda wa utekelezaji wa Oparesheni.

Baada ya oparesheni hii kuidhinishwa rasmi na Baraza la Mawaziri muda huo nilioutaja hapo juu, Meja Jenerali Yekutiel Adam na Brigedia Generali Dan SHomron walikusuka kikosi cha kijeshi kwa ajili ya kutekeleza oparesheni hiyo kama ifuatavyo;

The Ground Command

Hiki kilikuwa ni kikosi (japo sio kikosi haswa) ambcho kilikuwa na watu wawili tu, Brigedia Generali Dan Shomron na mwakilishi wa jeshi la Anga la Israel Kanali Ami Ayalon na watu wachache wa masasiliano ya jeshi. Kikosi hiki ndicho ambacho kilikuwa na amri ya mwisho juu ya nini wanajeshi walikuwa wanatakiwa kufanya pindi wakakapoanza utekelezaji wa oparesheni.

The Asault Team

Timu hii ilipewa kazi ya kuvamia jengo la uwanja wa ndege ambalo mateka walikuwa wanashikiliwa na kuokoa mateka wote waliomo humo.

Kikosi hiki kilikuwa na wanajeshi 29 ambacho kiliongozwa na Luteni Kanali Yonathan Netanyahu (kaka yake Waziri Mkuu wa sasa wa Israel, Benjamin Netanyahu). Kikosi hiki kilijumuisha makomando wenye weledi wa hali juu kutoka katika kitengo maalumu cha jeshi la Israel kiitwacho SAYERET MATKAL.

Nieleze kidogo kuhusu Sayet Matkal.

Hiki ni kikosi cha weledi maalumu (special force) ndani ya jeshi la Israel la IDF. Makomando wanofuzu kutumika katika kikosi hiki, licha ya kupata mafunzo yote ya kijeshi kama wanajeshi wengine lakini wanaongezewa mafunzo mengine adhimu zaidi kuwafanya waweze kutekeleza oparesheni hata katika mazingira ambayo kwa akili ya kijeshi ya kawaida inaonekana kwamba hakuna uwezekano wa kufanikiwa kwa oparesheni hiyo.

Mfano wa mafunzo haya adhimu ambayo wanapatiwa ni pamoja na ukusanyaji wa intelijensia, kufanya ‘deep recon’ (nimekosa Kiswahili chake) katika uwanja wa vita, upenyezaji wa intelijensia za kimkakati (strategic intelligence) mafunzo adhimu ya counterterrorism pamoja na uokozi wa mateka nje ya mipaka ya Israel.

Kwa namna fulani ili kukielewa kikosi hiki unaweza kukifananisha na kikosi cha SAS kwenye jeshi la nchi ya Uingereza japo vinatofauti fulani bado. Ila kwa ufupi huo ndio muonekano wa Sayeret Matkal na shughuli zake.

The securing Element

Kikosi hiki kiligawanywa katika vikundi vidogo vidogo vitatu ili kuleta ufanisi.

1.Paratroopers – hawa waliongozwa na Kanali Matan Vilnai. Kazi yao ilikuwa ni kuhakikisha hakuna shughuli zozote zinaendelea ndani ya uwanja wa ndege wa Entebbe qawakati ambao oparesheni hiyo inatekelezwa. Pia walikuwa wanatakiwa kuhakikisha kuwa njia ya kurukia ndege (runway) iko ‘clear’ muda wote. Pamoja na hayo kikosi hiki pia walikuwa ndio wanaowajibika kulinda ndege za kijeshi za Israel muda wote zinatakapo kuwa kwenye uwanja wa ndege wa Entebbe pamoja na ujazaji mafuta.

2. The Golani Force – kikundi hikicha kijeshi kiliongozwa na Kanali Uri Sagi. Kazi yao ilikuwa ni kuhakikisha kunakuwa na ulinzi wa yale madege makubwa aina ya Lockheed Harcules C-130. Pia walitakiwa kuyasogeza madege hayo karibu kabisa na terminal ambayo mateka walikuwepo ili waweze kuwapakia pindi ambapo uokozi ukiwa umefanikiwa. Lakini pia kikundi hiki kilifanya kazi kama ‘kikosi’ cha akiba endapo ambapo kungetoke dharura ya upungufu katika kikosi kingine.

3. The Sayeret Matkal Force – kikosi hiki nacho pia kama ilivyo kwa ‘Assault Team’ ambayo nimeiongelea hapo juu, nacho pia kiliundwa na makomando wa Sayeret Matkal na kazi yao ilikuwa ni kuhakikisha kuwa hakukuwa na ‘interception’ yoyote kutoka kwenye jeshi la anga la Uganda na kuwa tayari kuwazuia na kuzuia shambulizi lolote la kijeshi ikitokea kwamba wanajeshi wa Uganda walioko uwanja wa ndege wakiomba msaada kutoka kambi ya jeshi iliyoko ndani ya jiji la Entebbe.

Kwa ujumla huo ndio ulikuwa muonekano kamili wa Kikosi kizima na majukumu ya wanajeshi wote waliohusia katika oparesheni ya uokozi kwenye uwanja wa ndege wa Entebbe.

USIKU WA TAREHE 3 JULY, 1976

Hatimaye siku ya siku ikawadia, saa lililotarajiwa likafika. Ndege nne kubwa aina ya Lockheed Harcules C-130 zikiwa zimebea zaidi ya makomando 200 pamoja na ile gari Mercedes Limousine (pamoja na gari nyingine aina ya Land Rover) ambayo Ehud Barak alipendekeza waje nayo, ziliruka kutoka kwenye uwanja wa ndege wa kijeshi ulioko eneo la Sharm El Sheikh mpakani kabisa na Misri.

Ndege hizi nne kubwa Lockheed Harcules C-130 zilisindikizwa nyuma na ndege mbili aina ya Boeing 707 ambazo moja ilikuwa imelengwa kutumiwa kama ‘command post’ na nyingine itumike kama hospitali kutibu majeruhi ambao watatokana na mapambano ya risasi ambayo walikuwa wanayategemea kati yao na watekaji pamoja na jeshi la Uganda.

Ndege ziliruka katika njia ya kimataifa kupita Red sea na kwa muda mwingi wa safari yake zililazimika kuruka si zaidi ya mita 30 angani (kuna muda inaelezwa kuwa iliwabidi kuruka mpaka futi 35 kutoka ardhini) ili kuepuka kuonekana na rada za Misi, Sudan na Saud Arabia.

Safari ilikuwa ngumu haswa hasa ukizingatia kuwa ndege kubwa kama zile zikiruka katika usawa wa karibu hivyo na ardhi mtikisiko unakuwa mkubwa haswa ndani ya ndege.

Waliokaribia mchepuko wa kusini wa Red Sea ndege zilikata kona na kupita kusini mwa nchi ya Djibouti. Kutokea hapo walielekea mpaka kutokea kaskazini mashariki mwa Nairobi, Kenya na kisha Somalia na kupita eneo la Ogaden nchini Ethiopia.

Kutoka hapo wakapinda magharibi kufuata bonde la ufa ba mpaka kutokea juu ya ziwa Victoria.

Ikumbukwe kwamba kati ya ndege zile mbili za Boeing 707 zilizokuwa zinafuatia nyuma na zile Harcules nne, moja ambayo ilipangwa itumike kama hospitali ilitua Nairobi, uwanja wa ndege wa Jomo Kenyetta. Ile nyingine ambayo nimeeleza kwamba ilipangwa itumike kama ‘command post’ ilikuwa inaruka kuzunguka uwanja wa ndege wa Entebbe wakati ndege zile za kijeshi zikitua. Ndege hii (command post) haikutua uwanjani na kamanda mkuu wa oparesheni hii Meja Jenerali Yekutiel Adam alikuwa ndani yake kuwaongoza wenzake walipo ardhini.

Mnamo saa 23:00 ndege za kijeshi za Israel zilitua kwenye uwanja wa ndege wa Entebbe huku milango ya nyuma ya mizigo kwenye ndege ikiwa wazi.

Hapa nieleze kidogo…

Mbinu kuu ambayo jeshi la Israel walikuwa wanataka kuitumia ili kufanikisha Oparesheni hii ilikuwa ni kufanya shambulio la kushtukiza. !

Kivipi?

Katika sehemu iliyopita nilieleza kuwa Ehud Barak baada ya kukusanya intelijensia za kutosha akiwa Kenya, aliwaeleza wenzake kuwa wapakie gari aina ya Mercedes Limousine inayofanana kabisa na ile ambayo inatumiwa na Rais Idd Amin a Uganda ambayo ilikuwa na rangi nyeusi.

Kwa kuwa walifahamu Rais Idd Amin alikuwa safarini nchini Mauritius kukabidhi uenyekiti wa O.A.U, hivyo walitaka kuigiza kana kwamba Idd Amin alikuwa anarejea kutoka safarini na alikuwa anaenda kutembelea mateka pale uwanja wa ndege kama ambavyo ilikuwa kawaida yake. Hii ndio sababu ya wao kwenda na ile gari nyeusi aina ya Mercedes Limousine pamoja na Land Rover… ambavyo ndivyo ilikuwa namna ambavyo Idd Amin alikuwa anapenda kwenda kutembelea pale uwanjani…. Mercedes Limousine ambayo ina mbeba yeye na nyuma yake gari aina ya Land Rover iliyo na walinzi wake.

Kwa hiyo ndege ya kwanza ya jeshi la Israel ilipotua kwenye uwanja wa ndege wa Entebbe ambao kwa muda huo wa saa tano usiku kulikuwa na giza tupu taa zote za uwanja wa ndege zikiwa zimezimwa. Ndege ilitua ikiwa imefunguliwa mlango wa nyuma wa mizigo, ambako ilitoka gari aina ya Mercedes Limousine ikiongozana na Landa Rover na moja kwa zikaendeshwa kuelekea kwenye geti la Terminal ambayo mateka walikuwa wamehifadhiwa.

Walikuwa wamefaulu kuigiza kabisa msafara wa Idd amin unavyokuwa. Msafara ulikuwa unafanana kabisa na ule wa Idd Amin lakini tofauti ilikuwa kwamba gari hizi ndani yake kuliwa na makomamdo.

Jambo la ajabu ni kwamba walipofika mbele ya geti la Terminal badala ya kuruhusiwa kupita, wanajeshi wa Uganda waliokuwa wanalinda getini waliinua bunduki zao na kuwanyoosha kuelea magari haya.

Walichokuwa hawakijua makomando hawa ambacho wanajeshi hawa waliokuwa wanalinda hapa uwanjani walikijua ni kwamba, Siku moja ya kabla ya Idd Amin kwenda Mauritus alibadili rangi ya gari yake kutoka nyeusi kwenda rangi nyeupe.

Kwa hiyo wanajeshi hawa wa Uganda walipoona magari haya walikuwa wanajua fika kuwa huyu hakuwa Rais wao Idd Amin.

Wanajeshi hawa wawili wa Uganda waliokuwa getini walinyanyua bunduki zao aina ya Kalashnikov na hawakuonyesha dalili kwamba labda walikuwa wanataka kufanya ukaguzi wa kawaida tu kabla ya kuwaruhusu, walionyesha dhahiri kabisa kwamba walikuwa wanataka kufanya shambulio.

Kabla wanajeshi hao wa Uganda kufanya lolote lile, Netanyahu na komando mwingine ambao walikuwa ndani ya gari walitumia weledi wao kufanya uamuzi makini wa haraka kwa kufyatua risasi kutoka kwenye bastola zao zenye ‘silencer’ na mara moja wale wanajeshi wawili wa Uganda walienda chini.

Lakini moja ya wale wanajeshi wa Uganda waliodondoka chini baada ya kufyatuliwa risasi, hakufa mara moja na alikuwa anajitahidi kuinuka. Hii ilisababisha komando mwingine wa Israel kufyatua risasi lakini safari hii huyu komando wa Israel alifyatua risasi kutoka kwenye bunduki ambayo haina ‘silencer’. Hii iliwashitua wanajeshi wengine wa Uganda waliokuwa nje ya Terminal na kuanza kukimbilia walipokuwa wanasikia milio ya risasi inatokea huku wanafyatua risasi.

Kwa maneno mengine ilikuwa kwa kiasi fulani walichokuwa wamekipanga makomando wa Israel, kufanya shambulio la kushitukiza lakini mpaka muda huu tayari ile ‘element of surprise’ ilikuwa haipo tena, jeshi la Uganda lilikuwa limeshitukia ‘mchezo’.

Bila kuchelewa sana, makomando wote walikuwa kwenye zile gari mbili (Mercedes na Land Rover) waliruka nje ya gari na kukimbia kuelekea ndani ya terminal.

Vichwani mwao walikuwa bado hawajaondokewa na kumbukumbu ya oparesheni kama hii iliyotokea miaka miwili iliyopita nchini Israel kwenye mji wa Ma’a lot ambapowatekaji wa KIpalestina baada ya kushituka kuwa kulikuwa na makomando wa Israel wamefika kufanya uokozi, waliwapiga risasi mateka wao 25 ambao kati yao 22 walikuwa ni watoto wadogo.

Hivyo Netanyahu na wenzake hawakutaka kitu kama hiki kjitokeze tena… Netenyahu na makomando wenzake wa Syeret Matkal kwa ustadi wa hali ya juu walikimbia na kuingia ndani ya terminal na kuwaacha vile vikosi vingine kuwadhibiti wanajeshi wa Uganda waliopo nje ya terminal

Mateka wanaeleza kwamba baada ya mpambano ya risasi kuanza huko nje ya terminal waliwaona watekaji kadhaa wakiongozwa na yule aliyeonekana kama kiongozi wao, Wilfred Bose waliingia ndani ya terminal wakiwa wanahaha kama wamechanganyikiwa wasijue wafanye nini, ilionekana dhahiri kuwa walikuwa hawajajiandaa kwa hili shambulio la ghafla, ilionekana dhahiri kwamba katika akili yao walikuwa wanasubiria Israel kutimiza masharti yao ili waweze kuachia mateka.

Kuna muda Wilfred Bose alionekana kunyoonya bunduki yake kwa mateka kama vile anawataka kuwamininia risasi lakini alikuwa anashindwa kufanya uamuzi huo. Bose aligeuka ghafla baada ya kusikia kishindo cha mlango wa terminal ukifunguliwa.

Makomando wa Israel walikuwa wametumia weledi na ustadi wao wa hali ya juu kuingia ndani ya terminal kwa muda sahihi kabla ya Wilfred Bose na wenzake kufanya uamuzi wowote wa kuua mateka.

Makomando wa Israel walipoingia tu ndani ya terminal, mmoja wao mkononi walikuwa na kipaza sauti aina ya ‘megaphone’ na alikuwa anaongeea kwa nguvu kwa lugha ya kihebrania, “Lay down, Lay down. We are Israel soldiers. Lay down. Lay down!!”.

Mateka wote wa kiisrael hata wale waliokuwa wamekaa kitako walilala chini, hivyo ndani ya sekunde chache tu kila mtu ambaye alibakia amesimama alikuwa ni halali yao kumtandika risasi.

Kwa bahati mbaya kulikuwa na mateka kadhaa ambao wwalikuwa hawajui kihebreania sawia na hii iliwagharimu sana. Kwa mfano kulikuwa na kijana wa mika 19 aliyeitwa Jean-Jacques Maimoni, huyu alikuwa amehamia Israel siku si nyingi sana kutokea nchini ufaransa. Lilipotolewa tangazo hilo la kila mtu kulala chini hakuelewa na alibakia akiwa amesimama na alitandikwa risasi na makomando wa Israel pamoja na wale watekaji. Kijana huyu hakuwa peke yake, lakini pia kulikuwa na mateka mwingine aliyeitwa Ida Borochovitch, ambaye alihamia Israel kutoka nchini Urusi.

Risasi zilirindima kwa takribani dakika mbili nzima na baadae ukimya wa kama sekunde 15 ukatawala na moja wa makomando wa kiisrael akauliza kwa kiebrania, “where are the rest of them?” (“wako wapi wengine?”). Mateka wakaonyesha kidole kwenye chumba kidogo kilichopo pembeni.

Makomando wakarusha mabomu kadhaa ya kutupa kwa mkono na kisha kuingia ndani ya chumba hicho na kuwamiminia risasi wote ambao walikuwa humo.

Milio ya risasi ndani ya terminal hatimaye ilikuwa imekoma japo bado huko nje walisikia majibizano ya risasi. Mwanajeshi mmoja wa Israel kati ya wale waliopo ndani ya terminal, kwa sauti ya utulivu kabisa na katika lugha ya kihebrania aliwatangazia mateka, “listen guys, we’ve come to take you home!” (“sikilizeni, tumekuja kuwachukua kuwarudisha nyumbani!”).

Baada ya hapo makomando walianza kuwatoa mateka kutoka kwenye terminal na kuwapakia kwenye ndege kwa tahadhari kubwa huku wale wenzao wengine wakiendelea kuwadhibiti wanajeshi wa Uganda waliokuwa wanarusha risasi kutoka kwenye maeneo ya kujificha ndani ya uwanja wa ndege.

Wakiwa wanaendelea kuwapakia mateka waliowaokoa kwenye ndege, kumbe kulikuwa na mwanajeshi wa Uganda amebakia juu kwenye mnara wa uongozaji (airport control tower). Kwa mujibu wa taarifa za hivi karibunui kutoka kwa mtoto wa Idd Amin anasema kwamba mwanajeshi huyu alikuwa ni binamu wa Idd Amin. Kutokea hapo kwenye mnara alimimina risasi mfululizo kwa makomando wa Israel na moja ya risasi hizi ilimpaka Koamando Yonatan Netanyahu ambaye ndiye alikuwa kiongozi wa ‘unit’ ya Sayeret Matkal iliyopo hapoa na alipoteza uhai pale pale.

Wanajeshi wa Isarel walijibu mapigo kwa kurusha bomu la roketi ndogo ya begani na kusambaratisha kabisa kiota cha mnara na kumuua mwanajeshi wa Uganda aliyekuwa anawashambulia.

Baada ya hapo waliwapakia kwenye ndege mateka wote ambao waliokolewa pamoja na miili ya Waisrael ambao walifariki kwenye majibizano hayo ya risasi.

Kisha ili kuhakikisha kuwa hakuna ndege itakayowafuatia nyuma wakiondoka au kushambuliwa, walilipua ndege zote za jeshi la Uganda ambazo zilikuwa uwanjani hapo.

Oparesheni yote hii ilichukua takribani dakika 53 ambapo dakika 30 pekee ndio zilikuwa za mapigano na 23 zilizosalia zilikuwa za kupakia mateka walio okolewa na kuondoka.

Mpaka kufikia mwishio mwa oparesheni, jumla ya watekaji wote 7 walikuwa wameuwawa, pia wanajeshi 45 wa jeshi la Uganda walikuwa wameuwawa pia. Lakini pia ndege za kijeshi 11 aina ya MiG-17 na Mig-21 zililipuliwa na makomando wa Isarel. Ikumbukwe kwamba ndege hizi ndizo zilikuwa ni ndege zote za kijeshi ambazo zilikuwa zinamilikiwa na jeshi la anga la Uganda. Hii inaonyesha moja kati ya mapungufu makubwa ya kiuongozi ya Amin. Hakukuwa na busara yoyote au faida yoyote ya kimkakati kuweka ndege zote za jeshi lako la anga kwenye uwanja wa ndege wa kiraia ili kulinda mateka wa tukio ambalo wengine walikuwa wanaweza kuliona kama tukio la kigaidi na kwa namna Fulani kama ugomvi ambao ulikuwa haumuhusu moja kwa moja.

Katika mateka wote 106 waliobakia (kumbuka nilieleza kuwa kulikuwa na mikupuo miwili ya mateka wasio wa Kiisrael au asili ya Kiyahudi waliachiwa kwa kupelekwa na ndege ufaransa nchini), kwahiyo kati ya wale 106 waliobakio, mateka watatu waliuwawa muda wa mapambano (hawa ndio wale ambao walikuwa hawaelewi kihebrania kwa ufasaha na kwa hiyo hawakulalala chini kama ilivyoamrishwa na makomando wa Israel), na mateka mmoja bibi wa miaka 74 aliyeitwa Dora Bloch aliachwa akiwa Hospitali mjini Entebbe ambako alipelekwa na Amin siku kadhaa nyuma kutokana na kuhitaji uangalizi maalumu wa kidaktari.

Kati ya Makomando wa Isarel, ni mmoja tu ndiye aliuwawa tena dakika za mwisho (Yonatan Netanyahu) japo pia kuna makomando wengine kama watano ambao walijeruhiwa. Kifo cha kiongozi wa ‘unit’ ya Sayeret Mitkal, Yonatan Netanyahu katika oparesheni hii ndio iliyofanya siku kadhaa baadae oparesheni hii pia kubatizwa jina la OPERATION YONATAN kwa heshima yake na ushujaa wake wa kutoa maisha yake ili kutetea na kuooa roho za raia alioapa kuwalinda.

Baada ya kila kitu kuwekwa sawa na watu wote kupanda ndani ya ndege, waliruka mpaka Nairobi Kenya kwa mapumziko mafupi ili kutibia wale ambao walijeruhiwa (kama ambavyo nilieleza kuwa ile moja ya Boeing 707 iliyotengwa kama ‘hospitali’ ilibaki Nairobi).

Baada ya matibabu hapo Nairobi, madege yote yaliruka kurudi Israel. Kwa kifupi operation hii was a big SUCCESS.!

Japokuwa baada ya ulimwengu mzima kutangaziwa juu ya kilichotokea, juu ya ‘umafia’ uliofanywa na Israel, ulimwengu uligawanyika kila nchi ukiunga mkono upande fulani, lakini nchi nyingi ziliunga mkono Israel kwa matumizi ya jeshi katika nchi nyingine, wengi walimlaumu Amin kwa kushindwa kutumia diplomasia kumaliza mzozo huu. Ajabu ni kwamba mwezi huo wa July, Mkuu wa Majeshi wa Iran moja wa mahsimu wa siku zote wa Israel aliandika barua kwa Waziri mkuu wa Israel kumpongeza kuhusu Oparation hiyo na kumpa pole kwa kifo cha Yonatan Netanyahu akimuita Yonatan kumsifu kuwa ni ‘martyr’.

Vyovyote vile ambavyo unaweza kuitazama oparesheni hii kwenye jicho la kisiasa ua kidiplomasia, kwamba kama ilikuwa ni sahihi au si sahihi lakini katika jicho la kijeshi na ujasusi hii ni moja ya oparesheni murua kabisa kuwahi kufanyika katika historia ya majeshi duniani. Moja ya manguli wa “ulimwengu wa giza”, Bw. Henry Kissinger aliwahi kutamka kuwa hii ilikuwa ni “an immposible mission”!

Umaridadi wa oparesheni hii umefanya hata vitengo kadhaa vya weledi vya majeshi mbali mbali kutaka kuiga mfano wake lakini bila mafanikio yoyote. Kwa mfano Wamarekani walijaribu kuiga umaridadi wa Oparesheni hii na kufanya ya kwao iliyoitwa Oparation Eagle Claw baada ya kutokea kwa utekeaji kwenye ubalozi wa Iran lakini oparesheni hiyo ilifeli vibaya.

Sasa hivi kama wewe ni mwanajeshi katika jeshi fulani kwenye kitengo cha weledi (special force) au labda ni jasusi maalumu, lazima katika hatua fulani ya japo hata ‘darasani’ kwenye makaratasi utafundwa kuhusu Oparetion Entebbe na namna ilivyo tekelezwa.

Oparesheni hii ilimuacha Amin na aibu kubwa kiasi kwamba akaendelea kufanya vitu ambavyo vilidhihirisha udhaifu wake wa kiungozi. Kwa mfano, yule bibi wa miaka 74 aliyeachwa hospitali mjini Entebbe, aliamuru auwawe kinyama. Lakini pia Amin alisimami kuwawa kwa McKenzie yule waziri wa kilimo wa Kenya ambaye alimsaidia Ehud Barak kumshinikiza Mzee Jomo Kenyetta kuruhusu ndege za jeshi la Israel kutumia viwanja vya ndege vya Kenya wakati wa utekelezaji wa OParesheni hiyo na pia kumsaidi kukusanya Intelijensia kwa kutumia ndege yake binafsi.

McKenzie aliuwawa kwa bomu lililotegwa kwenye gari yake.

Pia Amin alisimamia ulipuaji kwa bomu moja ya hoteli kubwa Nairobi kipindi hicho ambayo ilikuwa inaitwa The Norfolk Hotel, ambayo ilimilikiwa na moja ya wayahudi mashuhuri nchini Kenya
 
"" Sasa hivi kama wewe ni mwanajeshi katika jeshi fulani kwenye kitengo cha weledi (special force) au labda ni jasusi maalumu, lazima katika hatua fulani ya japo hata ‘darasani’ kwenye makaratasi utafundwa kuhusu Oparetion Entebbe na namna ilivyo tekelezwa. ""
.
emoji23.png
emoji23.png
emoji23.png
Hapa bwana hapa
 
Upo sahihi kabisa mkuu, maana hata nami naikumbuka ile mission ya korosho na jinsi jeshi letu lilivyo kuwa front na magwanda pamoja na silaha nzito za kiusalama
 
NDEGE ILIYOBEBA RAIA WA ISRAEL YATEKA ANGA LA UGIRIKI NA KUPELEKWA UGANDA - 1



Saa 12:45 asubuhi ya Jumapili Juni 27, 1976 ndege ya Shirika la Ndege ya Singapore 763 ilitua kwenye Uwanja wa Ndege wa Athens, Ugiriki, ikitokea Bahrain kupitia Kuwait.
Miongoni mwa abiria watano walioshuka kwenye ndege hiyo, wanne walielekea eneo ambalo abiria wa ndege ya Shirika la Ndege ya Ufaransa, Flight 139, wangeondokea kwenda Paris, Ufaransa.
Saa 2:59 asubuhi hiyo, ndege ya Shirika la Ndege ya Ufaransa, Flight 139 ikirushwa na Kapteni Michel Bacos ilipaa kutoka Uwanja wa Ndege wa Ben Gurion mjini Tel Aviv katika kile kilichopangwa kuwa ingekuwa ni safari ya kwenda Ufaransa kupitia Athens.
Wakati ndege hiyo Flight 139, ikitua Athens, abiria 58 waliokuwa wakiisubiri walikuwa katika hatua za mwisho za kukamilisha taratibu za uwanjani hapo.
Kwa mujibu wa Louis Williams katika kitabu chake, ‘The Israel Defense Forces: A People’s Army’, miongoni mwa abiria hao alikuwa msichana mmoja mwenye umri wa miaka 25 mwenye hati ya kusafiria ya Ecuardor. Jina lake ni Ortega na nyuma yake kwa mbali kidogo alikuwa kijana aliyekuwa na hati ya kusafiria ya Peru iliyoonyesha jina lake ni Garcia. Nyuma zaidi walikuwako wanaume wengine wawili waliokuwa na hati za kusafiria za Bahrain na Kuwait.
Flight 139 ilitua katika Uwanja wa Athens saa 5:30 asubuhi kuwabeba abiria hao 58. Wote wanne walipanda Flight 139. Saa 6:20 mchana ndege ikawa imepaa tena angani kuelekea Paris, Ufaransa, ikiwa na jumla ya abiria 246.

Baadaye, baada ya uchunguzi wa kina, ilikuja kujulikana kuwa jina halisi la mwanamke huyo ni Gabriele Kjoche-Tiedemann, ambaye aliwahi kushiriki kuwateka mawaziri wa nchi zinazochimba mafuta (Opec) katika makao yao makuu mjini Vienna, Austria katika tukio la Jumapili ya Desemba 21, 1975.
Gabriele aliwahi kuishi na aliyedaiwa kuwa ni gaidi maarufu zaidi aliyeitwa Carlos ‘The Jackal’ na mshirika wake katika hii ndege ya Ufaransa ni mwanachama wa kikundi cha kigaidi kilichojulikana kama Baader-Meinhof.
Mmoja wa Waarabu wawili waliokuwa na Ortega na Garcia baadaye walikuja kutambuliwa kama mwanzilishi na mpango mikakati wa kikundi cha Harakati za Ukombozi wa Palestina (PFLP).
Dakika nane tu baada ya kupaa angani, Ortega na Garcia na washirika wao wa Kiarabu wakaanza kile ambacho baadaye kimekuja kubaki katika vitabu vya historia duniani. Dakika nane tangu ndege kupaa, Ortega alikimbia kwa kasi kutoka kiti alichokaa hadi mbele huku akipiga kelele za kuwaamuru abiria waweke mikono kichwani. Dakika mbili baadaye mwanamama huyo Ortega akawaambia abiria kuwa wameiteka ndege hiyo na kwamba waliohusika na utekaji huo ni kundi la “Che Guevara” na kikundi cha “Gaza Unit” cha Harakati za Ukombozi wa Palestina.
Mawasiliano na ndege hiyo yalipotea muda mfupi baada ya kupaa angani kuelekea Ufaransa. Kitendo cha mawasiliano kupotea kilianzisha operesheni ya juma nzima lililoanza siku hiyo ya kutoweka kwa ndege hiyo-Jumapili ya Juni 27 hadi Jumapili ya Julai 4, 1967-iliyowahusisha makomandoo wa Jeshi la Israel (IDF). Operesheni hiyo iliitwa Thunderbolt na iliendeshwa kwa usiri mkubwa hadi pale ilipofanikiwa.
Kutoweka kwa ndege hiyo kuliingiza kazini Idara ya Ujasusi ya Israel. Kupotea kwa Myahudi yeyote ni jambo linalopewa umuhimu mkubwa sana kwa wao. Vitengo katika ujasusi wa Israel vilipoanza kufanya kazi, walipokea ujumbe mmoja uliosema:
“‘Ndege 139’ yenye idadi kubwa ya abiria ambao ni raia wa Israel ni ama imeanguka au imetekwa.” Ujumbe wa pili ukasema: “Ndege iliyopotea ni ndege ya Shirika la Ndege la Ufaransa, ambayo imetoka Uwanja wa Ndege wa Ben-Gurion (karibu na Tel Aviv) muda mfupi kabla ya saa tisa alasiri ...”
Ujumbe huo ulipelekwa kwenye Bunge la Israel ambalo lilikuwa katika kikao chake cha Jumapili. Waziri wa Usafiri ambaye alikuwa mchumi, Gad Yaakobi (41), aliupokea ujumbe huo na kuupeleka kwa waziri mkuu wake, Yitzhak Rabin. Muda ulikuwa ni saa 7:30 mchana, ikiwa ni dakika chache tu baada ya Ndege 139 kupoteza mawasiliano baada ya kupaa kutoka Athens.
Rabin, ambaye alikuwa jenerali mstaafu wa jeshi la Israel alimwambia Yaakobi: “Kama ndege itakuwa imetekwa, hakikisha unashughulikia habari zote zinazoihusu.” Hapo Gad Yaakobi akagundua mara moja kuwa amekabidhiwa jukumu la kushughulikia suala la kupotea kwa ndege hiyo—iwe ni kwa utekaji au kuanguka.
Baada ya dakika chache, taarifa zaidi kuhusu ndege hiyo zikaanza kumiminika. Ingawa huo ulikuwa ni muda wa kupata chakula cha mchana, njaa waliyokuwa nayo maofisa wa Serikali ya Israel ilitoweka. Badala ya kwenda kupata mlo, walianza kukusanya habari zozote kuhusu ndege hiyo.
“Airbus (ndege) iliyopotea imeondoka hapa (Tel Aviv) na abiria 245 na wafanyakazi 12,” waliripoti maofisa usalama wa Uwanja wa Ndege wa Ben-Gurion mjini Tel Aviv ambao walikuwa wakipitia mafaili yote yanayohusu safari ya ndege hiyo.
“Tunaamini kulikuwa na Waisraeli 83—lakini labda walikuwako wengi zaidi kwa sababu baadhi ya abiria wana uraia katika nchi nyingine ... idadi isiyojulikana ya Waarabu wanaaminika kuwa walihamishiwa kutoka Shirika la Ndege la Singapore ambayo iliingia Athens muda mfupi kabla ya ndege Flight 139 (kutua na kupaa)…” anaandika Brigadier J. Nazareth katika kitabu chake, ‘Creative Thinking in Warfare’.
Timu ya kushughulikia tatizo hilo ikaundwa saa 9:30 alasiri—ikiwa ni saa mbili kabla ya taarifa za kijasusi kuanza kumiminika na robo saa tu kabla ya kuvunjika kwa kikao cha bunge la nchi hiyo. Waliojumuishwa katika timu hiyo ni pamoja na waziri mkuu na mawaziri wengine watano wa baraza lake. Miongoni mwao alikuwamo pia mnadhimu mkuu wa IDF, Luteni Jenerali Mordechai “Motta” Gur, ambaye alikuwa akisifiwa sana kama “mwanajeshi mahiri”.
Kila mjumbe wa timu hii alikuwa na wataalamu wake waliobobea katika nyanja mbalimbali za kigaidi, kijeshi, kisiasa, kidiplomasia na kijamii. Walikutana kwa haraka kwa ajili hiyo. Kwao hili la kupotea kwa ndege yenye Wayahudi lilikuwa jambo la udharura wa hali ya juu sana. Hadi muda huu hakuna hata mmoja wao aliyekuwa amejua kama ndege ilikuwa imetekwa au ilikuwa imepata ajali.
“Nina wasiwasi ndege imetekwa,” Waziri Mkuu Rabin alimwambia mshauri wa kisayansi wa ulinzi wa Israel, Dk Yehezkel Dror (baadaye alikuja kuwa profesa). “Tukabiliane na ukweli halisi wa jambo hili.”
Wakati wakijadiliana hilo, ndege 139 ilikuwa bado angani ikielekea kusini badala ya kaskazini kuelekea Paris kama ilivyokuwa imepangwa.
Fuatilia nini kilitokea kesho
 
Sawa mkuu nitag
NDEGE ILIYOBEBA RAIA WA ISRAEL YATEKA ANGA LA UGIRIKI NA KUPELEKWA UGANDA - 1



Saa 12:45 asubuhi ya Jumapili Juni 27, 1976 ndege ya Shirika la Ndege ya Singapore 763 ilitua kwenye Uwanja wa Ndege wa Athens, Ugiriki, ikitokea Bahrain kupitia Kuwait.
Miongoni mwa abiria watano walioshuka kwenye ndege hiyo, wanne walielekea eneo ambalo abiria wa ndege ya Shirika la Ndege ya Ufaransa, Flight 139, wangeondokea kwenda Paris, Ufaransa.
Saa 2:59 asubuhi hiyo, ndege ya Shirika la Ndege ya Ufaransa, Flight 139 ikirushwa na Kapteni Michel Bacos ilipaa kutoka Uwanja wa Ndege wa Ben Gurion mjini Tel Aviv katika kile kilichopangwa kuwa ingekuwa ni safari ya kwenda Ufaransa kupitia Athens.
Wakati ndege hiyo Flight 139, ikitua Athens, abiria 58 waliokuwa wakiisubiri walikuwa katika hatua za mwisho za kukamilisha taratibu za uwanjani hapo.
Kwa mujibu wa Louis Williams katika kitabu chake, ‘The Israel Defense Forces: A People’s Army’, miongoni mwa abiria hao alikuwa msichana mmoja mwenye umri wa miaka 25 mwenye hati ya kusafiria ya Ecuardor. Jina lake ni Ortega na nyuma yake kwa mbali kidogo alikuwa kijana aliyekuwa na hati ya kusafiria ya Peru iliyoonyesha jina lake ni Garcia. Nyuma zaidi walikuwako wanaume wengine wawili waliokuwa na hati za kusafiria za Bahrain na Kuwait.
Flight 139 ilitua katika Uwanja wa Athens saa 5:30 asubuhi kuwabeba abiria hao 58. Wote wanne walipanda Flight 139. Saa 6:20 mchana ndege ikawa imepaa tena angani kuelekea Paris, Ufaransa, ikiwa na jumla ya abiria 246.

Baadaye, baada ya uchunguzi wa kina, ilikuja kujulikana kuwa jina halisi la mwanamke huyo ni Gabriele Kjoche-Tiedemann, ambaye aliwahi kushiriki kuwateka mawaziri wa nchi zinazochimba mafuta (Opec) katika makao yao makuu mjini Vienna, Austria katika tukio la Jumapili ya Desemba 21, 1975.
Gabriele aliwahi kuishi na aliyedaiwa kuwa ni gaidi maarufu zaidi aliyeitwa Carlos ‘The Jackal’ na mshirika wake katika hii ndege ya Ufaransa ni mwanachama wa kikundi cha kigaidi kilichojulikana kama Baader-Meinhof.
Mmoja wa Waarabu wawili waliokuwa na Ortega na Garcia baadaye walikuja kutambuliwa kama mwanzilishi na mpango mikakati wa kikundi cha Harakati za Ukombozi wa Palestina (PFLP).
Dakika nane tu baada ya kupaa angani, Ortega na Garcia na washirika wao wa Kiarabu wakaanza kile ambacho baadaye kimekuja kubaki katika vitabu vya historia duniani. Dakika nane tangu ndege kupaa, Ortega alikimbia kwa kasi kutoka kiti alichokaa hadi mbele huku akipiga kelele za kuwaamuru abiria waweke mikono kichwani. Dakika mbili baadaye mwanamama huyo Ortega akawaambia abiria kuwa wameiteka ndege hiyo na kwamba waliohusika na utekaji huo ni kundi la “Che Guevara” na kikundi cha “Gaza Unit” cha Harakati za Ukombozi wa Palestina.
Mawasiliano na ndege hiyo yalipotea muda mfupi baada ya kupaa angani kuelekea Ufaransa. Kitendo cha mawasiliano kupotea kilianzisha operesheni ya juma nzima lililoanza siku hiyo ya kutoweka kwa ndege hiyo-Jumapili ya Juni 27 hadi Jumapili ya Julai 4, 1967-iliyowahusisha makomandoo wa Jeshi la Israel (IDF). Operesheni hiyo iliitwa Thunderbolt na iliendeshwa kwa usiri mkubwa hadi pale ilipofanikiwa.
Kutoweka kwa ndege hiyo kuliingiza kazini Idara ya Ujasusi ya Israel. Kupotea kwa Myahudi yeyote ni jambo linalopewa umuhimu mkubwa sana kwa wao. Vitengo katika ujasusi wa Israel vilipoanza kufanya kazi, walipokea ujumbe mmoja uliosema:
“‘Ndege 139’ yenye idadi kubwa ya abiria ambao ni raia wa Israel ni ama imeanguka au imetekwa.” Ujumbe wa pili ukasema: “Ndege iliyopotea ni ndege ya Shirika la Ndege la Ufaransa, ambayo imetoka Uwanja wa Ndege wa Ben-Gurion (karibu na Tel Aviv) muda mfupi kabla ya saa tisa alasiri ...”
Ujumbe huo ulipelekwa kwenye Bunge la Israel ambalo lilikuwa katika kikao chake cha Jumapili. Waziri wa Usafiri ambaye alikuwa mchumi, Gad Yaakobi (41), aliupokea ujumbe huo na kuupeleka kwa waziri mkuu wake, Yitzhak Rabin. Muda ulikuwa ni saa 7:30 mchana, ikiwa ni dakika chache tu baada ya Ndege 139 kupoteza mawasiliano baada ya kupaa kutoka Athens.
Rabin, ambaye alikuwa jenerali mstaafu wa jeshi la Israel alimwambia Yaakobi: “Kama ndege itakuwa imetekwa, hakikisha unashughulikia habari zote zinazoihusu.” Hapo Gad Yaakobi akagundua mara moja kuwa amekabidhiwa jukumu la kushughulikia suala la kupotea kwa ndege hiyo—iwe ni kwa utekaji au kuanguka.
Baada ya dakika chache, taarifa zaidi kuhusu ndege hiyo zikaanza kumiminika. Ingawa huo ulikuwa ni muda wa kupata chakula cha mchana, njaa waliyokuwa nayo maofisa wa Serikali ya Israel ilitoweka. Badala ya kwenda kupata mlo, walianza kukusanya habari zozote kuhusu ndege hiyo.
“Airbus (ndege) iliyopotea imeondoka hapa (Tel Aviv) na abiria 245 na wafanyakazi 12,” waliripoti maofisa usalama wa Uwanja wa Ndege wa Ben-Gurion mjini Tel Aviv ambao walikuwa wakipitia mafaili yote yanayohusu safari ya ndege hiyo.
“Tunaamini kulikuwa na Waisraeli 83—lakini labda walikuwako wengi zaidi kwa sababu baadhi ya abiria wana uraia katika nchi nyingine ... idadi isiyojulikana ya Waarabu wanaaminika kuwa walihamishiwa kutoka Shirika la Ndege la Singapore ambayo iliingia Athens muda mfupi kabla ya ndege Flight 139 (kutua na kupaa)…” anaandika Brigadier J. Nazareth katika kitabu chake, ‘Creative Thinking in Warfare’.
Timu ya kushughulikia tatizo hilo ikaundwa saa 9:30 alasiri—ikiwa ni saa mbili kabla ya taarifa za kijasusi kuanza kumiminika na robo saa tu kabla ya kuvunjika kwa kikao cha bunge la nchi hiyo. Waliojumuishwa katika timu hiyo ni pamoja na waziri mkuu na mawaziri wengine watano wa baraza lake. Miongoni mwao alikuwamo pia mnadhimu mkuu wa IDF, Luteni Jenerali Mordechai “Motta” Gur, ambaye alikuwa akisifiwa sana kama “mwanajeshi mahiri”.
Kila mjumbe wa timu hii alikuwa na wataalamu wake waliobobea katika nyanja mbalimbali za kigaidi, kijeshi, kisiasa, kidiplomasia na kijamii. Walikutana kwa haraka kwa ajili hiyo. Kwao hili la kupotea kwa ndege yenye Wayahudi lilikuwa jambo la udharura wa hali ya juu sana. Hadi muda huu hakuna hata mmoja wao aliyekuwa amejua kama ndege ilikuwa imetekwa au ilikuwa imepata ajali.
“Nina wasiwasi ndege imetekwa,” Waziri Mkuu Rabin alimwambia mshauri wa kisayansi wa ulinzi wa Israel, Dk Yehezkel Dror (baadaye alikuja kuwa profesa). “Tukabiliane na ukweli halisi wa jambo hili.”
Wakati wakijadiliana hilo, ndege 139 ilikuwa bado angani ikielekea kusini badala ya kaskazini kuelekea Paris kama ilivyokuwa imepangwa.
Fuatilia nini kilitokea kesho
 
Hii n movie nishaichek naona umeamua kuja kusimulia wana huku
 
asante sana Mkuu.
Imeandikwa na Josephat Keraryo Nyambeya

AMBATANA NA MIMI

Oparesheni Entebbe ni operesheni ya kuokoa mateka wa Kisrael waliotekwa na magaidi , oparesheni hii ilifanywa na makomando wa Israel (IDF) katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Entebbe tarehe 4 July 1976, wiki moja kabla yaani tarehe 27 June ndege ya shirika la Air France ikiwa na abiria 248 ilitekwa na wanachama wawili wa chama cha vuguvugu a ukombozi wa Palestina (PFLP-EO) baada ya amri ya mtu aliyefahamika kama Wadie Haddad, pia katika utekaji huo kulikuwa na wanachama wawili wa vuguvugu za kimapinduzi huko Ujerumani.

Watekaji walikuwa wanadai Israel iwaachie huru wafungwa 40 na wengine 13 waliokuwa wamefungwa kwenye magereza mbalimbali nchini humo ili iwaachie mateka hao. Ndege hiyo iliyoanzia safari yake mjini Tel-Aviv nchini Israel ikiwa inatarajiwa kutua jijini Paris-Ufaransa ilibadilishwa uelekeo na kushuka jijini Athens-Ugiriki kwa ajili ya kujaza mafuta kabla haijapaa kuelekea Benghazi-Libya kasha Entebbe uwanja mkuu wa ndege nchini Uganda.

Serikali ya Uganda ilikuwa inawasapoti watekaji hao, na binafsi dikteta Idd Amin aliwakaribisha watekaji hao (huyu Idd Amin akili zake zilimtosha mwenyewe). Baada ya kuwaondoa mateka wote kutoka uwanjani na kuwapeleka kwenye jengo lililokuwa halitumiki hapo uwanjani, watekaji waliwatenganisha Waisrael na wasio Waisrael .

Siku mbili baadae mateka 148 ambao hawakuwa raia wa Israel waliachiwa na kurejea jijini Paris. Raia 94 wa Israel ikiwemo na wafanyakazi 12 wa shirika hilo la ndege waliachwa kama mateka na kutishiwa kuawawa .

Jeshi la Israel (IDF) lilizipata taarifa walizopewa na shirika la Ujasusi la nchi hiyo Mossad juu ya tishio la mateka hao kuuliwa kama Israel haitatii matakwa ya watekaji hao ambayo yalikuwa kuwaachia huru wafungwa wote wa Kipalestina waliokuwa kwenye magereza nchini humo. Kitisho hiki kilipelekea IDF kupanga misheni ya Uokozi, operesheni hii ilipangwa ikiwa ni pamoja na kukabiliana na Mapambano kutoka Jeshi la Uganda maana walijua fika kuwa endapo watafanikiwa kuingia Uwanja wa Entebbe kwa ajili ya uokoaji huo lazima wangekabiliana na upinzani kutoka jeshi la Idd Amini hivyo walijiandaa kwa ajili ya hilo.

Oparesheni ilifanyika usiku , Israel ilichukua ndege iliyobeba makomandoo 100 na kusafiri zaid ya Maili 2500 (Kilomita 4000) kuelekea Uganda kwa ajili ya uokozi. Oparesheni iliyochukua wiki nzima kuiandaa ilipangwa kuchukua dakika tisini tu kukamilika, Mateka 102 waliokolewa , makomando watano wa Israel walijeruhiwa, Kamanda aliyekuwa akiongoza Operesheni hiyo Lt. Kanali Yonathan Netanyahu aliuwawa. Watekaji wote, mateka watatu, na wanajeshi 45 wa jeshi la Uganda waliuliwa . Pia ndege vita 11 za jeshi la Uganda ziliharibiwa.

Opareheni hii iliyopewa jina la fumbo (codename) la Oparesheni Thunderbolt, mara nyingine huitwa oparesheni Yonathan kama kumbukumbu ya Kiongozi aliyeiongoza oparesheni hii. Kiongozi wa oparesheni hii alikuwa kaka mkubwa Benjamin Netanyahu waziri mkuu wa sasa wa Israel.

Katika uwanja wa ndege wa Entebbe watekaji wane waliungana na wenzao wanne wakiwa wanapewa sapoti na Jeshi la Uganda. Idd Amini alikuwa akiwatembelea mateka kila siku na kuwapa maendeleo ya mazungumzo juu ya kile kilichokuwa kikiendelea, na kuwaahidi kuachiwa huru kama maafikiano yatafikiwa. Tarehe 28 siku moja baada ya utekaji watekaji walidai fidia ya dollar Millioni 5 ili waiachie ndege na pia wapalestian 53 waliokuwa wamefungwa kwenye magereza ya Israel wachiiwe huru. Walidai kama madai yao hayatatekelezwa wataanza kuwaua mateka kuanzia tareh 1 July mwaka huo wa 1976.

Wiki hiyo Israel ilijaribu kutumia majukwaa ya kisiasa ili kuwaokoa mateka. Vyanzo vingi vinadai baraza la Mawaziri la Israel lilipanga na kukubaliana kuwaachia wafungwa hao wa Kipalestina ili kuokoa roho za waisrael hao waliotekwa. Burka bar-Lev afisa mstaafu wa jeshi la Israel alikuwa anamjua Idd Amin kwa mda mrefu alipewa jukumu la kumbembeleza Idd Amin ili awaachie mateka hao, Bar-lev alikuwa akimpigia simu mara nyingi Idd Amin kumuomba awaachie mateka bila mafanikio, Idd Amin hakuelewa somo. Israel iliomba Marekani kuongea na rais wa Misri Anwar Sadat aliyekuwa na mahusiano mazuri na Idd Amin kumuomba awaachie mateka bila mafanikio. Sadat alijaribu kuongea na PLO na seriakli ya Uganda , pia Mwenyekiti wa PLO wa kipindi hicho Yasser Arafat alituma ujumbe wake nchini Uganda kuongea na watekaji ila watekaji walikataa katakata kuonana na mjumbe huyo aliyetumwa.

Tarehe ya mwisho ilifika (yaani tarehe 1, July) na hapo baraza la mawaziri la Israel liliomba watekaji kusogeza mda hadi tareh 4 ili waweze kukubalina . Idd Amin pia aliwaomba wasogeze siku hadi tarehe hiyo hadi arudi kutoka kwenye mkutano mkuu wa Umoja wa Afrika (Kipindi hicho OAU) alipokuwa anaenda kukabidi Uenyekiti wa mkuu mwingine wan nchi.

Kukubaliwa kwa ombi hili kuliwafanya Waisrael kujipanga zaidi jinsi ya kuifikia Entebbe. Tarehe 3 July saa 12:30 jioni Baraza la mawaziri la Israel lilibariki kufanyika kwa oparesheni hii, utekelezaji wa Oparesheni hii ukiwasilishwa na Meja Jenerali Yekutiel Kuti Adam na Brigedia Jenerali Dan Shomron mbele ya baraza hilo.

Mwanzoni operesheni ilipangwa kwa kuwadondosha makomando wa Kiyahudi ndani ya ziwa Vicktoria na kuwaacha watumie boti za mipira hadi kwenye ncha ya uwanja wa ndege wa Entebee ulipo pembezoni kabisa mwa Ziwa Vicktoria. Walipanga kuwauwa watekaji wote na kuwaokoa mateka, ila baadae Israel iliukaaa mpango huu kwa sababu ya kuwa walipata taarifa kuwa Ziwa Vicktoria lina mamba wengi hivyo ingekuwa hatari kwa mateka waliokolewa.

Wakati wakipanga oparesheni hiyo walijiuliza watajazia mafuta wapi kwenye ndege yao waliyopanga kuitumia kufika Entebbe, walikosa ndege ya kuweza kufika Entebbe na kurudi Israel bila kujazwa mafuta, hivyo kitu hicho kikawaumiza kichwa tena. Walipanga kuongea na moja ya mataifa ya Afrika ya Mashariki ili kuweza kuwaruhusu kutumia uwanja wao wa ndege kwa ajili ya ndege yao kutua na Kujaza mafuta. Katika kuitafuta nchi ambayo ingewakubalia ombi lao wakaamua kuichagua Kenya na kuwatuma mabalozi wake waliokuwepo nchini Kenya pamoja na wafanyabiashara wa Kiyahudi wenye ushawishi mkubwa nchini Kenya kwenda kuongea na Rais Jomo Kenyatta juu ya ombi lao hilo, msomaji naomba ufahamu kuwa Tanzania haikuwa na uhusiano mzuri na Israel kwa hiyo njia pekee iiyokuwepo ni kuitumia Kenya.

Oparesheni hii isingeweza kufanikiwa bila msaada wan chi yoyote ya Afrika Mashariki, waliotumwa kwa Kenyatta walibubujikwa na machozi ya furaha baada ya ombi lao la kuutumiwa uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta kukubaliwa. Kenyatta pia aliwaruhusu MOSSAD kuitumia Kenya kama njia ya kukusanya taarifa za kiintalenjesia.

Mossad ilipata picha kamili ya mahali walipo mateka, idadi ya watekaji pia walizipata taarifa za juu ya uhusikaji wa Jeshi la taifa la Uganda kutoka kwa wale mateka walioachiwa na kurudi Paris (moja ya udhaifu wa watekaji hawa). Taarifa za mateka hao waliochiwa zililisaidia sana Jeshi la Israel na Mossad kujua idadi ya kikosi watakachokituma Entebbe.

Kama bahati ya mtende kuota Jangwani Mossad pia ilipata taarifa za kuwa kuwa Uwanja huo wa ndege wa Enttebe ulijengwa na kampuni moja la Kisrael mnamo mika ya sitini, hivyo iliwasiliana na kampuni hilo liitwalo Solel Boneh na kupata ramani kamli ya uwanja huo na majengo yaliyopo uwanjani hapo.

Kikosi kazi kikiwa na Makomandoo wapatao 100 na silaha nzito nzito walijindaa kuelekea Uganda. Kikosi kazi hizi kiligawanyika katika vitengo vitatu,

Moja, kamandi ya Ardhini iliyoongozwa na Brigedia dan Shomron na muwakilishi wa Kikosi cha anga Kanali Ami Ayalon, kikosi hiki kilikuwa na jukumu moja tu la kuhakikisha ulinzi unaimarishwa uwanjani hapo pamoja na kuyakata mawasiliano yote kutoka uwanjani hapo. Kikosi cha pli kikiongozwa na Kamanda kijana wa miaka 29 tu Luteni Kanali Yonathan Netanyahu kikosi hiki kilikuwa na makomando kutoka kambi ya Sayeret Matkal kilipewa kazi ya kuuteka uwanja wa ndege wa kuingia kwenye terminal na kuwaokoa mateka, Meja Betser alichukua nafasi ya kukiongoza kikosi hiki baada ya Yonathan kuuwawa kwa risasi. Kikosi kazi kingine kilipewa jukumu la kuzilinda njia za Kutulia ndege (runways-siko vizuri Kiswahili mnisamehe) na kulinda sehemu ya kujazia mafuta na kuhakikisha ndege za Israel zinajaza mafuta uwanjani hapo kabla ya kupaa (Yaani hii ni sawa na kuvamiwa na Majambazi ukiwa umelala na mkeo wewe unainamishwa nay eye anainamishwa mbele yako). Kikosi hiki kiliongozwa namakamanda watatu walikouwa na majukumu tofauti, kikosi hiki pia kilipewa jukumu la kuharibu ndege vita zote za jeshi la Uganda zilizokuwepo uwanjani hapo.

Kikosi hiki makini cha makomando wa kiyahudi kilipaa kutoka Sharm el-Sheikh ndege iliyowabeba makamanda hawa ikiwa inaruka umbali wa Mita 30 (futi 100) tu ili kuepuka kunaswa na Rada za Sudan, Misri na Saudi Arabia (kwa wataalamu wa RADAR nadhani watakubaliana na mimi) kilipita bahari ya shamu kuelekea Kusini na kasha kupita Djibouti kutoka huko walitua uwanja wa ndege jijini Nairobi, wakiwa na ndege mbili za Boeing 707 ndege moja ikiwa ikiwa imebeba madawa na vifaa tiba na ndege ya pili kikiwa imewabeba makamanda.

Jeshi la Israel lilitua uwanja wa Entebbe saa tano kamili usiku July 3, ndege ya mizigo ikiwa tayari imefunguliwa milango gari nyeusi aina ya Mercedes Benz iliyofanana na ile aliyokuwa anatembelea rais Idd Amin ilishuka kutoka kwenye ndege ikiwa imeambatana na Land Rovers kadhaa sawa na zile zilizokuwa zinampa Idd Amin eskoti, walizitumia hizi kupita check points zote za uwanjani hapo. Ndege ya pili iliyowabeba makamanda wa kazi ilitua dakika sita baadae na hapo hapo wakayadandia magari hayo kuelekea kwenye jengo walipo mateka wakiwa wanafanana sawa sawa kabisa na Idd Amin, wakiwa wamekaribia terminal ya pili Maaskari waliokuwa guard wakiwa wanatambua kabisa kuwa Idd Amin alikuwa siku chache zilizopita alikuwa kanunua Mercedes nyeupe na kuachana na ile nyeusi walisimamisha msafara huo, makomando hao waliwafiatulia risasi kwa kutumia bastola za sailensa lakini hawakuwaua lakini komando mmoja aliyekuwa kwenye rand Rover za msafara aliwamalizia kwa kutumia bunduki kubwa isiyotoa sauti.

Wakiwa wameingia kwenye jengo lililokuwa linawafuga mateka hawa makomando walipaza sauti kutumia Vipaza sauti wakisema kwa Kingereza na Kiebrania kuwa “KAA CHINI, KAA CHINI” sisi ni wanajeshi wa Israel , kijana wa Kiyahudi wa miaka 19 alijaribu kusimama na alipigwa risasi kwa kudhaniwa kuwa alikuwa mtekaji. Pia mzee wa miaka 52 aliuwawa kimakosa baada ya kujeruhiwa na risasi ya jeshi la nchi yake, pia mateka mmoja mwenye asili ya Urusi aliuuliwa kwa risasi ya watekaji.

Wakiwa wanaendelea na oparesheni hii makamanda wa kiyahudi waliwauliza mateka kwa kiebrania walipo watekaji wengine na waliwaonyesha kwa vidole kuwa watekaji hao wamejificha kwenye chumba kinachofuata, makomandoo walikibomoa chumba hicho kwa magruneti kabla ya kuingia ndani na kuwamiminia risasi watekaji hao wa Kipalestina.

Kipindi wakiendelea a zoezi hilo la uokozi ndege vita tatu aina ya C-130 zilitua uwanjani hapo ili kutoa ulinzi wa anga ikiwa pia na kuzilinda ndege za jeshi la israel zikiwa zinajaza mafuta uwanjani hapo, oparesheni ya kuwaokoa mateka pia ilienenda sambamba na kuziharibu ndege za jeshi la Uganda zilizokuwepo uwanjani hapo.

Wakiwa wanaendelea kuwapakia mateka kwenye ndege zao wanaeshi wa Uganda waliendelea kurusha risasi, wanajeshi hawa wa Uganda wakiwa wanarusha risasi kutoka mnara wa kuongozea ndege walifanikiwa kuwajeruhi makomando watano na kumuua Kiongozi mmoja wa oparesheni Luteni Kanali Yonathan Netanyahu, makomando wa Israel walirusha RPG (wanaojua dhana za kijeshi RPG siyo jina geni kwao) na kuuharibu kabisa mnara huo wa kuongozea ndege, kulingana na mmoja wa vijana wa Idd Amin askari aliyempiga risasi Yonathan Netanyahu aliuliwa katika majibizano hayo ya risasi.

Zoezi hili lilichukuwa dakika 53 pekee japo lilipangwa kuchukua dakika 90. Katika oparesheni hii jumla ya wanajeshi 45 wa Uganda waliuliwa, mateka wote wanane waliuliwa, komando mmoja wa Israel alikufa, pia makomando 5 kujeruhiwa, ndge vita 11 za jeshi la Uganda aina ya Mig-17s na Mig-21 zilliharibiwa, pia kati ya mateka 106 mateka 3 waliuwawa kama nilivyoelezea mwanzoni pia na mateka mmoja kikongwe wa miaka 75 alisahaulika Uganda kikongwe huyu alichukiliwa nakupelekwa hospitali ya taifa ya Uganda-Mulago ambapo aliuliwa na wanajeshi wa Uganda kesho yake akiwa kitandani .

Ni hayo tu kwa leo, sina mengi ya kueleza juu ya oparesheni hii ila hayo kiduchu ninaamini yamekufanya uipate picha juu ya kile kilichotokea miaka 40 iliyopita. Ninaweza nikawa sijaandika kwa mtiririko mzuri ila nadhani hoja yangu imefika na imeeleweka.

Unaweza wasiliana nami kupitia +255653737353 (WhatsApp) au nyambeya@yahoo.com

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Netanyahu ndio maana haishi kwenda kuhiji Uganda
Kaka yake was a casualty of the operation
 
Back
Top Bottom