A BITTER TRUTH: Kwanini watu weusi walishindwa kwenda Ulaya/Amerika (Ughaibuni) kuwachukua wazungu (Whites) kisha kuwaleta Afrika kuwafanya watumwa?

Unaacha kitu baada ya kukupa faida...mifumo hubadilika na kuboreshwa ..kwa sasa tuko katika utumwa wa kiaina nyingne tofaut...na watu weupe wanalijua hilo...hapo zaman vita za mabomu na silaha vilitumika kwa sasa vita za kibiashara na uchumi na maradh ndio znatumika....utumwa wa karibu miaka 600 ulikua na faida sana kwa waliofanya..kwahyo tuendelee tafuta jib y mtu mweupe alijanjaruka mapema namna hyo.....kwangu mm jib langu ni 1..sabab za kimazingira tu..ukiwa mboga saba huwez jua kutafta chakula.ila mtoto aliezaliwa mlo m1 kwa siku atajua tafuta chakula..and the principle goes on and on.
 
Nguvu ya damu katika ulimwengu wa roho ni kubwa ila Mungu kwa uwezo wake mkuu hangeweza kutoa kafara ya damu kama tunayofanya binadamu.
 
Watu wa kwanza walikuwa weusi ..baada Khanna kuzaliwa weupe tukaanza kuwatenga katika miji yao ama kuwatupa wakawa hawana kauli kwenye jamii ya weusi..sisi tulianza wao wanamaliza hahahaha
 
Ukweli ni kwamba ngozi nyeupe ina ubongo mahiri kuliko sisi mfano mtoto wa kizungu wa miaka 3 na mtoto wa ki Africa wa miaka hiyo hiyo ukimuuliza swali flani halafu ukalinganisha majibu utagundua mtoto wa kizungu Ana bongo iliyochangamka kidogo kuliko sisi.
 
Si kweli ni issue ya makuzi na handling ya mtoto, watoto wa kizungu tangia anapozaliwa huwa anafunzwa kujiamini na kuwa mdadasi hii ni kwakuwa mtoto anajifunza kwenye mazingira aliyomo na wazungu wana mazingira rafiki sana ya watoto kujifunza.

Mengine ni conspiracies na racism za wazungu kuna uthibisho mwingi waafrica wameonekana kuwa brilliant kuliko wazungu mara nyingi tu.
 
Wana kitu cha ziada kwenye ubongo, kitendo cha kugundua "maisha ni mchezo " wanatuchezea nasi tunafunga macho kwa kupiga maombi. Angalia kwa upande wa Wakristu Yesu alizaliwa Ulaya, sisi ni kupokea taarifa bila hata kuhoji. Tukatupilia mbali utamaduni wetu na kufuata wa kwao. Ila tukijikita katika "life is a game " tutacheza kwa makini ili tuwakaribie.

Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app
 
kwenye neno " watu weusi " weka neno "wana CCM" alafu jiulize "yanafaa kwenda ulaya nchi gani hasa"?

watu asio na utu ?
 
Wao walipata wapi hiyo elimu.
Elimu hiyo ilitokana na ustaarabu uliopo eneo hilo kigeographia, mashariki ya kati na ulaya ustaarabu ulianzia hapo maelfu ya miaka mapema sana,

*Najua utaniuliza na huo ustaarabu kwanini ulianzia hayo maeneo?!

Jibu ni rahisi tu: kila kitu kina mwanzo, lazima kuwepo na sehemu ya chanzo, hata wewe una wazazi sasa nikikuuliza kwanini wewe usingewazaa wazazi wako ila wamekuzaa wewe nadhani tutakuwa tunarudi kwenye kioja cha kuku na yai kipi kilianza?!

Elewa tu kila kitu lazima kiwe na chanzo (source), au amini ni Mungu kama ni mtu Wa dini. Maana eneo hilo la mashariki ya kati ndipo inakosadikika ilipokuwepo bustani ya edeni kwenye nchi ya Iraq ya sasa karibu na mto frati, palipoitwa nchi ya Babeli au Babylon.
 
Africa sehemu kubwa sana unaweza kupanda mazao na kulima mwaka mzima.

Ulaya kipindi kirefu cha baridi huwezi kulima.

Ni wazi mtu ambaye kwake hakuna neema hii atataka kwenda sehemu nyingine ambayo ina neema hii.

Sent using Jamii Forums mobile app

Lakini Kwenye Geography yetu tulisoma, Kilimo cha Ngano Canada, Mahindi US, Mpunga Malaysia, Mpira Burma, Nyama Denmark, Sufi Australia nk
Pamoja na Vipindi vyao virefu vya Baridi na barafu
 
Lakini Kwenye Geography yetu tulisoma, Kilimo cha Ngano Canada, Mahindi US, Mpunga Malaysia, Mpira Burma, Nyama Denmark, Sufi Australia nk
Pamoja na Vipindi vyao virefu vya Baridi na barafu
Ulisoma Canada inaotesha mazao miezi mingapi ya mwaka?
 
Kaka jaribu kuangalia ramani. Bethlehemu iko wapi?
Yesu hakuzaliwa Ulaya. Imani katika yeye ilipofika Ulaya, wakristow aliteswa kwa kuleta imani ya kigeni. Nchi kama Ulaya, Uingereza na penginepo unapata makundi ambao hadi leo wanadai kurudi kwenye "dini ya mababu" (kwa nini hakuna anayetaka dini ya mabibi???) soma Neopaganism, Druidry, Wicca. Urithi wa Ulaya kabla Ukristo unaona katika siku za wiki: zote zina majina ya miungu yao: Moon-day, Tiu's-day, Wodan's-day, Thor's-day...
Ukristo ulikuwa kigeni Ulaya wakati umeshakuwa nyumbani Misri, Sudani na Ethiopia miaka mingi...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…