A BITTER TRUTH: Kwanini watu weusi walishindwa kwenda Ulaya/Amerika (Ughaibuni) kuwachukua wazungu (Whites) kisha kuwaleta Afrika kuwafanya watumwa?

A BITTER TRUTH: Kwanini watu weusi walishindwa kwenda Ulaya/Amerika (Ughaibuni) kuwachukua wazungu (Whites) kisha kuwaleta Afrika kuwafanya watumwa?

Umesema:
"Ulaya kuna kundi kubwa la mataifa ambayo huitwa "Slavonic", maana yake kiasili "slaves" = watumwa."
Siyo kweli, pitia hapa au tupatie source yako.
Kuhusu uhusiano wa jina la kundi la mataifa ya Ulaya Mashariki na "slave = mtumwa" angalia hapa:
"The English term slave derives from the ethnonym Slav. In medieval wars many Slavs were captured and enslaved, which led to the word slav becoming synonym to "enslaved person".[21][22][23] In addition, the English word Slav derives from the Middle English word sclave, which was borrowed from Medieval Latin sclavus or slavus,[22][24][25] itself a borrowing and Byzantine Greek σκλάβος sklábos "slave," which was in turn apparently derived from a misunderstanding of the Slavic autonym (denoting a speaker of their own languages)."
 
Ndio. Kumfanya mtu mwenzako mtumwa ni kitu kizuri kama kina maslahi mapana kwa taifa. It's the survival of the fittest.

Slavery was the necessary evil just like wars, na wazungu (ambao ndio wametuletea dini) walijua fika ya kuwa hili si suala jema lakini wakalazimika kulifanya kwa maana lilikuwa na maslahi makubwa kwa mataifa yao
Jibu zuri sana hili
 
Bila kuathiri majibu ya watu wengine, sababu ya ziada ninayofikiri ni kwamba inawezekana Wazungu walikuwa na shida nyingi kuliko Waafrika. Kabla hawajagundua teknolojia watu wao wengi walikufa kutokana na mazingira magumu ya kuishi, ikiwa ni pamoja na baridi kali, njaa, magonjwa nakadhalika -- yaliyotokana na jiografia ya nchi zao. Ilibidi watumie akili za ziada kuishi. Wakajikuta wanatoka 'nje ya box' hadi kufika kwetu. Kwa upande wetu huku Africa, Mungu alitupendelea sana kwa raslimali nyingi, hali ya hewa nzuri n.k. ikawa huhitaji kutumia akili nyingi sana 'kusavaivu' Afrika. Tukabweteka. Bahati mbaya sana tunaendelea kubweteka hadi leo.
Inaleta mantiki kwa kiasi fulani
 
Kwahiyo mtu akifanyiwa kitu flan na asipoumia bas hajafanyiwa ubaya
Kuumia maana yake ni nini?

Unaweza kunipa mfano wa ubaya unaoweza kufanywa bila mtu kuumizwa?

Ninapoongelea kuumizwa maana yake si lazima mtu asikie maumivu.

Mtu akiibiwa na kuharibiwa uchumi wake, hata kama hajajua, bado kaumizwa kiuchumi hapo.

Na inawezekana asipojua ndiyo kaumizwa zaidi maana atashindwa hata kujipanga kupambana na hali halisi ambayo haijui.

Kaibiwa mali, lakini pia kakosa na ujuzi wa kujua kaibiwa mali.
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty. Eti ndugu zangu watanzania;

Kwanini watu weusi walishindwa kuwa wa kwanza kwenda Ulaya/Amerika (Ughaibuni) kuwachukua wazungu kisha kuwaleta Afrika kuwafanya watumwa?

Kwanini wazungu/waarabu waliweza kuwa wa kwanza kuwaza kuja kuwazoa babu zetu na kuwafanya bidhaa?

Waafrika tulikosa nyenzo gani za kutufanya kuwa wa kwanza kwenda Ughaibuni kisha kuwazoa wazungu kuja kufanya kazi za kitumwa katika mashamba yatu?

Je, hii inadhihirisha ya kuwa wazungu/waarabu wana kitu cha ziada kwenye akili/bongo zao (highly intelligent) tangia zama za kale mpaka wakawaza kuja Afrika kwa mara ya kwanza?

HILI SWALI WADAU WENGI WANALIKWEPA
Je, kuna umuhimu wowote wa watu wa bara la Afrika kuendelea kulialia na kulalamikia biashara ya utumwa kama ni janga lililowarudisha nyuma kimaendeleo mpaka sasa?


NINAOMBA KUWASILISHA MADA HII FIKIRISHI. KARIBUNI SANA KWA MICHANGO YENU NDUGU ZANGU

KUMBUKA
: KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TAFADHALI TIMIZA WAJIBU WAKOIPASAVYO.
Kwa sababu hawakuona sababu ya kufanya hivyo.
 
Kuna kitu Mungu alipunguza kwenye akili ya mwafrika, ndio maana tulipokea imani zao ukristu (uzungu) na uislamu (uarabu) bila hata kuhoji. Huenda miakav1000 ijayo Waafrika tutaibuka na Yesu wetu aliyezaliwa kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro na kuwapelekea habari njema huko Ulaya.
 
Bila kuathiri majibu ya watu wengine, sababu ya ziada ninayofikiri ni kwamba inawezekana Wazungu walikuwa na shida nyingi kuliko Waafrika. Kabla hawajagundua teknolojia watu wao wengi walikufa kutokana na mazingira magumu ya kuishi, ikiwa ni pamoja na baridi kali, njaa, magonjwa nakadhalika -- yaliyotokana na jiografia ya nchi zao. Ilibidi watumie akili za ziada kuishi. Wakajikuta wanatoka 'nje ya box' hadi kufika kwetu. Kwa upande wetu huku Africa, Mungu alitupendelea sana kwa raslimali nyingi, hali ya hewa nzuri n.k. ikawa huhitaji kutumia akili nyingi sana 'kusavaivu' Afrika. Tukabweteka. Bahati mbaya sana tunaendelea kubweteka hadi leo.
Jibu zuri ila sidhani kama linatosha
 
Elewa hoja...kwanini watu weusi hatukuweza kuwafanya hivi wao?

Basi niongeze...kwanini tulishindwa kupinga hali hii?
Mtu mweusi anayapa kipaumbele mahusiano kuliko kushinda kiuchumi.

Ndiyo maana kiutamaduni mtu mweusi sehemu nyingi ni mjamaa, yuko radhi kuweka kipaumbele kugawana na wenzake kidogo alichonacho kuliko kujilimbikizia yeye awe nacho kingi huku wenzake hawana kitu.

Ukiwa na mentality hii ni vigumu kumfanya mwingine mtumwa on a massive scale kama walivyofanya wazungu na waarabu.

Kuhusu kupinga.

Tumeshindwa kupinga hili, na pengine moja ya sababu ya kushindwa kufanya wengine watumwa, kwa ajali ya kijiografia.

Watu weusi wa kusini mwa jangwa la Sahara wametengwa na dunia kwa bahari ya maji na na bahari ya mchanga (jangwa la Sahara).

Wakati watu wa Eurasia na North Africa wanabadilishana ujuzi na kufanya biashara kwa miaka mingi, watu wa huku Afrika kusini mwa jangwa la Sahara walijuwa wametengwa na dunia hiyo, na kutengwa huko kuliwafanya wasiendelee kibiashara na kiuchumi, na hivyo kiteknolojia.

Kutoendelea huko ndiko kulifanya hata wasiweze kupinga biashara ya utumwa.

Zaidi, watu weusi hawakujiona kama wamoja, wengi waliuzana kwa kuangalia tofauti za makabika na madaraja katika jamii. Weusi wengi, mfano machifu, waliwauza weusi wenzao.
 
1.Technology-mzungu na muafrica walikutana kwa mara ya kwanza mnamo karne ya 15 wakati huo mzungu yupo mbali kidogo katika teknolojia mfano silaha hivyo tusingeweza kuwateka kama tungeenda

2.Umasikini -Mzungu aliweza kufika huku kututeka kutokana na kwamba alikuwa na capital sasa kwa mfano mkwawa angeweza ku finance jeshi lake kwenda Ulaya ?

3.Kutokuwa na Wazo hilo- Mu Africa hakuwa na wazo la kumtawala mzungu kama mtumwa kwa sababu wazungu walimuitaji mtu mweusi kumfanya mtumwa kwenye mashamba ya Miwa nk lakini sisi tuliitajiana kufanyana misukule

4.SABABU ZA KIUTAWALA-Wazungu walikuwa na mfumo mzuri wa kiutawala kwa mfano Uingereza ilikuwa chini ya utawala wa kifalme pamoja na nchi zingine za Ulaya lakini huku kwetu tuliongoz kitemi kila kabila na mtemi wake hivo isingewezekana wote wakubaliane katika kwenda Ulaya na kuteka wazungu
Umenena vema mkuu.
 
Bila kuathiri majibu ya watu wengine, sababu ya ziada ninayofikiri ni kwamba inawezekana Wazungu walikuwa na shida nyingi kuliko Waafrika. Kabla hawajagundua teknolojia watu wao wengi walikufa kutokana na mazingira magumu ya kuishi, ikiwa ni pamoja na baridi kali, njaa, magonjwa nakadhalika -- yaliyotokana na jiografia ya nchi zao. Ilibidi watumie akili za ziada kuishi. Wakajikuta wanatoka 'nje ya box' hadi kufika kwetu. Kwa upande wetu huku Africa, Mungu alitupendelea sana kwa raslimali nyingi, hali ya hewa nzuri n.k. ikawa huhitaji kutumia akili nyingi sana 'kusavaivu' Afrika. Tukabweteka. Bahati mbaya sana tunaendelea kubweteka hadi leo.
Kwahiyo hapa tukubaliane waafrika tulikuwa malastborn wa dunia🤣🤣 tulipendelewa sana na Mungu baba kutugea kila kitu hadi tukajisahau
 
Kwasababu africa tumeubwa na moyo wa ukalimu,utu na upendo hatuwezi mfanyia binadam mwenzetu yale tusiyopenda sisi kufanyiwa
Afrika na ukarim wap na wapii?? Usichanganye ukarimu na ushamba😂😂😂
The truth is, sisi sio wakarimu ila tunapoziona zile rangi nyeupe tunakuwa na kamchecheto fulani cha ushamba..
Sisi kwa sisi tunafanyiana mambo mengi sana ya kutisha na kustahajabisha, hatupendani.
 
Back
Top Bottom