A BITTER TRUTH: Kwanini watu weusi walishindwa kwenda Ulaya/Amerika (Ughaibuni) kuwachukua wazungu (Whites) kisha kuwaleta Afrika kuwafanya watumwa?

This question is a result of the lack of History knowledge.Kwa bahati mbaya kwa ujinga wetu tumekubali Wazungu kufuta Historia yetu.Kizazi ambacho kimekuwa affected sana ni mile kikicho kwenda shule kipindi cha Mwinji,Mkapa na Kikwete.I call it a lost generation.Ipo urgent need ya kubadilisha mitaala na kufundisha historia ya Mwafrika.Vitabu kama "A short history of Tanganyika," viko wapi?
 

Wewe unajibu kwa mipasho, jamaa ameuliza maswali ya msingi na muhimu sana, kuna watu wanafuatilia huu uzi wakiwa na nia ya kujifunza.
 
Sasa mbona makao makuu ya madhahebu ya kikirsto yapo Ulaya na Marekani?
Si vile. Kwanza ni Wakatoliki tu, makao makuu Roma. Madhehebu mengie hayana makao makuu kweli; Anglikana Askofu wa Canterbury yuko Uingereza, lakini si mkuu wao, ni kama mwenyekiti wa maaskofu wao kwa heshima. Si zaidi, hakuna makao makuu. Vilevile Walutheri. Wanalo shirikisho, wamepeleka ofisi kuu (lakini ni ofisi tu, haina mamlaka) pale Geneva Uswisi kwa sababu ilikuwa nchi isiyoshikamana na upande wowote wakati wa vita za karne ya 20 (kumbuka Tanzania ilishiriki vita zote mbili WWI na WWII kama eneo la Uingereza). Waorthodoksi askofu mkuu wa heshima yuko Uturuki (Ecumenical Patriarch), Makanisa makubwa ya kale ya Afrika ni Kopti wa MIsri na Waethiopia, hawana mkuu pale Ulaya.

Makanisa ya Ulaya yalienea sana kwa sababu walikuwa na pesa (wakiwa katika nchi za viwanda) wakatumia nafasi ya ukoloni wa nchi zao. Ukiona wapi Walutheri katika Afrika utaona kwanza koloni za zamani za Ujerumani . . . . (serikali ya Ujerumani haikupenda kuona wamisionari Waingereza ...)
 
Wewe unajibu kwa mipasho, jamaa ameuliza maswali ya msingi na muhimu sana, kuna watu wanafuatilia huu uzi wakiwa na nia ya kujifunza.
Hapana mkuu huyu jamaa hana nia ya kujifunza,ana nia ya kutudhalilisha kama Waafrika.Ndio maana nimempasha kidogo.
 

Kwanini mzungu awe mbali kidogo? Huu ndio msingi wa swali langu. Ina maana wazungu wapo very intelligent tangia zamani sana na ndio maana wanatawala dunia mpaka sasa?
Actually sababu iliyofanya Afrika tusiitawale Europe,Asia,nk
Ni kwamba Afrika tulikuwa "Self contended" yaan tunajitosheleza kwenye kila aspect ya maisha,na hatuku (lust for more)tamani zaidi,tuliridhika na viletulivyokuwa,hivyo hatukuona umuhimu/ulazima wa kwenda Europe,asia or elsewhere kuwacolonize au kuchukua malighafi zao kwani kilakitu tulichohitaji kilikuwahapahapa Afrika

On the other end

Wenzetu from Europe,Asia etc,walikulia kwenye mazingira magumu (unfavourable condition) ,bad climate, overpopulation etc hivyo walikuwa forced kumove elsewhere ulimwenguni kutafuta mazingira rafiki kwaajili ya makazi(surplus settlement),kilimo,na malighafi nyingine muhimu kwa maisha.
Conclusion
Siyo kwamba waafrika ni wavivu/wazembe/wasio na akili, bali ni kwamba tumeumbwa kuwa wenye kuridhika na tulivyo navyo(ie furaha yetu haidepend sana kwenye material things bali inward) na hali hiyo ni bora kuliko wale wenye kucrave for more ,kwani "tamaa" na kutokuridhika ni chanzo cha mateso, maumivu na majanga mbalimbali,na ndiyo maana sometimes utagundua kuwa life la vijijini/primitive life(walioishi babu zetu) ni zuri na lenye furaha kuliko maisha yetu haya ya kukimbizana(kidigitali) yaliyojaa msongo wa mawazo, magonjwa na psychological trauma ,kadiri tunavyocrave for more the bitter we become na less craving less bitterness.
So in terms of material and technological advancement mzungu katuzidi lakini interms of inner peace and joy babu zetu walikuwa juu

#Proud to be Black
Back to Africa movement
 



✔✔✔✔✔✔✔💯% True.
 
Sio kitu kizuri ila kinaonyesha una akili kumzidi
Kufanya kitu kisicho kizuri ni alama ya kuzidi akili?

Nilifikiri mtu mwenye akili zaidi anatakiwa kufanya vitu vizuri zaidi, au?
 
Hilo ndio JIBU . Umepata 100%
 
Wanaotengeneza mabomu ya nyuklia na mabunduki wanahesabika wana akili kuliko waliobaki wakitumia mishale na manati.
Kufanya kitu kisicho kizuri ni alama ya kuzidi akili?

Nilifikiri mtu mwenye akili zaidi anatakiwa kufanya vitu vizuri zaidi, au?
 
Swali lako limekaa kifalsafa zaidi. Hakuna jibu la moja kwa moja litakalojitosheleza kukujibu. Bila kupinga majibu ya watu wengine, nitakujibu kama ifuatavyo.

1. Sehem kubwa ya Historia ya Afrika imeandikwa na Mzungu (watu wa ghaibuni). Sehem kubwa ya historia lazima itafichwa ili kuifanya Afrika kuonekana dark continent (bara lilikokuwa gizani) Hivyo ni vigumu kidogo kwa wao kuelezea uhalisia wa Afrika, ukweli walioukuta. Huenda sisi tuliwahi kwenda Ulaya kabla yao. Huenda waafrika walifika Ulaya kabla ya wazungu kuja huku, lakini hawqkutaka kuweka wazi. Nchi kama Misri, ipo kusini mwa Afrika. wao ndo wakwanza kugundua Maandishi duniani. Je kama Misri waliweza kugundua Maandishi ya kwanza duniani, je wangeshindwa kuwa na teknolojia ya kwenda Ulaya na wanapakana tu kwa umbali mdogo? Hakuna jibu la uhakika katika hilo.
 
2. Si kweli kwamba Afrika tuliridhika na Rasilimali zetu mpaka kufikia hatua ya kutotoka Nje ya Afrika. Kuna kitu kinaitwa "Ngoni Migration" ni maelezo ya namna kabila la Wangoni walivyotoka Afrika Kusini mpaka kufika Tanzania. Historia ya Ngoni Migration iliandikwa na Wazungu wao wenyewe, swali la kujiuliza. Je! Ni kweli Wangoni walikuja kuelekea Tanzania tu? Je hawakuenda na sehem zengine mpaka kupelekea kutoka nje ya Afrika? Mimi na wewe hatujui. Huenda tulifichwa. Wangoni walikuwa wakijigawa kutoka kituo kimoja kwenda kingine. Ukisoma vizuri na kwa kutafakari Ngoni Migration nadhani unaweza kunielewa
 
3. Aliyoyafamya Idd Amini. Kwa wasiomjua Idd Amin aliwahi kuwa mtawala wa Uganda, aliyefahamika na kusifika kwa namna ya utawala wake (dictator). Idd Amin aliwahi kuwatumikisha Wazungu na wakambeba juu juu. Tukio la Idd Amin halijawahi kuongelewa kwenye kitabu chochote cha Historia kilichoandikwa na Mzungu na hakitowahi kuandikwa hata siku moja kwasababu kwao hii huitwa "bitter truth" swali la kujiuliza, je! Kama Idd Amin aliwahi kufanya hivyo na hutukufundishwa haitoshi kufikiria kuwa kuna mengi tuliyafanya kwa wazungu na tumefichwa? Ukute tumewahi kwenda kwao na tukawatumikisha na kuwafanya watumwa lakini hatukawekwa wazi. View attachment 1834083
 
Ukitaja Misri tayari umejibu swali asilia. Kuna historia ndefu jinsi gani Wamisri wa Kale walikuwa na watumwa kutoka pande mbalimbali - kutoka Asia Magharibi (Wayahudi pale awali walikuwa watumwa Misri) na pia kutoka kusini (Sudan) .
Utumwa kimsingi haukuwa swali la "rangi" au Uafrika au Uzungu. Katika historia ni nchi zenye nguvu zilizotafuta watumwa. Menginevyo watumwa walikuwa wafungwa wa vita (wale ambao hawakuuawa) waliochukuliwa na washindi na kuwa watumishi. Nchi zenye nguvu ya kiuchumi zilitafuta wafanyakazi wa kulazimishwa kwa ujenzi (kama Wayahudi huko Misri), kwa kazi katika migodi, mara nyingi pia kama wanajeshi.
Ulaya kuna kundi kubwa la mataifa ambayo huitwa "Slavonic", maana yake kiasili "slaves" = watumwa. Maana walitafutwa kama watumwa na Wazungu wa Ulaya magharibi na pia na Waarabu / Waislamu.
Waafrika upande wa kusini mwa jangwa Sahara hakutafuta watumwa katika nchi za mbali. Pale ambako milki kubwa zilitokea, walikuwa na watumwa wa kutosha hapahapa. Wale upande wa kaskazini mwa Sahara walichukua watumwa mara kwa mara kutoka Ulaya na pia sehemu za kusini mwa Sahara.
 
Hata ukiangakia Ukristu ni utamaduni wa mzungu, Uislamu ni utamaduni wa waarabu, sisi Waaftika tumezika imani zetu na kupokea zao. Ninaona upeo wa Mwafrika ni mdogo pamoja na umasikini. Hatungeweza kwenda kwao na kuwafanya watumwa.
 
Hapana, tende taratibu, wao walitoa wapi huo mtaji?


Umejibu kitoto sana


Hii inawezekana lakini sio kwa ukubwa huo


Ufaransa je? german kuwa na kingship leadership sio hoja
Wote walikuwa na wafalme. Pitia historia yako tena.
 
Umesema:
"Ulaya kuna kundi kubwa la mataifa ambayo huitwa "Slavonic", maana yake kiasili "slaves" = watumwa."
Siyo kweli, pitia hapa au tupatie source yako.
 
Hapa mkuu umenena vyema, tuna tatizo kubwa sana hasa ubinafsi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…