Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 78,790
- 128,275
Naweza kupinga utumwa kama atheist kwa sababu utumwa ni immoral.Sio kitu kizuri ila ukweli ni kwamba maendeleo yote yamepatikana juu ya jasho la watumwa.
Hivi ukiwa atheist sababu zipi utazitoa kupinga utumwa?
Ukishangaa ni vipi atheist anaweza kupinga utumwa, unaniambia kwamba huelewi atheism, na pia, huelewi utumwa.
Mimi kuwa atheist ilibidi nielewe kanuni kwamba kila mtu ni sawa na mimi.
Kwamba mimi si Mkristo niliye juu ya Waislamu, Wahindu, Wa Buddhist na wengine wa dini zingine zozote.
Niko sawa na wote.
Leo kuna Coronavirus inayosababisha Covumid-18.
Haiheshimu dini.
Inaheshimu sayansi tu.
Nikiwa atheist nitapinga vipi utumwa?
Ngoja nikuoe sababu kumi. Kwa sababu napenda kuishia kwenye sababu kumi, nikitoa zaidi zitapita namba ya amri kumi za Mungu wa wengi humu.
1. Napinga utumwa kwa sababu sitaki mtu mwingine awe juu yangu bila sababu ya msingi.
2. Napinga itumwa kwa sababu sotaki mtu mwingine awe chini yqngu bila sababu ya msingi.
3. Napinga utumwa kwa sababu hauna haki. Haumpi nafasi ya juu yule anayestahili kwa uwezo wake.
4. Napinga utumwa kwa sababu unazuia maendeleo. Mtumwa mwenye akili kubwa anaweza kuwa na Bwana asiye na akili, akili kubwa za mtumwa zisiwe na maana.
5. Napinga utumwa kwa sababu utumwa hauendani na usomi. Utumwa unasisitiza kadhia na nasaba aliyozaliwa mtu, hausisitizi uwezo wa mtu binafsi.
6. Napinga utumwa kwa sababu una promote impunity.
7. Napinga utumwa kwa sababu za kihistoria. Itumwa umepigwa marifuku dunia nzima, kwa sababu watu wenye akili wameona , on a large scale, umekuwa mfumo uliopita.
8.Napinga utumwa kwa sababu ni mfumo unaofuga kisasi, na kisasi si jambo zuri kwa ustawi wa biashara.
9. Napinga utumwa kwa sababu hauruhusu waja ja wadogo kupaishwa. Wajanja wadogo ni muhimu aana.
10. Napinga utumwa kwa sababu unaruhusu wewe na mimi kuwa ni mali za mtu mwingine kama mimi na weee!
Sent using Jamii Forums mobile app