mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,309
- 4,798
"Tunajua mna tatizo kubwa la uhamiaji. Hata mimi walishawahi kunisumbua, wakaniambia mimi si raia wa nchi hii na kunitaka nipeleke vyeti vya babu yangu aliyemzaa babu yangu. Lengo lao lilikuwa kunisumbua tu, lakini chama changu cha ACT kilisimama nami mpaka mwisho. Hivyo kupitia ACT, hakuna raia atakayechukuliwa na Uhamiaji bila Mwenyekiti kupata taarifa."Ameeleza Nondo.
"Hakuna raia atanyakuliwa na Uhamiaji kuambiwa si raia bila Mwenyekiti wa kijiji kusimama na kusema, 'Huyu ni raia. Mzazi wake ninamjua, ni mzee fulani.' Mwenyekiti wa ACT atahakikisha haki na usalama wa raia wake vinaheshimiwa." Amesema Nondo.
"Chagueni viongozi ambao watakuwa watetezi wenu. Hawa mkiwachagua wanakwenda kuwa wakuu wa ulinzi na usalama katika maeneo yenu. Mwenyekiti huyo anakuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Kijiji. Hakuna raia atapotea bila taarifa kwa Mwenyekiti, na hakuna polisi atakayemchukua raia kiholela bila Mwenyekiti kujua."
"Hakuna raia atanyakuliwa na Uhamiaji kuambiwa si raia bila Mwenyekiti wa kijiji kusimama na kusema, 'Huyu ni raia. Mzazi wake ninamjua, ni mzee fulani.' Mwenyekiti wa ACT atahakikisha haki na usalama wa raia wake vinaheshimiwa." Amesema Nondo.
"Chagueni viongozi ambao watakuwa watetezi wenu. Hawa mkiwachagua wanakwenda kuwa wakuu wa ulinzi na usalama katika maeneo yenu. Mwenyekiti huyo anakuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Kijiji. Hakuna raia atapotea bila taarifa kwa Mwenyekiti, na hakuna polisi atakayemchukua raia kiholela bila Mwenyekiti kujua."