Abdulrahman Kinana asamehewa, Bernard Membe afukuzwa rasmi CCM

Abdulrahman Kinana asamehewa, Bernard Membe afukuzwa rasmi CCM

Pia ana sifa mbaya sana ya ubadhirifu wa mali ya asili hususani magendo ya meno ya tembo. Mwalimu aliwahi sema Mke wa Kaisari aliachwa sababu ya kutuhumia kutokuwa mwaminifu kwa Mumewe!!! Sasa tuache unafiki hapa…..
 
Membe alikuwa anadai Halmashauri kuu pekee ndo ina mamlaka ya kumfukuza uanachama na si kamati kuu,sasa kuweka kumbukumbu sawa hao aliowataka wagonge msumari ndo hao wamehitimisha ili asije kujifaragua baadae!

Akijitahidi sana ku-survive nje ya CCM ni miaka mitano.

Kwanza,atapoteza marafiki wa muda mrefu.

Pili, atapoteza washirika muhimu na wa siku zote.

Tatu,atakosa kilichompeleka huko aendako.

Nne,ata-swallow his pride na kurudi alikotoka.

Imeisha hiyo!!!
 
Kutubu bila kosa nako ni utumwa,ni heshima kufukuzwa kuliko kuomba msamaha kwa kosa ambalo halikuwa kosa ukabaki na heshima yako utahesabika ni shujaa asiyeendekeza njaa.
Kinana nadhani ni maslahi yamekuwa hatarini. Huyu mzee huko CCM amezoea kubebwa na kuheshimiwa sioni namna anavyoweza kuishi bila kupakatwa na Chama Tawala. Na nadhani mambo yake mengi pengine na familia yake yanategemea huruma za CCM. Hawa ndiyo wale ukienda ofisi za serikali utasikia wanasema ''huu ni mzigo wa mheshimiwa Kinana jamani, msiuchanganye na mingine''.
 
Mmiliki wa chama ataki mchezo
Wamiliki wa chama ni Mama Nyerere,Fatuma Karume.Wengine temporary membership kama UNO ya China,UK,Russia,USA,France permanet membership na Tanzania,Canada, Japan n.k temporary membership
 
Kutubu bila kosa nako ni utumwa,ni heshima kufukuzwa kuliko kuomba msamaha kwa kosa ambalo halikuwa kosa ukabaki na heshima yako utahesabika ni shujaa asiyeendekeza njaa.
Mnawadanganya wenzenu hivihivi wanatumbukia shimoni mnawaangalia halafu mnabaki mnawacheka. .
 
Halmashauri kuu ya CCM imemsamehe Katibu mkuu mstaafu kanali Kinana ambaye alipewa onyo kali na kuwekwa katika matazamio.

Halmashauri kuu pia imemfukuza kabisa yule mwingine ( Membe) ambaye hakufanya juhudi yoyote ya kuomba msamaha.
Membe alirudisha kadi yake CCM badala ya kutubu.

Maendeleo hayana vyama!

======

View attachment 1502881
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi, Abdulrahman Kinana
Akizungumza wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM cha kumteua mgombea Urais wa Zanzibar, Rais Magufuli amsamehe aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana. Rais Magufuli amesema:

Ilikuwa mwezi wa wa pili Central Committee ilaamua kutoa adhabu kwa baadhi ya wanachama wetu ambao walikiuka maadili na misingi ya chama chetu.

Kikao kile kilitoa mapendekezo ya adhabu kwa baadhi ya wanachama wetu kutokana na misingi na Katinba halali ya chama chetu. Lakini ni hivi karibuni baada ya miezi kama mnne au mitano, mwenzetu mmoja ambaye ni Former Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi alijitokeza hadharani kule Arusha, na nafikiri shahidi ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha – akaomba radhi., akautia kwa kitendo alichokifanya. Na kikubwa zaidi, ndugu yetu huyu aliomba radhi hadharani.

Ni kitendo kigumu sana kwa mtu kukifanya. Kinahitaji nguvu ya Mwenyezi Mungu tu kutubu hadharani. Mimi alinigusa sana. Nina uhakika hata ninyi wajumbe muliguswa sana. Alikuwa amepewa adhabu ya miezi 18. Hakukataa kutumikia adhabu ile.

Sasa niliona Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama tawala, chama chenye huruma. Chama chenye mapenzi mema. Chama dume. Niwaombe kwa huruma yenu kama itawezekana, huyu ndugu yetu ambaye amekubali mpaka sasa kutumikia adhhabu miezi mine, tumsamehe.

Kupitia kikao hiki napenda kusema Abdulrahman Omari Kinana amesamehewa rasmi. Niwashukuru wajumbe wa kikao hiki kwa huruma ya upendo

Yule mwingine ambaye hata jina lake sitaki kulitaja yeye ameshaondoka moja kwa moja. Adhabu yake si mnaikubali?
Unamfukuza mtu ambaye si mwanachama! Hana kadi ya CCM.
 
Sababu umeandika baada ya tukio kutokea, hutaonekana hata kidogo una uelewa mpana wa mambo, ujue tukio likishatokea, alafu ukajitungia hadithi, haipati uzito au utamu, sbb ishajulikana event yenyewe, yaani ww unaremba remba tu na urembo ukizidi huonekana ni uchafu. Kinana ana uchafu wake mwingi tu kama binadamu, sio asset kubwa kama ww usemavyo, lakini amefanya mengi tu CCM hilo liko wazi, nikuulize, je ingekuwa enzi za waasisi kama Mwl Nyerere yuko hai, unafikiri angekubali Kinana kupewa cheo kikubwa CCM? Jibu unalo, hivyo yaliyotokea, usianze kuyatungia maneno yako binafsi, yaache ukweli au uongo unajulikana, waswahili husema kwa vitu vinavyojulikana usiwawekee maneno mdomoni mwao. Busara kaa kimya, labda udogo wako ktk uelewa wa mambo sio mkubwa sana. Uamuzi wa awali wa mh. Rais Magufuli kutoa adhabu ulikuwa sahihi sana sana tu, sbb anawajua hawa watu mmoja mmoja. Ila tunyamazee
Ndugu mwenye ufinyu wa kuelewa historia ya siasa nchini kwetu ni wewe. Kwanza hujui kinana alivyoweza kufika hapa alipifikia. Kinana amelelewa kisiasa na Marehemu Mwalimu Nyerere, yeye ndiye aliyekuwa Mentor wake, na ndiye alifanya juhudi ya Kinana kupewa unaibu waziri awamu ya ya mzee mwinyi, na baadaye akawa waziri wa ulinzi, wakati wote huo Nyerere yuu Hai. Hata aliyemfanya kuwa campigner kwenye uchaguzi wa mkapa alikuwa Nyerere.

Ulizia wamjuaye Kinana alikuwa kipenzi cha nyerere. Hata Makongoro alipokuwa anaishi Arusha alikuwa akimtania kuwa Baba yake anampenda Kinana zaidi ya Makongoro
 
Membe alikuwa anadai Halmashauri kuu pekee ndo ina mamlaka ya kumfukuza uanachama na si kamati kuu,sasa kuweka kumbukumbu sawa hao aliowataka wagonge msumari ndo hao wamehitimisha ili asije kujifaragua baadae!

Akijitahidi sana ku-survive nje ya CCM ni miaka mitano.

Kwanza,atapoteza marafiki wa muda mrefu.

Pili, atapoteza washirika muhimu na wa siku zote.

Tatu,atakosa kilichompeleka huko aendako.

Nne,ata-swallow his pride na kurudi alikotoka.

Imeisha hiyo!!!
Jifunze kuishi na marafiki wa kweli na si wanafiki wanaokuchekea wakienda kwa bosi wanakugeuka.
Kwenye siasa hakuna rafiki wa kweli.
 
Wanamfukuza mtu ambaye tayari alisharudisha kadi na sio mwanachama wao?
Sio kufukuzwa, ni kuthibitisha adhabu aliyopewa. Kufukuzwa ni siku nyingi na ndio maana Kinana alishaanza kutumikia adhabu ya miezi 18. Huyu anaekuja kwenu anawafanyia usanii tu ila anatambua fika alishatimuliwa na kwa vile anawajua ni nyumbu bado mtadai amejiondoa kisha mtaliwa kichwa.
 
Siyo kila Vita inayokujia ni lazima ushindane, sometimes ni vema uka surrender kwa manufaa ya baadae. Lowassa mwenyewe karudi CCM ila pengine si kwa ajili yake binafsi bali pia kwa kizazi chake maana Siasa za kiafrica huwa hazina mipaka, hata maisha yako binafsi yataingiliwa kukudhoofisha.

MEMBE ujeuri utamponza maana kiuhalisia bado ana kundi lake kubwa CCM AMBALO lingemchagua pengine 2025 ambapo itakuwa ni kama gombania goli kwa watia nia ya Urais Kupitia CCM ila kwa sasa anajisumbua tu.

Ni imani yangu hata kipindi hiki IKITOKEA Kura ya maoni, MEMBE anaweza mpiga chini MAGUFULI maana CCM wengi wanaojifanya kumuunga mkono Rais ni wanafki kwakuwa ndo hao hao waliokuwepo nchi ikitafunwa na wachache.
Waliotupigania mpaka tukawa huru wangeangalia hayo mpaka leo tungekuwa bado tuko chini ya watawala wa kikoloni, unapopigania haki unayodhani kuwa pengine umenyimwa ni kujitoa muhanga wa kupata kile unachopigania au kupoteza rasimali zako mwenyewe, pengine na kupoteza maisha kabisa.
 
Membe anajivunia ulinzi wake anauwezo wa kujilinda binfsi huyo mwingine ulinzi wa kulindwa je atakapo aliza muda wake wakikutana chobis itakuwaje?
 
Back
Top Bottom