Absalom Kibanda akamatwa!

Absalom Kibanda akamatwa!

wanajamii naendelea kufuatilia huu mtanange wa nami zaidi kati ya wabunge hawa vijana..lakini naona kama mda wa kupiga kura umeongezwa kimyakimya,je hiyo ni njama ya kumbeba mtu au ni mpango binafisi wa mwenye blog(mjengwa)

mjengwa ni kweli umeongeza mda wa kupiga kura!!?


nawakilisha......:lol:
Hili linahusiana vipi na topic iliyopo hapa mezani? watu wengine kichefuchefu kweli!!
 
hizi ndizo ahadi jk anazoweza kuzitekeleza. . Sio za maendeleo

what a shame
 
daah! Yaani badala ya kumzawadia Beberu na Mbuguma la ng'ombe kwa kuwapa Unabii! Leo mnamkamata, heee! Kweli nabii hakubaliki kwao!
 
Waraka maalumu kwa askari wote
By
Samson Mwigamba
MAKALA hii ilikuwa itoke
Jumatano ya wiki iliyopita
lakini kwa sababu za kiufundi
ikashindikana. Imekuwa ni
bahati nzuri kwamba
inapotoka leo, ijibu swali la askari polisi dereva wa gari la
maji ya kuwasha. Askari huyo alimweleza
Mwalimu Mkuu wa watu jinsi
roho inavyomuuma pale
anapowamwagia Watanzania
wenzake maji hayo ya
kuwasha wakati wakidai haki yao. Askari uliyeuliza na
wenzako wote someni makala
hii kwa utulivu. Huu ni waraka
maalumu kwa askari wote wa
majeshi yote vikosi vyote
Tanzania Bara na Visiwani. Kwa lugha ya wazi zaidi
nazungumza na askari wa
Jeshi la Polisi Tanzania, Askari
wa Jeshi la Kujenga Taifa,
askari wa Kikosi Maalumu cha
Kuzuia Magendo (KMKM), askari wa Jeshi la Magereza na
wale wa Jeshi la Wananchi
(JWTZ). Kuwa mwanajeshi lolote kati
ya hayo niliyoyataja si dhambi
na si kweli kwamba kuwa
mwanajeshi kunakuondolea
uwezo wa kufikiri na badala
yake ukawa unafikiriwa na watu wengine. Wala haimaanishi kuwa askari
kuwa kama robot ndio
nidhamu bora kuliko zote
duniani. La hasha! Mimi
nilikataa utumwa huo! Mwaka 1999 nilihitimu elimu
ya cheti cha ufundi mchundo,
yaani Full Technician
Certificate (FTC) katika
uhandisi wa Elektroniki na
Mawasiliano ya Anga, yaani Electronics &
Telecommunications
Engineering kutoka Taasisi ya
Teknolojia ya Dar es Salaam
(DIT). Nikiwa bado sijapata kazi ya
maana, mwezi Aprili mwaka
2000 niliona tangazo la kazi ya
Radio Technician katika Jeshi
la Magereza. Nikatuma
maombi na kuitwa kwenye usaili uliofanyika Chuo cha
Maofisa wa Jeshi la Magereza
Ukonga, Dar es Salaam mwezi
Juni 2000. Wote tuliofaulu usaili
tulipangiwa siku ya kuripoti
Chuo cha Magereza Kiwira kule
Tukuyu, Mbeya. Kufika kule nilishuhudia
mambo ya ajabu. Ingawa wao
hufurahia na kusema eti
wanakutoa uraiani na kuwa
mwanajeshi lakini baadhi ya
matendo yanayofanyika wakati wa mafunzo ya jeshi ni
ya kuwapumbaza askari wetu
ili baadaye wakiwa kazini,
watawala wawatumie
watakavyo. Nilishindwa kuvumilia
kaulimbiu ya wakufunzi wa
jeshi pale walipoelekeza
kwamba chochote kruta
(askari mpya mafunzoni)
unachoambiwa lazima uitikie “ndiyo afande”. Nilishindwa
kuitikia kwa mfano pale
mkufunzi mmoja mwenye
cheo cha koplo alipotutamkia
mfululizo wa sentensi
zifuatazo: Mkufunzi: Nyinyi makruta
mbona wote hamkuja na
majembe? Makruta: Ndiyo afande! Mkufunzi: Hamkuambiwa
makao makuu ya jeshi
kwamba lazima mje na
majembe? Makruta: Ndiyo afande! Mkufunzi: Kwa hiyo kwa
kuwa hamkuambiwa na
nyinyi hamkuyabeba? Makruta: Ndiyo afande! Mkufunzi: Wote ni
wapumbavu pamoja na mama
zenu waliowazaa. Makruta: Ndiyo afande! Ni hayo pamoja na mambo
mengine ya kulazimishwa
kwenda kwenye kile
kinachoitwa disko, ambapo
pamoja na uchovu wa kutwa
nzima wa kazi ngumu na nyingi bado ni lazima ukae
hapo mpaka saa 4 usiku tena
ukinyooshewa kidole tu na
mwenzako lazima usimame
na kuimbisha wimbo tena
kwa tabasamu, wimbo mmoja wapo ukisema “Magereza
ninavyokupenda nitakunywa
sumu juu yako”, ndiyo
yaliyonifanya nikakataa kazi
ya jeshi baada ya wiki moja tu
ya mafunzo. Siku niliyokataa jeshi ilikuwa
ni Jumatano asubuhi ambapo
sikwenda mchakamchaka na
wakati wenzako
wanatawanyika kufanya usafi
wa nje maeneo mbalimbali, mimi nilibeba begi langu na
kuanza kuondoka chuoni
majira ya saa moja na nusu
hivi asubuhi. Nilikamatwa na mkufunzi
mmoja wa jeshi na kupelekwa
pamoja na begi langu kwa
Ofisa Mafunzo wa chuo.
Aliponiuliza sababu nilimtajia
mbili, kwanza kwamba sifurahii mambo ya jeshi na
kubwa zaidi kwamba mimi ni
Msabato na nimeambiwa na
wenzangu kwamba hapa
hakuna kwenda kusali, siku
zote za juma ni kazi. Kitu ambacho sitaweza maana
Sabato takatifu lazima
nipumzike! Bila kuuliza zaidi
aliconclude kwa kuniambia
kwamba, “Sijawahi kuona
mtu anaacha kazi kwa ajili ya mambo ya dini. ”Ni dhahiri wewe ulikuja
kutupeleleza na hivyo kazi
yako imeisha sasa unataka
kurudi. Tutakuweka rumande,
tena ile ya polisi kwa wiki
mbili wakati tunafanya upelelezi juu yako.” Askari aliyenileta alianza
kunivuta ili kunipeleka
rumande lakini nilikataa huku
nikiendelea kujieleza kwa
ofisa mafunzo ili ajue kwamba
sikuwa na mpango huo aliousema. Baada ya kuelemewa na hoja
zangu alinipeleka kwa
makamu mkuu wa chuo
ambaye yeye alitumia zaidi
Biblia kunihubiri kwamba
nakaidi amri ya mamlaka wakati hakuna mamlaka
isiyotoka kwa Mungu. Jibu langu lilikuwa fupi na
lenye msimamo mzito
kwamba ikiwa mamlaka ya
wanadamu inafika mahali
inanena tofauti na Mungu,
Mtume Petro ametuandikia kwamba katika hali ya namna
hiyo, “Imetupasa kumtii
Mungu kuliko mwanadamu”. Na yeye alinishindwa
akanipeleka kwa mkuu wa
chuo na wao wote wakiwapo.
Ushauri waliokuwa wakimpa
mkuu wa chuo ni kwamba
mimi niwekwe rumande kwanza ili wafanye upelelezi.
Lakini sikuyumba katika
msimamo wangu. Nilimweleza mkuu wa chuo
kwamba mimi ni raia na si
mpelelezi. Nilizirudia rudia
sababu zangu za kuacha jeshi
tena kwa ujasiri mkubwa na
kumhakikishia mkuu wa chuo kwamba akinipa hayo
ninayoyataka niko tayari
kubaki jeshini. Hatimaye kauli ya mwisho ya
mkuu wa chuo ilikuwa ni hii:
“Jeshi ni wito. Tunaweza
kumlazimisha huyu kijana
kuwa mwanajeshi lakini
baadaye ikatuletea madhara makubwa sana.” Akamalizia
kwa kusema, “chukueni
maelezo yake kwa maandishi
kisha arudishe vifaa vya jeshi.” Wakati naondoka nilimsikia
ofisa mafunzo akitoa
maelekezo kwa walio chini
yake kwamba mwanafunzi
mwingine wa jeshi akija
kuripoti na kwenye daftari akajaza kwamba ni Msabato,
msimsajili kwanza mpaka aje
kwangu! Sijui kama Wasabato
wameendelea kupokewa
kwenye hicho chuo cha
magereza lakini ninachotaka askari wote wa majeshi yetu
yote na vikosi vyote, ni
kwamba askari unaweza
kusimama kwa miguu yako na
kufikiri kwa akili yako
mwenyewe! Ndugu zangu askari, nchi
imefika mahali ambapo
Waingereza hupenda kupaita
‘critical point’. Ni mahali
ambapo wananchi wako
tayari kwa mabadiliko na watawala wako tayari kwa
mapambano ili kubaki
madarakani. Katika point hii askari wetu
wanakuwa na nafasi kubwa
ya aidha kuwezesha
mabadiliko hayo kutokea kwa
wakati wanaoutaka
wananchi, tena kwa amani ama kuyachelewesha (si
kuyazuia) na kusababisha
yatokee baadaye kidogo
kuliko wananchi walivyotaka,
tena baada ya kumwaga damu
nyingi ya Watanzania wasio na hatia! Napenda kurudia kwamba
hakuna jeshi lolote duniani
hata kama tungekusanya
majeshi yote ya dunia hii na
kuyaleta Tanzania
hawataweza kuizuia nguvu ya umma pale inapokuwa
imeamua kufanya mabadiliko. Napenda tena kurudia
kwamba si lazima askari
mfanye kile ambacho
wakubwa wenu wanataka na
kuwaamuru kufanya.
Tunaweza kusimama imara na kutetea haki za Watanzania
tukiwamo na sisi askari.
Niliwahi kugoma kutii amri ya
kukamatwa na kuwekwa
rumande. Lakini pia mifano ni mingi na
nisingependa kuchukua
mifano kutoka nchi za Ulaya
kama Uingereza ambako
tulishuhudia wananchi
wakiandamana mitaani na askari wao hawakuwahi hata
kumpiga kofi tu
mwandamanaji hata mmoja. Walipohojiwa na vyombo vya
habari walisema dhahiri
kwamba waandamanaji ni
raia halali wenye haki ya
kufanya kile wanachokifanya
kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi yao. Katiba ya
Tanzania na sheria za nchi hii
zinatoa haki kama zile za
Uingereza. Tofauti ni
utekelezaji wa matakwa hayo
ya kikatiba na kisheria. Watawala wa Uingereza wako
tayari hata kung’oka
madarakani ili kutekeleza
matakwa ya nguvu ya umma. Lakini wale wa Tanzania
wako tayari kung’oa uhai wa
raia wengi ili mradi kuzuia
nguvu ya umma inayodai haki
na wananya hivyo kwa
sababu ya hofu ya kung’oka madarakani, jambo ambalo
hawataki kabisa kulisikia. Na
ndugu zangu askari napenda
kuwaambia kwamba yote
yanafanywa na watawala
wetu kwa kuwategemea nyinyi. Wanaminya haki zenu nyinyi
wenyewe, haki za wazazi
wenu, dada na ndugu zenu,
marafiki zenu, jamaa zenu na
majirani zenu. Chukulia mfano
rafiki zangu Mtaki na Edwin. Tumesoma wote shule ya
msingi pale Magu. Nilichaguliwa kujiunga na
Mazengo Sekondari, shule
kubwa na ya muda mrefu
ambayo sasa imegeuzwa
kuwa chuo kikuu bila
mabadiliko ya majengo. Shule iliyokuwa na maabara
nne kwa maana ya maabara
ya baiolojia, kemia, fizikia na
jiografia. Ilikuwa ni sekondari
ya ufundi na hakuna karakana
ambayo haikuwapo. Shule iliyokuwa na walimu wa
kutosha, vyumba vya kutosha
vya madarasa na vya kulala
mabwenini. Katika bweni la Ujamaa kwa
mfano, nilikokuwa naishi
mimi, kuna vyumba kadhaa
havikuwa na watu. Darasa la
Form IVA ambalo nilikuwamo
lilikuwa na wanafunzi 21 tu darasani. Na mazingira mengine mengi
ambayo sitaweza kuyataja
hapa ambayo yanafanya
wanafunzi wa leo wa Chuo
Kikuu cha Mt. John wajiulize
kama kweli ile ilikuwa ni shule ambayo haina maktaba
wala vitabu vya kutosha, na
mengineyo mengi
mnayoyafahmu. Nikafaulu kwa kiwango cha
daraja la juu lililoniwezesha
kuendelea mpaka chuo kikuu
na kupata kazi nzuri kwenye
Umoja wa Mataiifa. Rafiki zangu nakumbuka
mlivyoamua kujiunga na Jeshi
la Polisi si kwa sababu
mlipenda kazi hiyo ama
kwamba mlikuwa na wito wa
kuwa polisi kama mnavyodanganywa kwamba
jeshi ni wito. Nakumbuka mlijiunga huku
mkilalamika kwamba
mnalazimika kujiunga huko
kwa sababu kiwango chenu
cha ufaulu hakiwapi fursa ya
kazi bora zaidi ya hiyo. Lakini mimi nawafahamu vizuri.
Najua uwezo wenu wa
darasani. Mliathiriwa na
mazingira ya hovyo ya shule
mlizosoma. Rafiki zangu nyinyi wote leo ni
wakuu wa vituo vikuu vya
polisi vya wilaya katika wilaya
za Mbozi na Igunga. Leo hii mimi nimeacha kazi ya
Umoja wa Mataifa kwa ajili ya
kushiriki vema katika
mapambano ya kutafuta
ukombozi wa taifa hili. Wadogo zenu na wadogo
zangu mnawajua wako katika
juhudi za kutafuta maisha
lakini ni magumu. Wengine
walikosa kabisa nafasi ya
kujiunga hata na hiyo Magu Day. Wakaishia Bulima na Kinango,
ambako hali ilikuwa mbaya
zaidi. Wakafeli kabisa na leo
wanahangaika hapa na pale
lakini watawala
wanawawekea mazingira magumu mno ya kuendesha
maisha. Na sasa chukulia nao
wametambua hali yao duni
inasababishwa na watawala
walafi na walaghai.
Wamejaribu kutumia njia za
kidiplomasia kudai haki zao wanakutana na watu
wanaitwa wakuu wa wilaya
na mikoa. Wanaamua kuandamana,
mnashiriki kuamrisha askari
walio chini yenu kuwapiga na
kuwaweka rumande na
hatimaye kuwafungulia kesi
za kubumba! Askari wetu igeni mfano wa
askari wa Misri! Pale wananchi
walipoamua kuandamana
kukomesha utawala wa
kidhalimu wa miaka 30 chini
ya Hosni Mubarak, askari waliwalinda badala ya
kuwapiga. Walikataa kwa sababu hata
wao walikuwa wakiumizwa
na Mubarak lakini zaidi ya
hayo, waliokuwa
wakiandamana walikuwa ni
dada zao na ndugu zao na marafiki zao. Hivi sasa nchi iko njia panda.
Ugumu wa maisha
umeongezeka mara nne na
zaidi. Watawala hawalioni hilo
wala hawajishughulishi
kurekebisha hali ya mambo hususan hali ya uchumi. Wako busy na kujiandaa kwa
uchaguzi wa 2015. Mawaziri
wako busy na kampeni za
kuteuliwa kuwa wagombea
wa urais kupitia chama tawala
hapo 2015 na rais naye yuko busy kuandaa mtu wake
ambaye anadhani akimrithisha
jumba jeupe la pale Magogoni
atasema mwacheni Ndugu
Kikwete apumzike kwa
amani. Taifa limeamua kuandika
katiba mpya, rais na serikali
yake na chama chake
wameamua kuuteka
mchakato ingawa haikuwemo
kwenye ilani yao ya uchaguzi ili tu waturudishie katiba ya
mwaka 1977 na kuipa jina juu
ya jalada KATIBA YA JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
YA MWAKA 2014. Natambua juhudi
zinazoendelea hasa
zikiongozwa na CHADEMA
kujaribu kumkumbusha rais
kwamba katiba iko juu yake
na katiba ni mali ya wananchi na yeye anaajiriwa kwa katiba
hiyo na si yeye kujiandalia
katiba ili atawale kwa ulaini. Lakini juhudi za kidiplomasia
zikishindikana hapo ndipo
itabidi haki ya watu idaiwe
kwa maandamano na hapo
askari wote tuungane na
kuwa kama Misri, kwa kuwa Katiba mpya ni kwa masilahi
yenu pia! Jaribuni kutafakari!.
 
[h=1]Forbidden[/h] You don't have permission to access / on this server.
Additionally, a 404 Not Found error was encountered while trying to use an ErrorDocument to handle the request.

mkuu hii inapatikana www.freemedia.co.tz/daima
 
MINYANYANYASO KWA 'SAUTI HURU' MOJA SIKU ZOTE HUIBUA ZINGINE TISA NA KWA MBOLEA MPYA NA KUZIIMARISHA ZAIDI AZMA NA MSUKUMO THABITI MOYONI!!

Haki kwanza, uzalendo mbeeeeeeleeeeeeee kama tai huku waandishi mbali mbali nchini wakianza kupitishwa kwenye tanuri la mkono wa chuma tangu enzi za Tido Mhando hadi leo hii Absalom Kibanda bila kujue kesho ni NINI kwa nani na wapi.

Mhimili wa nne katika nguzo za serikali yoyote ile duniani, ambayo ni tasnia ya uandishi wa habari, siku zote ukitikiswa na wao nao kuhisi kuvamiwa kwenye maeneo yao ya kujidai, basi tangu hapo ujue serikali lazima ijiandae zaidi kusugua mgongo wake ukutani zaidi huku ikiendelea kupokea mashambulizi takatifu toka kila upande. Sina uhakika kama kweli serikali ya CCM kweli litakua limejiandaa kwa hilo.

Kukamatwa kwa Mhariri Absalom Kibanda, wanaharakati wengine kutiwa misukosuko, na hata Rais Kikwete hivi sasa kugeuka polisi, hakimu na mwendesha mashitaka yote yeye kwa wakati mmoja kwa wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini siku mbili tu tangu Mhasham Askofu Mkuu Polycarp Pengo aongee na taifa, nasema hivi sasa Tanzania kisisa tumefungua UKURASA MPYA ZAIDI.
Jeshi la polisi linamshikilia mhariri wa gazeti la Tanzania Daima, A. Kibanda kwa tuhuma za uchochezi. Kibanda anashikiliwa kwenye makao makuu ya polisi jijini Dar es Salaam.
 
Hii nchi utakula kwa kadiri unavyojipendekeza kwa serikali. Wabunge wamepitisha hoja za serikali bungeni, wameongezwa posho (Japo kimenuka) , sasa polisi nao wanafanya kazi ya chama ili maslahi yao nao yapande. Sasa hivi utasikia mishahara yao imeongezwa kwa kuwa maisha ya polisi magumu...

Natania tu, hawa ni wenzetu basi tu wanatumiwa vibaya (a.k.a naogopa kusema ukweli)
 
Waraka wenyewe huu hapa,

Waraka maalumu kwa askari wote
Samson Mwigamba
MAKALA hii ilikuwa itoke Jumatano ya wiki iliyopita lakini kwa sababu za kiufundi ikashindikana. Imekuwa ni bahati nzuri kwamba inapotoka leo, ijibu swali la askari polisi dereva wa gari la maji ya kuwasha.
Askari huyo alimweleza Mwalimu Mkuu wa watu jinsi roho inavyomuuma pale anapowamwagia Watanzania wenzake maji hayo ya kuwasha wakati wakidai haki yao. Askari uliyeuliza na wenzako wote someni makala hii kwa utulivu. Huu ni waraka maalumu kwa askari wote wa majeshi yote vikosi vyote Tanzania Bara na Visiwani.
Kwa lugha ya wazi zaidi nazungumza na askari wa Jeshi la Polisi Tanzania, Askari wa Jeshi la Kujenga Taifa, askari wa Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo (KMKM), askari wa Jeshi la Magereza na wale wa Jeshi la Wananchi (JWTZ).
Kuwa mwanajeshi lolote kati ya hayo niliyoyataja si dhambi na si kweli kwamba kuwa mwanajeshi kunakuondolea uwezo wa kufikiri na badala yake ukawa unafikiriwa na watu wengine.
Wala haimaanishi kuwa askari kuwa kama robot ndio nidhamu bora kuliko zote duniani. La hasha! Mimi nilikataa utumwa huo!
Mwaka 1999 nilihitimu elimu ya cheti cha ufundi mchundo, yaani Full Technician Certificate (FTC) katika uhandisi wa Elektroniki na Mawasiliano ya Anga, yaani Electronics & Telecommunications Engineering kutoka Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT).
Nikiwa bado sijapata kazi ya maana, mwezi Aprili mwaka 2000 niliona tangazo la kazi ya Radio Technician katika Jeshi la Magereza. Nikatuma maombi na kuitwa kwenye usaili uliofanyika Chuo cha Maofisa wa Jeshi la Magereza Ukonga, Dar es Salaam mwezi Juni 2000.
Wote tuliofaulu usaili tulipangiwa siku ya kuripoti Chuo cha Magereza Kiwira kule Tukuyu, Mbeya.
Kufika kule nilishuhudia mambo ya ajabu. Ingawa wao hufurahia na kusema eti wanakutoa uraiani na kuwa mwanajeshi lakini baadhi ya matendo yanayofanyika wakati wa mafunzo ya jeshi ni ya kuwapumbaza askari wetu ili baadaye wakiwa kazini, watawala wawatumie watakavyo.
Nilishindwa kuvumilia kaulimbiu ya wakufunzi wa jeshi pale walipoelekeza kwamba chochote kruta (askari mpya mafunzoni) unachoambiwa lazima uitikie “ndiyo afande”. Nilishindwa kuitikia kwa mfano pale mkufunzi mmoja mwenye cheo cha koplo alipotutamkia mfululizo wa sentensi zifuatazo:
Mkufunzi: Nyinyi makruta mbona wote hamkuja na majembe?
Makruta: Ndiyo afande!
Mkufunzi: Hamkuambiwa makao makuu ya jeshi kwamba lazima mje na majembe?
Makruta: Ndiyo afande!
Mkufunzi: Kwa hiyo kwa kuwa hamkuambiwa na nyinyi hamkuyabeba?
Makruta: Ndiyo afande!
Mkufunzi: Wote ni wapumbavu pamoja na mama zenu waliowazaa.
Makruta: Ndiyo afande!
Ni hayo pamoja na mambo mengine ya kulazimishwa kwenda kwenye kile kinachoitwa disko, ambapo pamoja na uchovu wa kutwa nzima wa kazi ngumu na nyingi bado ni lazima ukae hapo mpaka saa 4 usiku tena ukinyooshewa kidole tu na mwenzako lazima usimame na kuimbisha wimbo tena kwa tabasamu, wimbo mmoja wapo ukisema “Magereza ninavyokupenda nitakunywa sumu juu yako”, ndiyo yaliyonifanya nikakataa kazi ya jeshi baada ya wiki moja tu ya mafunzo.
Siku niliyokataa jeshi ilikuwa ni Jumatano asubuhi ambapo sikwenda mchakamchaka na wakati wenzako wanatawanyika kufanya usafi wa nje maeneo mbalimbali, mimi nilibeba begi langu na kuanza kuondoka chuoni majira ya saa moja na nusu hivi asubuhi.
Nilikamatwa na mkufunzi mmoja wa jeshi na kupelekwa pamoja na begi langu kwa Ofisa Mafunzo wa chuo. Aliponiuliza sababu nilimtajia mbili, kwanza kwamba sifurahii mambo ya jeshi na kubwa zaidi kwamba mimi ni Msabato na nimeambiwa na wenzangu kwamba hapa hakuna kwenda kusali, siku zote za juma ni kazi.
Kitu ambacho sitaweza maana Sabato takatifu lazima nipumzike! Bila kuuliza zaidi aliconclude kwa kuniambia kwamba, “Sijawahi kuona mtu anaacha kazi kwa ajili ya mambo ya dini.
”Ni dhahiri wewe ulikuja kutupeleleza na hivyo kazi yako imeisha sasa unataka kurudi. Tutakuweka rumande, tena ile ya polisi kwa wiki mbili wakati tunafanya upelelezi juu yako.”
Askari aliyenileta alianza kunivuta ili kunipeleka rumande lakini nilikataa huku nikiendelea kujieleza kwa ofisa mafunzo ili ajue kwamba sikuwa na mpango huo aliousema.
Baada ya kuelemewa na hoja zangu alinipeleka kwa makamu mkuu wa chuo ambaye yeye alitumia zaidi Biblia kunihubiri kwamba nakaidi amri ya mamlaka wakati hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu.
Jibu langu lilikuwa fupi na lenye msimamo mzito kwamba ikiwa mamlaka ya wanadamu inafika mahali inanena tofauti na Mungu, Mtume Petro ametuandikia kwamba katika hali ya namna hiyo, “Imetupasa kumtii Mungu kuliko mwanadamu”.
Na yeye alinishindwa akanipeleka kwa mkuu wa chuo na wao wote wakiwapo. Ushauri waliokuwa wakimpa mkuu wa chuo ni kwamba mimi niwekwe rumande kwanza ili wafanye upelelezi. Lakini sikuyumba katika msimamo wangu.
Nilimweleza mkuu wa chuo kwamba mimi ni raia na si mpelelezi. Nilizirudia rudia sababu zangu za kuacha jeshi tena kwa ujasiri mkubwa na kumhakikishia mkuu wa chuo kwamba akinipa hayo ninayoyataka niko tayari kubaki jeshini.
Hatimaye kauli ya mwisho ya mkuu wa chuo ilikuwa ni hii: “Jeshi ni wito. Tunaweza kumlazimisha huyu kijana kuwa mwanajeshi lakini baadaye ikatuletea madhara makubwa sana.” Akamalizia kwa kusema, “chukueni maelezo yake kwa maandishi kisha arudishe vifaa vya jeshi.”
Wakati naondoka nilimsikia ofisa mafunzo akitoa maelekezo kwa walio chini yake kwamba mwanafunzi mwingine wa jeshi akija kuripoti na kwenye daftari akajaza kwamba ni Msabato, msimsajili kwanza mpaka aje kwangu! Sijui kama Wasabato wameendelea kupokewa kwenye hicho chuo cha magereza lakini ninachotaka askari wote wa majeshi yetu yote na vikosi vyote, ni kwamba askari unaweza kusimama kwa miguu yako na kufikiri kwa akili yako mwenyewe!
Ndugu zangu askari, nchi imefika mahali ambapo Waingereza hupenda kupaita ‘critical point’. Ni mahali ambapo wananchi wako tayari kwa mabadiliko na watawala wako tayari kwa mapambano ili kubaki madarakani.
Katika point hii askari wetu wanakuwa na nafasi kubwa ya aidha kuwezesha mabadiliko hayo kutokea kwa wakati wanaoutaka wananchi, tena kwa amani ama kuyachelewesha (si kuyazuia) na kusababisha yatokee baadaye kidogo kuliko wananchi walivyotaka, tena baada ya kumwaga damu nyingi ya Watanzania wasio na hatia!
Napenda kurudia kwamba hakuna jeshi lolote duniani hata kama tungekusanya majeshi yote ya dunia hii na kuyaleta Tanzania hawataweza kuizuia nguvu ya umma pale inapokuwa imeamua kufanya mabadiliko.
Napenda tena kurudia kwamba si lazima askari mfanye kile ambacho wakubwa wenu wanataka na kuwaamuru kufanya. Tunaweza kusimama imara na kutetea haki za Watanzania tukiwamo na sisi askari. Niliwahi kugoma kutii amri ya kukamatwa na kuwekwa rumande.
Lakini pia mifano ni mingi na nisingependa kuchukua mifano kutoka nchi za Ulaya kama Uingereza ambako tulishuhudia wananchi wakiandamana mitaani na askari wao hawakuwahi hata kumpiga kofi tu mwandamanaji hata mmoja.
Walipohojiwa na vyombo vya habari walisema dhahiri kwamba waandamanaji ni raia halali wenye haki ya kufanya kile wanachokifanya kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi yao. Katiba ya Tanzania na sheria za nchi hii zinatoa haki kama zile za Uingereza. Tofauti ni utekelezaji wa matakwa hayo ya kikatiba na kisheria. Watawala wa Uingereza wako tayari hata kung’oka madarakani ili kutekeleza matakwa ya nguvu ya umma.
Lakini wale wa Tanzania wako tayari kung’oa uhai wa raia wengi ili mradi kuzuia nguvu ya umma inayodai haki na wananya hivyo kwa sababu ya hofu ya kung’oka madarakani, jambo ambalo hawataki kabisa kulisikia. Na ndugu zangu askari napenda kuwaambia kwamba yote yanafanywa na watawala wetu kwa kuwategemea nyinyi.
Wanaminya haki zenu nyinyi wenyewe, haki za wazazi wenu, dada na ndugu zenu, marafiki zenu, jamaa zenu na majirani zenu. Chukulia mfano rafiki zangu Mtaki na Edwin. Tumesoma wote shule ya msingi pale Magu.
Nilichaguliwa kujiunga na Mazengo Sekondari, shule kubwa na ya muda mrefu ambayo sasa imegeuzwa kuwa chuo kikuu bila mabadiliko ya majengo.
Shule iliyokuwa na maabara nne kwa maana ya maabara ya baiolojia, kemia, fizikia na jiografia. Ilikuwa ni sekondari ya ufundi na hakuna karakana ambayo haikuwapo.
Shule iliyokuwa na walimu wa kutosha, vyumba vya kutosha vya madarasa na vya kulala mabwenini.
Katika bweni la Ujamaa kwa mfano, nilikokuwa naishi mimi, kuna vyumba kadhaa havikuwa na watu. Darasa la Form IVA ambalo nilikuwamo lilikuwa na wanafunzi 21 tu darasani.
Na mazingira mengine mengi ambayo sitaweza kuyataja hapa ambayo yanafanya wanafunzi wa leo wa Chuo Kikuu cha Mt. John wajiulize kama kweli ile ilikuwa ni shule ambayo haina maktaba wala vitabu vya kutosha, na mengineyo mengi mnayoyafahmu.
Nikafaulu kwa kiwango cha daraja la juu lililoniwezesha kuendelea mpaka chuo kikuu na kupata kazi nzuri kwenye Umoja wa Mataiifa.
Rafiki zangu nakumbuka mlivyoamua kujiunga na Jeshi la Polisi si kwa sababu mlipenda kazi hiyo ama kwamba mlikuwa na wito wa kuwa polisi kama mnavyodanganywa kwamba jeshi ni wito.
Nakumbuka mlijiunga huku mkilalamika kwamba mnalazimika kujiunga huko kwa sababu kiwango chenu cha ufaulu hakiwapi fursa ya kazi bora zaidi ya hiyo. Lakini mimi nawafahamu vizuri. Najua uwezo wenu wa darasani. Mliathiriwa na mazingira ya hovyo ya shule mlizosoma.
Rafiki zangu nyinyi wote leo ni wakuu wa vituo vikuu vya polisi vya wilaya katika wilaya za Mbozi na Igunga.
Leo hii mimi nimeacha kazi ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kushiriki vema katika mapambano ya kutafuta ukombozi wa taifa hili.
Wadogo zenu na wadogo zangu mnawajua wako katika juhudi za kutafuta maisha lakini ni magumu. Wengine walikosa kabisa nafasi ya kujiunga hata na hiyo Magu Day.
Wakaishia Bulima na Kinango, ambako hali ilikuwa mbaya zaidi. Wakafeli kabisa na leo wanahangaika hapa na pale lakini watawala wanawawekea mazingira magumu mno ya kuendesha maisha.
Na sasa chukulia nao wametambua hali yao duni inasababishwa na watawala walafi na walaghai. Wamejaribu kutumia njia za kidiplomasia kudai haki zao wanakutana na watu wanaitwa wakuu wa wilaya na mikoa.
Wanaamua kuandamana, mnashiriki kuamrisha askari walio chini yenu kuwapiga na kuwaweka rumande na hatimaye kuwafungulia kesi za kubumba!
Askari wetu igeni mfano wa askari wa Misri! Pale wananchi walipoamua kuandamana kukomesha utawala wa kidhalimu wa miaka 30 chini ya Hosni Mubarak, askari waliwalinda badala ya kuwapiga.
Walikataa kwa sababu hata wao walikuwa wakiumizwa na Mubarak lakini zaidi ya hayo, waliokuwa wakiandamana walikuwa ni dada zao na ndugu zao na marafiki zao.
Hivi sasa nchi iko njia panda. Ugumu wa maisha umeongezeka mara nne na zaidi. Watawala hawalioni hilo wala hawajishughulishi kurekebisha hali ya mambo hususan hali ya uchumi.
Wako busy na kujiandaa kwa uchaguzi wa 2015. Mawaziri wako busy na kampeni za kuteuliwa kuwa wagombea wa urais kupitia chama tawala hapo 2015 na rais naye yuko busy kuandaa mtu wake ambaye anadhani akimrithisha jumba jeupe la pale Magogoni atasema mwacheni Ndugu Kikwete apumzike kwa amani.
Taifa limeamua kuandika katiba mpya, rais na serikali yake na chama chake wameamua kuuteka mchakato ingawa haikuwemo kwenye ilani yao ya uchaguzi ili tu waturudishie katiba ya mwaka 1977 na kuipa jina juu ya jalada KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 2014.
Natambua juhudi zinazoendelea hasa zikiongozwa na CHADEMA kujaribu kumkumbusha rais kwamba katiba iko juu yake na katiba ni mali ya wananchi na yeye anaajiriwa kwa katiba hiyo na si yeye kujiandalia katiba ili atawale kwa ulaini.
Lakini juhudi za kidiplomasia zikishindikana hapo ndipo itabidi haki ya watu idaiwe kwa maandamano na hapo askari wote tuungane na kuwa kama Misri, kwa kuwa Katiba mpya ni kwa masilahi yenu pia! Jaribuni kutafakari!
 
leo%2B1.jpg
 
Haja kamatwa ila ameitwa kulisaidia Jeshi la polisi acheni uchochezi nyie mnajua maana ya kukamatwa!!!!!

Kwani kulisaidia Jeshi la Polisi ni lazima??? na kwanini uwasaidie watu wanaolipwa mishahara kwa kazi yao???
 
Hivi ile Ripoti ya tume iliyoundwa kuchunguza kifo cha Jwani mwakyusa ilishatoka? au uchunguzi bado unaendelea?

Hili nalo neno
"When I was a boy I was told that anybody could become a President. Now I’m beginning to believe it."

 
Wameanza. Watakamata hata kuku, maana siku zao zinahesbika. Hawana uvumilivu. Issue hata ikiwa ndogo vipi wataishupalia na kuipandisha chati. kial kitu wanakipa umaarufu wao wenyewe. Hata yule ambaye hakusoma ile makala sasa ataitafuta, akasome ajadili na wenzake. Mwisho wa yote ni aibu kwao.
 
Back
Top Bottom